Makanyaga
JF-Expert Member
- Sep 28, 2007
- 10,340
- 6,856
Kuna baadhi ya watu ambao Hayati JPM alikuwa anawaamini lakini pengine walikuwa hawamshauri vizuri sana. Haya ni makosa ya msingi yaliyofanyika na kupelekea ionekana kama Serikali ilihusika. Walinzi watakuwa hawakuondolewa; watakuwa walijishau wenyewe kutokana na yale mazoea kwamba sehemu hiyo imekuwa ni salama miaka nenda rudi na hapakuwa pamewahi kutokea tukio lolote la ajabu hapo kabla. Waliofanya tukio watakuwa waliwasoma walinzi mwenendo wao kwa siku nyingi. Kwani Hamza aliyeshambulia askari wetu kwa kutumia silaha zao, mtu akija akadai kuwa askari walimpa silaha zao Hamza, kama ni mahakamani kuwa-challenge inakuwa ni shida..serikali imeshindwa kujitetea ilikuwaje walinzi wake wakaondolewa area D eneo aliposhambuliwa Tundu Lissu.
..pia kitendo cha serikali ya awamu ya 5 kukataa ombi la kushirikisha wachunguzi wa kimataifa, na yenyewe kushindwa kuwabaini wahusika mpaka leo, kinaleta hisia kuwa waliohusika kumshambulia Lissu wako miongoni mwao.