JK: Vumilieni shida




Hitimisho, Mheshimiwa Spika,

Waheshimiwa Wabunge:

nimesema Mengi. Kwa Leo Inatosha. Ninamalizia Kwa kuwahakikishieni Kuwa Nafahamu Vizuri Sasa Ukubwa Wa Heshima Na Uzito Wa Majukumu Niliyokabidhiwa Na Watanzania Wenzangu. Ninafahamu Matarajio Ya Chama Changu, Chama Cha Mapinduzi. Nitaongoza Kwa Dhati Utekelezaji Wa Ahadi Zetu Kwa Wananchi, Na Kwa Dunia. ninayajua Matarajio Ya Watanzania Wenzangu Walipoitikia Wito Wa Ari Mpya, Nguvu Mpya Na Kasi Mpya. Ninayajua Matarajio Ya Nchi Jirani, Bara La Afrika Na Dunia Kwa Awamu Ya Nne Ya Uongozi Wa Taifa Letu. Ninajua Wahisani Wetu Na Wawekezaji, Wa Ndani Na Nje, Wananisikiliza Kwa Makini, Wakitaka Kujiridhisha Iwapo Nitavijaza viatu Alivyoniachia Rais Wetu Mpendwa Wa Awamu Ya Tatu, Benjamin William Mkapa. Nitajitahidi Ingawa Ni Vikubwa Kwangu.

Kwenu Nyote, Na Kwao Wote, Naahidi Kwa Msaada Wa Mwenyezi Mungu, Na Kwa Ushirikiano Na Bunge Hili Na Wananchi Kwa Ujumla, kuwa Naweza Kutimiza Matarajio Ya Kila Mmoja. Tanzania Yenye Neema Tele Inawezekana. Maisha Bora Kwa Kila Mtanzania Yanawezekana. Kila Mmoja Wetu Atimize Wajibu Wake.

Mungu Ibariki Afrika. Mungu Ibariki Tanzania.

Ahsanteni Kwa Kunisikiliza.

na Hapa Ndipo Lilipokuwa Hitimisho La Sanaa,
 
Kauli ya Kikwete moto

na
Kulwa Karedia na Sauli Giliard
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

SIKU moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kutoa kauli ya kuwataka Watanzania kuvumilia kutokana na hali ngumu ya maisha, baadhi ya wananchi, wanasiasa na wasomi wamesema kauli hiyo imewakatisha tamaa.

Wakizungumza na Tanzania Daima kwa nyakati tofauti jana mjini Dar es Salaam, wananchi hao walisema hali hiyo imeonyesha wazi jinsi Rais Kikwete alivyoshindwa kuitawala nchi kwa kuwabebesha mzigo mzito walalahoi.

Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Wilfred Lwakatare, alisema Rais Kikwete ametoa kauli hiyo kwa nia ya kutafuta huruma kutoka kwa wananchi baada ya kuona uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 umekaribia.

“Rais ametoa kauli hiyo akiwa bado ana muda mfupi kukaribia uchaguzi wa serikali za mitaa mwakani na uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, sisi tunasema kwamba ujanja huu hatuwezi kuuafiki” alisema Lwakatare.

Alisema umefika wakati sasa Watanzania kuelewa wazi kwamba nchi inakabiliwa na janga la kitaifa la kutokuwa na uongozi mzuri wa kushughulikia matatizo.

“Kama baba na mama ndani ya nyumba wanalia matatizo… je, watoto watafanya nini? alihoji kiongozi huyo huku akiwafananisha viongozi wa serikali kuwa ni sawa na wazazi, ambao hawatakiwi kulalamika mbele ya watoto.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Idara ya Oganaizesheni, Kampeni na Uchaguzi wa Chama cha NCCR - Mageuzi, Faustine Sungura, alisema Watanzania hawawezi kuvumilia ugumu huu wa maisha ilhali serikali imeshindwa kupambana na mafisadi wanaochangia ugumu wa maisha kila kukicha.

Sungura alisema kuwa kupanda kwa bei ya mafuta ni suala la dunia, lakini kwa namna moja ama nyingine kila nchi inaangalia njia mbadala ya kutatua tatizo hilo na si viongozi kuwasukumia wananchi.

Naye Haroun Mlawa, mkazi wa Dar es Salaam, alisema hatua hiyo ya Rais Kikwete imewakumbusha Watanzania enzi za utawala wa Awamu ya Kwanza chini ya hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, aliyewataka Watanzania kufunga mikanda baada ya kumalizika kwa vita ya Uganda na Tanzania mwaka 1979.

“Rais ametusikitisha sana kwa kauli yake hii, yeye ndiye mkuu wa nyumba, sasa anaanza kulalamika… ametukumbusha enzi zile Nyerere alipowataka Watanzania kufunga mikanda kutokana na hali mabaya ya uchumi,” alisema Mlawa.

Alisema kauli ya Rais Kikwete inakatisha tamaa kwa watu wenye kipato cha chini, kwa vile haionyeshi wazi kwamba amedhamiria kupambana na umaskini, na kauli ya maisha bora kwa kila Mtanzania itabaki kuwa ndoto.

