JWTZ kupiga doria barabarani: Mwamunyange ameenda mbali mno...

Unataka raia waendelee kuuawa ndiyo uridhike?, maelezo yako kuhusu tofauti ya jeshi na polisi hayana uzito wowote wa maana.Naunga mkono asilimia 100 wanajeshi kuingia mitaani, na waendelee hivyo hivyo.
 
Kwa akili za haraka kama zako wewe muweka hili bandiko utajumuisha kuwa JWTZ wamekosea. Nimesoma bandiko lako lakini sijaona sababu ya msingi uliyoandika kukinzana na kilichotokea.
Hivi katika kujiuliza kwako huko, hujafikiria hata kidogo kuwa ni nani na raia wa nchi gani wanaoratibu hili vuguvugu?
Je, una uhakika kuwa usalama wa nchi haukuwa mashakani hata kama kulikuwa na kikundi kidogo tu cha watu?..mwisho je hizi vurugu zingeleta maafa kwa Rais aliyekuwa akirejea jana, huoni kuwa JWTZ nao wangekuwa ni sehemu ya kundi la kulaumiwa?
 
Mwamunyange yuko sahihi kabisa kutuma vijana wake kufanya doria mitaani. Zingatia kuwa maandamano yalilenga kwenda ikulu, sasa hujui hawa jamaa wanampango upi.! Wanaweza kutumia fursa hiyo pengine hata kutangaza kwamba kuanzia muda huo wakiwa tayari ndani ya ikulu kutangaza kwamba nchi iko mikononi mwao.! So alichofanya Mwamunyange ni kitendo cha busara ya hali ya juu sana.
 
Ni hivi mimi nilitaka majeshi yote yakae barabarani halafu yatembezwe makofi mpaka kunakucha.Hii ni matokeo ya watu walio wengi kumwomba MUNGU atuepushie hawa watu wanaotaka kuvunja Amani kwa kisingizio cha kumpigania / kumtetea yeye aliye juu. Si Kweli MWENYEZI MUNGU Hatetewi wala kupiganiwa ila anataka tuombe na kufuata mAadili mema kwa kumtukuza yeye na kulitangaza vema jina lake. Kwa maana wote waliompokea aliwapa uwezo kuwa WANA WA MUNGU.Tukiyafanya haya tutawapenda adui zetu ampapo ni kitu kikubwa sana linapokuja suala la Amani.Kuchoma makanisa hakuwezi hata siku moja kufanya DINI ikafa wakabaki wao tu bali ni kutengeneza chuki vizazi hadi vizazi. So Naipongeza serikali na majeshi yake katika jambo hili nawaomba liwe endelevu.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Kuchukua tahadhari mapema ni jambo la muhimu zaidi kuliko kusubiri hali iwe mbaya. Nawapongeza JWTZ kwa kuongeza nguvu kwenye kadhia ya jana.

Lakini nina mtazamo tofauti kidogo pale mwandishi aliposema 'kikundi kidogo cha waislamu wachache". Kile hakikuwa kikundi kidogo. Watu wa kuanzia buguruni, kinondoni, magomeni, kariakoo, kigongo chekundu n.k. waliitikia wito wa kushiriki maandamano. Kwa mantiki hiyo huo umati wa watu waliotoka katika maeneo yote hayo usingekuwa mdogo.

Lingekuwa ni kikundi kidogo, waisalamu walio wengi na wenye kupenda haki wangekipinga, lakini kinyume chake ni kwamba hakuna hata kikundi kimoja cha kiislamu kilichopingana na wenzao. Walichofanya ni kukaa kimya, ikimaanisha kwamba waislamu wengi wapo nyuma hao jamaa hata kama si moja kwa moja.
 
wanajeshi walipita tu ( show off) kuonyesha kwamba ulinzi wa nchi upo na hawakushuka kudhibiti vurugu kwani lengo lilikuwa kuonyesha kwamba serikali ina ulinzi wa kutosha ikibidi kufanya hivyo.
 
JWTZ nimewapenda sana yaani walikuwa wanapita katika mitaa wanaangalia kinachoendelea yaani ile kuwepo tu kwenye tukio hawa jamaa zetu walikimbilia kusikojulikana.safiiiii

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
jukumu mojawapo ya JWTZ ni kumlinda Amiri Jeshi Mkuu ambaye pia ni Rais wa Nchi.

kitendo cha waandamanaji kutaka kwenda Ikulu JWTZ walikuwa sahihi kutoka mafichoni na kuja barabarani
 
hivi unataka hizi fujo iendeelee tu? naamin kazi za majesh yote ni kuinda amani ya nchi ndani na kwenye mipaka yake. sasa hakuna kosa lilitokea na afadhali ili wawajibishwe wahuni wote.
 
Umenikumbusha combination ya BWM and Jemedari MAhita.
Hata wakati wa Mrema walikuwa hawahemi!
Sometimes I am wondering if we have a minister of Home Affairs!

hapo penye red eti ndio anaota siku moja na yeye awe RAIS wa TANZANIA.maajabu mengine ya dunia,waislamu waleta vurugu 10 amewashindwa anaota kuwa rais.
 
