GIB
JF-Expert Member
- Mar 2, 2012
- 336
- 92
Zaidi ya mwaka mmoja umeshapita sasa tangu Rais Jakaya Mrisho Kikwete aingie madarakani katika muhula wake wa pili wa kuliongoza taifa hili. Ingawa mwaka mmoja sio muda wa kutosha kwa kiongozi kukamilisha malengo na ahadi zote,ni muda wa kutosha kutoa picha ya mfumo na mtindo wa ki-uongozi.
Je,mwaka mmoja baadae,uchaguzi ungefanyika unadhani kura yako ungempa nani katika ya Rais Jakaya Kikwete na aliyekuwa mpinzani wake mkuu katika uchaguzi uliopita,Dr.Wilbrod Slaa?
Kwanini?
Ninapoandika post hii,"madaktari wametangaza kuanza mgomo leo, wanaharakati nchini wamemtisha Rais Jakaya Kikwete kwamba endapo hatawaondoa kwenye nyadhifa zao Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Haji Mponda na Naibu wake, Dk. Lucy Nkya, wataamua la kufanya"(Tanzania daima 7 march 2012).
Madaktari nao wasisitiza "Kama tulivyotaarifiana kwenye kikao chetu cha Machi 3, mwaka huu ni kwamba makubaliano yaliyofikiwa na hatimaye kutiliana saini kati ya madaktari na Serikali Machi 2, mwaka huu ni kuwa ili mazungumzo ya kujadili madai yetu yaweze kuendelea na hatua ya pili ni lazima, Waziri Dk Mponda na Naibu wake, Dk Nkya ama wawe wamejiuzulu au wamewajibishwa."
NB: Unaweza kutumia fursa hii kutoa maoni ya kujenga kwa maana ya kwamba kutoa maoni yenye tija na sio lawama na matusi.
Nawasilisha
Read more: JK Vs SLAA: UNGEMCHAGUA NANI? - BongoCelebrity