Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

Bikra

Member
May 13, 2009
55
112
  • Raia ana haki ya kumwomba askari ajitambulishe kwako.
    • Mwulize jina lake
    • Mwulize namba yake ya uaskari
  • Raia ana haki ya kujulishwa kwanini anatiliwa mashaka ama kukamatwa.
  • Raia ana haki ya kuwajulisha ndugu, jamaa ama sehemu anakofanyia kazi kwamba ama amekamatwa na polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
  • Raia ana haki ya kuomba na kupewa dhamana wakati akiwa kituo cha polisi ama Taasisi ya kuzuia rushwa.
    • Hutakiwi kutoa fedha kama dhamana uwapo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa, isipokuwa maelezo utakayoandika.
  • Raia ana haki ya kufikishwa mahakamani katika muda usiozidi saa 24 tangu alipokamatwa na kufikishwa kituo cha polisi.
-----

Nyongeza kutoka kwa MwanaHaki
  • Iwapo askari polisi ataamua kumpekua mtuhumiwa, mtuhumiwa ana haki ya kumpekua askari polisi KABLA ya kupekuliwa yeye mwenyewe
  • Pia, askari polisi hawana haki ya kuingia kwenye gari, nyumba au ofisi ya mtu wanayemtuhumu, kwa madhumuni ya kufanya upekuzi, pasi na kuwapo kwa (a) hati ya upekuzi ambayo hutolewa mahakamani, (b) mashahidi wanaotambulika rasmi kisheria, kama vile, mwenyekiti/mjumbe wa serikali ya mtaa au mwenyekiti wa nyumba kumi kumi (iwapo mfumo huo unatumika), au (c) jirani wa myu anayetuhumiwa
  • Aidha, mtuhumiwa hatakamatwa au kupekuliwa na askari polisi baada ya saa 12.30 jioni au kabla ya saa 12.30 alfajiri, kwa mujibu wa Mwendendo wa Makosa ya Jinai (Penal Code Act), isipokuwa tu, kama kutakuwa na ushahidi wa kutosha kwamba, kumpekua mtuhumiwa kabla ya saa 12.30 alfajiri au baada ya saa 12.30 jioni kunaweza kuleta madhara kwa askari polisi, mashahidi au watu wengine wowote wale
Nikikumbuka mengine nitawapa mkanda.



=============================

Haki zako za Kisheria unapokamatwa na Polisi

Raia unayo haki ya:-

*Kumwomba Askari ajitambulishe kwako....
-Muulize Jina lake.
-Muulize namba yake ya Uaskari.
*Kujulishwa ni kwa nini unatiliwa mashaka au kukamatwa.
*Kuwajulisha ndugu, jamaa na marafiki ama sehemu unakofanyia kazi kwamba ama umekamatwa na Polisi au TAKUKURU.
*Kuomba na Kupewa dhamana wakati ukiwa Kituo cha Polisi ama TAKUKURU.
*Hutakiwi kutoa Fedha kama Dhamana uwapo Kituo cha Polisi ama TAKUKURU, isipokuwa maelezo utakayoyatoa na kuandikwa Kituoni hapo.
*Kuwaeleza Polisi ama Maafisa wa TAKUKURU kwamba lolote utakalolisema linaweza kutumika kama ushahidi mahakamani na usiburuzwe wakati wa kuyatoa maelezo hayo.
*Kuomba wakili wako au mtu wa karibu yako utakayemchagua ili awepo Kituo cha Polisi ama Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa wakati unatoa maelezo yako.
*Haki ya kuyasoma maelezo yako kabla ya kutia sahihi katika maelezo hayo.
*Kudai risiti ya Orodha ya vitu vyako/fedha zako ulizotoa ama kukabidhi Kituo cha Polisi ama TAKUKURU.
*Haki ya kufikishwa mahakamani katika muda usiozidi Saa 24 tangu alipokamatwa na kufikishwa Kituoni.
Haki za Raia Kupekuliwa
*Mtuhumiwa anayo haki ya kumpekua Polisi kabla ya yeye kupekuliwa na Polisi huyo.
*Raia kama ni Mwanamke, anayo haki ya kupekuliwa na Askari wa Kike, na iwapo Askari wa Kike hayupo, basi Mwanamke yeyote anaweza kumfanyia upekuzi, vile vile kwa Mwanaume.
*Askari hawana haki ya kuingia kwenye Gari, Nyumba au Ofisi ya Mtu wanayemtuhumu, kwa madhumuni y kufanya upekuzi bila kuwa na:
(a) Hati ya Upekuzi ambayo hutolewa Mahakamani.
(b) Mashahidi wanaotambulika rasmi Kisheria, kama vile Mwenyekiti/Mjumbe wa Serikali ya Mtaa au Kijiji husika.
(c) Jirani wa Mtu anayetuhumiwa.

