Kila la heri watoto Darasa la Saba!

Mhache

JF-Expert Member
Jun 20, 2008
345
24
Leo wanafunzi wa darasa la saba wapatao zaidi ya milioni moja wanafanya mtihani wa kumaliza shule. Hii ni hatua muhimu sana kwao. Matokeo ya mtihani huo ndio utakaowapa wahitimu hao mwelekeo wa maisha. Kwani wapo watakaoendelea na masomo na wapo watakao rudi majumbani mwao bila chochote.

Mimi kama mdau wa elimu ninawatakia mtihani mwema na wenye mafanikio mema. Yapo mambo ambayo yasipoangaliwa yanaweza kuwaharibia matokeo yao. Mojawapo ni kufutiwa matokeo kutokana na kuonyeshwa nitihani na walimu wao au wasimamizi wa mitihani hiyo. Ninaomba walimu na wasimamizi wa mitihani hiyo wafuate sheria na taratibu wasije kuwaharibia watoto wetu matokeo yao. Na watakaobainika wachukuliwe hatua kali za kisheria.
 
I wish them the very best in their exams and the special stage in their lives.
May God give them strenght, confidence and lead them in a right direction.
I still remember myself how special that day was.
God bless all the African children.
 
Lakini mmemsikia alichosema Waziri Magembe? Watahiniwa ni kama 1m, nafasi za sekondari ni laki tano. Hivyo kuna hatari ya baadhi kukosa nafasi pamoja na kufaulu vizuri.
 
Leo huko Tanzania watoto wa darasa la saba katika skuli za msingi mbalimbali za Tanganyika wanafanya mitihani yao wa mwisho wa kumaliza elimu ya msingi.

nachukua nafasi hii kuwatakia kila la kheir na mafanikio mema,wafanye vizuri na hatimaye wafaulu na kuendelea na skuli za sekondari.

nawatakia kila la kheir darasa la saba katika mitihani yenu
 
May The Leading Light Shine On Them Through Critical Thinking and Exams!,

B.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom