Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

Askari wetu hawafuati hizi sheria sio kwa kosa lao, hapa ntailaumu serikali, maaskari wanapata mafunzo ya ovyo, wanarush~rush tu then wanaingia kazini, wangekua wanafundishwa vizuri hizi sheria na kuzikazia ili umuhimu wake uonekane wangezifata, tena walitakiwa wachukuliwe hatua za kisheria kama wataenda kinyume, maaskari wangezifata hizi kirahisi tu. Watu nao inabidi watangaziwe hata kwenye tv mara kwa mara wajue, na iwepo institution ya kuwatetea wananchi ambao wamekua victims wa askari wasiofuata sheria.

Serikali yetu kama sasa hivi inakaribia kua ka ya kidikteta hili haliwezekani, kauli za "kamata kwanza tutafix baadaye" hizi sheria zitabaki kwenye karatasi tu.
Police force(force=nguvu), jiandae kukumbana na nguvu pale inapobidi... Hakuna namna
 
Polisi akikuambia Kaa chini kwann tu usikae, kwani ukikaa unakufa?
Sasa virungu na vya nini? Lazima ajitambulishe na asema kwanini anataka kunikama na kwa kosa gani. Mambo mbengine haya hitaji nguvu ni kumwambia tu mtu aende mwenyewe kituoni anahitajika lakini wao ni nguvu tu!
 
Police force(force=nguvu), jiandae kukumbana na nguvu pale inapobidi... Hakuna namna

Hii ideology ndio maana hatuendelei, nguvu pale inapobidi sijakataa, ila situations za kutumia nguvu ni kama mtu ana silaha, ila kukamata watu ovyo na kuanza kuwapiga huku bado hawajahukumiwa its stupid na mtu mwenye akili mbovu ndio ataona ni sawa.
 
Weka na option zake kuna watu wanakalili hivyo hivyo ulivyoandika kwa mfana issue ya masaa ishirini na nne kama upelelezi haujakamilika inakuaje na kama ukikamatwa ijumaa kuu inakuaje maana kuna siku nne za mapumziko na watu wanakalilo tu 24!!!!&
 
Hii ideology ndio maana hatuendelei, nguvu pale inapobidi sijakataa, ila situations za kutumia nguvu ni kama mtu ana silaha, ila kukamata watu ovyo na kuanza kuwapiga huku bado hawajahukumiwa its stupid na mtu mwenye akili mbovu ndio ataona ni sawa.
Msiwafanganye Raia wema na Ideology zenu za kale nipe maana ya kituo cha USALAMA ungekuwa dereva aliyeleta ajali au uliyesingiziwa uhalifu km mgoni au mwizi kumbe unasingiziwa ndipo ungeona Kituoni POLISI ni peponi
Bila Traffic gari ndogo na pikipiki zisingekuwepo
Bila Fraud Officer huko makazini usingebaki kitu
Hakuna watu wabaya km wanasheria Advocate maana wanaomba / wanadai hela kuliko POLISI

Sent from my TECNO-Y3+ using JamiiForums mobile app
 
Msiwafanganye Raia wema na Ideology zenu za kale nipe maana ya kituo cha USALAMA ungekuwa dereva aliyeleta ajali au uliyesingiziwa uhalifu km mgoni au mwizi kumbe unasingiziwa ndipo ungeona Kituoni POLISI ni peponi
Bila Traffic gari ndogo na pikipiki zisingekuwepo
Bila Fraud Officer huko makazini usingebaki kitu
Hakuna watu wabaya km wanasheria Advocate maana wanaomba / wanadai hela kuliko POLISI

Sent from my TECNO-Y3+ using JamiiForums mobile app

Mkuu we polisi nini? Kama hujawahi experience kitu tulia, sio kila unayeongea naye JF ni hooligan, naona una shida na wanasheria, hapa tunaongelea kitu tofauti usigeuze mada
 