Aidha, Mtuhumiwa hatakamatwa au kupekuliwa na Askari Polisi baada ya Saa 12:30 Jioni au kabla ya Saa 12:30 Alfajiri, kwa mujibu wa makosa ya Jinai (Penal Code Act).

Isipokuwa tu, kama kutakuwa na ushahidi wa kutosha kwamba kumpekua Mtuhumiwa kabla ya Saa 12:30 Alfajiri au baada ya Saa 12:30 Jioni kunaweza kuleta madhara kwa Askari Polisi, Mashahidi au Watu wengine wowote wale.


./Mwana wa Haki

Zaidi soma=>Sheria :Zitambue haki zako unapokamatwa na Polisi

Zifahamu sheria pale unapokamatwa na polisi
 
Last edited by a moderator:
Hizo haki na nyingine nyingi tu Zinavunjwa kila leo na polisi. Ama kwa makusudi ama kwa wao polisi kudhani wako juu ya sheria. Kwa nchi kama Tanzania Polisi hujifanya mahakimu. nitajie aliywahi kulalmikia kuhusu unyanyasaji wa polisi na akashinda! sana sana polisi wakibaini mwenzao kacheza Faul basi ni quick transfer! Hayo labda ughaibuni. Maana Polisi waweza kuwakoromea mpaka wakaingia mitini!! as afar as wakigundua kuwa kuwa wajua haki zako. Jifanye kujua hakia zako katika vituo vya Polisi Tanzania uone vijana wa Said Mwema watakavyokurarua na virungu!!
 
Polisi na haki za raia...mh. Hivi wale jamaa waliovamiwa na kushambuliwa na polisi pale Kinondoni kwa madai kuwa majambazi sugu issue yao illishia wapi? Sidhani kama kuna chochote kilichofanyika. Mwenye fununu atudokeze tafadhali.
 
Umesahau hizi:

  • Iwapo askari polisi ataamua kumpekua mtuhumiwa, mtuhumiwa ana haki ya kumpekua askari polisi KABLA ya kupekuliwa yeye mwenyewe
  • Pia, askari polisi hawana haki ya kuingia kwenye gari, nyumba au ofisi ya mtu wanayemtuhumu, kwa madhumuni ya kufanya upekuzi, pasi na kuwapo kwa (a) hati ya upekuzi ambayo hutolewa mahakamani, (b) mashahidi wanaotambulika rasmi kisheria, kama vile, mwenyekiti/mjumbe wa serikali ya mtaa au mwenyekiti wa nyumba kumi kumi (iwapo mfumo huo unatumika), au (c) jirani wa myu anayetuhumiwa
  • Aidha, mtuhumiwa hatakamatwa au kupekuliwa na askari polisi baada ya saa 12.30 jioni au kabla ya saa 12.30 alfajiri, kwa mujibu wa Mwendendo wa Makosa ya Jinai (Penal Code Act), isipokuwa tu, kama kutakuwa na ushahidi wa kutosha kwamba, kumpekua mtuhumiwa kabla ya saa 12.30 alfajiri au baada ya saa 12.30 jioni kunaweza kuleta madhara kwa askari polisi, mashahidi au watu wengine wowote wale
Nikikumbuka mengine nitawapa mkanda.

./Mwana wa Haki
 
  • Aidha, mtuhumiwa hatakamatwa au kupekuliwa na askari polisi baada ya saa 12.30 jioni au kabla ya saa 12.30 alfajiri, kwa mujibu wa Mwendendo wa Makosa ya Jinai (Penal Code Act), isipokuwa tu, kama kutakuwa na ushahidi wa kutosha kwamba, kumpekua mtuhumiwa kabla ya saa 12.30 alfajiri au baada ya saa 12.30 jioni kunaweza kuleta madhara kwa askari polisi, mashahidi au watu wengine wowote wale

Kwa hiyo jizi likivamia usiku wa manane inabidi kisheria tusubiri kuche ndio tiulikimbize kulikamata na kulisachi?
 
