Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,712
Nimejiuliza wakati napitia uzi wa Cantalisia kuhusu jamaa alietoka nduki baada ya kugundua mpenzi wake ana mawe zaidi yake.Sasa swali linakuja,kwanza wanawake wanakubali kuwa mwanaume ni kichwa cha familia?(Kuwa kichwa kuna maana ya kutolea maamuzi ya mwisho jambo lolote linalohusu familia)kama wanakubali mwanaume ni kichwa kwa tafsiri hiyo,Je mwanamke anapoolewa akakutwa na mali aliyoichuma mwenyewe hii nayo itaingia katika usimamizi na maamuzi ya mwisho ya mume?(hapa nazungumzia maamuzi chanya sio ya kufuja mali)Yaani mke hatakua tena na kauli ya mwisho na namna ya kuendesha mali hiyo kwa sababu mwanamke huyo tayari anamilikiwa na mume ama mali ya mwanamke haitamhusu mume?Jambo hili huenda ndio sababu ya ugumu wa kuoa mwanamke mwenye mali!