Kamlete - akibisha...

Halafu unakumbuka mipira iliyokuwa inatengenezwa na manailoni halafu unaifuma na kamba? Hii ndo ilikuwa alternative yetu ya magozi kwa vile yalikuwa adimu sana. Mdingi akienda kiwanja akikuletea gozi kama zawadi basi mwenyewe unataaamba...Lol.

Mipira ya manailoni tena nisahau ndugu yangu?

Mpira wa Gozi, huko unaenda mbaaaali mno. Kitenesi tu ishu!

Kuna vile vi gofu vile, vya Tiger Woods vile. Ukikipata kile dili. Ndio kinakuwa cha ndimu mpaka kipotee!

Tulikuwa tunaambiwa kigofu ndani kimejaa raba bendi. Me and my brother tukawa tunatamani tukipasue tupate raba bendi (mwanangu, raba bendi nazo iiiiiishuu!) Sasa tulikuwa tunapenda mpira kupindukia. Tukaona tukipasua kigofu, hatuna cha ndimu. Tukibaki nacho kigofu, we'll never find out ndani kuna nini. Big dilemma!

We never cracked the golf ball or the puzzle!
 
Mipira ya manailoni tena nisahau ndugu yangu?

Mpira wa Gozi, huko unaenda mbaaaali mno. Kitenesi tu ishu!

Kuna vile vi gofu vile, vya Tiger Woods vile. Ukikipata kile dili. Ndio kinakuwa cha ndimu mpaka kipotee!

Tulikuwa tunaambiwa kigofu ndani kimejaa raba bendi. Me and my brother tukawa tunatamani tukipasue tupate raba bendi (mwanangu, raba bendi nazo iiiiiishuu!) Sasa tulikuwa tunapenda mpira kupindukia. Tukaona tukipasua kigofu, hatuna cha ndimu. Tukibaki nacho kigofu, we'll never find out ndani kuna nini. Big dilemma!

We never cracked the golf ball or the puzzle!

Watoto wa Gymkhana utawajua tu na vigofu ball vya baba zao :). Uswahilini kigofu ball utakipatia wapi? Ukisikia ki-gofu unajua gari la polisi.

Halafu wana ji fake ugumu wa chandimu.
 
angalau wenzetu mlikuwa na vitu vya kuchezea.. wenzenu kijijini.. mkono mmoja umeshika kaputula isidondoke huku kwapani umeweka daftari za "Mazoezi"; mkono mwingine una bonge la kijiti na ringi la baiskeli unakimbizana nalo kuwahi shule... uzuri wake jinsi ulivyokuwa unakatisha nayo kona mtu akikuambia uendeshe pikipiki hutaki!!

hapo sijakuambia kuhusu manati inayoning'inia shingoni for "after school activity"...
 
angalau wenzetu mlikuwa na vitu vya kuchezea.. wenzenu kijijini.. mkono mmoja umeshika kaputula isidondoke huku kwapani umeweka daftari za "Mazoezi"; mkono mwingine una bonge la kijiti na ringi la baiskeli unakimbizana nalo kuwahi shule... uzuri wake jinsi ulivyokuwa unakatisha nayo kona mtu akikuambia uendeshe pikipiki hutaki!!

hapo sijakuambia kuhusu manati inayoning'inia shingoni for "after school activity"...


Nimemshtukia M.M Mwanakijiji ni the former "Madenge"

madenge.gif
 
We mwanakijiji ni mchokozi kweli...uliweka link ukisema watu wasisikilize huku ukijua kuwa karibu asilimia 90 hawataweza kujizuia!:) Well, mimi nilifungua link na nikacheka kama mjinga na watu ofisini wakabaki kushangaa. I really needed that laugh (itareplace button isemayo "that was easy" from Staples).

Kezilahabi aliandika vitabu vizuri sana kama mkuu mmoja alivyotamka, binafsi nilipendelea "Kichwa Maji". Agoro Anduru (RIP) naye alikuwa mzuri, na katika miaka ya mwisho wa 80 na 90 kulikuwa na bwana mmoja aitwaye Simbamwene aliyekuwa na characters wake Inspekta Sindi na Kachero Haji. Musiba amekuwa active katika TCCIA na alikuwa rais wake kwa muda mrefu.

Mwanakijiji, Nyani Ngabu na wengineo wenye kupenda riwaya zetu, itabidi tufungue book club hapa jamvini. Watu inabidi wacheke sana na kukumbuka jinsi Chonya alivyokuwa na lafudhi ya kihehe na kusema "Spitali" badala ya "Hospitali"
 
Hivi mnakumbuka kasheshe za mwaka mpya? Basi mnapiga madebe na kuchoma matairi mtaani. Mapaa ya mabati mbona yalikuwa yanakoma kwa kurushiwa mawe.

Halafu kama una ugomvi na mtu, basi usiku huo ndio mtaumaliza. Unapigana, ukishindwa una lala mbele....maana hakuna kuamlia
 
Vipago vya mpera ndo vilikuwa bomba kuliko vyote. Kuna mtu anakumbuka kuingia matatani kwa kutumia mche wa fagio (miwili) ili aweze "kuendelesha" tairi (weka maji ndani)? Au kumbukumbu ya watoto kusema binduki na edikopta badala ya bunduki na helikopta?