Aidha, mtuhumiwa hatakamatwa au kupekuliwa na askari polisi baada ya saa 12.30 jioni au kabla ya saa 12.30 alfajiri, kwa mujibu wa Mwendendo wa Makosa ya Jinai (Penal Code Act), isipokuwa tu, kama kutakuwa na ushahidi wa kutosha kwamba, kumpekua mtuhumiwa kabla ya saa 12.30 alfajiri au baada ya saa 12.30 jioni kunaweza kuleta madhara kwa askari polisi, mashahidi au watu wengine wowote wale

Hivi muandishi wa hiki kifungu amedhamiria kuandika kilichoandikwa ama la?

Kimsingi amesema mtu asikamatwe au kupekuliwa na polisi baada ya saa 12.30 jioni na kabla ya saa 12.30 alfajiri ila tu pale kutakapokuwa na ushahidi wa kutosha kwamba kumpekua au kumkamata baada ya saa 12.30 jioni na kabla ya saa 12.30 alfajiri kunaweza kuleta madhara.

Kwa hiyo asipekuliwe wala kukamatwa katika muda huo mpaka pale kutakapokuwa na ushahidi kwamba kutakuwa na madhara, tunatafuta madhara kwa nguvu, nani kaandika utumbo huu?
 
Hizo haki na nyingine nyingi tu zinavunjwa kila leo na polisi. Ama kwa makusudi ama kwa wao polisi kudhani wako juu ya sheria.

Kwa nchi kama Tanzania Polisi hujifanya mahakimu, nitajie aliyewahi kulalamikia kuhusu unyanyasaji wa polisi na akashinda! Sana sana polisi wakibaini mwenzao kacheza faulo basi ni quick transfer!

Hayo labda ughaibuni. Maana Polisi waweza kuwakoromea mpaka wakaingia mitini as far as wakigundua kuwa wajua haki zako.

Jifanye kujua hakia zako katika vituo vya Polisi Tanzania uone vijana watakavyokurarua na virungu

Acha kulalamika, chukua hatua sasa.

Umekwishajulishwa HAKI zako sasa ni WAJIBU wako wewe kuhakikisha unatumia haki hizo. Mimi binafsi ninazifahamu haki hizo na huzitumia wakati wote inapobidi. Ukijiamini na kuonesha kuwa unatambua haki zako wale Polisi wasiokuwa waaminifu hawezi kukutendea kinyume na taratibu za kazi yao.

Hili bandiko ni zuri sana kwani ni moja katika mambo mengi ambayo raia hawayafamu au hawataki kuyafahamu.
 
  • Raia ana haki ya kumwomba askari ajitambulishe kwako.
    • Mwulize jina lake
    • Mwulize namba yake ya uaskari
  • Raia ana haki ya kujulishwa kwanini anatiliwa mashaka ama kukamatwa.
  • Raia ana haki ya kuwajulisha ndugu, jamaa ama sehemu anakofanyia kazi kwamba ama amekamatwa na polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
  • Raia ana haki ya kuomba na kupewa dhamana wakati akiwa kituo cha polisi ama Taasisi ya kuzuia rushwa.
    • Hutakiwi kutoa fedha kama dhamana uwapo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa, isipokuwa maelezo utakayoandika.
  • Raia ana haki ya kufikishwa mahakamani katika muda usiozidi saa 24 tangu alipokamatwa na kufikishwa kituo cha polisi.


Kuna sheria au sababu zinazoweza kuondoa haki au ku-overrule sheria moja kwa nyingine. Ningependa kujua ni katika mazingira gapi hilo linaweza kutokea.
 
Mbona vihaki vyenyewe vichache hivi(si haba hata hivyo)!! Vitakidhi haja dhidi ya uonevu na manyanyaso tunayopata kutoka kwa polisi na wenye mamlaka? Na kama polisi akivunja haki hizi nichukue hatua gani. UELEWA WA SHERIA KWETU WA TZ NI TATIZO KUBWA SAAANA.
 