  • Raia ana haki ya kumwomba askari ajitambulishe kwako.
    • Mwulize jina lake
    • Mwulize namba yake ya uaskari
  • Raia ana haki ya kujulishwa kwanini anatiliwa mashaka ama kukamatwa.
  • Raia ana haki ya kuwajulisha ndugu, jamaa ama sehemu anakofanyia kazi kwamba ama amekamatwa na polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
  • Raia ana haki ya kuomba na kupewa dhamana wakati akiwa kituo cha polisi ama Taasisi ya kuzuia rushwa.
    • Hutakiwi kutoa fedha kama dhamana uwapo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa, isipokuwa maelezo utakayoandika.
  • Raia ana haki ya kuwaeleza polisi ama Maafisa wa Kuzuia Rushwa kwamba lolote atakalosema linaweza kutumiwa kama ushahidi mahakamani, na asiburuzwe kuandika tu.
  • Raia ana haki ya kuomba Wakili wake awepo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa wakati anatoa maelezo yake.
  • Raia ana haki ya kuyasoma kabla ya kutia sahihi yake.
  • Raia ana haki ya kudai risiti ya orodha ya vitu vyake/fedha zake alizozitoa ama kukabidhi kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
  • Raia kama ni mwanamke ana haki ya kupekuliwa na polisi wa kike, na iwapo hakuna polisi mwanamke, basi mwanamke yeyote na vile vile kwa mwanamume.
  • Raia ana haki ya kufikishwa mahakamani katika muda usiozidi saa 24 tangu alipokamatwa na kufikishwa kituo cha polisi.

Mimi naombeni tu mnisaidie zinapatikana wapi kwenye katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Mkuu we polisi nini? Kama hujawahi experience kitu tulia, sio kila unayeongea naye JF ni hooligan, naona una shida na wanasheria, hapa tunaongelea kitu tofauti usigeuze mada
Kwani ww ni Moderator
Mnawadanganya raia kujifanya maBushlawyer
Msidhani kila muelewa atauendekeza uongo wenu kituoni ni pahali pa USALAMA WA RAIA Duniani pote hakuna sehemu salama palipochagululiwa km hapo kabla ya kufika Mahakamani

Sent from my TECNO-Y3+ using JamiiForums mobile app
 
  • Raia ana haki ya kumwomba askari ajitambulishe kwako.
    • Mwulize jina lake
    • Mwulize namba yake ya uaskari
  • Raia ana haki ya kujulishwa kwanini anatiliwa mashaka ama kukamatwa.
  • Raia ana haki ya kuwajulisha ndugu, jamaa ama sehemu anakofanyia kazi kwamba ama amekamatwa na polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
  • Raia ana haki ya kuomba na kupewa dhamana wakati akiwa kituo cha polisi ama Taasisi ya kuzuia rushwa.
    • Hutakiwi kutoa fedha kama dhamana uwapo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa, isipokuwa maelezo utakayoandika.
  • Raia ana haki ya kuwaeleza polisi ama Maafisa wa Kuzuia Rushwa kwamba lolote atakalosema linaweza kutumiwa kama ushahidi mahakamani, na asiburuzwe kuandika tu.
  • Raia ana haki ya kuomba Wakili wake awepo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa wakati anatoa maelezo yake.
  • Raia ana haki ya kuyasoma kabla ya kutia sahihi yake.
  • Raia ana haki ya kudai risiti ya orodha ya vitu vyake/fedha zake alizozitoa ama kukabidhi kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
  • Raia kama ni mwanamke ana haki ya kupekuliwa na polisi wa kike, na iwapo hakuna polisi mwanamke, basi mwanamke yeyote na vile vile kwa mwanamume.
  • Raia ana haki ya kufikishwa mahakamani katika muda usiozidi saa 24 tangu alipokamatwa na kufikishwa kituo cha polisi.
mkuu asante sana kwa thread nzuri kama hii. naomba pia nifahamu ni hatua gani ambazo mtuhumiwa anaweza kuzichukua endapo askari polisi atakiuka moja kati ya taratibu hizo..........mtuhumiwa anapaswa kumchukulia polisi hatua gani???????
 
