Kiingereza cha Watanzania wengi ni cha kuandika, kusoma na kuongea kwa kusoma maandishi. Tatizo ni kusikiliza, kuelewana na kuongea freely

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,033
Kiingereza cha watanzania wengi kinawasaidia na kinaishia kwenye kuandika status, kuelewa kilichoandikwa kwa kiingereza mfano magazetini na pale kinapotumika kuongea kwa kufatiliza maneno ambayo yameshaandikwa kwa mpangilio kwamfano kutoa hotuba kwa kufatiliza speech iliyochapishwa kwenye karatasi.

Ukija kwenye kiingereza cha kuwasiliana, wengi kusikia maneno na kuyaelewa inakuwa shida, pia kwenye kuongea kwa uhuru mfano kujielezea inakuwa kazi sana tofauti na pale wanaposoma speech, hapa panakuwa na ze ze ze izi izi izi zati.

Nakumbuka hata mwalimu wa kiingereza wa sekondari alikuwa haelewi chochote kwenye nyimbo za marekani zilizojaa matusi, hii ilikuwa mpaka chuoni wengi walikuwa hawaelewi kinachoimbwa zaidi ya ku enjoy biti, flow, kucheza pamoja na kuiga mtindo wa maisha ya wasanii hao wakidhani kwamba kinachoimbwa kina uzito kumbe ni uharo mtupu.

Pia watanzania huwa tunakosea sana tunapoona mtu kasoma speech kwa kiingereza na kumpongeza tukidhani anajua, LA HASHA!! huku ni kupotoshana, wa kupongezwa inabidi awe muandaaji alietumia utashi wake na muda mwingi kupangilia hayo maneno, kuanzia grammer, prepositions, n.k. maana bila hivyo hata huyo ambaye anafatiliza maneno hataweza, tukiachana na kiingereza cha kufatiliza maneno hicho, wengi wakiambiwa waongee kwa uhuru wa kutunga swntensi zake kichwani kama anavyoongea kiswahili, hapo inageuka kuwa aibu.hata mzungu ambae nae kiswahili kinampiga chenga akiandikiwa hotuba anaweza kuonekana anajua kiswahili.

Kwa watu maarufu wanaojua kiingereza kwa hapa Tz naweza kusema ni kina Vanessa mdee, Wema Sepetu, P Funk, n.k. hawa kidogo hata shule na maisba waliyokulia walikuwa exposed na lugha ya kiingereza katika maisba yao.

Pia nawakumbusha kujua kiingereza si9 kipimo cha akili.
 
Kiingereza cha watanzania wengi ni kizuri sana wanapoandika status, wanaposoma magazetu ya the guardian na pale wanapoongea kwa kiingereza kwa kusoma speech ambayo mtu alitumia hata masaa mawili kuiandaa.

Ukija kweny kiingereza cha kuwasiliana, wengi kusikia maneno na kuyaelewa inakuwa shida, kwenye kuongea kwa uhuru mfano kujielezea inakuwa kazi sana tofauti na pale wanaposoma speech.

Nakumbuka hata mwalimu wa kiingereza wa sekondari alikuwa haelewi chochote kwenye nyimbo za marekani zilizojaa matusi, hii ilikuwa mpaka chuoni wengi walikuwa hawaelewi kinachoimbwa zaidi ya ku enjoy biti na flow.

Pia watanzania huwa tunakosea sana tunapoona mtu kasoma speech kwa kiingereza na kumpongeza anajua, nadhani wa kupongezwa inabidi awe muandaaji alietumia utashi wake na muda mwingi kupangilia hayo maneno, maana bila hivyo hata huyo ambaye anaisoma akiambiwa aongee kwa uhuru huwa inageuka kituko ni kheri aongee kiswahili.

Mwenda kulima na aliyekuwa Waziri wa nanihii bandiko hili hakuna linapowahusu kweli, kabla ya kuturukia wakina sisi?
 
Ila tunapiga mwingi kuliko inchi nyingine mfano Msumbiji na nchi nyingine kingereza hata cha kwenye simu shida lakini bongo hata ambao hawajasoma kivile ideas za yes no na chakuombea maji kipo
 
Kiingereza cha watanzania wengi kinawasaidia na kinaishia kwenye kuandika status, kuelewa wanachosoma magazeti ya the guardian na pale wanapoongea kwa kiingereza kwa kusoma speech ambayo mtu maalum kaiandaa ivutie na kusomeka kirahisi.

Ukija kwenye kiingereza cha kuwasiliana, wengi kusikia maneno na kuyaelewa inakuwa shida, pia kwenye kuongea kwa uhuru mfano kujielezea inakuwa kazi sana tofauti na pale wanaposoma speech, hapa panakuwa na ze ze ze izi izi izi.

Nakumbuka hata mwalimu wa kiingereza wa sekondari alikuwa haelewi chochote kwenye nyimbo za marekani zilizojaa matusi, hii ilikuwa mpaka chuoni wengi walikuwa hawaelewi kinachoimbwa zaidi ya ku enjoy biti na flow.

Pia watanzania huwa tunakosea sana tunapoona mtu kasoma speech kwa kiingereza na kumpongeza anajua, nadhani wa kupongezwa inabidi awe muandaaji alietumia utashi wake na muda mwingi kupangilia hayo maneno, maana bila hivyo hata huyo ambaye anaisoma akiambiwa aongee kwa uhuru huwa inageuka kituko ni kheri aongee kiswahili.
Unanikumbusha muzungu moya iliwahi salimia sisi wanafunzi "shikamoo" tukiwa asembli graundi.

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
 
Unadhani nikwanini Subtitle zinahusika kwenye movie za wazungu wao wenyewe wanajua Kuna akina siye hatuelewi chochote.

Mtu mweusi aliyekulia huko mufindi na alisoma shule za kata akienda ulaya na akaongea kizungu lazima wazungu wacheke
 
Kingereza kilibaki Namanga wakati kinavuka border kuingia Tz
Mhe. tafadhali tuache kidogo tufanye ibada kwa ajili ya Ukraine 🙏
 
CCM badala ya kutuma ndege ziwafate raia wake huko Ukraine wao wametoa ka-barua eti kakutoa ushauri, ujanja ujanja tu kila kitu
Hujasikia mkwara wa mwenye nchi? Hataki ndege ya nchi yeyote, ipite kwenye anga la Urusi, la sivyo asije kulaumiwa kwa kitakachoipata!
 
Kujua kiingereza halafu huna mbuni kipande mfukoni ni uharibifu wa lugha za watu tu.
Kiingereza hakipaswi kuwa kipimo cha maendeleo, kiingereza ni lugha kama ilivyo kisukuma tu.

Putin anajambisha dunia sasa hivi lakini ni nadra kumsikia akiongea kiingereza na si kwamba hakijui, lakini kwake hakina umuhimu wala si kipimo cha mafanikio yake.

Huyo wa ze ze ze angekuwa kituko kama angevurunda kwenye kiswahili, lakini kwa lugha ya watu mbona huyo ni shujaa tu maana ana uthubutu tena anapaswa kupigiwa makofi kama anavyoshangiliwa mzungu akiongea kiswahili broken.

Mambo ya kusifia sana lugha za kigeni ndio tunaambulia watu design ya mkalimani Matungwa, aliyekuwa anatupiga fix kwenye msiba wa Magufuli.
 
Back
Top Bottom