RAIS Jakaya Kikwete amesema utekelezaji wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi hasa katika kipengele kinachokataza takrima, ni mgumu.
Rais Kikwete alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na viongozi wa dini katika semina ya siku mbili iliyoandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu na kufanyika katika Hoteli ya WhiteSands jijini Dar s Salaam.
Tumeendelea kuboresha Sheria ya Gharama za Uchaguzi, lakini, lile la takrima ni gumu. Mfano katika mkoa wa Kilimanjaro huwezi kuwaita wazee ukazungumza nao bila kitochi, alisema Kikwete.
Kitochi ni kipimo cha lita moja ya pombe ya kienyeji aina ya mbege inayotengenezwa mkoani Kilimanjaro.
Rais aliendelea kusema Wakati wa kampeni mwaka 2005 nilifika mahali wakawa wananiambia, mzee hili ni jambo la kawaida hata Chadema, CUF wakija wanafanya hivi, hiyo ni sehemu muhimu kwao, huwezi kuwaita wazee bila mbege.
Katika kuthibitisha kauli yake hiyo Rais Kikwete alimtaka mmoja wa maaskofu wanaotoka Kanda ya Kaskazini kueleza endapo inawezakana kuwaita wazee wa mkoa huo bila kitochi.
Askofu huyo ambaye jina lake halikufahamika mara moja, alimjibu Kikwete "Kwa kweli hili haliwezekani. Hiyo ni sehemu ya maisha ya watu wa Kilimanjaro."
Baada ya jibu hilo la askofu, ukumbi mzima akiwa Rais Kikwete mwenyewe ulilipuka kwa kicheko na baadaye rais aliendelea kuzungumza na viongozi hao bila kusema nini kifanyanyike ili sheria hiyo iweze kutekelezeka maeneo kama hayo.
Kwa mujibu wa Rais Kikwete kabla ya kutungwa kwa Sheria hii mpya ya Gharama za Uchaguzi, hali ilikuwa mbaya kiasi kwamba kabla ya mtu kufikiria kugombea, alianza kufikiri kwanza jinsi ya kupata fedha za kununua watu ili wampitishe kwenye kura za maoni.
Mwende mkawahubirie watu kuwa wawachague watu wenye nia njema, watakaoweza kuliendeleza taifa, msiengemee chama chochote na pia tuendelee kukumbushana kuyakubali matokeo, aliagiza Rais Kikwete.
Katika hatua nyingine, Rais Kikwete pia alitumia fursa hiyo kuwaonya viongozi hao juu ya tabia inayoanza kujitokeza ya dini moja kuikejeli dini nyingine.
Alisema ingawa Tanzania ina uhuru wa kuabudi, pale dini yoyote itakapofanya kitendo hicho hadharani, serikali itaingilia kati.
Wengine wanasema kuwa tunaingilia uhuru wa kuabudu, lakini siyo kweli, sisi sheria zetu zinasema usikejeli dini ya mwenzako, ukifanya hivyo sisi tunaingilia kati, alisema Kikwete.
Kikwete pia alisisitiza umuhimu wa kushirikiana kati ya viongozi wa dini na serikali akieleza kuwa pande hizo zote zina lengo moja la kutaka upendo na maendeleo kwa jamii.
Alisema wakati mwingine serikali inaweza kufanya jambo ambalo kwa namna moja au nyingine linaweza kuwakera viongozi hao wa dini na kuwa hali hiyo itakapotokea, viongozi hao wasisite kuwasiliana naye moja kwa moja au kupitia mawaziri.
Sisi wote ni binadamu kwa hiyo tutaweza kukosea lakini, nyie mna watu, unaweza kumwambia waziri au mtu mwingine amwambie waziri mkuu kuwa mnataka kuonana naye au aniambie mimi.Pia mnaweza kutumia simu yangu iko wazi muda wote unaweza kunipigia uniambie moja kwa moja, alisisitiza Kikwete.
Awali Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Iringa Dk Owdemburg Mdegella alisema kikao hicho kimepitisha maazimio saba ambayo pande zote mbili; serikali na viongozi wa dini wamekubali kuyatekeleza.
Kwa kuwa Serikali imeona umuhimu wa kutayarisha Sheria ya Gharama za Uchaguzi na kuwashirikisha viongozi wa dini ili kuielewa, kuijadili na kuifikisha kwa waumini; viongozi wa dini tunapongeza na kuhimiza serikali kuwa waaminifu katika kuitekeleza, alisema Askofu Dk Mdegella.
Alisoma maazimio hayo kuwa ni serikali kuweka utaratibu maalum wa kukutana na viongozi wa dini mara mbili kwa mwaka na Serikali kudumishe utaratibu wa kutumia mtandao wa viongozi wa dini kwa kupanua wigo wa ushiriki ili kufikisha taarifa sahihi kwa jamii yote.
