KITUO cha Taarifa kwa Wananchi (TCIB) kimemshitaki Rais Jakaya Kikwete The HAGUE

I'm not disputing that. Nyinyi mliomchagua JK wachumia tumbo na wasiojielewa

..siku hizi ikulu imekua kitengo cha damage control propaganda....kwasababu ya blunder ya ------....hakika nitawalaumu hadi siku ya mwisho ile NEC na CC iliyopitisha jina la huyu mswahili kugombea urais 2005...maana nchi hii imekua stagnant kwa karibia miaka 9 sasa...


...Hivi nani humu anaweza kusema kwa mda huu i sera gani alikuja nayo na kuisimamia vema mkwerekiasi cha TZ kufaidi?..sera ipi??hamna ...nchi imekua inaendeshwa kizimamotozimamoto tu....na sasa jamaa anataka kumalizia mda wake kwa mbwembwe za kutuangamiza....inauma...

....Kwa kulinganisha tu watawala wetu waliopita...Nyerere alituletea ujamaa na kujitegemea na tukauona....Mwinyi akaja na biashara huria (free markets)..ama "ruksa"....Mkapa akaja na ubinafsishwaji (privatization)...pamoja na mapungufu yake...Je yeye JK kaja na nini cha kukumbukwa akiondoka???...kama si maneno na blah blah tu zisizo na mwisho...na kututia hasara zaidi ka kutuongezea deni la taifa ambalo yeye na family yake wala hawatahusika kulilipa...


...Ile NEC na CC ya ccm iliacha jina la mtu kama Dr.Salim ..mtu makini mwenye maono(vision)na asiye na njaa....tena ni mwenyekiti wa kamati ya Dr.Mo Ibrahim inayochagua viongozi bora Africa (kipimo tosha cha umakini na uadilifu)....Wakamwacha huyu wakatuletea mtu mwenye njaa...msanii....kaifanya ikulu yetu kijiwe cha kuwanufaisha washkaji na family yake...


...Nchi ya TZ imejaa utajiri lakini imegeuzwa ombaomba wa dunia ...sababu tu ya kuendekeza njaa kwa watawala...Inasikitisha sana mtu anaona ujiko kupanda ndege kwa kodi za walala hoi wa TZ kila kukicha kwenda kuhemea vibaba nje ya nchi....wakati madini na pembe zetu zinapakiwa kila kukicha kupelekwa nje ya nchi....hii hali kama si jana kuu kwa nchi hii ni nini??....alfu eti kuna genge la wezi wa ccm waliokuwa kwenye mtandao wake wa urais bado wanaonyesha nia ya kutaka kuja kututawala tena????...ili waendeleze majanga haya!!!....no way...we need to veto them .....TZ needs a role model president..and not a mere beggar....


......Aniambie mtu humu ndani ni ipi sera alikuja nayo JK na akaisimamia vema na hata akiondoka akumbukwe nayo!!...hamna kitu kwa kifupi...zaidi ya sera ya safari za nje....hata issue ya katiba mpya wameleta wapinzani anaowaita maadui wa ccm...amka TZ!!!!!


....Neno la faraja kwa wapinzani wenye mapenzi mema na nchi....Dunia hutawaliwa na principle moja muhimu kuwa..."mla huliwa".....ama..."ukidhulumu nawe utadhulumiwa"(hata kama si leo)...hivyo wakati JK anatangaza kuwashughulikia wapinzani kwa kutumia nafasi yake kama rais ..nae ajue kuwa anawindwa kushughulikiwa na watu kama kina Kagame....hata kama atakuwa amemaliza mda wake wa urais....Wakati JK anatangaza uadui na wanasiasa wa upinzani ndani ya TZ...nae ajue ana maadui nje ya nchi....tena wanaotokana na mdomo wake mwenyewe...Huu ni uhalisia ambao unatakiwa uwape faraja wapinzani wanaotishiwa na JK ndani ya TZ....yeye anaweza kuonekana shujaa kwa watu kama NEC ya ccm wanaofaidi matunda ya utawala wake.....lakini ajue nae anaweza kuonekana adui mkubwa kwa wengine (kama kina Kagame).....tafakari.....

....
 
Hawa kina Kibamba wote wachumia tumbo tu hakuna lolote wafanyalo pamoja na kwamba kauli za JK hazikuwa za kiungwana...

Ni mangapi yaliyofanywa na serikali ya Kikwete yaliyovunja haki za binadamu lakini walinywea nywiii...

elewa kwamba kikwete ni rais na ni mtu wa mwisho katika nafasi za uongozi hivyo kauli yake ni amri na wala si ushauri.
huwa napata shida sana kutambua hotuba zake utadhan kama anaongea kwenye harusi za send off kana kwamba hachagui maneno yepi yanafaa na yep hayafai.
 