Alisema hii si mara ya kwanza kauli hiyo kutolewa, kwani katika utawala wa Awamu ya Tatu, Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, aliwahi kusema kwamba mtu yeyote maisha yakimshinda atarudi kijijini mwenyewe.

“Hatushangai kabisa, kwani hata Waziri Mkuu mstaafu, Sumaye, aliwahi kusema mtu ambaye maisha yatamshinda atarudi kijijini mwenyewe bila kulazimishwa,” alisema Mlawa.

Naye mhadhiri kutoka Idara ya Siasa na Utawala ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini alisema, rais na washauri wake wanapaswa kujipanga upya katika safu ya uongozi ili kukidhi matakwa ya wananchi.

Alisema hatua hiyo ndiyo njia pekee ambayo itasaidia kurejesha imani kwa wananchi ambao hivi sasa wanaonekana kukatishwa tamaa na utawala wa Awamu ya Nne.

Alisema suala la usimamizi mzuri wa malighafi za nchini kuwa ni jambo la msingi linalopaswa kuzingatiwa, kwani hata kama nchi zinazozalisha mafuta zinafaidika kwa ongezeko la bei.

“Jamani sisi Tanzania tumefanikiwa kuwa na vitu kama madini ya tanzanite, madini pekee duniani yanayoapatikana hapa nchini yakitumiwa vema yangeweza kutatua matatizo yetu ya kiuchumi badala ya kuwa tegemezi,” alisema.

“Gharama za uzalishaji na usafirishaji wa lita moja hadi hapa nchini ni sh 967.67, na kwa lita hiyo hiyo, serikali inadai ushuru wa sh 602, bei itaacha kuwa kubwa kweli?” alihoji.

Rais Kikwete alitoa kauli hiyo juzi akiwa katika siku ya tisa ya ziara yake wilayani Muheza, mkoani Tanga, ambapo aliwataka Watanzania kuvumilia hali ngumu ya maisha inayowakabili hivi sasa.
 
Kwa kweli watanzania tumekuwa wavumilivu mpaka tumefikia mwisho. Maana kila kiongozi anayeingia katika madaraka anakuja akituaminisha kuwa yeye ndiye anakuja kuwa suluhisho la matatizo yetu lakini akishakaa anatuambia tuvumilie matatizo yetu. Hivi uvumilivu huu utakwisha lini?
Kama kuvumilia mbona tumevumilia sana?
Sasa naona tuko mwisho wa uvumilivu maana wengine tunapovumilia Kikwete na kundi lake wanaendelea kutuibia! why tuvumilie zaidi? wameshindwa kutawala, waachie ngazi wengine watuvushe!
 

Naye Haroun Mlawa, mkazi wa Dar es Salaam, alisema hatua hiyo ya Rais Kikwete imewakumbusha Watanzania enzi za utawala wa Awamu ya Kwanza chini ya hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, aliyewataka Watanzania kufunga mikanda baada ya kumalizika kwa vita ya Uganda na Tanzania mwaka 1979.

Naamini JK naye ametoa kauli hii kufuatia kushindwa kwake kwenye vita ya kupambana na ufisadi pamoja na rushwa tofauti na Mwalimu ambaye alishinda vita yake.
Kila tatizo la kiuchumi lina solution, lakini kwa Rais ambaye ameweza kusimama jukwaani na kupayuka kwamba 'ajali haina kinga', kauli hii haijanishangaza sana- I was expecting it!
 
Hivi JK hana washuri wa kumwambia kuwa wakati huu kuongelea maisha ya mtanzania ni kutonesha kidonda kinachotoka damu, kauri gani ya kutoa kwa watu walilala njaa, wavumilie na kuendelea kulala njaa kwa muda usiojulikana. Hii inabidi iwekwe kwenye quote ya wiki.
 
Hii naifananisha na fainali katika mpira wa miguu, watanzania kama watu wa bench la ufundi tukiangalia mechi hiyo kwa hamu kubwa na ya ushindi, miongoni mwa wachezaji wetu ni nahodha wetu bw mkubwa hata kipindi cha kwanza hakijaisha jamaa amechoka sana, ana ngozi nzuri na jasho halimtoki sana, lakini yeye ndiye anayejua hali yake, ni mbaya sana pumzi imemwisha, anatamani aombe substitution lakini kamwe hata fanya hivyo, kuna binti kaja na marafiki zake na lengo yao kubwa ni kumuangalia bw mkubwa akilisakata kabumbu ni ugeni wa bw mkubwa, wachezaji wenzake wameshashtuka kwamba bw mkubwa kachemsha, lakini hawawezi sema kitu mle kwenye play-ground kwa kuwa yeye ndiyo nahodha, tusubiri tuome kama kipindi cha pili atarudi uwanjani.
 
Kwani kabla hajasema anadhani tulikuwa tunafanya nini kama sio kuvumilia?
He is reflection of ourselves.
You cant trust what you are being told by a mswahili.
You just have to watch your back.
Sisi tulijisahau
Sasa tunalipa na kuregret at leisure!!!
No hurry. Regret, regret, regret ...................
 
