Kambi ya Jeshi Gongo la Mboto ihamishwe kijengwe kituo cha basi

Unaongea mambo ya zamani sana zama za vita vya Kagera.

Huu ndio ujinga na hoja za kipuuzi mnazotumia kuitawala Zanzibar kimaguvu sasa hivi mpaka mtu wa Mkuranga anakuwa Rais Zanzibar wakati Wazanzibar wenyewe wapo.
Hujui unachoongea.
 
Wewe ndio hujui lolote, ndio mnaowadanganya watu eti Zanzibar ni muhimu kwa usalama wetu wakati sasa hivi unaweza kushambuliwa kutokea mbali.
Sio Zanzibar tu.... Comorros na Seyschelles zote ni muhimu kwa usalama wetu.

Kama hujui umuhimu wa kuwa macho na majirani, nenda Eastern DRC ukaone kinachoendelea.
 
Amani inalevya sana. Kwa vile watu hawajaona au kushudia vita Dar es Salaam, sasa wana pendekeza kambi za jeshi zilizoko hapa hazina umuhimu hivyo zihamishwe.
 
Hadi leo nasikitika sana jinsi wanajeshi walivyonajisi kambi ya Lugalo kwa kujenga frame.

Kuna wakati naona bora hata jina Lugalo libadilishwe ili kulinda heshima ya Mtwa Mkwawa. Waipe jina la makamanda wao wa kidigital wanye mawazo ya ujenzi wa frem kuzunguka kambi za jeshi
Waende Misri (Masri) wakajifunze jeshi lao limetumia njia zipi kumiliki uchumi mkubwa?

Mfano pale Victoria kuna Masri Military detachee zile ni appartment zinamilikiwa na jeshi la Masri, huwa kukuta fremu kwenye base zao Masri.

Hapa ieleweke hatukatai jeshi letu kumiliki uchumi, lakini siyo uchumi wa wa fremu.

Binafsi nyumba yangu ipo mtaa mkubwa wenye movement lakini nimekataa ujinga wa kugeuza makazi kuwa na fremu za maduka, wajinga wengi huwa wananishauri kuweka fremu lakini nawajibu hapa ni residence siyo cormecial premises.
 
Mkitaka kujua umuhimu wa Kambi za Jeshi katika mkoa muhimu ambao ni Lango la Tanzania ... Fanyeni zihame
Nafikiri kambi hazina shida, bali shida ipo kwa watu wa mipango miji hawana maono ya mbali
Jeshi lilipaswa kutengewa eneo la kutosha kiasi kwamba inakua ngumu kufika kwenye ina core ya jeshi
 
Mbele Kituo Cha Mwendokasi Huoni Fremu Zetu Kuzunguuka Kikosi Chote
 
Mkitaka kujua umuhimu wa Kambi za Jeshi katika mkoa muhimu ambao ni Lango la Tanzania ... Fanyeni zihame
Nafikiri kambi hazina shida, bali shida ipo kwa watu wa mipango miji hawana maono ya mbali
Jeshi lilipaswa kutengewa eneo la kutosha kiasi kwamba inakua ngumu kufika kwenye ina core ya jeshi
Kwa tuliopo Dar kitambo hizo kambi zilikuwa maeneó sahihi, lakini sasa hivi kambi zote zimezingukwa na makazi mji umepanuka sana.

Kambi zenye sifa ya kubaki mjini ni Air wing na Navy peke yake. Angalau na kambi ya Twalipo.
 
Wananchi ndio wanalifuata jeshi, uliza wenyeji kati ya kambi na wao nani alitangulia kuwepo..?

Hoja ya kuweka frame kwenye maeneo ya jeshi sio kosa ila wangekusanya hela waweke miradi mikubwa kama mahoteli, malls
 
Kwahiyo kwa uelewa wako kambi zikijengwa polini, hadui hawazi kuzifia. Hivi hujiulizi kwanini kambi ya gongolamboto kambi, kisarawe na kambi ya uwanja wa ndege zilijengwa karibukaribu.
Halafu nenda Lugalo, ukitoka Lugano nenda uhasibu.

Na ukishapata jibu jiulize tena mbona huko wanakopigana hatusikii leo, jeshi fulani wameshambulia kambi fulani, iliyejengwa poli fulani. Bali miji tu ndiyo inayoshambuliwa.

Acha kufuata mawazo ya wajinga wanaojifanya kujua kila maeneo ya watu, maana nawe utaingia kwenye ujinga.
Hoja, aombe kujengewa kituo cha mabasi gongolamboto, na siyo kuhamisha kambi eti sababu wanajengwa frem.
Rubbish
 
Nadhani ifike wakati serikali yetu hata kama ina wajinga wengi basi tutumie nafasi yetu kushauri badala ya kukosowa tu.

Mimi si mtaalam wa mambo ya ulinzi lakini naelewa fika nimezaliwa Dar gongo la mboto ilikuwa iko wilaya ya kisarawe ni shamba.

Sasa kuwepo kambi ya JWTZ kwa kipindi kile ilikuwa sahihi, lakini sasa hivi dunia imehama hatuko huko tena kuna vita za kiteknolojia, haya makambi mijini ni useless kabisa.

Nimepita leo kambi ya gongo la mboto nimeshangaa kuona jeshi liko bize na ujasiriamali wa fremu za biashara kwa sababu kambi iko barabarabani hili siyo sahihi hii ni miradi ya watu wakubwa jeshini.

Gongo la mboto ni route ya magari mbalimbali ya safari za jijini lakini hakuna bus terminal, ni kwa nini kambi kama hii ya gongo la mboto isihamishwe na kupisha matumizi ya umma badala ya kugeuza eneo la jeshi kama mgodi wa watu flani?

Najuwa Rais hapendi kulikera jeshi lakini kwa hili hakuna manufaa yoyote kwa jeshi zaidi ya ulaji wa maboss wachache wa jeshi.

Muda wa kufumbia macho maovu na ufisadi kwenye jeshi letu umepita sasa ni lazima tuambiane ukweli, mama mulika makambi ya jeshi Dar, omba ushauri wa kisasa kwa Military analyst achana na wale wenye akili za kijima kwamba Zanzibar ni muhimu kwa Tanganyika kwa sababu za kiusalama, wewe waulize Iran aliporusha drones zake Israel alipitia nchi jirani?
Nakushauri nenda pale gongo la mboto halafu omba kuonana na CO wa pale then mueleze haya maneno atakusikiliza maana nawajua wanajeshi ni watu waelewa sana. Tafadhali sana usisahau kuleta mrejesho mzee.
 
Back
Top Bottom