Thread kama hizi zinakufanya urealize how blessed you are. Nakushukuru Mungu kwa neema na zawadi hii kubwa, hadi Leo hii na uzee wangu, bado nipo na mama (na baba), and I'm her best friend. Mungu Uendelee kunitunzia shoga angu yule, hakuna cha kumfanyia ambacho kitafikia upendo na sacrifices zake. Thanks momma HS
Happy birthday mama Bavaria!
Hayahesabiki wala siwezi kuyahesabu, kitendo cha kuitunza mimba yangu, kunileta duniani na kunilea katika shida na kunifikisha pale aliponifikisha yatosha kusema ahsante mama.
Your the one and no one to compare, nakumiss kila iitwapo leo. Mungu azidi kukupa pumziko la amani....... RIP mama ram!
Daa ni kweli ndugu upendo na mapenzi ya mama hayana mfano. Mungu awabariki wamama wote popote walipo duniani na sisi watoto tuwapende, tuwaheshimu na kuwatunza maana hakuna kama mamaRip my mom...huwa natamani ata siku zirudi nyuma
Mungu akulinde uko ulipo..mlio na mama wapendeni sana mana ipo siku utatamani umwone lkn ndo itakua ngumu
Kuvumilia kuniweka tumboni miezi tisa na kunizaa kwa uchungu,kamwe hakuna kiumbe mwingine duniani ashawahi kunionyesha upendo wa namna hiyo.Leo ni siku ya kuzaliwa mama Bavaria.
Huwa nakumbuka mengi kuhusu mama, vimbwanga vyote nilivyofanya nikiwa mdogo.
Ni moja kati ya wanawake 'strong' sijawahi ona. Pamoja na kubanwa na majukumu yote aliyokuwa nayo, ila hakukosa kuihudumia ipasavyo.
Moja kati ya vitu sitasahau, nilikuwa shule ya msingi. Tulikuwa na safari ya shule kwenda makumbusho ya taifa jmosi moja hivi. Kwa jinsi mzee alivyokuwa mkali, sikutaka kumuomba. Nikamtuma mama akaniombee. Mzee akazingua.
Basi asubuhi nimeshajiandaa nikijua lazima bimkubwa amerekebisha mambo. Kumbe la. Wakati najiandaa nikamuuliza bimkubwa akasema mshua amezingua. Nilikuwa dissapointed sana. Ila nikasema lazima niende hata iweje.
Kumbe bi mkubwa alienda kwenye kibubu chake akachukua 5000 anipe. Akaiweka mezani. Nilivyomaliza kujiandaa nikasepa zangu bila hata kuangalia pembeni, nikijua mzee hajaacha mpunga.
Maza alikuwa anachambua maharagwe abandike jikoni. Alivyomaliza akaiweka sufuria mezani juu ya ile hela bila kujua. Baada ya kuwasha mkaa akaweka maharage jikoni akasepa. Hakujua kama ile hela iligandamana na ile sufuria. Ikaungua.
Jioni narudi, maza akaanza kuulizia chenji. Nikamwambia hakunipa hela ila yeye akasisitiza ameiweka mezani. Nikamwambia sikuiona. Akagundua kumbe ilikuwa imegandamana kwenye sufuria, ikaungua.
Niliumia sana siku ile, nililia kwa uchungu mno. Sijui kilichoniliza ila hadi leo nakumbuka kile kitendo.
Huwa nikimwangalia moyoni najisemea i love you mama.
Thats my wish too, tuombe uzima tu.Ameen!!asante sana!
Nimekulia na mama mlezi for 24yrs!!wanangu sitakubali walelewe na mtu yoyot labda nife mapema!
Nataka wapate Yale ambayo Mimi sikuyapata kwa mama angu!!