JK: Vumilieni shida


TANZANIA DAIMA, 21ST JULY, 2008

na Anna Makange, Tanga



RAIS Jakaya Kikwete, amewataka Watanzania kuwa wavumilivu kutokana na hali ngumu ya maisha inayowakabili kwa sasa, inayosababishwa na kupanda kwa bei ya mafuta duniani.

Rais Kikwete ametoa kauli hiyo katika kipindi ambacho Watanzania wengi, hasa wa kipato cha chini wamekuwa wakilia kutokana na kupanda kwa gharama za maisha.

Rais Kikwete alitoa kauli hiyo jana, wilayani Muheza, wakati alipokuwa akizungumza na wananchi wa wilaya hiyo, ikiwa ni siku ya tisa ya ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo, mkoani Tanga.

Rais Kikwete alisema kupanda kwa bei ya mafuta, kumechangia kwa kiasi kikubwa kulipuka kwa mfumuko wa bei za bidhaa mbalimbali duniani kote.

Alisema hali hiyo pia imechangia kuzorotesha kasi ya ukuaji wa uchumi hasa kwenye nchi zinazoendelea na hivyo watu wenye kipato duni kukabiliwa na hali ngumu ya maisha, hususan katika upatikanaji wa mahitaji muhimu, jambo ambalo aliongeza kuwa hata yeye limekuwa likimuumiza kichwa.

“Ndugu zangu Watanzania wenzangu…naelewa sana jinsi maisha yanavyozidi kuwa magumu siku hadi siku…na hali hii inasababishwa na kupanda kwa bei ya mafuta hapa nchini, hivyo kila bidhaa kwa sasa gharama zake ni za juu sana, kuanzia vyakula hadi vitu vingine ambavyo ni muhimu kwa maisha ya kila siku. Linatuumiza sana hasa wale wananchi ambao ni maskini wa kipato,” alisema Rais Kikwete.

Hata hivyo alisema Watanzania wasikate tamaa kwa kuona kwamba maisha yataendelea kuwa hivyo, na kusisitiza kwamba yeye kama Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) kwa kushirikiana na viongozi mbalimbali duniani wanalishughulikia suala hilo.

Wakati Rais Kikwete akiwataka Watanzania kutokatishwa tamaa na hali hiyo, Chama cha NCCR- Mageuzi, jana kilisema wananchi hawana sababu ya kuilaumu Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra) kwa kupandisha bei ya nauli na badala yake lawama hizo zielekezwe kwa serikali ya Rais Kikwete.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Idara ya Oganaizesheni, Kampeni na Uchaguzi, Faustine Sungura, alisema kutokana na matatizo hayo, kuna haja ya kuwepo kwa serikali mbadala, kwa madai kuwa serikali imeshindwa kutatua matatizo yanayowakabili wananchi, hasa ya upandaji wa gharama za bidhaa mbalimbali.

“Watanzania wanapaswa kujifunza kutokana na makosa, kwani muda waliowapa viongozi wa CCM kutawala unatosha na haujaonyesha mafanikio yoyote katika maisha zaidi ya kuzidisha ugumu wa maisha,” alisema.

“Watu wanakosea sana wanapoilaumu Sumatra badala ya kuilaumu serikali ambayo imeshindwa kudhibiti upandaji wa bei kwenye bidhaa mbalimbali yakiwemo mafuta,” alisema Sungura.

Alisema hata ziara anazofanya Rais Jakaya Kikwete na Makamu wake, Ali Mohamed Shein ni dhihaka kwa Watanzania, kwani ahadi zao hazitekelezeki na wameshindwa kuwasaidia wastaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ambao wanashinda Ikulu.

“Hivi hawa ni viongozi wa aina gani kama wameshindwa kuwasaidia wazee wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wanaoshinda pale Ikulu, wataweza vipi kuwasaidia watu wa huko mikoani?” alihoji Sungura.

Katika hatua nyingine, Rais Kikwete amesema serikali itahakikisha inafanya kila jitihada za kutafuta wawekezaji wa ndani na nje ya nchi ili kuwekeza kwenye kiwanda cha usindikaji wa matunda wilayani Muheza, kwa lengo la kuwatafutia wakulima wa machungwa soko la uhakika.

Alisema lengo la kujenga kiwanda hicho licha ya kumtafutia soko mkulima, lakini pia itakuza kipato cha wakulima sambamba na kupunguza kiwango kikubwa cha machungwa yanayoharibika mashambani kwa kukosa wanunuzi hasa nyakati za msimu.

“Serikali inaamini kwa kufanya hivi tutakuwa tumemsaidia mkulima kwa kiasi kikubwa kuwa na soko la uhakika sambamba na kukuza kipato chake ambacho hivi sasa kinapotea kutokana na kiasi kikubwa cha matunda kuharibika…nawaahidi kwamba hili tutalitekeleza haraka iwezekanavyo,” alisisitiza Rais Kikwete.

