Kamanda Lema ndani ya Arumeru

Mkuu hii ni Tanzania wanayoitaka iwe. By the way, kwa mtu aliyepewa dhamana na title ya u-jaji aropoke vile, unategemea watu wenye kuta 28 za elimu maishani mwao wafanye nini?
Shame on you Tendwa.

7x4 = std 7

Umenikumbusha mtu mmoja anaitwa Dr. Ngirwa! teh teh teh mkuu. Ulikuwa na maana hiyo au nimeshambulia chaka?
 
Kwa nini Lema pamoja na viongozi wa Chadema wasiombe ulinzi kutoka jeshi la polisi, kwa usalama na mustakabali wa nchi yetu tujiepushe vita vya kikabila ambavyo vitatupeleka pabaya, sio vizuri kulindwa na walinzi wa jadi, tujifunze kutoka Tarime.

Mkuu Tarime hakuna walinzi wa jadi! Tarime kuna wamura wenye hasira.
 
Kwa nini Lema pamoja na viongozi wa Chadema wasiombe ulinzi kutoka jeshi la polisi, kwa usalama na mustakabali wa nchi yetu tujiepushe vita vya kikabila ambavyo vitatupeleka pabaya, sio vizuri kulindwa na walinzi wa jadi, tujifunze kutoka Tarime.

Mkuu wangu Ritz hakuna ukabila wala nini.Bali hizi ni vurugu wanazotaka kuzileta Arumeru kwa kumtuma Tendwa kuongea upuuzi ule ambao umemvunjia heshima yake.Ninamuonea huruma sana kwa kukubali kutumika kama dodoki.Kuhusu ulinzi wa Lema ni wana Arumeru wenyewe wamejikusanya na kuamua kujitolea kumlinda Lema ili wale waliochochewa na Tendwa wasifanikiwe njama yao ovu.Mungu ibariki Arumeru.
 
CDM mnaipeleka wapi Arumeru? Kila mtu akiwa warlord kama Somalia, akawa na wanamgambo wake, na silaha zake, si uchaguzi utageuka chanzo cha vita vya wanamgambo?

Msituletee mambo yenu ya shari, lazima usalama ulindwe na Polisi....full stop!
 
Mkuu matatizo haya tunayapata kwa sababu ya watendaji wa aina ya Tendwa wasiojua wajibu wao kwa nchi yetu.

Mkuu hivi Tendwa aliipata wapi ile kauli? Hawa Washiri (sijui Wasiri) wana nguvu kiasi gani? Hawa Washiri ni sawa na wale ambao Nyaronyo anaita Abaghaka wa huko Tarime?

Hivi tatizo ni Tendwa au hao washiri?
 
Kwa nini Lema pamoja na viongozi wa Chadema wasiombe ulinzi kutoka jeshi la polisi, kwa usalama na mustakabali wa nchi yetu tujiepushe vita vya kikabila ambavyo vitatupeleka pabaya, sio vizuri kulindwa na walinzi wa jadi, tujifunze kutoka Tarime.

kwani huo wa morani ameomba? Wameratibu wapenzi na wafurukutwa wake,ivi ritz unakubali akili unayo2mia hapa?
 
CDM mnaipeleka wapi Arumeru? Kila mtu akiwa warlord kama Somalia, akawa na wanamgambo wake, na silaha zake, si uchaguzi utageuka chanzo cha vita vya wanamgambo?

Msituletee mambo yenu ya shari, lazima usalama ulindwe na Polisi....full stop!

Unanikumbusha akina Mohamed Farrah Aideed, Osman Ali Atto, Mohammed Said Hersi Morgan na Musa Sudi Yalahow wa huko Somalia. Kila kamanda alikuwa na kundi la moran wa kisomalia.
 
Mkuu hivi Tendwa aliipata wapi ile kauli? Hawa Washiri (sijui Wasiri) wana nguvu kiasi gani? Hawa Washiri ni sawa na wale ambao Nyaronyo anaita Abaghaka wa huko Tarime?

Hivi tatizo ni Tendwa au hao washiri?