Wakuu tunagalie suala hili kwa maeneo haya matatu tuone tumefika wapi kabla ya kumlaumu mwamunyange.

1. Unregulated and uncontrolled FREEDOM OF SPEECH AND EXRESSION
Je ni kutokana na kuwa katiba yetu inatupa “uhuru” kupita kiasi? Yaani sheria zinazolinda uhuru huu zina mianya na kutoa nafasi kwa watu kutumia vibaya uhuru tuliopewa kikatiba [kukusanyika, kuabudu na kutoa maoni], kutukana, kufanya vurugu, vurumai, uharibifu na uuaji? Kwa muktadha huu tuangalie kama kweli hizi ni vurugu za kidini zinatokana na kitendo cha mtoto mkristo kukojolea Koran aliyopewa na mtoto mwislamu na kumwambia akiikojolea atabadilika kuwa Nyoka au Panya? Au suala hili limedakwa na baadhi ya watu ambao kwa muda wamekuwa wakitumia uhuru tunaopewa na katiba kuchochea vurugu, lakini hawakuwa na kisingizo cha kutekeleza yale ambayo wamekuwa wakihubiri kwa zadi ya miaka saba sasa?
Tukiangalia kwa undani uhuru huu kwa sasa tunaweza kusema hata teknolojia imetifikisha mahali ambao tuna vyombo kama JF, Radio Maria, Radio Imaan, gazeti za Kandanda kitandani, Msemakweli etc etc etc ambayo mto yoyote anaweza kutoa maoni kupitia vyombo hivyo na yeyote anaweza kusoma maoni, bila kuwa na chombo imara cha kudhibiti yaliyomo. Kuna vehicles zenye nguvu sana zenye uwezo wa kusafirisha maoni kwa muda mfupi na kwa haraka sana, serikali yetu bado haijafanya lolote la maana kushughulikia suala hilo.

Kibaya zaidi “wahuni na majambazi” wamekuwa ni karata nzuri sana kwa baadhi ya vyama na kwa baadhi ya wanasiasa, na kupewa fursa ya kutumia uhuru na vyombo vipya vya kutoa maoni kuchezea amani, umoja, utulivu na muungano wa Tanzania. Kwa hiyo unaona hata wakitoa kauli za kichochezi namna gani serikali inakuwa kimya tu, kana kwamba inawaogopa, hata ra

2. Nasty POLITICAL COMPETITION (ndani ya CCM, CCM vs Upinzani).
Kuna mambo mengi sana yamekuwa yakitokea kipindi hiki ndani ya CCM, makundi matatu au manne yanatafuta nafasi ya kushika dola kwa udi na uvumba, lakini ni bahati mbaya sana makundi hayo hayana kitu cha maana kuwaonesha watanzania, kwanini wanastahili kushika dola. Kwa hiyo inaonesha kuwa ni “power at any cost”. Tumesikia wanaCCM wakiwekeana sumu, waandamizi wakijiengua, wengine wakijiimarisha, wengine wakilalamika ufisadi na “foul play”, wengine wakitoa lugha za ajabu ambazo hawajawahi kuzitoa huko nyuma, na ambazo si desturi yao, yote hayo yanaonesha kuwa kuna mvutano mkali. Lakini kuna wengine wamekuwa kimya sana, kikauli, lakini wana-act. Kuna uwezekano mkubwa kabisa kuwa vurugu za hivi karibuni zilichochewa na mwanasiasa fulani, au kundi fulani la wanasiasa, kwa malengo ya kisiasa kuelekea 2015, au kuweka platform nzuri ya kudhibiti kwa muda wimbi la kukua upinzani.

If you stand from a vintage point [jifanye wewe sio CUF, CDM wala CCM] you can see that there are very clear signs that the incumbent is launching a dire attempt to remain in power in the wake of surging fortunes of the opposition. Visiwani ni kama opinion inaegemea zaidi kwenye upande wa CUF, kwa hiyo karata ya “uislamu” na vurugu za ‘uamsho’ zinaweza kuwa ni kisingizio kizuri cha cha kidivert attention from real issues.
Sidhani kama ni bahati mbaya kwa matukio kutokea bara na visiwani kwa wakati mmoja, ‘waislamu’ wa bara na visiwani kuwa na matatizo tofauti kwa wakati mmoja ni jambo la ajabu kidogo.
Huku bara ni wazi kabisa kuwa serikali imefanya madudu mengi sana kiasi kwamba maisha ya wananchi yamekuwa magumu sana, watu wamepoteza matumaini na kuchanganyikiwa. Ufisadi sasa ni kama unatambuliwa wazi kuwa ni sera inayokubalika kivitendo, na kupingwa kikauli na kimaandishi. Lakini kuwa beneficiary ni lazima uwe kwenye hatamu. Kitu ambacho wananchi wa kawaida na wanaccm na wapinzani hawakitaki, lakini hakiwezi kutoka kwenye Chama.
Kutokana na kuonesha incapability na kuto-deliver kwa wananchi, ni kama kuna haja ya kuwa na justification ya kuwepo madarakani at least kwa sasa, na kufunika aibu ya kuwa ‘hatuja-deliver” na kushindwa ku-deal na real issues (union in tatters, inflation, amani na usalama, no jobs, misongamano barabarani, mishahara duni, umeme, maji, elimu, justice). Kuleta kitu ambacho kitawagawa wananchi na kujiweka katikati yao kutasaidia kujustify uwepo wa serikali. At the end of the day utaona wahusika wakuu wananufaika, na wananchi wa kawaida wote wakristo na waislamu wanaathiriwa.