Miongoni mwa ahadi alizotoa rais wilayani Muheza ni pamoja na kupeleka darubini katika zahanati ya Kijiji cha Kicheba, kuchangia sh milioni mbili katika ujenzi wa madarasa ya Shule ya Sekondari ya Mtindiro, sambamba na kutafuta magari ya wagonjwa katika wilaya zilizokosa huduma hiyo mkoani hapa.

HII SASA KALI, KAZI KWENU WADAU

Does our president having a long term strategies ? mi namuona kila siku anasafiri mara huku mara kule hivi ni wakati gani anafanya kazi zake za ofisini ? na labda niulize hivi raisi wetu ana plan kweri ? nina maana kujua nini kitakuwepo kesho and anatakiwa kufanya nini mara baada ya siku mbili au tatu ? sina maana ya sherehe au inagurations maana hizi anapangiwa.

naona kaishiwa hana mpya kabisa. hili jambo tumeshajadili hapa siku nyingi hapa anacheza kombolela.
 
Hii ni dalili mbaya sana na inaonyesha tunako elekea sio salama tunaelekea kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe ,nauona Uchaguzi mkuu unaokuja utakuwa na maafa mengi kuliko Uchaguzi wowote uliowahi kutokea hapa Tanzania ,Uchaguzi ambao waliopo madarakani kama hawatakubali kuendesha uchaguzi ulio huru na usio na mizengwe basi yule nyoka aliepitia kenya Zimbabwe sasa anaitambalia Tanzania.tukae mkao wa kujitayarisha.
 
Hii ni dalili mbaya sana na inaonyesha tunako elekea sio salama tunaelekea kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe ,nauona Uchaguzi mkuu unaokuja utakuwa na maafa mengi kuliko Uchaguzi wowote uliowahi kutokea hapa Tanzania ,Uchaguzi ambao waliopo madarakani kama hawatakubali kuendesha uchaguzi ulio huru na usio na mizengwe basi yule nyoka aliepitia kenya Zimbabwe sasa anaitambalia Tanzania.tukae mkao wa kujitayarisha.

I have the same feelings! Ila vyama vyetu vya upinzani navyo vijipange mapema, yaani hapa ndipo pa kuongeza idadi ya wanachama wa upinzani bungeni. Serikali ya awamu ya tatu pamoja na ufisadi wao lakini walijitahidi kufanya mambo mengi yaliyowapa faraja wananchi kwamba baada ya miaka kadhaa nchi yetu itakuwa bomba!
 
Kama kuvumilia wananchi tusha vumilia vya kutosha. Sasa kama alikuwa hajui tunaishi kwa kuvumili then ana maana hali itakuwa ngumu kuliko ilivyo sasa may be kuliko enzi zile za folen ya bulga na unga wa yanga kwenye maduka ya kaya.
 
Hivi huyu ni mwanasiasa au ni baba yetu?

Vumilia ni maneno niliyopata kwa baba na mama na sitegemei kuambiwa hivyo na mwanasiasa. Kama hana ufumbuzi aondoke Statehouse. MWISHO.

Usanii una kikomo.
 
Vumilieni shida wakati mafisadi wa sirikali na chama cha mafisadi bado wanaendesha magari ya bei mbaya ambayo yana tumia mafuta sana na hii yote inalipwa na walipa kodi. Bado haoni umuhimu wa kubana matumizi ya magari hayo ili kupunguza gharamaa serikali na pia kufuta safari zake zisizo na msingi.
 
KASHFA NZITO YA KIKWETE. !!!!!


Baada ya kusoma kwa makini kwa siku nne mfululizo, kwenye forum yetu hii tukufu, na baada ya kuona kuwa uongozi wa forum hii tukufu umeamua kuwa kila anayeona uovu wa viongozi wa kisiasa na haswa wenyeviti wa vyama vya siasa ana haki ya kuleta ujumbe wake hapa bila kubugudhiwa kitu ambacho nakiheshimu sana kwenye ujenzi wa demokrasia na pia haki ya kupata habari kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya muungano ya Tanzania ibara ya 18.

Na pia nimeguswa kuandika ujumbe huu kutokana na kile nilichokiona kwenye gazeti la majira la jana (front page) na pia kauli iliyotolewa na katibu mkuu wa CCM ndugu Makamba kuunga mkono hoja iliyowekwa hapa forum na wanachadema! Kama ilivyorushwa kwenye taarifa ya habari ya channel ten jana saa moja jioni .

Makamba alisema kuwa viongozi wa upinzani waache kurusha mawe ile hali wao wako wakiishi kwenye nyumba za vioo!nimeshtuka na kuogopa kama huyu ndio anatakiwa kuonyesha njia ya kuweza kufikia maisha bora kwenye taifa hili , nashindwa kuamini kuwa huyu ndio dereva wa chama tawala !

Leo nimeona niweke ushahidi wangu hapa juu ya ufisadi wa ziada na au uovu uliotendwa na JK pamoja na timu yake wakati wa kuwania kuteuliwa na chama chake, na pia jinsi alivyotumia cheo chake cha waziri wa mambo ya nje kuendekeza ngono na kulisababishia taifa hili madhara makubwa ikiwa ni pamoja na mahusiano ya kidiplomasia kuwa mabaya.

