Paschal Matubi
JF-Expert Member
- Sep 15, 2008
- 235
- 302
Chanzo Cha Habari: Gazeti la TUMAINI LETU
Mmiliki wa Gazeti: Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la D'Salaam
Toleo: 00302
Tarehe: MARCH 19, 2010
Ukurasa: 07
Wakati wananchi wa Philipines wakijiandaa kwa uchaguzi wa viongozi wa Serikali nchini huo baadaye mwaka huu, Kanisa Katoliki limetoa waraka wa kichungaji likiwataka waamini na wananchi kwa ujumla kuwa makini na wanasiasa wanaotumia fedha kupata ili kupata uongozi.
Waraka huo wa kichungaji ulioanza kusambazwa Jumapili liyopita umetolewa na Askofu Mkuu wa jimbo Kuu la Manila Mwadhama Gaudensio Kardinali Rosales na kusainiwa na maaskofu wengine kumi na tano wa nchi hiyo.
Katika waraka huo, Kardinali Rosale alisema kuwa ni vyema wananchi wakawa na tahadhari kubwa na wanasiasa wanaotumia fedha nyingi wakati wa kampeni kwa kuwa wanasiasa wa namna hiyo hawana lengo zuri kwa wapiga kura wao.
Aliwataka wananchi kupiga kura kwa uhuru na kuchagua viongozi bila kujali shinikizo la aina yoyote likiwemo la fedha ili kuwapata viongozi wa nchi watakaowajibika na kuwatumikia wapiga kura wao.
Kardinali Rosale alisema ni vyema kila mpiga kura akasoma kwa makini maelezo binafsi ya wagombea na kuzipima kauli zao badala ya kuangalia kiasi cha fedha kinachotumika katika kampeni.
Aidha waraka huo wa maaskofu umezitaka mamlaka zinazohusika nchini humo kuhakikisha uchaguzi nchini humo unafanyika kwa misingi ya kuzingatia demokrasia bila kuwepo vitisho.
Uchaguzi nchini Philipines utafanyika Mei 10 mwaka huu.
Mmiliki wa Gazeti: Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la D'Salaam
Toleo: 00302
Tarehe: MARCH 19, 2010
Ukurasa: 07
Wakati wananchi wa Philipines wakijiandaa kwa uchaguzi wa viongozi wa Serikali nchini huo baadaye mwaka huu, Kanisa Katoliki limetoa waraka wa kichungaji likiwataka waamini na wananchi kwa ujumla kuwa makini na wanasiasa wanaotumia fedha kupata ili kupata uongozi.
Waraka huo wa kichungaji ulioanza kusambazwa Jumapili liyopita umetolewa na Askofu Mkuu wa jimbo Kuu la Manila Mwadhama Gaudensio Kardinali Rosales na kusainiwa na maaskofu wengine kumi na tano wa nchi hiyo.
Katika waraka huo, Kardinali Rosale alisema kuwa ni vyema wananchi wakawa na tahadhari kubwa na wanasiasa wanaotumia fedha nyingi wakati wa kampeni kwa kuwa wanasiasa wa namna hiyo hawana lengo zuri kwa wapiga kura wao.
Aliwataka wananchi kupiga kura kwa uhuru na kuchagua viongozi bila kujali shinikizo la aina yoyote likiwemo la fedha ili kuwapata viongozi wa nchi watakaowajibika na kuwatumikia wapiga kura wao.
Kardinali Rosale alisema ni vyema kila mpiga kura akasoma kwa makini maelezo binafsi ya wagombea na kuzipima kauli zao badala ya kuangalia kiasi cha fedha kinachotumika katika kampeni.
Aidha waraka huo wa maaskofu umezitaka mamlaka zinazohusika nchini humo kuhakikisha uchaguzi nchini humo unafanyika kwa misingi ya kuzingatia demokrasia bila kuwepo vitisho.
Uchaguzi nchini Philipines utafanyika Mei 10 mwaka huu.