Maazimio mengine ni viongozi wa dini washirikishwe mapema katika hatua za awali wakati wa kushughulikia masuala mbalimbali muhimu ya kitafa na viongozi wa dini wasishabikie siasa katika nyumba za ibada.
Kwa mujibu wa Askofu Mdegella maazimio mengine ni ilani za vyama vya siasa zitayarishwe kwa namna ambayo hazitawagawa Watanzania kwa misingi ya dini, kabila, rangi, jinsi ama eneo analotoka na Serikali na taasisi za dini na zile za kijamii zishirikiane kuandaa mikakati endelevu ya maadili ya kitaifa
Rais Kikwete alikubali hoja zote zilizofikiwa katika mkutano huo akipendekeza kuwa katika suala la kukutana mara mbili kwa mwaka na viongozi hao, ligawanywe katika mafungu mawili.
Alisema fungu la kwanza liwe lile la kukutana na viongozi kutoka katika madhehebu na jumuiya mbalimbali kwa nyakati tofauti na lile la pili viongozi wote wa dini na serikali wakutane kwa wakati mmoja.
Hata hivyo, kama ilivyokuwa katika siku ya kwanza ya mkutano huo, wahandishi wa habari jana pia hawakuruhusiwa kuingia katika mkutano huo wakati majadiliano hayo yanaendelea.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Uratibu na Bunge) ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa Mkutano huo, Philip Marmo alikijiuta katika wakati mgumu jana asubuhi baada ya waandishi wa habari kumbana awape maelezo endapo hawatakiwi kwenye mkutano huo.
Waandishi hao walitaka Marmo aeleze kwanini amekiuka ahadi aliyoitoa mwanzoni kuwa waandishi wa habari wangeruhusiwa kuingia katika mkutano huo na kwanini vyombo vingine viliruhusiwa na vingine kukataliwa. Chombo kilichoruhusiwa katika mkutano huo ni TBC1 pekee.
Hata hivyo, Waziri Marmo hakutaka kujibu swali hilo akieleza kuwa ana haraka, kitendo ambacho kiliwafanya waandishi wa habari wamzuie kwa nguvu na kuendelea kumhoji.
Baadaye Marmo aliwaomba waandishi hao kutulia akiwaahidi kwamba wataingia katika majadiliano, lakini pia hakutekeleza ahadi yake hiyo.
Jana niliona hali inataka kuchafuka ndiyo sababu nikiwa kama mwenyekiti nikachukua hatua ile ya kuwafukuza. naomba mnisamehe na hao TBC1 walirusha zile habari kimakosa walitakiwa wachukue picha kwa ajili ya kumbukumbu za kiofisi tu,.
Rais Kikwete alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na viongozi wa dini katika semina ya siku mbili iliyoandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu na kufanyika katika Hoteli ya WhiteSands jijini Dar s Salaam.
Tumeendelea kuboresha Sheria ya Gharama za Uchaguzi, lakini, lile la takrima ni gumu. Mfano katika mkoa wa Kilimanjaro huwezi kuwaita wazee ukazungumza nao bila kitochi, alisema Kikwete.
Kitochi ni kipimo cha lita moja ya pombe ya kienyeji aina ya mbege inayotengenezwa mkoani Kilimanjaro.
Rais aliendelea kusema Wakati wa kampeni mwaka 2005 nilifika mahali wakawa wananiambia, mzee hili ni jambo la kawaida hata Chadema, CUF wakija wanafanya hivi, hiyo ni sehemu muhimu kwao, huwezi kuwaita wazee bila mbege.
Katika kuthibitisha kauli yake hiyo Rais Kikwete alimtaka mmoja wa maaskofu wanaotoka Kanda ya Kaskazini kueleza endapo inawezakana kuwaita wazee wa mkoa huo bila kitochi.
Askofu huyo ambaye jina lake halikufahamika mara moja, alimjibu Kikwete "Kwa kweli hili haliwezekani. Hiyo ni sehemu ya maisha ya watu wa Kilimanjaro."
Baada ya jibu hilo la askofu, ukumbi mzima akiwa Rais Kikwete mwenyewe ulilipuka kwa kicheko na baadaye rais aliendelea kuzungumza na viongozi hao bila kusema nini kifanyanyike ili sheria hiyo iweze kutekelezeka maeneo kama hayo.
Kwa mujibu wa Rais Kikwete kabla ya kutungwa kwa Sheria hii mpya ya Gharama za Uchaguzi, hali ilikuwa mbaya kiasi kwamba kabla ya mtu kufikiria kugombea, alianza kufikiri kwanza jinsi ya kupata fedha za kununua watu ili wampitishe kwenye kura za maoni.
Mwende mkawahubirie watu kuwa wawachague watu wenye nia njema, watakaoweza kuliendeleza taifa, msiengemee chama chochote na pia tuendelee kukumbushana kuyakubali matokeo, aliagiza Rais Kikwete.
Katika hatua nyingine, Rais Kikwete pia alitumia fursa hiyo kuwaonya viongozi hao juu ya tabia inayoanza kujitokeza ya dini moja kuikejeli dini nyingine.