  • Raia ana haki ya kumwomba askari ajitambulishe kwako.
    • Mwulize jina lake
    • Mwulize namba yake ya uaskari
  • Raia ana haki ya kujulishwa kwanini anatiliwa mashaka ama kukamatwa.
  • Raia ana haki ya kuwajulisha ndugu, jamaa ama sehemu anakofanyia kazi kwamba ama amekamatwa na polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
  • Raia ana haki ya kuomba na kupewa dhamana wakati akiwa kituo cha polisi ama Taasisi ya kuzuia rushwa.
    • Hutakiwi kutoa fedha kama dhamana uwapo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa, isipokuwa maelezo utakayoandika.
  • Raia ana haki ya kuwaeleza polisi ama Maafisa wa Kuzuia Rushwa kwamba lolote atakalosema linaweza kutumiwa kama ushahidi mahakamani, na asiburuzwe kuandika tu.
  • Raia ana haki ya kuomba Wakili wake awepo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa wakati anatoa maelezo yake.
  • Raia ana haki ya kuyasoma kabla ya kutia sahihi yake.
  • Raia ana haki ya kudai risiti ya orodha ya vitu vyake/fedha zake alizozitoa ama kukabidhi kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
  • Raia kama ni mwanamke ana haki ya kupekuliwa na polisi wa kike, na iwapo hakuna polisi mwanamke, basi mwanamke yeyote na vile vile kwa mwanamume.
  • Raia ana haki ya kufikishwa mahakamani katika muda usiozidi saa 24 tangu alipokamatwa na kufikishwa kituo cha polisi.
**NJE YA MADA KIDOGO**
Kutokana na kuongezeka kwa idadi kubwa ya wagonjwa walio katika hali mbaya kwenye hospitali mbalimbali hapa nchini kutokana na kuugua magonjwa yasiyokuwa na tiba na wao kuendelea kuteseka vitandani huku watu wasijue la kufanya, je, muda umefika kwa tanzania kuwa na utaratibu wa "kuua kwa huruma" kama ambavyo nchi za wazungu zinafanya? naomba maoni yako kwenye mjadala huu:

click here: Should "Mercy killing" be practiced in Tanzania?
 
Issue hapa Je,Askari Polisi wanajua mpaka yao ya kazi?Je wanajua haki za RAIA na haki za Mtuhumiwa? Kama wanajua basi kuna mahali panatatizo ni wakati wa RAIA kulishtaki jeshi la polisi kwa kutofuata taratibu na mpaka ya kazi yake.Kama.hawajui basi ni wakati wa serikali kukielimisha jeshi kuanzia wa ngazi ya chini hadi juu.
Pia je wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya wanajua mipaka yao na mpaka ya jeshi la polisi kwenye utendaji wa Polisi?Kama wanajua basi wanafanya makusudi kutumia nafasi zao kuumiza RAIA bila sababu.Kama hawajui basi ni Lazima Serikali ichukue hukumu la kuwaelimisha wasitie orders zinazopelekea kupiga au kujeruhi RAIA bila sababu zozote kwani mwenye hati ya Kuhukumu ni Mahakama tu
 
Hizo haki na nyingine nyingi tu Zinavunjwa kila leo na polisi. Ama kwa makusudi ama kwa wao polisi kudhani wako juu ya sheria. Kwa nchi kama Tanzania Polisi hujifanya mahakimu. nitajie aliywahi kulalmikia kuhusu unyanyasaji wa polisi na akashinda! sana sana polisi wakibaini mwenzao kacheza Faul basi ni quick transfer! Hayo labda ughaibuni. Maana Polisi waweza kuwakoromea mpaka wakaingia mitini!! as afar as wakigundua kuwa kuwa wajua haki zako. Jifanye kujua hakia zako katika vituo vya Polisi Tanzania uone vijana wa Said Mwema watakavyokurarua na virungu!!
Kaka umeongea ukweli ila wachache tunaujua big up.
 
tumshukuru bwana Mpinga kwa kuweka misingi ya upolisi hasa wa barabarani. maana akikuonea kama una uhakika komaa hata mwende kituoni na dmand kuonana na responsible officer. sema sisi raia huwa hatuna muda ni quick fix ya 5,000 ama 10,000 au 30,000 ya receipt!!
 
