hasan124
JF-Expert Member
- Jan 2, 2012
- 716
- 128
Mh. Aden Rage,
Mheshimiwa wakati unachangia hotuba ya upinzani, umepotoka kwa kumuita mwenzako (Mchungaji Msigwa) a fool!! Nilikuwa nakuona kama mtu wa maana kumbe hauko hivyo. Uko kwenye mfungo mtukufu unamwita mwenzako mpumbavu ( a fool) . Lugha kama hiyo kwa mtu aliyefunga kwa maungamo, haifai. Fungua tu, wala hutapata thawabu. Lugha kama hiyo haifai toka kinywani mwako. Kumbe ndio maana Simba haisongi mbele kama hekima yako ndio hiyo.
Mhe. Rage kasema "Never urgue with a fool, No one will know the difference" na kuongezea "Sheik/Padri akifanya uzinifu haimaanishi na waumini wote ni wazinzi" Nijuavyo mimi hii ni misemo tu ya wanasiasa wanapotaka kujenga hoja, Hajampoint Mhe. Msigwa kwamba yeye ndio fool.
Zaidi nilivyomsikia alikua anazungumzia kwamba Mhimili mmoja wa nchi hauwezi kuingilia maamuzi ya muhimili mwingine. ie; Bunge haliwezi kuingilia maamuzi ya Mahakama and vice versa.