Alisema ingawa Tanzania ina uhuru wa kuabudi, pale dini yoyote itakapofanya kitendo hicho hadharani, serikali itaingilia kati.
Wengine wanasema kuwa tunaingilia uhuru wa kuabudu, lakini siyo kweli, sisi sheria zetu zinasema usikejeli dini ya mwenzako, ukifanya hivyo sisi tunaingilia kati, alisema Kikwete.
Kikwete pia alisisitiza umuhimu wa kushirikiana kati ya viongozi wa dini na serikali akieleza kuwa pande hizo zote zina lengo moja la kutaka upendo na maendeleo kwa jamii.
Alisema wakati mwingine serikali inaweza kufanya jambo ambalo kwa namna moja au nyingine linaweza kuwakera viongozi hao wa dini na kuwa hali hiyo itakapotokea, viongozi hao wasisite kuwasiliana naye moja kwa moja au kupitia mawaziri.
Sisi wote ni binadamu kwa hiyo tutaweza kukosea lakini, nyie mna watu, unaweza kumwambia waziri au mtu mwingine amwambie waziri mkuu kuwa mnataka kuonana naye au aniambie mimi.Pia mnaweza kutumia simu yangu iko wazi muda wote unaweza kunipigia uniambie moja kwa moja, alisisitiza Kikwete.
Awali Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Iringa Dk Owdemburg Mdegella alisema kikao hicho kimepitisha maazimio saba ambayo pande zote mbili; serikali na viongozi wa dini wamekubali kuyatekeleza.
Kwa kuwa Serikali imeona umuhimu wa kutayarisha Sheria ya Gharama za Uchaguzi na kuwashirikisha viongozi wa dini ili kuielewa, kuijadili na kuifikisha kwa waumini; viongozi wa dini tunapongeza na kuhimiza serikali kuwa waaminifu katika kuitekeleza, alisema Askofu Dk Mdegella.
Alisoma maazimio hayo kuwa ni serikali kuweka utaratibu maalum wa kukutana na viongozi wa dini mara mbili kwa mwaka na Serikali kudumishe utaratibu wa kutumia mtandao wa viongozi wa dini kwa kupanua wigo wa ushiriki ili kufikisha taarifa sahihi kwa jamii yote.
Maazimio mengine ni viongozi wa dini washirikishwe mapema katika hatua za awali wakati wa kushughulikia masuala mbalimbali muhimu ya kitafa na viongozi wa dini wasishabikie siasa katika nyumba za ibada.
Kwa mujibu wa Askofu Mdegella maazimio mengine ni ilani za vyama vya siasa zitayarishwe kwa namna ambayo hazitawagawa Watanzania kwa misingi ya dini, kabila, rangi, jinsi ama eneo analotoka na Serikali na taasisi za dini na zile za kijamii zishirikiane kuandaa mikakati endelevu ya maadili ya kitaifa
Rais Kikwete alikubali hoja zote zilizofikiwa katika mkutano huo akipendekeza kuwa katika suala la kukutana mara mbili kwa mwaka na viongozi hao, ligawanywe katika mafungu mawili.
Alisema fungu la kwanza liwe lile la kukutana na viongozi kutoka katika madhehebu na jumuiya mbalimbali kwa nyakati tofauti na lile la pili viongozi wote wa dini na serikali wakutane kwa wakati mmoja.
Hata hivyo, kama ilivyokuwa katika siku ya kwanza ya mkutano huo, wahandishi wa habari jana pia hawakuruhusiwa kuingia katika mkutano huo wakati majadiliano hayo yanaendelea.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Uratibu na Bunge) ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa Mkutano huo, Philip Marmo alikijiuta katika wakati mgumu jana asubuhi baada ya waandishi wa habari kumbana awape maelezo endapo hawatakiwi kwenye mkutano huo.
Waandishi hao walitaka Marmo aeleze kwanini amekiuka ahadi aliyoitoa mwanzoni kuwa waandishi wa habari wangeruhusiwa kuingia katika mkutano huo na kwanini vyombo vingine viliruhusiwa na vingine kukataliwa. Chombo kilichoruhusiwa katika mkutano huo ni TBC1 pekee.
Hata hivyo, Waziri Marmo hakutaka kujibu swali hilo akieleza kuwa ana haraka, kitendo ambacho kiliwafanya waandishi wa habari wamzuie kwa nguvu na kuendelea kumhoji.
Baadaye Marmo aliwaomba waandishi hao kutulia akiwaahidi kwamba wataingia katika majadiliano, lakini pia hakutekeleza ahadi yake hiyo.
Jana niliona hali inataka kuchafuka ndiyo sababu nikiwa kama mwenyekiti nikachukua hatua ile ya kuwafukuza. naomba mnisamehe na hao TBC1 walirusha zile habari kimakosa walitakiwa wachukue picha kwa ajili ya kumbukumbu za kiofisi tu,.