Kiroja cha Ngerengere

Leo tunatambiana Mkuu wa Majeshi kaonekana Ngerengere, tunapigana vijembe vya udaku wa afya yake na tetesi za yeye "kutoweka".

Hatulizungumzii hata kidogo tukio lenyewe kubwa pale Ngerengere.

Hatujiulizi Tanzania tumekosa fedha za kujenga na kuboresha kikosi chetu cha anga mpaka tuende Uchina kuomba msaada na kufadhiliwa?

Yaani hatuna dola za kimarekani Milioni mia moja popote? ni heri hata masalia ya Escrow na EPA yangetumika hapo Ngerengere au pale Kigamboni kuliko kuonyesha utegemezi wa hali ya juu kwa China.

Wanatukopesha kujenga Bandari, mitambo ya gesi, reli, barabara, kujenga majengo, matumizi ya serikali, zana za kijeshi na sasa kambi nzima ya jeshi?

Tutalipaje hili deni? Tutalipaje hizi fadhila?

Mkuu,

1. China ni strategic partner tangu uhuru. Ni rafiki wa kweli. Wametusaidia katika sekta mbalimbali za kijamii, kiuchumi, kielimu, kijeshi nk
2. Bado wanaendelea kutusaidia kujiimarisha kijeshi-kuna ubaya gani ? Au unataka tuwe shamba la bibi ? Angalia nchi zilizotuzunguka zinavyofanya halafu nadhani utapata jibu.
3. Usitafsiri kila kitu katika muktadha wa uchaguzi wa kesho ! Baada ya uchaguzi Tanzania itaendelea kuwepo. Kila serikali inahitaji jeshi imara ili iweze kulinda mipaka yake. Tanzania will prevail for our chidren and grandchildren !
4. Siku chache zijazo Wachina wataanza kujenga kiwanda cha nyukilia nchini Uingereza kwa ajili ya kuzalisha umeme. Hii ni dalili nyingine kuwa China hivi sasa inatambulika siyo tu kwa sababu ya uwezo wake kiuchumi lakini pia kiteknolojia.
5. Ama kweli ahsante ya Punda ni teke ! Waombe radhi Wachina na ukumbuke kuwa wao siku hizi hawana kiherehere na siasa za ndani. Wao ni kazi tuu !
 
Mlizusha ya CDF Sasa mmeumbuka hamtaki watu wahoji hiyo tabia ya kutunga na kusambaza tuhuma ili kujipatia mtaji wa kisiasa ... Aibu zenu..... Njia ya mwongo ni fupi sana ......

Walisemaje Kuhusu CDF? Nakumbuka yule kijana alidai "CDF Kala chakula chenye sumu na akakimbizwa hospitali kwa matibabu". Tunajuaje kama "kurudi" kwake "hajatokea hospitali matibabuni?". Kwani alisema ameaga dunia? Ikumbukwe kuwa taarifa rasmi ilidai kaenda ziara ya siku 9 Lakini ameonekana baada ya mwezi (almost).
 
Yaani uwanja wa jeshi mnaipa jeshi la nchi nyingine liwajengeee?
Kiukweli hii nchi Mungu pekee ndio anatushikiria na sio tofauti na hapo
 
Nashukuru Mkuu kwa kunifumbua macho nikuulize swali lingine.

Je kwa Maliasili tulizonazo ambazo zingine hazipatikani sehemu nyingine Duniani isipokua Nchini kwetu tumeshindwa kua Taifa lisilotegemea Misaada na Mikopo?

Kwa nijuavyo mimi na nilivyojifunza Shuleni ni kua asilimia kubwa ya Mataifa ya Ulaya hasa yaliyokua na Makoloni Bara la Africa yaliendelea kiviwanda kutokana na Malighafi walizochuma toka kwetu.

Sisi tumeshindwa nini japo kua hata na Viwanda vya kati ili tuepu..

hata hivyo naamini miaka 100 toka sasa uwezo huo tutakua nao wa kutumia rasilimali zetu kufikia maendeleo....hata marekani wamechukua miaka 350 kufika hapo walipo
 
Yaani uwanja wa jeshi mnaipa jeshi la nchi nyingine liwajengeee?
Kiukweli hii nchi Mungu pekee ndio anatushikiria na sio tofauti na hapo

hatuna technplogy ya kifanya hayo,,,hiyo ni military base,,huwezi kuipa kampuni ya MECCO CONSTRUCTION au NYANZA ROAD wajenge,,kuna vifaa vya kijeshi vitawekwa mfano rada,,,,sasa hapa wapi tunatengeza military rada?
 
Shida mikopo ya awamu hii inayoongozwa na Jakaya Kikwete,imekuwa ina lazimisha kukopa hata mikopo isiyo na tija wakati yeye amegawana na baadhi wanafamilia yake pesa za Escrow na kila siku anakunywa nao chai Ikulu.
 