Naanza kuweka hoja zangu na ushahidi wake kama ifuatavyo,

1.Kikwete wakati anagombea kuteuliwa kuwa mgombea wa CCM ,aliunda timu za aina mbalimbali ila kwa hapa nazungumzia timu yake ya uharamia ambayo aliiunda, aliunda timu ya kuwafanyia maasi wagombea wenzake na mojawapo ni hii iliyokuwa inaongozwa na mtu anayeitwa Gogo kutoka kule Bagamoyo.

Huyu alinunuliwa gari aina ya Nissan patrol ,na ndio mwanzo alitumika kupita kwenye misikiti mbalimbali na kutengeneza mtandao wa kiislamu,ila huyu Gogo ndio alihusika na aliongoza kikosi kilichohusika kumpora mke wa mzee Malecela fedha taslimu zaidi ya milioni mia mbili wakati anatoka dar kwenda dodoma kwa ajili ya kampeni. ENEO LA GAIRO.

Gogo akiwa na vijana wenzake walimteka mama Kilango nje kidogo ya mji wa morogoro na kumpora fedha hizo na pia kumfanyia mambo ya ajabu ambayo kwa mtu mzima kama mimi siwezi kuyaandika hapa.(ushahidi upo na nitautoa muda wowote kama utahitajika hapa ,niandikie kwenye PM yangu.)

2.Akiwa waziri wa mambo ya nje mwaka 2004 alipokwenda nchini marekani kuiwakilisha nchi kwenye kikao cha UN alifanya ngono na aliyekuwa waziri wa mambo ya nje wa Uganda kitu kilichowafanya kutokuweza kuhudhuria mkutano kwa siku mbili mfululizo, na ndipo rais museven alimwandikia rais mkapa rasmi malalamiko yake na pia alimtimua kazi waziri huyo .

Hili linaifanya nchi yetu kutokuwa na mahusiano mazuri na serikali ya Uganda na haswa kati ya Kikwete na Museven na hili limechangia kwa kiasi kikubwa hata kutokufikiwa kwa shirikisho kwani Museven anaamini kuwa hawawezi kujadili mambo serious na JK kutokana na kutokwenda kuwakilisha nchi na badala yake ikawa ni kwenda kufanya ngono na waziri aliyetumwa na nchi nyingine bila hata aibu.

3.Kikwete akiwa na swahiba wake wa karibu anayeitwa Jack Gotham,wakiwa maeneo ya millennium towers hotel kijitonyama ,walimchukua binti wa mfanyibiashara mmoja wa jijini ambaye alikuwa anasoma shahada ya kwanza chuo kikuu cha DSM na kufanya naye ngono hapohapo hotelini na kumfanya kuchelewa kwenda kwenye ziara za kampeni kwani kipindi hiki kilikuwa ni wakati wa mchakato wa kampeni ukiwa unaendelea.

Huyu anaacha hata masuala ya maana na kwenda kumchukua binti wa rafiki yake ambaye amemchangia kiasi kikubwa cha fedha za kampeni zake na kufanya naye ngono.

4. Fedha chafu.
Kikwete aliingiza nchini kiasi kikubwa sana cha fedha chafu kutoka kwenye nchi za uarabuni na nyingine alizitoa Jamhuri wa Kidemokrasia ya Congo (DRC)kutoka kwa Joseph Kabila na fedha hizi ziliingizwa kupitia mkoani Kigoma na nyingine ziliingilia mkoani Mwanza .
Ujumbe wa watu wa kongo uliongozwa na Luten Jenerali Peter Gessimba Gabonne akiwa na wasaidizi wake watatu ambao walikuwa ni viongozi wa jeshi tiifu kwa Kabila.


Fedha hizi zilitolewa kwa masharti kuwa endapo angeshinda ni lazima ahakikishe kuwa Kabila naye anashinda kule Congo kitu ambacho alikifanya na hata kutumia pesa za taifa hili kwa ajili ya uchaguzi wa congo kwa wale mnaokumbuka Asha Rose Migiro alisema kiasi cha pesa zilizotolewa na misaada mingine ……..

5. Ngono.
JK akiwa na maswahiba wa mwanae wa karibu waitwao Benno (huyu kwa sasa anagombea ujumbe wa NEC ndani ya chama chetu),Said (huyu ni msaidizi maalumu wa kumsaidia mzee Makamba) ,Mussa (huyu alikuwa ni kiongozi mwandamizi wa mbio za mwenge mwaka huu), na Sisko (huyu ni chief protocol wa ikulu)wakiwa kwenye club mojawapo jijini dar,(ipo mkabala na red cross-barabara ya Alhassan mwinyi) kabla ya mchakato wa kampeni kuanza rasmi walimchukua binti anayeitwa Hadija ……aliyekuwa anasoma UDSM (Third year Sociology) na pia ni mfanyibiashara wa mjini Arusha, ila alikuwa pia ni mke wa aliyekuwa meneja msaidizi wa kituo kimoja cha kimataifa nchini , na kufanya naye ngono .

