Kudanganya......

...na hapa ndipo iliposimamia mada yangu. Unajua kabisa Mkeo anakudanganya, mfano; asb ulimuacha ofisini,....bahati mbaya, mchana ukampitia um surprise kwa lunch.... Pale ukajibiwa hakuingia kazini kabisa siku hiyo.

Jioni mpo nyumbani wamuuliza za kazi anakwambia alikuwa v.busy kwa ofisi, ....unapomwambia ulipita hukumkuta, anabadili maneno anakwambia alikwenda hospitali!

hahahahaha

Aisee..... kumbe ukipiga fix afu wakatabasamu wanakuwa wanajua umewafix ila wanakuwa hawana jinsi... ngastuka!!

AU kwa kuwa wanajua hata wakijua unawafix hawana jeuri ya kukuzuia lol

Ndo manake
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
.....mwanajamiiOne, nilitaka kuku Quote server ipo slow....

Umegusia jambo la maana sana, " .......saa ingine jambo dogo mwenzio analibebea bango"....

Dogo kwako, kubwa kwa mwenzio bana. I agree nawewe haina haja ya kuliweka rohóni, ndio maana Mbu mie nikishakubaliana na mwenza wangu jambo fulani halifai, likirudiwa nakumbushia makubaliano yetu, mara ya tatu siulizi tena. Najipa jibu 'nimedharauliwa' tulivyokubaliana.

....unless kwa thread hii (na bado sijafanikiwa) naweza pata jibu tofauti...

Dear Mbu pole sana okay now nimekuelewa
Okay ninaposema jambo dogo simaanishi life-threatening bana! Mfano mie Mbu ushanipiga marufuku kusalimiana na rafiki yangu 'flani' with no reasons at all. Sasa mie siwezimweleza rafiki kuwa my darling kanikataza kuongea na wewe......siku nikikutana na yeye barabarani tukasalimiana tu na kuexchange some words. Mbu wangu ukapata taarifa nimeonekana na fulani.... nakujua ushalisema na kuliseema...ukiniuliza nitakwambia nilimwona kwa mbali, tukapungiana mikono tu.......Nimedanganya si ndio? But..............
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Nikaonelea si vibaya nikaweka ufafanuzi wa kidikshineri ili kuwapa nafasi wakenya nao kuchangia kwenye hii sredi.


Lie:

1. a false statement made with deliberate intent to deceive; an intentional untruth; a falsehood.

2. something intended or serving to convey a false impression; imposture: His flashy car was a lie that deceived no one.

3. an inaccurate or false statement.

4. the charge or accusation of lying: He flung the lie back at his accusers.
 
Katika mahusiano uongo una nafasi yake na hadhi yake. Binadamu tumeumbwa kukosea na kujirekebisha pale tunapokosea.

"Mimi Klorokwini naahidi kutumia uongo kuilinda ndoa yangu popote pale nitakapoteleza kibinaadamu, Ewe mola nisaidie".


itikieni amen mbariki kiapo changu
 
Katika mahusiano uongo una nafasi yake na hadhi yake. Binadamu tumeumbwa kukosea na kujirekebisha pale tunapokosea.

"Mimi Klorokwini naahidi kutumia uongo kuilinda ndoa yangu popote pale nitakapoteleza kibinaadamu, Ewe mola nisaidie".


itikieni amen mbariki kiapo changu

...........................Kha loya kwa hiyo kuna a bad lie na good one?

nakubaliana na wewe hapo kwenye nia ya kunusuru but haipaswi kurudiwa!
 
MwanajamiiOne, nimeku Quote tena bila mafanikio. Mtu anayekukataza uache urafiki na fulani, myb anania nzuri tu kwamba huenda ur influenced easily kuasi na huyo rafiki.

Ila, kuna wanaokataza kwa maslahi yake binafsi....labda utapata 'classified infos, etc'.....haya yote mawili hayanisumbui sana.

Kudanganywa wazi wazi ni mifano kama niliyoweka awali....unamkuta mwenza wako kakamata kiuno cha hse girl anakula denda,....unapo panic...'anakutuliza' na maneno,"....calm down myloving wife, it is not what you think!"....au, unamkuta na Condom, anakwambia hajui zimefikaje hapo...
 