Walisemaje Kuhusu CDF? Nakumbuka yule kijana alidai "CDF Kala chakula chenye sumu na akakimbizwa hospitali kwa matibabu". Tunajuaje kama "kurudi" kwake "hajatokea hospitali matibabuni?". Kwani alisema ameaga dunia? Ikumbukwe kuwa taarifa rasmi ilidai kaenda ziara ya siku 9 Lakini ameonekana baada ya mwezi (almost).

so what is your point here?,,,yeah tu assume alipata food poisoning,,,si keshapona,,nini kinakukereketa labda,,,eeh?...

unataka tukusaidiaje hasa?
 
marekani amekoloniwa na china kama hujui,,,,china inaidai marekani pesa ndefu sana,,,pia wanahold bond za marekani wakiziachilia uchumi wa marekani utaadhirika vibaya

Kwahiyo kwa ajili marekani wanadaiwa na china basi hata sisi ni ruksa kudaiwa?
 
Educated Tanzanian are not only found OVERSEAS bro!!! we are here in Tanzania supporting UKAWA to take the power,you stay where you are with your fellow dreaming for god to do every thing for you.
Rev unafahamu wachina ndio waliwafunza wanajeshi wetu wa anga na zile ndege za mwanzo zilitoka kwao, huo ulikuwa ule mlolongo wa mikataba kama vile ya kiwanda cha Urafiki etc. Wao ndio walijenga Ngerengere kama kambi ya anga. sifahamu details za mikataba yao, pia ukumbuke ndio waliweza kutupa uwezo wa kujenga reli ya uhuru. Huyu Jambazi sugu mwenye kuleta mvua kutoka malasyia sijui atafanya nini zaidi ya wizi wa kukata na shoka.We need to manage our resources and make our choices strategically in order to safe guard the inheritance for our children.

Kuhusu tutalipaje huo ni ujinga wa JK et al, yeye ndiye chimbuko la kuendeleza ule mlolongo wa marais wasioweza kuongoza kama vile Mwinyi. I urge Tanzanians who are educated to go back home and claim their right to see Tanzanians are lead to prosperity, not these thieves from Chadema and Ukawa.
 
Tunataka vichwa vya kututoa kwenye ukoloni mamboleo. Na dawa ni elimu tu. Mali asili tunazo.
.
 
Nashukuru Mkuu kwa kunifumbua macho nikuulize swali lingine.

Je kwa Maliasili tulizonazo ambazo zingine hazipatikani sehemu nyingine Duniani isipokua Nchini kwetu tumeshindwa kua Taifa lisilotegemea Misaada na Mikopo?

Kwa nijuavyo mimi na nilivyojifunza Shuleni ni kua asilimia kubwa ya Mataifa ya Ulaya hasa yaliyokua na Makoloni Bara la Africa yaliendelea kiviwanda kutokana na Malighafi walizochuma toka kwetu.

Sisi tumeshindwa nini japo kua hata na Viwanda vya kati ili tuepuh






hakuna nchi yenye rasilimali duniani kama russia,,lakini kama unakosa capital na technology huwezi utilize rasilimali zakO.




katika link mojawapo hapo juu,umeona uingereza wanajengewa kinu cha nyuklia na mchina,,,,wao waingereza wana technology lakini pesa za kuufanya mradi hawana ndo maana wakampa mchina ajenge...



sasa tuseme uingereza nao hawana rasilimali?,kama uingereza anakosa pesa ya kufund mradi na mpaka anaipa china project,,itakua Tanzania?..
 
Rev. acha uoga bana... Wachini ni ndugu wa damu na ccm .... wanasaidia kuwaua Tembo wa haribifu ... Unlike Wazungu wenye kujichukulia Dhahabu, Uranium, Almasi, Gas na Nickel Bure ... Wachina wako hapa kufanyakazi za Vibarua pia ...
 
Tanganyika not yet uhuru. Huyu mchina anaonekana kuwa mtamu sana. Mbona kila mradi mkubwa anapewa yeye? Uwanja wa taifa, uwanja wa ndege, bandari ya bagamoyo, miradi yote ya gesi, zana za kijeshi, na mingine itakayosainiwa kabla ya tarehe 26 october. Ni nini kilichojificha nyuma ya miradi hii tena kwa wachina tu? Au wamefadhili uchaguzi ili waweze kurudisha mitaji na faida zao? Ama kweli goli la mkono haliepukiki ili kuilinda hii mijitu iliyoiuza Tanganyika yetu.
 
Bado hujafunua na kugundua hiyo ni mikataba binafsi ya mtawala ila tumetwisha zigo
 
Back
Top Bottom