Kitendo hiki kilimfanya Hadija kuachika /kuachwa na mumewe na kumnyanganya magari pamoja na mtaji kitu kilichopelekea binti huyu kuishi kwa taabu hadi JK alipoweza kushinda urais wa nchi na kumpangishia nyumba maeneo ya Kijitonyama ambako anaishi hadi sasa.
Pia JK alimwamuru Benno ambaye ni afisa mwajiri wa jumuiya ya UVCCM kumwajiri bint huyu makao makuu na kwa sasa ameajiriwa kama katibu wa uhamasishaji wa taifa cheo ambacho hakipo hata kwenye katiba ya umoja huo, kwa toleo la 2003 ambalo ninalo hapa.

6. Ngono ,
Alifanya ngono iliyoligharimu taifa hili zaidi ya shilingi milioni mia nne Na themanini, (480 milioni) akiwa kule Zanzibar Hotel Kempinski pale alipokuja na mkewe mpya kutoka uarabuni na kukaa naye kwenye mapumziko hayo ambayo yaliliingizia taifa hasara hiyo kwa muda wa siku 9 tuu.
Mkuu wetu wa nchi anatumia rasilimali zetu kwa ajili ya kujistarehesha yeye binafsi na wanawake zake kutoka huko uarabuni.

7.Ubadhirifu.
Aliweza kujichukulia eneo ndani ya mbuga za wanyama kule Serengeti na sasa anajenga hotel ya kisasa nah ii anaijenga yeye kwa ubia na mke wake huyo wa uarabuni akishirikiana na mashemeji zake hao , swali la kujiuliza ni je?huu mkataba hautaishia kwenye kuliuza taifa hili?
Mke anaenda kupewa mahari ya rasilimali zetu? Kama kila rais akioa ni sharti atoe sehemu ya mbuga zetu je? Mpaka lini tutakuwa tunachezea taifa kwa faida za kuoa ama kupata ngono!

Huyu ndio mwenyekiti wa chama chetu na bado tunamwona kama malaika aliyetoka mbinguni kama sio kuzimu!

Nitakuja na taarifa pia za kina juu ya ndugu Nchimbi ambaye naambiwa kuwa anaweza kuwa ndio katibu mkuu wa chama chetu, jambo ambalo mimi nalipinga kwa nguvu zote kwani huyu naye anaendelea kufanya mambo ya aibu na wanafunzi wa vyuo mbalimbali vya umma nchini.

Ni mimi mwanachama mtiifu na mpenda maendeleo ya chama chetu kitukufu.
 
Hizi habari zilizoandikwa hapa juu za "ngono" zinazomhusu kiongozi,rais Kikwete zinasikitisha mno. Lakini ndio viongozi wetu wote wa Afrika walivyo!

Kama yeye anamke au wake wa kiarabu basi twamwambia kwa lugha ya kiarabu kwamba ameambiwa LA TAKABBAR ZINAA. Msijishughulishe na mambo ya zinaa. Huko kupima kwake UKIMWI ni kinyume cha mapendekezo hayo ya Mola Wake!

Tanzania amabyo ina gesi ya Songosongo isingelikuwa na shida ya kutumia petrol wala disel kama kungelikuwepo na uongozi mzuri. Mabasi yetu na gari zetu zingeliweza kutumia gesi. Techonology hii ipo na kuna nchi kadhaa za Ulaya ambazo sasa zinatumia gesi katika Mabasi na gari binafsi.

Makaa ya mawe pia yangeliweza kutimika katika kutengeneza umeme. Windmills na na mianzi ya Jua pia ingelitumika kutengeneza umeme.
Kikwete na serikali yake ya CCM hawana uongozi mzuri.

Watanzania wenye madini kibao, upepo kibao,gesi kibao, misitu kibao, ardhi kibao, bahari kibao na dhahabu kibao haya shida iko wapi?
Kikwete hawezi kushindana na mahali pale alipotoka!
 
JANGALA MICHOSHO KIWETE...

..leo ..TUVUMILIE....

kwake yeye kuleta VIONJO VYA KUFIKIRIKA VYA KISIASA HATA KWENYE HOJA NZITO NI KAWAIDA....

MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA YANAWEZEKANA....

TANZANIA YENYE NEEMA INAWEZEKANA......

TANZANIA BILA UKIMWI INAWEZEKANA..

SASA BORA NAYE AWE MUHUBIRI WA DINI....TUNGEMUELEWA..

KAMA YULE ANAYEENDESHA MAOMBEZI YA...

HAKUNA LISILOWEZEKANA........

KWA JK KILA KITU KINAWEZEKANA...KWA MDOMO!!

KWA ARI MPYA NGUVU MPYA NA KASI MPYA.........ANGUKA!!!!

AMEANGUKA!!!!!
 
ni vigumu kujua serikali ya kikwete ina malengo gani (kama inayo).....
aliapswa kusema vumilieni kwa mwezi fulani kwa sababu kwa mujibu wa mipango hii na hii baada ya hapo maisha yatakuwa bora.

ila hamna kitu
 
KASHFA NZITO YA KIKWETE. !!!!!