...........................Kha loya kwa hiyo kuna a bad lie na good one?

nakubaliana na wewe hapo kwenye nia ya kunusuru but haipaswi kurudiwa!

kuna kategori moja umeisahau, kuna recommended lie pia, kuna sehemu uongo unapendekezeshwa kabisa utumike ili to avoid unnecessary downtime marriage blackmailing (hii ni mada mpya ambayo itasibitisha kwamba waifu wangu ana bahati kweli kuolewa na mimi).

Usinibeep sana shem leo nina mapwenti kuliko balozi wa sudan ya kusini
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Ofu topik:
wee Maty mbona unaonekana Mbu akianzisha sredi tu. Ukimwagiwa tindikali na MJ1 , shauri yako.

hehehe turudini kwenye mada ya uongo sasa.

......mmmmnnh? majungu hayo sasa. Maty usijibu! mdanganye danganye akikufata kwa pm...
 
Last edited by a moderator:
Katika mahusiano uongo una nafasi yake na hadhi yake. Binadamu tumeumbwa kukosea na kujirekebisha pale tunapokosea.

"Mimi Klorokwini naahidi kutumia uongo kuilinda ndoa yangu popote pale nitakapoteleza kibinaadamu, Ewe mola nisaidie".


itikieni amen mbariki kiapo changu

Ameen!

Hahaha,....ehh? "....to avoid unnecessary downtime marriage blackmailing"

Will adhere to your instructions my Solicitor... Usijeniruka kesi tu.
 
Swahiba yangu Mbu niaje?

Uongo ni kitu muhimu sana katika mapenzi....Pia ni muhimu zaidi kaika maisha ya kawaida.

Bila uongo mahakama zote zingeshafungwa....!!

Ila kama una maana ya kungonoka nje kwamba nao ni uongo, basi huo Babu hakubaliani nao!!

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: Mbu
Kuna nini hapa?
Soulmate umedanganywa? pole

................. Unajua uongo hauepukiki kama vigezo na masharti havizingatiwi. Mie nitazungumzia uwongo ndani ya mahusiano ya kindoa au kwa wenye mahusiaono ya muda mrefu ambapo mara nyingi ile hali ya urafiki huwa imetoweka au haipo. Mf. mdanganywaji akiwa mkoloni sana, mkali sana anakaribisha mazingira ya kudanganywa.

Lakini pia akiwa ni mtu ambaye kitu kidogo anakibebea bango yaani hadi unashangaa, lazima atamfanya mwenzi wake amdanganye tu.

But mnapokuwa na mahusiano ya kirafiki inakuwa rahisi pia kwa mtu kuwa huru na asichukue nguvu nyingi kuanza kutafuta uongo wa kudanganyia.

Na pia ni vema kwa anayedanganywa, kama ni rafiki na kajua kuwa kadanganywa, awe muwazi tu kwa aliyemdanganya kuliko kugumia maumivu kisirisiri!

Mjukuu hujambo wewe?

Sasa MwanajamiiOne, hebu nambie vizuri kwanza, una maana kama mahusiano yenu ni mazuri sana hakuna haja kuwa na kabati dogo la uongo?

Unaweza kumueleza soulmate wako kila kitu bila kumficha?

Ukishajibu hapa, nitaangalia kwenye kabti langu nikupe mifano!!

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: Mbu
.....:screwy: .....hivi, unapokuwa unamdanganya mtu, bila 'woga' kwamba ANAJUA unamdanganya, ...kusudio lako huwa nini?

.....mimi bado sina tafsiri sahihi juu ya hili zaidi ya 'madharau' katika mapenzi. Au wewe waonaje? Mbu is only thinking ALOUD ....:what:

Nipeni maoni yenu waungwana...

Ukimaliza kudanganywa mwambie ukweli alikudanganya kuwa unajua ame/anakudanganya on spot (usipende kulimbikiza maradhi, tibu ugonjwa mara moja).

Enyi wadanganyaji, mmalizapo kudanganya basi wajulisheni mliowadanganya kuwa mnawadanganya.
 
Ukimaliza kudanganywa mwambie ukweli alikudanganya kuwa unajua ame/anakudanganya on spot (usipende kulimbikiza maradhi, tibu ugonjwa mara moja).

Enyi wadanganyaji, mmalizapo kudanganya basi wajulisheni mliowadanganya kuwa mnawadanganya.

Huo sasa utakuwa mchezo wa kitoto!!

Babu DC!!
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Back
Top Bottom