Deus Kibamba alipiga sana kelele juu ya katiba mpya, sasa kila kitu kimekubalika na mchakato umepamba moto ameona hatakuwa na cha kupigia kelele na kula fedha za wafadhili ameamua kutoka kivingine. Masikini hata kuwa mjumbe wa Bunge la Katiba halikuteuliwa.
 
Wanasema uhuru bila mipaka ni wendawazimu. JK ametoa uhuru sana Tanzania kwa hiyo kila mtu anafanya atakacho.
Ina maana rais ni mwendawazimu? maana kavuka mipaka ya uhuru aliopewa na katiba,

Sijawahi kuona wala kusikia rais akihamasisha wananchi wake wapigane labda marais madkteta tu.
 
Ina maana rais ni mwendawazimu? maana kavuka mipaka ya uhuru aliopewa na katiba,

Sijawahi kuona wala kusikia rais akihamasisha wananchi wake wapigane labda marais madkteta tu.

Mwendawazimu ni yule anayeshindwa kutofautisha mwenye akili na siye na akili!
 
Msimlaumu Kibamba maana kwenda kwake The Hegue hakuwezi kuleta machafuko. Ila kauli ya kichochezi ya mkuu wa kaya ni fedheha kwa kiongozi mkuu kama huyo kuitoa. Baba gani atawachochea watoto wake ndani ya nyumba moja wapigane! Hiyo ni failure kubwa ya kiuongozi. Nasisitiza tena UTAIFA KWANZA JK BAADAE. Siasa na wanasiasa wanapita bali sisi watanzania tushikamane kwa mustakhabali wa Taifa letu!
 
elewa kwamba kikwete ni rais na ni mtu wa mwisho katika nafasi za uongozi hivyo kauli yake ni amri na wala si ushauri..

Naona unasahau pia kuwa Jakaya ni Mwenyekiti wa CCM na vikao vyake vote vikubwa...

Pia umesahau kuwa wakati akitamka yale matamshi tatanishi alikuwa amevaa cheo hicho cya Uenyekiti wa CCM...

Hivyo maneno yake yalikuwa ni amri kwa wafuasi wa CCM pekee lakini sio Watanzania kama unavyodhani...
 
Naona unasahau pia kuwa Jakaya ni Mwenyekiti wa CCM na vikao vyake vote vikubwa...

Pia umesahau kuwa wakati akitamka yale matamshi tatanishi alikuwa amevaa cheo hicho cya Uenyekiti wa CCM...

Hivyo maneno yake yalikuwa ni amri kwa wafuasi wa CCM pekee lakini sio Watanzania kama unavyodhani...

Basi vema Rais wa nchi asiwe mwenyekiti wa chama chochote cha siasa ili kuondoa mianya ya miingiliano ya mambo ya chama na serikali.
 
Kibamba hapa amekurupuka. Huwezi kukimbilia kwenye jumuiya ya kimataifa kabla hata hujatafuta suluhu ya ndani ikiwa ni pamoja na kutaka ufafanuzi wa kauli au kumtaka aliyetoa kauli aifute. Sasa kila jambo tukikimbilia kwenye jumuiya kimataifa bila kujiridhisha kwamba ni juu ya uwezo wetu si watatuona walalamikaji na kutuchoka mapema? Tanzania hatujafikia mahali pa kuhitaji msaada wa kimataifa kwa matatizo yetu ya ndani.
Mimi nadhani tukubaliane tu kuwa yeye siyo wa kwanza ndani ya serikali kutoa kauli ya ovyo na yenye madhara. Yeye pia kama wenzake ana washauri kibao ambao anaruhusiwa kuwateua na kuwafukuza kazi muda wowote. Kama ni kosa la kukosa ushauri, si mara ya kwanza kuchapia na kujibu vioja. Ni kwa nini hajawafukuza kazi mpaka leo? Kwa hiyo hii ni makususdi.Ukizingatia wote tuna uzoefu na majibu wanayotoa wakiulizwa, Na jinsi wanavyokimbilia kuomba watetewe na maspika na kukingiwa kifua wasiwajibike. Ingekuwa ni kupoteza muda kusubiri wafute kauli au waombe radhi kwani hilo haliwezi kufanyika. Nadhani ni wazi kuwa dhana ya kuwajibika na utawala bora imetupiliwa kando na uongozi huu. kwa hiyo HAKUNA CHA KUSUBIRI
 
hivi ukimwambia mwanao mtu'akikupiga nawe mpige ni uchochezi!!!?

