Abdalah Abdulrahman
JF-Expert Member
- Aug 29, 2019
- 222
- 201
Nidhamu ndio msingi wa maendeleo ya kila kitu duniani, ukitaka kuwa tajiri ni lazima uwe na nidhamu ya fedha, ukitaka kuishi vema kwenye ndoa yako ni lazima uwe na nidhamu katika mahusiano yako, ukitaka kuwa na chama chenye ushawishi mkubwa na chenye uwezo wa kukamata dola ni lazima viongozi na wafuasi wa chama wawe na nidhamu. Ukosefu wa nidhamu kwa viongozi na wafuasi wa vyama vya upinzani umepoteza matumaini kwa wapiga kura na watanzania wa rika zote kwa jumla.
Vyama vya upinzani Tanzania vilianza kwa matumaini makubwa ya kushika dola,rejea matokeo ya mwaka 1995 ambapo Marehemu Lyatonga Mrema alipata ushindi wa asilimia 27.9% dhidi ya mpinzani wake marehemu Rais mstaafu Benjamin Mkapa ambae alipata ushindi wa asilimia 61.8%. Kutokana na kaida ya siasa, ushawishi mara nyingi hukua kwa chama pinzani na hupungua kwa chama tawala hasa kwenye jamii ambayo imekua na chama kimoja kwa muda mrefu,na jamii ambayo idadi kubwa ya watu ni vijana. Jambo la kushangaza ni kuwa ushawishi kwa vyama pinzani nchini unapungua kila kukicha kutokana na sababu nyingi. Sababu hizo ni pamoja na nidhamu, uchu wa madaraka kwa viongozi wa vyama vya upinzani, kukosa ajenda, kukosa umoja, kukosekana kwa demokrasia ndani ya vyama vya upinzani, na kuwa na sera kinzani na maadili ya Watanzania. Katika makala hii, nitaeleza kwa kina juu ya sabababu moja ya ukosefu wa nidhamu kwa vyama vya upinzani na athari zake.
Vyama vya upinzani vinajukumu kubwa la kukosoa serikali na kushauri serikali kwa kuonesha sera mbadala juu ya uendeshaji wa nchi. Jambo hili lapaswa kufanywa kwa nidhamu na ueledi mkubwa. Yapo mambo mengi mazuri ambayo vyama vya upinzani vimefanya na hivyo kujenga imani kwa baadhi ya wananchi. Baadhi ya mambo hayo ni kama vile kuibua ufisadi katika nyanja mbalimbali, kuhamasisha chama tawala kufanya kazi zake sawa sawa nakadhalika.
Juhudi hizi zimekua zikikwamishwa na ukosefu wa nidhamu ndani ya vyama hivi, miongoni mwa matukio ya kuonesha ukosefu wa nidhamu katika vyama vya upinzani ni pamoja na wabunge wa upinzani kutukana hadharani, wafuasi kuwatukana na kutumia lugha chafu katika mitandao, ugomvi kati ya vyama vya upinzani na uwepo wa makundi ndani ya vyama hivi.
“Siwalaumu wanachama wa CHADEMA, viongozi wao ndio wenye fujo na mimi, sasa najiuliza tatizo ni nini ,uzee wangu? kama ndio hivyo wawaachie wananchi, kama kuumwa mbona tangu 1984 naugua kisukari, kwa nini wananitendea haya?”
Kampeni hizi chafu na za fujo na lugha chafu pia zilitokea huko ndanda ambapo mbunge wa Ndanda Chadema ndugu Cecil Mwambe aliamua kujiondoa katika chama hicho. Na hapa ninanukuu alichokisema.
“Niliitwa majina yote mabayo mnayoyajua, lakini nilivumilia nikiwa najua na matusi yote yaliyotukanwa, mbaya zaidi mimi ni mwenyekiti wa Chama, vipi kwa mwanachama wa kawaida?”
Kwa ujumla kampeni za fujo, kuharibu mali za wananchi na kupora ni sehemu ya mkakati wa vyama vya upinzani. Baadhi ya njama hizi huratibiwa na viongozi wa ndani ya chama katika ngazi mbalimbali.
Madhara ya matusi, lugha chafu na fujo kwa vyama vya upinzani ni pamoja na kupoteza watu mahiri na wastaarabu ndani ya vyama vya upinzani wenye nyazifa kubwa ndani ya vyama vya upinzani na wabunge, kuondoa imani kwenye vyombo vya ulinzi, kupoteza kundi kubwa la wafuasi wastaarabu, kupoteza kundi kubwa la wapiga kura.
Hivi sasa vyama vya upinzani vinaokoteza vijana ambao ukitizama katika matamshi yao, ni vijana wasio na uzalendo na wanaotaka kuidumbukiza nchi katika matatizo.
Kupoteza Watu Makini.
Katika awamu ya tano viongozi wengi wa vyama vya upinzani ambao walikua nguzo katika vyama hivyo waliamua kuhamia chama tawala kutokana na sera nzuri za chama na utekelezaji wa sera zake. Viongozi hawa kwa uzalendo wao waliamua kuunga juhudi za Chama cha Mapinduzi ili kuwahudumia wananchi. Kutokana na sera nzuri za CCM viongozi hawa hawakubaguliwa na walikaribishwa na kupewa nafasi mbalimbali ili wawahudumie wananchi. Ni katika kipindi hki zaidi ya wabunge na madiwani wapatao 150 walijiuzulu nafasi zao na kuhamia CCM ili kuchangia katika maendeleo ya nchi. Viongozi haw ani pamoja na aliyekua mgombea wa nafasi ya Urais Mh. Edward Lowasa, David Silinde, Mwita Waitara, Julias Kalanga Laizer, Maulid Mtulia, Dr Mashinji ambae alikua katibu mkuu wa Chadema, na wengine wengi.
