Az 89
JF-Expert Member
- Nov 20, 2011
- 1,658
- 691
Mh. Rais kikwete katika kampeni zake za mwaka 2005 alikuja na slogan au falsafa ya "MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA" Ikibebwa Ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya!!!, kwa lugha hii alioitumia alikamata hadi viongozi wa dini, na watu wa nyanja zote!!! Kwa masikini ambao kwao Neno"MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA" Lilibeba sanduku la matumaini mapya, kujichomoa kwenye jalala la umasikini na kujiweka angalau katika uwezo wa kumpa maji mtu mwingine anaejiskia na kiu! KILICHOTOKEA ni tofauti na walivyotegemea...lindi la umaskini, rushwa, ufisadi viliongezeka! UCHAGUZI WA 2010 alikuja na "ARI ZAIDI, KASI ZAIDI NA NGUVU ZAIDI", Lugha hii pia iliwahadaa watu japo wengi walizinduka ilibaki kwa watu wa vijijini ambao walitoa nafasi kwa mara nyingine japo sina uhakika sana Kama alishinda tena au lah! kwa sababu Mambo yaliyojadiliwa kwenye WHITE PAPER HAYAJATIMIZWA....! Kwa sasa kila kitu kimebadilika! Watu wamechoka wameshajua kuwa "MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA" ILIKUWA ZUBAISHA *****.. ILIKUWA LUGHA YA UONGO! Kuweni makini 2015.