WanaJF, kuna jambo huwa linaniumiza kichwa tena kwa nchi hii ya Tanzania.

Polisi unapomueleza kisheria au kujua wajibu wako kisheria hapo ndipo adui yako.

Ukimtajia wajibu wake au kapindisha basi jibu lake "unijifanya unajua sheria".
 
wana jf kuna jambo huwa lina niumiza kichwa tena kwa nchi hii ya tanzania.
polisi hunapo mueleza kisheria au kujua wajibu wako kisheria hapo ndipo adui yako.
ukimtajia wajibu wake au kapindisha basi jibu lake "unijifanya unajua sheria".
wana jf...?
Nini kifanyike
 



Sio kila anayekamatwa na Jeshi la Polisi ni muhalifu inaweza kuwa ni raia mwema tu ambaye ameshukiwa na polisi ambao wapo kwenye uchunguzi wao, au vinginevyo na hata ukiwa ni mhalifu pia hizi ndizo haki za Raia akiwa akikamatwa na jeshi la Polisi .

Raia ana haki ya kujulishwa kwanini anatiliwa mashaka ama kukamatwa.
Raia ana haki ya kuwajulisha ndugu, jamaa ama sehemu anakofanyia kazi kwamba ama amekamatwa na polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
Raia ana haki ya kuomba na kupewa dhamana wakati akiwa kituo cha polisi ama Taasisi ya kuzuia rushwa.
Raia ana haki ya kumwomba askari ajitambulishe kwako.

Muulize jina lake
Muulize namba yake ya uaskari
Hutakiwi kutoa fedha kama dhamana uwapo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa, isipokuwa maelezo utakayoandika.
Raia ana haki ya kuwaeleza polisi ama Maafisa wa Kuzuia Rushwa kwamba lolote atakalosema linaweza kutumiwa kama ushahidi mahakamani, na asiburuzwe kuandika tu.

Raia ana haki ya kuomba Wakili wake awepo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa wakati anatoa maelezo yake.

Raia ana haki ya kusoma maelezo kabla ya kutia sahihi yake.
Raia ana haki ya kudai risiti ya orodha ya vitu vyake/fedha zake alizozitoa ama kukabidhi kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
Raia kama ni mwanamke ana haki ya kupekuliwa na polisi wa kike, na iwapo hakuna polisi mwanamke, basi mwanamke yeyote na vile vile kwa mwanamume.
Raia ana haki ya kufikishwa mahakamani katika muda usiozidi saa 24 tangu alipokamatwa na kufikishwa kituo cha polisi.

Iwapo askari polisi ataamua kumpekua mtuhumiwa, mtuhumiwa ana haki ya kumpekua askari polisi kabla ya kupekuliwa yeye mwenyewe
Pia, askari polisi hawana haki ya kuingia kwenye gari, nyumba au ofisi ya mtu wanayemtuhumu, kwa madhumuni ya kufanya upekuzi, pasi na kuwapo kwa (a) hati ya upekuzi ambayo hutolewa mahakamani, (b) mashahidi wanaotambulika rasmi kisheria, kama vile, mwenyekiti/mjumbe wa serikali ya mtaa au mwenyekiti wa nyumba kumi kumi (iwapo mfumo huo unatumika), au (c) jirani wa myu anayetuhumiwa
Aidha, mtuhumiwa hatakamatwa au kupekuliwa na askari polisi baada ya saa 12.30 jioni au kabla ya saa 12.30 alfajiri, kwa mujibu wa Mwendendo wa Makosa ya Jinai (Penal Code Act), isipokuwa tu, kama kutakuwa na ushahidi wa kutosha kwamba, kumpekua mtuhumiwa kabla ya saa 12.30 alfajiri au baada ya saa 12.30 jioni kunaweza kuleta madhara kwa askari polisi, mashahidi au watu wengine wowote wale
 
107 Reactions
Reply
Back
Top Bottom