Kipindi cha Njiapanda cha Clouds fm, lengo kuu ni nini?

Michewen

JF-Expert Member
Jun 27, 2012
24,641
32,417
Hiki kipindi hurushwa kila Jumapili kuanzia saa 8 mchana. Nimekuwa nikikisikiliza kwa muda sasa, lakini sijatambua lengo kuu hasa la hiki kipindi ni nini. Maana nionavyo ni kama mtangazaji " anawachora" wale wageni wanaoeleza matatizo mule, na "wageni" wanavyojiachia na matatizo yao utafikiri kuna la maana atakalopata humo zaidi ya kupewa pole na watuma sms/ wasikilizaji.

Wajameni, Watanzania tupunguze malalamiko redioni, huu umaskini tulionao haumalizwi kwa kuhojiwa redioni. Tunapaswa kufanya kazi kwa bidii na pia kuwa na nidhamu na matumizi.

Ni hayo tu kwa leo.
 
Binafsi sioni kama ni kibaya sana japo hakiwasaidii waathirika au wenye majanga of such
my take;
iwe cente ya kusaidia watu wenye uhitaji maarumu let us say anaye ingia hapo asaidiwe na watu wanao donate
bado tunahtaji kujua matatizo kwani kuna watu wnapata matumaini mapya ecourages nk
umma utambue matatizo si0wote wanajua kuwa kuna watu hawana hata mlo mmoja
sorry for typos
 
watanzania tumechoka kusikiliza matatizo ya watu maana binafsi tunayo ya kutosha, zaidi hata hao wanaoenda pale redioni hakuna la maana wanalosaidiwa zaidi ya kuanikwa tu. Tujifunze kupambana na matatizo yetu badala ya kusubiri " WASAMARIA" wa redioni
 
Tumezoeshwa vibaya na viongozi wetu kuomba omba misaada,kwa hiyo hata sishangai.:llama:
 
Hilo hitimisho lako ndilo sahihi kupita maelezo ila mengine yote ni kupingana na masilahi ya hicho chombo kumbuka kuwa ile ni sehemu ya biashara
 
Nipo tofauti kidgo nawe.
Katika story ya mtu,.kuna maonyo na mafunzo.mengi ambayo jamiii huweza kuipata,.pia kwa mtoa story huweza jikuta amesogea katika mikono itayoweza kumsaidia.
Kuna ambao huchangaiwa pale n.k
 
hizi redio za FM zimeleta/ajiri watu wasio na taaluma ya uandishi wa habari kwa hiyo wanajifanyia wanavyojua mambo mengine ukisikiliza hizo redio unasikia mpaka moyo unataka kupasuka
 
Binafsi sioni kama ni kibaya sana japo hakiwasaidii waathirika au wenye majanga of such
my take;
iwe cente ya kusaidia watu wenye uhitaji maarumu let us say anaye ingia hapo asaidiwe na watu wanao donate
bado tunahtaji kujua matatizo kwani kuna watu wnapata matumaini mapya ecourages nk
umma utambue matatizo si0wote wanajua kuwa kuna watu hawana hata mlo mmoja
sorry for typos
Siamini kama wewe ni msikilzaji wa dhati wa kipindi hiki kama kweli wewe ni msikilizaji wa dhati basi jitahidi kuwa mkweli. Hiki kipindi kimesaidia sana watu wengi sana waliokuwa na matatizo makubwa lakini hilo hutaki kuliona ,watanzania tunatabia mbaya sana ya kupenda kukatisha tamaa watu wachache waojitahidi kuleta mchango fulani katika jamii,wewe at your level umefanya nini kusaidia jamii hii ya kitanzania ,njia panda kimekua voted ndio kipindi bora kabisa cha kijamii hapa TZ,tujivunze kuapriciate yale yanayofanywa na wengine.
 
we unakisikilizaga vizuri kweli mana kuna wengine mpaka uwanja wa kujenga wamepatia pale ile kusikika hewani tu. kuna watu wana toa misada yao pale wew endelea kua na miroho hiyo tu ya kushanga but kile kipindi kina saidia wenye majanga tena. sugu tu. unashanga redioni tu ata jf uku mbona kuna watu wamelia shida zao nakupata misada tu watu wanaguswa sana zaidi sikiliza kwamoyo mzuri sio usikilize kwa kujifurahisha. duniani uku kuna mateso jamani oho. vikombe ivo viwaepukeni tu mana safari ya maisha maishani ni mzitoo sana. acheni tu..
 
wewe naona huwa husikilizi na kufuatilia bali unafuatilia pasipo kusikiliza....

watu wengi wanasaidiwa hadi wale wanaosaidia wanapiga simu redion katika kipindi na mhusika anatoa shukrani zake za dhati na wengine wengi tuu wanapata misaada.

watanzania wengi tu masikini kwasababu ya ubinafsi umekithiri hata kwenye vitu visivyohitaji ubinafsi wenyewe wanafanya tyy ubinafsi.

NB. mleta hoja nimekuelewa unataka uhakika ili umpeleke mtu wako akatangaze shida pale..wewe mpeleke tuu vigezo na masharti huzingatiwa.
 
Siamini kama wewe ni msikilzaji wa dhati wa kipindi hiki kama kweli wewe ni msikilizaji wa dhati basi jitahidi kuwa mkweli. Hiki kipindi kimesaidia sana watu wengi sana waliokuwa na matatizo makubwa lakini hilo hutaki kuliona ,watanzania tunatabia mbaya sana ya kupenda kukatisha tamaa watu wachache waojitahidi kuleta mchango fulani katika jamii,wewe at your level umefanya nini kusaidia jamii hii ya kitanzania ,njia panda kimekua voted ndio kipindi bora kabisa cha kijamii hapa TZ,tujivunze kuapriciate yale yanayofanywa na wengine.

Keep up
 
Labda hamjanielewa swali langu? lengo kuu la kile kipindi ni ipi hasaaa? kulia lia tu? je wangapi wamesaidia kwa KUBWABWAJA matatizo redioni? suala hapa ni kubadilisha mindset tu kuwa suluhisho la matatizo yako ni wewe mwenyewe na si kwenda kulia kule Redioni. Kama unapata nauli ya kwenda CLOUDS ( Mikocheni), na assume utakuwa umevaa nguo nadhifu unakosaje mtaji wa Tsh. 10,000 kununua machungwa/mihogo ukauza? WATANZANIA tuache kulia shida kila kukicha wakati mtu una uwezo wa kutengeneza pesa
 
Back
Top Bottom