Seriously, tutampataje huyu anayetafutwa na Interpol? Amekuwa incognito?
 
mpanda merikebu hiyo ya matairi inanikumbusha sijui wazimu gani tulikuwa nao wa kuingia kwenye tairi na kubingirishwa nalo ukitoka hapo basi ni kichina china...
 
Mwanakijiji, naamini kuwa katika umri huo, ndio nilikuwa na raha kuliko wakati wote. Hakuna wajibu (responsibilities) wowote, hakuna kujali unaonekanaje au una hatari ya kuumia na wazazi wetu walitusupport. Walituruhusu tucheze vita vya makungu au madongo bila hofu. Siku hizi, kila kitu lazima kiwe kimethibitishwa na chombo flani cha dola. Hivi ni nani aliyegundua mchezo wa, ashakum, mama na baba?
 
Mwanakijiji, naamini kuwa katika umri huo, ndio nilikuwa na raha kuliko wakati wote. Hakuna wajibu (responsibilities) wowote, hakuna kujali unaonekanaje au una hatari ya kuumia na wazazi wetu walitusupport. Walituruhusu tucheze vita vya makungu au madongo bila hofu. Siku hizi, kila kitu lazima kiwe kimethibitishwa na chombo flani cha dola. Hivi ni nani aliyegundua mchezo wa, ashakum, mama na baba?

Je ukipewa nafasi ya kuurudia umri huo utakubali?
 
... Walituruhusu tucheze vita vya makungu au madongo bila hofu.

On a serious note though, speaking of vita vya makungu, hivi kwa nini sisi ndio tuna chakula mpaka tunachezea lakini bado tunakufa njaa?

Kiwanja toka lini ukakuta mpera au mpapai umejiotea otea barabarani!

Nani atakupa tunda la bure Marekani? Is it the land of milk and honey kweli?
 
Kuhani mkuu.. this is what I figured out.. nikienda Kroger au Meijers.. huwa napita section za matunda na kujaribu kuwaza niko kwenye bustani ya "Paradiso" kule Peramiho (I'll tell the story about that one of these days) na pole pole as I push my cart ninajipongeza kwa matunda ya mafyulisi, zabibu, na mara moja moja matunda damu...

so to answer your question yes.. this is the land of milk and honey.. at least ukienda kwenye grocery stores...
 
Zaidi ya vitabu vya upelelezi na mapenzi... kuna kulikuwa na vitabu kama Machimbo ya Mfalme Suleiman.. akina Umplomagasi na msemo wake wa Pigo moja tu, pigo lenye nguvu pigo takatifu
 
On a serious note though, speaking of vita vya makungu, hivi kwa nini sisi ndio tuna chakula mpaka tunachezea lakini bado tunakufa njaa?

Kiwanja toka lini ukakuta mpera au mpapai umejiotea otea barabarani!

Nani atakupa tunda la bure Marekani? Is it the land of milk and honey kweli?

Infrastructure mwanangu,

wakati matunda yanaoza upande mmoja wa nchi yetu, upande mwingine kuna uhaba.

Eisenhower alicheza kweli kuweka ma interstate network of roads, tunahitaji Eisenhower wetu kule bongo.
 
Wadosi na nchi yetu sina la kusema tokea enzi za mashati na fulana za mtunguo hadi kutuuzia helkopta za kijeshi
 
Pundit.. nilidhani mkutano uliopita ulikuwa unahusu "miundombinu".. au walikuwa wanaunda mbinu...
 
...this is what I figured out.. nikienda Kroger au Meijers..... this is the land of milk and honey.. at least ukienda kwenye grocery stores...

Hicho ndio wanacho maanisha "land of milk and honey"? Laiti ningelijua!

Kroger na Meijers ni grocery stores?

Maana kuna matunda ambayo hata Kariakoo huyapati lakini nenda Pathmark na Wegmans! Kariakoo kuna makungu au matunda nyoka? Mi nshaona makungu Pathmark! Ninashaona mpaka mabungo na mastafeli kwenye grocery stores. Sijui wanayaibua wapi. Huwezi kuona sega la nyuki barabarani lakini Asari hukosi kwenye grocery store! Duuuh! Laiti!
 
Je ukipewa nafasi ya kuurudia umri huo utakubali?

Knowing what I know now, yes, I wouldn't mind going back. Lakini kama binadamu, ni lazima nikabiliane na kile kinachonijia. Labda miaka ishirini kutokea sasa (nikiwa hai) nitasema kuwa nilivyokuwa katika miaka X ilikuwa bomba sana. Kwa kifupi, experience zote ni nzuri tu, japo huwa hatuziappreciate mpaka muda upite!
 
Zaidi ya vitabu vya upelelezi na mapenzi... kuna kulikuwa na vitabu kama Machimbo ya Mfalme Suleiman.. akina Umplomagasi na msemo wake wa Pigo moja tu, pigo lenye nguvu pigo takatifu

Ahsante.

Mtafsiri wa Umslopagaas alipata credit za kuandika Umslopagaas!
 
Back
Top Bottom