3. UNYONGE
Kuna kitu kimoja ambacho tunatakiwa tukubaliane, kwamba kuna unyonge mkubwa sana katika jamii yetu. Inawezekana unyonge huu ndio unaowafanya watu wahusike kwenye ujinga kama huu uliotokea. Labda ndio maana Nyerere alikuwa anasema sema tupambane na adui ujinga.
Kuna watu wengi hawajui tatizo lao kubwa ni nini. Inawezekana hata leo ukimuuliza mtu mtaani tatizo lako ni nini unaweza kushangaa jibu. Jaribu kutumia akili kidogo kuangalia ni nini kitakufanya uandamane na kutaka mabadiliko, umaskini au udhalilishaji wa kidini. Kuna baadhi ya watu wanadhani kuwa wakristo hapa Tanzania wako better off kuliko watu wa dini nyingine. Lakini ukiangalia uhalisia unaona kuwa watanzania wote bila kujali dini zao wanaogelea kwenye dimbwi moja.

Will there be any change in the content if a person urinates on the Quran or on the bible for that matter? au bado Tanzania kuna ujinga kama wa watu ambao hawana shule hata kidogo wa Afghanistan? Ukiangalia kwa undani unaweza kuona kuwa hii ajenda ni kubwa kuliko kukojolea msahafu. Wajanja wamecapitalize kwenye unyonge wa watanzania. Unyonge mwingine ni kuwa bado tunashindwa kujua nani ni Sheikh hapa Tanzania na nani si Sheikh, bado hakuna vigezo wazi vya nani ni sheikh na nani si sheikh, na nani mwakilishi halali wa waislamu na anayeweza kuwasemea waislamu
 
jukumu la ulinzi na usalama linaweza fanywa na raia yeyote yule, LAKINI, kiprotocol ndani ya mfumo rasmi, aliyasema mdau hapa ni sahii, shughuli hii ilikuwa ni kufanywa na Police na Sio JWTZ, Ila hatuna haja ya kujadili au kulaumu sana hili. Tuangalie kusudio kuu muhimu ambalo ni "AMANI" ya TANZANIA

Je, Jukumu la kufanya fujo na vurugu na maandamano ni jukumu la Waislamu?
 
pegine kwa wasiojua ni kwamba,ukiitazama sare za JWTZ zina rangi kadhaa,mojawapo ni kama ya sare za polisi na FFU' hivyo kuna kipindi unaweza kuwaona FFU kumbe ni JW,kwa hali ya jana na kwa kuzingatia tuko pwani nadhani inteligesia ilionesha kunauwezekano kuwepo kwa vikundi vingine kutoka nje ya nchi,mfano ni dhahiri kuwa uamsho tayari wako kwa wingi bara!!
 
Udini umepandwa na CHADEMA, kupitia kwa Padri Slaa, mchungaji Msigwa n.k!

Hivi kiongozi akiitwa, Alhaji Mwinyi, Alhaji Mkulo, Alhaji Makamba ni kuonyesha kwamba katumwa na dini.

Rais Msataafu amekuwa anatoa hotba misikitini jambo ambalo ni jema utasema Rais anapandikiza udini kwani aliwahi kuwa Rais.
 
Ulipouliza nani alikaimu uraisi wakati jk anashangaa kasri oman,? Jibu ni kwamba hakuwepo wa kukaimu kwa sababu hakukuwa na haja, nchi inajiendesha yenyewe AUTO-PILOT mode

Jaribu kuchimba kwa undani utajua ni nini kimempeleka Oman, jaribu ku-connect na kinachotokea sasa.
 
wewe huna mawazo mazuri ,wakiwaua si wanaweza kuwaibukia church waka fanya the same...
Hapa itafutwe solution.
Wewe kama una hamu ya kuua waislam,fanya wewe usisakizie wengine...COWARD.
Church hawawezi kuingia ni nyumba inayolindwa na MWENYEZI MUNGU. Mi nafikili sg yupo sahihi maana c kawaida kwa mtu anayemwabudu MUNGU kufanya vurugu za kuua binadamu mwenzie.
 
Back
Top Bottom