Steve Dii
JF-Expert Member
- Jun 25, 2007
- 6,402
- 1,254
Ibrah, wazo lako ni zuri sana, wasi wasi wangu sijui hii kampeni yaweza fanyikaje? Nilisha uliza huko nyuma kwamba jamani hata hii mikataba mibovu ambayo wote tunaishuudia hata huu wa Buzwagi ambayo haijaanza ( kwa maana kwamba muwekezaji hajatumia pesa yake) hatuwezi izuia?? Jibu nililo pata lilinimaliza kabisa, kwamba hapa tumeisha saini mkataba! na hicho ndo kitanzi kinacho tumaliza! sasa na hili la kiwira, mkataba ulisha sainiwa sasa hapo ndo naona giza tupu! na kuishiwa nguvu na matumaini ya kampeini inayo weza fanyika na ikaleta nuru mpya!
Rwabugiri, ni kweli kuna utata mwingi katika hili, hata hivyo kuna maelezo fulani hivi yalipatikana kutoka kwa Bwn. Tundu Lissu, alipohojiwa na Mwanakijiji, mimi naona yana leta matumaini ya aina fulani hivi kama kusurutisha mikataba yote kunashindikana. unaweza kusikiliza kwa kubonyeza hapa. Inabidi usikilize mpaka mwisho.
SteveD.