Kozi ya kusoma halafu baada ya kumaliza chuo isaidie kujiajiri .

Gotze Giyani

Senior Member
Feb 28, 2022
122
181
Wadau poleni na majukumu kuna dogo home kamaliza HKL na ana division 1 ya 5 ni kozi gani nzuri anaweza kusomea na chuo kipi ili akimaliza aweze kujiajiri maana uwezekano wa ajira kwa sasa ni mdogo sana naomba mawazo yenu wadau.
 
Serikali inaposema kujiajiri haimaanishi kupitia hizo kozi wanazosomea wanafunzi

Kila kitu atakachokifikiria kinaweza kuwa ajira kwake lakini kozi anayosomea ni kama inampa namna bora ya kujisimamia yeye kama yeye.

Aende kozi yoyote anayowezana nayo,akitoka hapo akianziasha wazo la ishu yoyote ya kufanya inakuwa ndyo kujiajiri kwenyewe huko.
 
Akosome Veta
Electrical engineering
Mechanical engineering
Electronic
IT
Marine engineering
 
Aloooooooo
Nani aliwaambia kwamba chuo kikuu kuna kozi za kujiajiri na kuajiriwa.
hivyo vitu viwili vinategemea mindset ya mtu binafsi nakozi zote unaweza kujiajiri au kuajiriwa.
 
Back
Top Bottom