GeniusBrain
JF-Expert Member
- Nov 3, 2010
- 4,315
- 306
WAKATI CCM, ikihaha kujaza watu kwenye mkutano wake, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilbroad Slaa, amekidhihaki chama hicho kuwa hakiwezi kuendelea kutawala nchi kwa kuwalipia nauli, kuwabeba na kuwapa posho watu wanaokwenda kwenye mikutano.
Slaa, alisema ilani ya chama chochote makini inapaswa kuonekana machoni mwa wananchi na siyo kusemwa kama ambavyo Rais Jakaya Kikwete na timu yake ndani ya CCM wanavyofanya.
Kauli hiyo aliitoa jana katika Uwanja wa Likangala wilayani Ruangwa mkoani Lindi wakati akihutubia mkutano wa hadhara, huku akitanabaisha kuwa wafuasi wanaokipenda chama chao hawawezi kubebwa na magari kwenda kwenye mikutano kwa kulipiwa nauli.
Dk. Slaa alikuwa akijibu matamshi mbalimbali yaliyokuwa yakitolewa na viongozi wa CCM katika mkutano wao wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam na kurushwa moja kwa moja na vituo vya redio na runinga.
Alisema mawaziri wa CCM wamekuwa makasuku kwa kushindwa kutathmini kauli zao za awali, ambazo hazijatekelezwa na kwamba sasa wanakuja na hoja nyingine zisizotekelezeka.
Akiwachambua baadhi ya mawaziri na kuanza na Jumanne Maghembe, alisema kuwa anapaswa akumbuke miaka zaidi ya kumi iliyopita serikali ilikuja na mkakati wa kilimo cha umwagiliaji na kusema imeshapata kiasi cha dola milioni 12 za Marekani kwa ajili ya shughuli hiyo.
Tunataka watuambie hizi fedha zimeenda wapi mpaka sasa wanakuja na kauli nyingine, hivi hakumbuki tulikaa katika ukumbi wa mikutano wa Pius Msekwa wakatuambia hizi fedha zipo, sasa zimeenda wapi? alihoji Dk. Slaa.
Kuhusu ujenzi wa barabara kilomita 11,000 zilizoelezwa na Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, Slaa alisema huo ni upuuzi kwa kufananisha hali hiyo na mahitaji mazima ya nchi.
Alisema fedha zilizoibwa na watumishi wa serikali ya CCM ni nyingi kuliko hivyo wanavyojinadi kuwa wamefanya, na kuitaka serikali ieleze dola milioni 1.5 zilizokutwa katika akaunti ya mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge (CCM) zimefanyiwa nini.
Alibainisha kuwa, Serikali ya CCM inapaswa kutolea maelezo fedha za chenji ya rada zimefanya nini wakati katika mahesabu ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) hazionekani kutumika.
Kuhusu kauli ya Steven Wassira kuwa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Freeman Mbowe atalaaniwa kwa kuwa baba yake aligombea uhuru na Mwalimu Nyerere, Dk. Slaa alisema viongozi hao walisimama kwa ajili ya kuwatetea Watanzania na kama watasimama leo kuna hatari ya kuwachapa viboko viongozi wa CCM kwa kushindwa kuendeleza malengo waliyofikia.
Naye Mbowe alisema anamsikitikia Wassira kwa kile alichoeleza kuwa, anashindwa kusimamia hata utendaji wa nafasi yake na badala yake anahangaika kuropoka kila wakati mambo yasiyo na tija kwa taifa.
Alibainisha kuwa, Wassira si saizi yake kwenye majukwaa ya kisiasa kwa sababu hana hadhi ya kupigania ukombozi wa kweli, hivyo akamtaka awatafute watu wenye hadhi yake.
Alisema katika hali ya sasa, CCM haioni mahaba ya wananchi, hivyo wanajitahidi kukusanya watu katika maeneo mbali mbali ya nchi ikiwa ni pamoja na kununua kadi za CHADEMA kwa ajili ya kujiaminisha mbele ya wananchi.
Hawa watu vipi, wana nini sijui kwa kuwa wanatunga uongo wanauaminisha umma na mwisho wa siku wanauamini huo uongo walioutunga kama ambavyo wamefanya leo kule Jangwani, alisema Mbowe.
Source: Tanzania Daima
Sasa ndio naanza kuamini dokta feki wa dini ya ukatoliki anazeeka vibaya. Fedha ya rada ilirudi mwaka Jana mwishoni, hesabu za CAG ni za mpaka 30.06.2011, sasa hapo unategemea kweli zitakuwepo? zitakuwepo kwenye taarifa ya mwaka huu unaoishia 30.06.2012. Ni aibu kwa dokta feki kuongea uongo