Ubaya upo sana maana wewe hauwezi waambia watoto wako eti mwenzako akikupiga na wewe mpige woote ni watoto wako. Hii ndio inaleta ubaguzi Kikwete ni Rais wa wote bila kuangalia itikadi ya vyama. Kikwete akiharibu madhara sio kwa ccm tu bali na kwa chadema na cuf n watanzania wote.
 
Naona unasahau pia kuwa Jakaya ni Mwenyekiti wa CCM na vikao vyake vote vikubwa...

Pia umesahau kuwa wakati akitamka yale matamshi tatanishi alikuwa amevaa cheo hicho cya Uenyekiti wa CCM...

Hivyo maneno yake yalikuwa ni amri kwa wafuasi wa CCM pekee lakini sio Watanzania kama unavyodhani...
Una maana Kikwete akiwa anaongoza vikao vya CCM Tanzania inakuwa haina rais?

Lakini hata kama ilikuwa amri kwa wanaCCM tu je yalikuwa maneno ya busara?
 
kibamba_9c593.jpg


Wenye kuhusika wamshuhulikie Deus Kibamba kama walivyokwisha washuhulikiwa watu wenye mawazo kama yake.Hongera Rais kikwete kwa kutowa Muongozo vijana wako wa CCM tayari wamesha jipanga kikamilifu kukabiliana na lolote lile liwalo naliwe na wanakuhakikisha wataifanya kazi kwa ustadi kabisa Hongera Rais.
 
Invisible, imezuka tabia ya watu kutumia vikabila vyao humu.Huyu hapa jana tu kuna post kaandika kwa lugha ya ajabu,isiyo kiswahili wala kiingereza ambazo ndizo lugha rasmi humu.

Sisi wengine tusioelewa hiki kikabila tutajuaje hapa kama sheria za jf zimekiukwa?Mods je mnaelewa hiki kikabila na kuna mod wa kumoderate kila kikabila humu?Kama sivyo hamuoni hapa kama mnanyimwa haki ya kuchapa kazi yenu kama inavyopaswa kulinda heshima ya forum hii?

Kama sheria zipo kimya kuhusu matumizi sahihi ya lugha humu hamuoni kama mnaacha mwanya wa watu kupanga mipango hata ile haramu kama kuipindua nchi kwa kuruhusu mawasiliano ambayo ni wenyewe tu wanaelewana?

Tafadhali fanyeni kitu ili tabia hii ya wagoloko kutumia vitindiga vyao ikome humu.

Ndio matatizo ya Unafiki, mbona MMU kina Baba V et all. wanatumia lugha za kikabila na hujawah kulalamika?, kwani humu zinaruhusiwa lugha ngapi? hivi we li Afrika lini utakua na akili? unafiki tu.
 
Last edited by a moderator:
Una maana Kikwete akiwa anaongoza vikao vya CCM Tanzania inakuwa haina rais?

Sijasema kuwa Tanzania inakuwa haina Rais hayo ni yako...isipokuwa nimemaanisha kuwa maamuzi yoyote ayafanyayo kama Mwenyekiti wa CCM ni kwa ajili ya CCM na sio serikali ya Tanzania au Watanzania.

Lakini hata kama ilikuwa amri kwa wanaCCM tu je yalikuwa maneno ya busara?

Ungelikuwa umesoma posts zangu zilizopita huko mwanzoni, ungeliona kuna mahali nimeandika kuwa hayakuwa matamshi ya busara wala hekima.

Kimsingi ni bora kama alitaka kuyatamka hayo, angewaachia kina Nape wayatamke kwa niaba...
 
Basi vema Rais wa nchi asiwe mwenyekiti wa chama chochote cha siasa ili kuondoa mianya ya miingiliano ya mambo ya chama na serikali.

Ni kweli mkuu ndio haya mambo ambayo Watanzania wengi walikuwa wanayapigia kelele, Rais anahodhi mamlaka kubwa sana.
 
Jamii gani ambayo inamwona Kibamba ni kituko? Ni vema kuwa na akili huru, maana hata katika kauli kama hii inayotolewa na kiongozi mkuu wa nchi na ambaye ndiye mwenye mamlaka ya ulinzi na usalama wa nchi lakini anatoa kauli kama hii unadhani implication ya kauli kama hiyo itakuwa ni nini? Usisahau kauli ya Pinda ya "piga tu", mpaka hapo huoni kuwa Tanzania ni kama haina kiongozi? Nashangaa kama kuna mtu anayeifurahia kauli ya aina hii. Wote wanaotambua kuwa kazi ya kichwa sio kufuga nywele tu hata kama wana rangi ya green hawawezi kushangilia kauli kama hii ya mtu aliyechoka kabisa! Kauli hii ina tafakuri kubwa sana na hapa kila mwenye critical mind anajua nchi yetu ina viongozi ambao wamefikia bar ya mwisho katika kufikiri. Naomba 2015 ifike haraka.
 
