William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,588
- 10,374
Mahakama, Mheshimiwa Spika:
Serikali nitakayoiunda, pamoja na kuheshimu uhuru wa Mahakama, itatimiza ipasavyo wajibu wake na kuimarisha miundombinu ya kutoa haki kwa kuongeza idadi ya watumishi, kuwaendeleza kitaaluma, kukarabati majengo yaliyopo na kujenga mapya, na kupeleka huduma za utoaji haki karibu zaidi na wananchi.
Mapato na Matumizi ya Serikali, Mheshimiwa Spika:
Kusimamia vizuri mapato na matumizi ya Serikali nayo ni sehemu ya utawala bora. Isitoshe, utekelezaji mzuri wa jukumu hilo ndio unaipa Serikali uwezo wa kutekeleza mengine yote inayopaswa au inayokusudia kuyatekeleza. Serikali ya Awamu ya Tatu, chini ya uongozi shupavu wa Mheshimiwa Benjamin William Mkapa, iliongeza mapato ya Serikali mara tano sambamba na kuweka mfumo mpya na wa kisasa wa kudhibiti matumizi, na kuongeza uwazi katika bajeti ya Serikali.
Hatutalegeza kamba hata kidogo. Hatutavumilia wanaokwepa kulipa kodi stahiki za Serikali au wabadhirifu wa fedha na mali za umma. Sheria ya Fedha, na Sheria ya Manunuzi ya Umma, lazima zifuatwe. Watakaokiuka wachukuliwe hatua za nidhamu. Wasiorejesha masurufu ya safari nao wasivumiliwe.
Kazi za Serikali kwenye Uchumi wa Soko, Mheshimiwa Spika:
Utawala bora ni pamoja na Serikali kufanya vizuri kazi zake nyingine muhimu katika mazingira ya uchumi wa soko. Jukumu la msingi la Serikali ni kutengeneza mazingira mazuri kwa uchumi kukua na biashara kustawi.
Serikali nitakayoiunda, pamoja na kuheshimu uhuru wa Mahakama, itatimiza ipasavyo wajibu wake na kuimarisha miundombinu ya kutoa haki kwa kuongeza idadi ya watumishi, kuwaendeleza kitaaluma, kukarabati majengo yaliyopo na kujenga mapya, na kupeleka huduma za utoaji haki karibu zaidi na wananchi.
Mapato na Matumizi ya Serikali, Mheshimiwa Spika:
Kusimamia vizuri mapato na matumizi ya Serikali nayo ni sehemu ya utawala bora. Isitoshe, utekelezaji mzuri wa jukumu hilo ndio unaipa Serikali uwezo wa kutekeleza mengine yote inayopaswa au inayokusudia kuyatekeleza. Serikali ya Awamu ya Tatu, chini ya uongozi shupavu wa Mheshimiwa Benjamin William Mkapa, iliongeza mapato ya Serikali mara tano sambamba na kuweka mfumo mpya na wa kisasa wa kudhibiti matumizi, na kuongeza uwazi katika bajeti ya Serikali.
Hatutalegeza kamba hata kidogo. Hatutavumilia wanaokwepa kulipa kodi stahiki za Serikali au wabadhirifu wa fedha na mali za umma. Sheria ya Fedha, na Sheria ya Manunuzi ya Umma, lazima zifuatwe. Watakaokiuka wachukuliwe hatua za nidhamu. Wasiorejesha masurufu ya safari nao wasivumiliwe.
Kazi za Serikali kwenye Uchumi wa Soko, Mheshimiwa Spika:
Utawala bora ni pamoja na Serikali kufanya vizuri kazi zake nyingine muhimu katika mazingira ya uchumi wa soko. Jukumu la msingi la Serikali ni kutengeneza mazingira mazuri kwa uchumi kukua na biashara kustawi.