Baada ya kusoma kwa makini kwa siku nne mfululizo, kwenye forum yetu hii tukufu, na baada ya kuona kuwa uongozi wa forum hii tukufu umeamua kuwa kila anayeona uovu wa viongozi wa kisiasa na haswa wenyeviti wa vyama vya siasa ana haki ya kuleta ujumbe wake hapa bila kubugudhiwa kitu ambacho nakiheshimu sana kwenye ujenzi wa demokrasia na pia haki ya kupata habari kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya muungano ya Tanzania ibara ya 18.

Na pia nimeguswa kuandika ujumbe huu kutokana na kile nilichokiona kwenye gazeti la majira la jana (front page) na pia kauli iliyotolewa na katibu mkuu wa CCM ndugu Makamba kuunga mkono hoja iliyowekwa hapa forum na wanachadema! Kama ilivyorushwa kwenye taarifa ya habari ya channel ten jana saa moja jioni .

Makamba alisema kuwa viongozi wa upinzani waache kurusha mawe ile hali wao wako wakiishi kwenye nyumba za vioo!nimeshtuka na kuogopa kama huyu ndio anatakiwa kuonyesha njia ya kuweza kufikia maisha bora kwenye taifa hili , nashindwa kuamini kuwa huyu ndio dereva wa chama tawala !

Leo nimeona niweke ushahidi wangu hapa juu ya ufisadi wa ziada na au uovu uliotendwa na JK pamoja na timu yake wakati wa kuwania kuteuliwa na chama chake, na pia jinsi alivyotumia cheo chake cha waziri wa mambo ya nje kuendekeza ngono na kulisababishia taifa hili madhara makubwa ikiwa ni pamoja na mahusiano ya kidiplomasia kuwa mabaya.

Naanza kuweka hoja zangu na ushahidi wake kama ifuatavyo,

1.Kikwete wakati anagombea kuteuliwa kuwa mgombea wa CCM ,aliunda timu za aina mbalimbali ila kwa hapa nazungumzia timu yake ya uharamia ambayo aliiunda, aliunda timu ya kuwafanyia maasi wagombea wenzake na mojawapo ni hii iliyokuwa inaongozwa na mtu anayeitwa Gogo kutoka kule Bagamoyo.

Huyu alinunuliwa gari aina ya Nissan patrol ,na ndio mwanzo alitumika kupita kwenye misikiti mbalimbali na kutengeneza mtandao wa kiislamu,ila huyu Gogo ndio alihusika na aliongoza kikosi kilichohusika kumpora mke wa mzee Malecela fedha taslimu zaidi ya milioni mia mbili wakati anatoka dar kwenda dodoma kwa ajili ya kampeni. ENEO LA GAIRO.

Gogo akiwa na vijana wenzake walimteka mama Kilango nje kidogo ya mji wa morogoro na kumpora fedha hizo na pia kumfanyia mambo ya ajabu ambayo kwa mtu mzima kama mimi siwezi kuyaandika hapa.(ushahidi upo na nitautoa muda wowote kama utahitajika hapa ,niandikie kwenye PM yangu.)

2.Akiwa waziri wa mambo ya nje mwaka 2004 alipokwenda nchini marekani kuiwakilisha nchi kwenye kikao cha UN alifanya ngono na aliyekuwa waziri wa mambo ya nje wa Uganda kitu kilichowafanya kutokuweza kuhudhuria mkutano kwa siku mbili mfululizo, na ndipo rais museven alimwandikia rais mkapa rasmi malalamiko yake na pia alimtimua kazi waziri huyo .

Hili linaifanya nchi yetu kutokuwa na mahusiano mazuri na serikali ya Uganda na haswa kati ya Kikwete na Museven na hili limechangia kwa kiasi kikubwa hata kutokufikiwa kwa shirikisho kwani Museven anaamini kuwa hawawezi kujadili mambo serious na JK kutokana na kutokwenda kuwakilisha nchi na badala yake ikawa ni kwenda kufanya ngono na waziri aliyetumwa na nchi nyingine bila hata aibu.

3.Kikwete akiwa na swahiba wake wa karibu anayeitwa Jack Gotham,wakiwa maeneo ya millennium towers hotel kijitonyama ,walimchukua binti wa mfanyibiashara mmoja wa jijini ambaye alikuwa anasoma shahada ya kwanza chuo kikuu cha DSM na kufanya naye ngono hapohapo hotelini na kumfanya kuchelewa kwenda kwenye ziara za kampeni kwani kipindi hiki kilikuwa ni wakati wa mchakato wa kampeni ukiwa unaendelea.

Huyu anaacha hata masuala ya maana na kwenda kumchukua binti wa rafiki yake ambaye amemchangia kiasi kikubwa cha fedha za kampeni zake na kufanya naye ngono.