Mkuu wangu Kimbunga
Tendwa ni msajili wa vyama vya siasa.Anakimbilia kwa waandishi na kusema wazee wa kishiri wamesema Lema akienda tu Arumeru anaweza kuuawa.Kwa hiyo Tendwa jaji aliyebobea anasema usalama wa Lema ni kutokukanyaga Arumeru mpaka kampeni ziishe.Kampeni zikiisha anaruhusiwa kwenda.Huo ndio ushauri wa kiongozi aliyebobea.Mkuu Kimbunga wewe unaona mwenye matatizo makubwa zaidi ni Tendwa au hao Washiri??
 
CDM mnaipeleka wapi Arumeru? Kila mtu akiwa warlord kama Somalia, akawa na wanamgambo wake, na silaha zake, si uchaguzi utageuka chanzo cha vita vya wanamgambo?

Msituletee mambo yenu ya shari, lazima usalama ulindwe na Polisi....full stop!

Polisi wanaua raia,walinzi wa jadi wa waadhibu waalifu,sina imani na police tena
 
CDM mnaipeleka wapi Arumeru? Kila mtu akiwa warlord kama Somalia, akawa na wanamgambo wake, na silaha zake, si uchaguzi utageuka chanzo cha vita vya wanamgambo?

Msituletee mambo yenu ya shari, lazima usalama ulindwe na Polisi....full stop!

Swali hilo muulize Tendwa aliyechokoza nyuki
 
NAOMBENI NITOE ANGALIZO,kama anaeratibu ulinzi huo ni mtu aitwae Yohana kimuto mstaafu wa polisi basi green guard ama serikali msipite anga izo,huyu bwana ana historia ya kuhamasisha demostration mbalimbali huko meru na ndo aliongoza uvamizi ktk mashamba ya SADC.kama ni kimuto Lema upo salama meru,huyu ni balaa
 
Kwa nini Lema pamoja na viongozi wa Chadema wasiombe ulinzi kutoka jeshi la polisi, kwa usalama na mustakabali wa nchi yetu tujiepushe vita vya kikabila ambavyo vitatupeleka pabaya, sio vizuri kulindwa na walinzi wa jadi, tujifunze kutoka Tarime.

Mkuu umegusia suala la msingi sana, lakin huoni ni muhimu kwa polisi kuchukua hatua kwanza kwa mtu aliyetishia kuua? (Huu ni wajibu wao)
 
hapana : nyie tumieni dola sisi tunatumia umma, bila kuwapigia hii staili mtatunyanyasa na mabomu yenu sasa twendeni kazi. Mnadola, usalama wa taifa, chadema tuna nguvu ya umma. Msitulaumu mlaumuni Tendwa mliyemtuma.

Hii nimeipenda kweli!
 
Kwa nini Lema pamoja na viongozi wa Chadema wasiombe ulinzi kutoka jeshi la polisi, kwa usalama na mustakabali wa nchi yetu tujiepushe vita vya kikabila ambavyo vitatupeleka pabaya, sio vizuri kulindwa na walinzi wa jadi, tujifunze kutoka Tarime.

hao walioua watu kule Songea au ni wengine? HATUWATAKIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII!!!!!!!
 
