Kigogo UVCCM ahamia CHADEMA

Siku zote anayekupenda anakuambia ukweli, sasa sisi chadema tunataka tu tupate sifa tusikosolewe wala kupewa ushauri hata kama kwa maufaa yetu!hii sio sahihi mjomba. alosema huyu jamaa ni la maana sana, je kama jamaa ni mamluki mwisho wa siku nani ataumia? au kwa vile ccm hawafanyi assessment na chadema wasifanye? think big broda

Baba humrudi mtoto ampendaye kwa fimbo. Baadhi ya CDM washabiki, hawataki kusikia ikikosolewa, wenyewe wanataka kila siku mazuri tu. DUNIA HAIENDI HIVYO, KUNA KUPANDA NA KUSHUKA PIA. na siku zote akupendaye hakupaki mafuta kwa mgongo wa chupa
 
huyu anapigia mahesabu uchaguzi mdogo wa ubunge. Nadhani anafikiria kwamba hatimaye kafulila atapoteza kiti cha ubunge kutokana na kufukuzwa na nccr-mageuzi. Hivyo ameshaangalia upepo na kugundua kuwa chadema kiweza kupatia hiyo nafasi.
nakubaliana nawe kabisa. Timing yake inatia mashaka. si ajabu anataka kiti kinachoweza kuachwa na Kafulila!
 
viona mbali wanajua nani atachukua nchi 2015 lakini nakukumbusha CDM sio sehemu ambayo utapata cheo sababu umekimbia ccm,..hayo mambo wanayo ccm walipompa wassira cheo..

Hizi ndio zilikuwa sera za Makamba za kuwarubuni wapinzani kurudi CCM halafu kuwapa vyeo kama wakina Wassira, Kaborou, Malima eic; matokeo yake akakigawa chama katika makundi mawili hasimu ya wale wa zamani na wale wa kuja!! Elimu yake ilikuwa ndogo kwani hakujua kuwa kwa kufanya hivyo alikuwa anakidhoofisha chama!! I hope Mukama will not repeat that stupidity!!
 
Ni stori ya kutunga ama kutengeneza kwa waandishi ni suala la kawaida kikubwa pesa tu ni ngumu kwa mtu mwenye akili timamu kuahamia chama cha wahuni
 
Back
Top Bottom