4. Fedha chafu.
Kikwete aliingiza nchini kiasi kikubwa sana cha fedha chafu kutoka kwenye nchi za uarabuni na nyingine alizitoa Jamhuri wa Kidemokrasia ya Congo (DRC)kutoka kwa Joseph Kabila na fedha hizi ziliingizwa kupitia mkoani Kigoma na nyingine ziliingilia mkoani Mwanza .
Ujumbe wa watu wa kongo uliongozwa na Luten Jenerali Peter Gessimba Gabonne akiwa na wasaidizi wake watatu ambao walikuwa ni viongozi wa jeshi tiifu kwa Kabila.


Fedha hizi zilitolewa kwa masharti kuwa endapo angeshinda ni lazima ahakikishe kuwa Kabila naye anashinda kule Congo kitu ambacho alikifanya na hata kutumia pesa za taifa hili kwa ajili ya uchaguzi wa congo kwa wale mnaokumbuka Asha Rose Migiro alisema kiasi cha pesa zilizotolewa na misaada mingine ……..

5. Ngono.
JK akiwa na maswahiba wa mwanae wa karibu waitwao Benno (huyu kwa sasa anagombea ujumbe wa NEC ndani ya chama chetu),Said (huyu ni msaidizi maalumu wa kumsaidia mzee Makamba) ,Mussa (huyu alikuwa ni kiongozi mwandamizi wa mbio za mwenge mwaka huu), na Sisko (huyu ni chief protocol wa ikulu)wakiwa kwenye club mojawapo jijini dar,(ipo mkabala na red cross-barabara ya Alhassan mwinyi) kabla ya mchakato wa kampeni kuanza rasmi walimchukua binti anayeitwa Hadija ……aliyekuwa anasoma UDSM (Third year Sociology) na pia ni mfanyibiashara wa mjini Arusha, ila alikuwa pia ni mke wa aliyekuwa meneja msaidizi wa kituo kimoja cha kimataifa nchini , na kufanya naye ngono .

Kitendo hiki kilimfanya Hadija kuachika /kuachwa na mumewe na kumnyanganya magari pamoja na mtaji kitu kilichopelekea binti huyu kuishi kwa taabu hadi JK alipoweza kushinda urais wa nchi na kumpangishia nyumba maeneo ya Kijitonyama ambako anaishi hadi sasa.
Pia JK alimwamuru Benno ambaye ni afisa mwajiri wa jumuiya ya UVCCM kumwajiri bint huyu makao makuu na kwa sasa ameajiriwa kama katibu wa uhamasishaji wa taifa cheo ambacho hakipo hata kwenye katiba ya umoja huo, kwa toleo la 2003 ambalo ninalo hapa.

6. Ngono ,
Alifanya ngono iliyoligharimu taifa hili zaidi ya shilingi milioni mia nne Na themanini, (480 milioni) akiwa kule Zanzibar Hotel Kempinski pale alipokuja na mkewe mpya kutoka uarabuni na kukaa naye kwenye mapumziko hayo ambayo yaliliingizia taifa hasara hiyo kwa muda wa siku 9 tuu.
Mkuu wetu wa nchi anatumia rasilimali zetu kwa ajili ya kujistarehesha yeye binafsi na wanawake zake kutoka huko uarabuni.

7.Ubadhirifu.
Aliweza kujichukulia eneo ndani ya mbuga za wanyama kule Serengeti na sasa anajenga hotel ya kisasa nah ii anaijenga yeye kwa ubia na mke wake huyo wa uarabuni akishirikiana na mashemeji zake hao , swali la kujiuliza ni je?huu mkataba hautaishia kwenye kuliuza taifa hili?
Mke anaenda kupewa mahari ya rasilimali zetu? Kama kila rais akioa ni sharti atoe sehemu ya mbuga zetu je? Mpaka lini tutakuwa tunachezea taifa kwa faida za kuoa ama kupata ngono!

Huyu ndio mwenyekiti wa chama chetu na bado tunamwona kama malaika aliyetoka mbinguni kama sio kuzimu!

Nitakuja na taarifa pia za kina juu ya ndugu Nchimbi ambaye naambiwa kuwa anaweza kuwa ndio katibu mkuu wa chama chetu, jambo ambalo mimi nalipinga kwa nguvu zote kwani huyu naye anaendelea kufanya mambo ya aibu na wanafunzi wa vyuo mbalimbali vya umma nchini.

Ni mimi mwanachama mtiifu na mpenda maendeleo ya chama chetu kitukufu.


watanzania wa kawaida wasiomjua wakiona hizi kashfa wanaweza kufikiri utani...lakini ndio hali halisi...nyingi hapa .....tayari zinajulikana ...

hiyo ya kina gogo inasikitisha sana....mama kilango anayo machungu makubwa rohoni...HUYU GOGO ...ni yule ndugu yake jk ...ambaye anapiga deals maskani kariakoo jirani na idrissa mosque...anaitwa HAMIS ...Yupo na jamaa wengine wa bagamoyo mmoja wao kuna wakati alikuwa cuf..?
 
Yaani huyu jamaa hana tofauti na zero(Sumaye)... Alichosema ni upumbavu kabisa....Yeye si alisema maisha bora kwa kila mtanzania sasa haya mambo ya kuvumilia shida yanatoka wapi, yeye angeweza kuvumilia shida?
 
Back
Top Bottom