Binafsi nashukuru kwa elimu hii muhimu
ingawa inabidi kuipeleka na vijijini kwa sababu nako uko wako gizani kabisa polisi wanakula pesa za wananchi kama nini kwa wananchi kutokujua wajibu wao
 
Uko sawa kabisa mkuu;

Lakini tatizo ni kwamba je huyo(hao) maaskari wa kibongo watakupa mda wa ww kumuuliza hayo maswali? na ni wangapi wanasota kwenye vituo vya polisi zaidi ya wiki bila kwenda mahakamani mpaka wengine wanapewa cheo cha ubalozi?

Nadhani muda umewadia kwa askari wetu kupata lessons freequently kuhusu haki za raia na limitation za haki zao maana raia wengi wasokuwa na hatia huishia kupata adha ya kipondo heavy tena ukijidai unajua sheria au una confident ndo kabisa wanakutoa wenge.

Lakini pia swala la mahabusi kusota bila sheria kufata mkondo wake inavyostahili ni jipu jingine lililosahaulika, nadhani mlisikia last time kule Arusha mahabusu walivyolalama mpaka wakakataa kushuka kwenye karandinga.

Anyway, ni maoni yangu tuu...
 
Nashukuru kwa mwanga wa kisheria niloupata kupitia JF kwa kweli tuliowengi atujui haki zetu na ata police wengi awajui sheria kwann nasema hivyo police waliwaikuja kunikamata ofisini kwangu kinguvu bila ya rb wala restwarant nilipouliza nimefanya kosa gani naambiwa utajua ukokituoni ukifika nilopojaribu kuwambiaa wanitajie kituo gani niende mwenyewe kabla sijamaliza nimevutwa kinguvu nje wakanipeleka kituoni nilijisikia vbaya kweli. ila leo nimepata mwanga zaidi itumu JF yetu
 
hapana haimaanishi hata kidogo kwamba mtuhumiwa akifanya kosa baada ya sdas kumi na mbili na nusu ina maana kwamba ni absolute,that is the general rule which bears some exception,ndo maana kifungu hicho kina proviso(exception) kwamba katika mazingira fulani fulani,that kind of rule can be waived to pave the way to justice.
 
nashukuru kwa mwanga wa kisheria niloupata kupitia JF kwa kweli tuliowengi atujui haki zetu na ata police wengi awajui sheria kwann nasema hivyo police waliwaikuja kunikamata ofisini kwangu kinguvu bila ya rb wala restwarant nilipouliza nimefanya kosa gani naambiwa utajua ukokituoni ukifika nilopojaribu kuwambiaa wanitajie kituo gani niende mwenyewe kabla sijamaliza nimevutwa kinguvu nje wakanipeleka kituoni nilijisikia vbaya kweli. ila leo nimepata mwanga zaidi itumu JF yetu
Umeeleza hali halisi ya ukamataji wao na hata baada ya kujua haki zako hizo bado wanaweza wakatenda kama kawaida yao na ubishi wwt wa kujua haki zako ujue virungu vitautenda mwili wako bila simile kwa kisingizio cha TUMIA NGUVU KIASI KUFANIKISHA UKAMATAJI ENDAPO MTUHUMIWA ANAGOMA KUKAMATWA. Hicho ni kifungu ndani POLICE GEN. ORDER Kinachowapa jeuri ya kututenda.

Kumbuka ukamatwaji wa MURO silaha nzito za kivita utadhani jambazi MAFISADI ah ah kwa raha zao haki itoke wapi bwana kwa kapuku
 
Umeeleza hali halisi ya ukamataji wao na hata baada ya kujua haki zako hizo bado wanaweza wakatenda kama kawaida yao na ubishi wwt wa kujua haki zako ujue virungu vitautenda mwili wako bila simile kwa kisingizio cha TUMIA NGUVU KIASI KUFANIKISHA UKAMATAJI ENDAPO MTUHUMIWA ANAGOMA KUKAMATWA. Hicho ni kifungu ndani POLICE GEN. ORDER Kinachowapa jeuri ya kututenda. Kumbuka ukamatwaji wa MURO silaha nzito za kivita utadhani jambazi MAFISADI ah ah kwa raha zao haki itoke wapi bwana kwa kapuku

kama hivyo ndivyo kwanini waweke sheria ambazo awazitekelezi jamani so tutaendelea kuburuzwa tu au ila mm nakataa kuburuzwa tena wataniforce na ukweli nitawaeleza tu
 
107 Reactions
Reply
Back
Top Bottom