CCM INA UHAKIKA WA KUTAWALA AWAMU 5 MBELE
Vyama vya upinzani Tanzania vilianza kwa matumaini makubwa ya kushika dola,rejea matokeo ya mwaka 1995 ambapo Marehemu Lyatonga Mrema alipata ushindi wa asilimia 27.9% dhidi ya mpinzani wake marehemu Rais mstaafu Benjamin Mkapa ambae alipata ushindi wa asilimia 61.8%. Kutokana na kaida ya siasa, ushawishi mara nyingi hukua kwa chama pinzani na hupungua kwa chama tawala hasa kwenye jamii ambayo imekua na chama kimoja kwa muda mrefu,na jamii ambayo idadi kubwa ya watu ni vijana. Jambo la kushangaza ni kuwa ushawishi kwa vyama pinzani nchini unapungua kila kukicha kutokana na sababu nyingi. Sababu hizo ni pamoja na nidhamu, uchu wa madaraka kwa viongozi wa vyama vya upinzani, kukosa ajenda, kukosa umoja, kukosekana kwa demokrasia ndani ya vyama vya upinzani, na kuwa na sera kinzani na maadili ya Watanzania. Katika makala hii, nitaeleza kwa kina juu ya sabababu moja ya ukosefu wa nidhamu kwa vyama vya upinzani na athari zake.
Vyama vya upinzani vinajukumu kubwa la kukosoa serikali na kushauri serikali kwa kuonesha sera mbadala juu ya uendeshaji wa nchi. Jambo hili lapaswa kufanywa kwa nidhamu na ueledi mkubwa. Yapo mambo mengi mazuri ambayo vyama vya upinzani vimefanya na hivyo kujenga imani kwa baadhi ya wananchi. Baadhi ya mambo hayo ni kama vile kuibua ufisadi katika nyanja mbalimbali, kuhamasisha chama tawala kufanya kazi zake sawa sawa nakadhalika.
Juhudi hizi zimekua zikikwamishwa na ukosefu wa nidhamu ndani ya vyama hivi, miongoni mwa matukio ya kuonesha ukosefu wa nidhamu katika vyama vya upinzani ni pamoja na wabunge wa upinzani kutukana hadharani, wafuasi kuwatukana na kutumia lugha chafu katika mitandao, ugomvi kati ya vyama vya upinzani na uwepo wa makundi ndani ya vyama hivi.
- Wabunge wa Upinzani kutukana hadharani.
- Wafuasi wa Upinzani kutoa lugha chafu
- Kampeni chafu
“Siwalaumu wanachama wa CHADEMA, viongozi wao ndio wenye fujo na mimi, sasa najiuliza tatizo ni nini ,uzee wangu? kama ndio hivyo wawaachie wananchi, kama kuumwa mbona tangu 1984 naugua kisukari, kwa nini wananitendea haya?”
Kampeni hizi chafu na za fujo na lugha chafu pia zilitokea huko ndanda ambapo mbunge wa Ndanda Chadema ndugu Cecil Mwambe aliamua kujiondoa katika chama hicho. Na hapa ninanukuu alichokisema.
“Niliitwa majina yote mabayo mnayoyajua, lakini nilivumilia nikiwa najua na matusi yote yaliyotukanwa, mbaya zaidi mimi ni mwenyekiti wa Chama, vipi kwa mwanachama wa kawaida?”
Kwa ujumla kampeni za fujo, kuharibu mali za wananchi na kupora ni sehemu ya mkakati wa vyama vya upinzani. Baadhi ya njama hizi huratibiwa na viongozi wa ndani ya chama katika ngazi mbalimbali.
- Kutoaminiana na kutohurumina na kuthaminiana.
Madhara ya matusi, lugha chafu na fujo kwa vyama vya upinzani ni pamoja na kupoteza watu mahiri na wastaarabu ndani ya vyama vya upinzani wenye nyazifa kubwa ndani ya vyama vya upinzani na wabunge, kuondoa imani kwenye vyombo vya ulinzi, kupoteza kundi kubwa la wafuasi wastaarabu, kupoteza kundi kubwa la wapiga kura.
Hivi sasa vyama vya upinzani vinaokoteza vijana ambao ukitizama katika matamshi yao, ni vijana wasio na uzalendo na wanaotaka kuidumbukiza nchi katika matatizo.
Kupoteza Watu Makini.
Katika awamu ya tano viongozi wengi wa vyama vya upinzani ambao walikua nguzo katika vyama hivyo waliamua kuhamia chama tawala kutokana na sera nzuri za chama na utekelezaji wa sera zake. Viongozi hawa kwa uzalendo wao waliamua kuunga juhudi za Chama cha Mapinduzi ili kuwahudumia wananchi. Kutokana na sera nzuri za CCM viongozi hawa hawakubaguliwa na walikaribishwa na kupewa nafasi mbalimbali ili wawahudumie wananchi. Ni katika kipindi hki zaidi ya wabunge na madiwani wapatao 150 walijiuzulu nafasi zao na kuhamia CCM ili kuchangia katika maendeleo ya nchi. Viongozi haw ani pamoja na aliyekua mgombea wa nafasi ya Urais Mh. Edward Lowasa, David Silinde, Mwita Waitara, Julias Kalanga Laizer, Maulid Mtulia, Dr Mashinji ambae alikua katibu mkuu wa Chadema, na wengine wengi.
CCM INA UHAKIKA WA KUTAWALA AWAMU 5 MBELE