Vijana 363 katika jimbo la Arumeru Mashariki, wilayani Arumeru, wameandaliwa kwa ajili ya kumlinda mbunge wa Arusha Mjini, Godbles Lema (CHADEMA), katika kampeni za ubunge Arumeru Mashariki kutokana na tishio la wazee wa kimila wa kabila la Wameru (Washiri).
Hatua hiyo imefikiwa siku chache baada ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa, kumtaka Lema awaombe radhi wazee wa Washiri kwa madai kuwa aliwaudhi wakati wa mazishi ya Jeremiah Sumari.
Wakizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, vijana hao kupitia viongozi wao, walisema kuwa licha ya kuchukua hatua hiyo ya kumlinda Lema pia wanasubiri kuona Jeshi la Polisi litachukua hatua gani dhidi ya wazee hao kwa kutishia kuua.
Walisema kuwa kama polisi haitamchukulia hatua mwenyekiti wa Washiri, aliyetoa tamko hilo, wao watawapiga marufuku wabunge wote wa CCM na viongozi ambao hawaishi Meru, kuonekana katika jimbo hilo kuanzia Machi 9 mara kampeni zitakapoanza.
Akizungumza kwa niaba ya wenzake, Yohane Kimuto (51) mkazi wa Sing’isi Meru, alisema kuwa ili kumhakikishia ulinzi Lema, tayari wameandaa kundi la vijana (Morani wa Kimeru) wapatao 363, kwa ajili ya kumlinda kila atakakopita wakati wote wa kampeni.
Kimuto alisema kuwa maandalizi ya vijana hao yamekamilika na wako tayari kwa ulinzi wa mbunge wao, ambaye wanamhitaji kwa hali na mali kwenye kampeni za Arumeru Mashariki.
Alisema kinyume na hapo kampeni hizo hazitakuwa salama, kwa sababu tayari kutakuwa na makundi mawili ya kumlinda Lema na lingine linalotaka kumuua na hapo amani itatoweka.
“Lazima ikumbukwe Meru tumekuwa kwenye vita tangu wakati wa vile vya kidini walipouawa wamisionari na ikajirudia tena mwaka 2009, katika mashamba ya Madira na watu kuswekwa gerezani na wengine kupoteza maisha, hili sasa hatutaki lijirudie,” alionya Kimuto.
Aliongeza kuwa kwa niaba ya Wameru wenzake wanamtaka mwenyekiti wa Washiri, aliyetoa tamko hilo ajiuzulu mara moja, kwa sababu anafanya kazi ya siasa na kuacha kazi yake ya kuratibu mila na jadi za Kimeru.
Akizungumzia sakata hilo Kaimu Kamanda wa Polisi, Akili Mpwapwa, alisema mpaka sasa hawana wa kumchukulia hatua kwani hakuna mtu aliyekwenda kushtaki kutishiwa maisha.
“Ninachofahamu mimi ni kuwa mtu anapotishiwa maisha lazima atoe taarifa polisi ili apatiwe ulinzi na hivyo hadi sasa hakuna aliyetoa taarifa kuhusiana na vitisho vya Washiri,” alisema Mpwapwa.

Source:Tanzania Daima
Tendwa anasemaje tena!? Lema ametishiwa kuuawa akaombe "Ee wazee wangu naomba msiniue" Kutishia kuua siyo kosa kisheria?! Tendwa amesomea sheria za wapi? Kweli polisi yote ni Jeshi la CCM!! ingekuwa upande wa pili sasa hivi watu wangekuwa wanatumia vyoo vya ndoo!!. Jeshi la polisi ni jeshi la chama cha majambazi!!
Tendwa JIUZULU!!!
 
Mkuu wangu Kimbunga
Tendwa ni msajili wa vyama vya siasa.Anakimbilia kwa waandishi na kusema wazee wa kishiri wamesema Lema akienda tu Arumeru anaweza kuuawa.Kwa hiyo Tendwa jaji aliyebobea anasema usalama wa Lema ni kutokukanyaga Arumeru mpaka kampeni ziishe.Kampeni zikiisha anaruhusiwa kwenda.Huo ndio ushauri wa kiongozi aliyebobea.Mkuu Kimbunga wewe unaona mwenye matatizo makubwa zaidi ni Tendwa au hao Washiri??

Mwenye matizo ni Tendwa na hao Wazee wa Kishiri, but aliyelikuza zaidi ni Tendwa kwani alistahili kutoa taarifa hizi kwa jeshi la polisi (kwa uvunjaji wa sheria). Nchi hii kila mtu yuko huru kwenda popote ili mradi asivuje sheria (sasa lema alivunja sheria ipi?). Je ingekuwa ni mtu wa CCM ametishiwa namna hiyo angeyasema hayo?
To me it's more like him taking advantage of the opposition (CDM) to make extra votes for CCM.
 
Back
Top Bottom