Kibamba hapa amekurupuka. Huwezi kukimbilia kwenye jumuiya ya kimataifa kabla hata hujatafuta suluhu ya ndani ikiwa ni pamoja na kutaka ufafanuzi wa kauli au kumtaka aliyetoa kauli aifute. Sasa kila jambo tukikimbilia kwenye jumuiya kimataifa bila kujiridhisha kwamba ni juu ya uwezo wetu si watatuona walalamikaji na kutuchoka mapema? Tanzania hatujafikia mahali pa kuhitaji msaada wa kimataifa kwa matatizo yetu ya ndani.

Alex Manonga,

Kibamba hajakurupuka. Wewe ndiye uliyekurupuka kuja na hoja dhaifu ya kutaka kutetea upuuzi wa J.Kiwete!
kwa akili yako ulitaka suluhu gani ya ndani ati ya kutaka Kiwete afafanue kauli yake??? Tunajua viongozi wa Chama Twawala wamejaa kibri ya madaraka!

Kauli ya Rais Kiwete ya kuwahimiza wafuasi wake wa CCM ikiwemo vyombo vya dola(Polisi,UWT,FFU,JWTZ)kuwa UNYONGE BASI haihitaji ufafanuzi wowote! Pengine ni kwa mtu mjinga na punguani ndo anaweza asielewe kauli hii! Tumesikia Rais Kiwete amesema CCM wamechoka kuona wafuasi na wanachama wao wakimwagiwa Tindikali kule IGUNGA na sijui kutobolewa macho kwa bisibisi kule Kahama!!!Kwa maana nyingine Chaguzi zinazofuata ni mapambano kati ya CCM na CHADEMA!

Kitu kinachoudhi sana kuhusu kauli hii ya mkulu wa kaya yetu ni kwanini hakuzungumzia kuhusu wanachama na wafuasi wa vyama vungine hasa CHADEMA ambao WAMEUAWA kwenye maeneo hayo aliyoyataja na mengine ambayo hakuyataja. Kama kweli Kiwete ni mnyoofu na mwaminifu kama alivyoapa kuilinda na kuitetea KATIBA YA JMT alitakiwa pia zungumzie matukio yafuatayo:

  • Kule Igunga kuna kada wa CHADEMA aliuawa kwa kunyongwa na kuchomwa moto.
  • Kule Arumeru Mashariki Kiongozi wa CHADEMA aliuawa kwa kuchinjwa kwa msumeno wa Chain-saw!
  • Kule Iringa Nyololo wakti wa mkutano wa ndani wa CHADEMA mwandishi wa Habari wa Ch10 ndugu Daudi Mwangosi aliuawa kwa BOMU la Polisi!
  • Kule Morogoro mwuuza magazeti aliyekuwa kwenye shughuli zake kando ya barabara halipigwa risasi(kitu kizito cha Polisi)wakti wa maandamano ya CHADEMA.
  • Kule Arusha tarehe 5/Januari/2011 walikufa watu 3 kwa kupiga risasi na Polisi kwenye maandamano ya CHADEMA kupinga Uchaguzi wa meya Jiji la Arusha.
  • Tarehe 15/june/2013 kulekule Arusha-Soweto kwenye Mkutano wa kufunga kampeni za Udiwani katika Jiji la Arusha waliuawa watu 4 akiwemo kiongozi wa CHADEMA kwa kupigwa Bomu la kutupwa na mkono na Polisi.Lengo hasa ilikuwa kuwaua viongozi waandamizi wa CHADEMA akiwemo Mhe. Freeman Mbowe!

Sasa Kiwete anapokuja na hoja dhaifu kwa lugha ya uchochezi ya kuwataka wana-CCM kuacha unyonge kwa maana ya kuwataka kujibu mapigo kwa wapinzani sijui anategemea nini hasa????Jibu bila shaka ni hili la kumpeleka kwa Bensouda wa ICC, full stop.

Lazima Kiwete atakapomaliza muda wake au hata kama ataendelea baada ya mizengwe ya Bunge la Katiba Mpya basi kwa kuongoza muda wake hakuna namna isipokuwa kumpeleka Hague The akaungane na Uhuru Kenyatta kule,there is no way!!!
 
Back
Top Bottom