Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,620
- 46,264
Baada ya Mkuu mpya wa KKKT, Askofu Malasusa kutoa kauli kwamba hajalelewa kuwa kinyume na serikali kuliibuka maneno makali na shutuma kutoka kwa wafuasi wa CHADEMA. Askofu Shoo mkuu aliyestaafu wa KKKT yeye alishutumiwa kujiegemeza zaidi kwa upinzani.
Viongozi wa BAKWATA wao hushutumiwa na wapinzani kujiegemeza zaidi kwa CCM, Katoliki wao hushutumiwa kwamba kelele zao huwa kubwa sana anapokuwa sio mtu wa kwao tofauti akiwa ni wa kwao.
Sasa kukata mzizi wa fitna kuna njia mbili tu. Ya kwanza ni kuruhusu Viongozi wa dini kushiriki siasa za upande wanaoupenda kikamilifu kama zilivyo nchi nyingi ambazo dini ni kitu muhimu sana kwao mfano Kenya, Marekani, Africa Kusini n.k Katika hizi nchi viongozi wa dini huchukua misimamo yao na kusimama na vyama au wanasiasa wanaowakubali kikamilifu bila kujiibaiba na kelele za kinafiki za kutochanganya dini na siasa.
Njia ya pili ni ya China na nchi nyingi za mashariki ya mbali ambazo kwao dini inawekwa mbali kabisa na masuala yoyote ya kisiasa. Yani viongozi wa dini hakuna kuzungumza masuala ya siasa kabisa, hakuna kualikwa katika shughuli za serikali na China wameenda mbali zaidi hata kupendelea viongozi wa chama na serikali kutokuwa watu wa kidini.
Kama nchi na vyama vya siasa ni vyema kuchagua njia moja na kuondoa mjadala kabisa wa kanisa fulani, taasisi fulani ya kidini au kiongozi fulani wa dini fulani wamechotwa na chama fulani au ni waserikali. Ni vyema kuachana na mijadala ya kitoto kwa kuruhusu na kuwa na misimamo thabiti ya wazi inayoeleweka.
Viongozi wa BAKWATA wao hushutumiwa na wapinzani kujiegemeza zaidi kwa CCM, Katoliki wao hushutumiwa kwamba kelele zao huwa kubwa sana anapokuwa sio mtu wa kwao tofauti akiwa ni wa kwao.
Sasa kukata mzizi wa fitna kuna njia mbili tu. Ya kwanza ni kuruhusu Viongozi wa dini kushiriki siasa za upande wanaoupenda kikamilifu kama zilivyo nchi nyingi ambazo dini ni kitu muhimu sana kwao mfano Kenya, Marekani, Africa Kusini n.k Katika hizi nchi viongozi wa dini huchukua misimamo yao na kusimama na vyama au wanasiasa wanaowakubali kikamilifu bila kujiibaiba na kelele za kinafiki za kutochanganya dini na siasa.
Njia ya pili ni ya China na nchi nyingi za mashariki ya mbali ambazo kwao dini inawekwa mbali kabisa na masuala yoyote ya kisiasa. Yani viongozi wa dini hakuna kuzungumza masuala ya siasa kabisa, hakuna kualikwa katika shughuli za serikali na China wameenda mbali zaidi hata kupendelea viongozi wa chama na serikali kutokuwa watu wa kidini.
Kama nchi na vyama vya siasa ni vyema kuchagua njia moja na kuondoa mjadala kabisa wa kanisa fulani, taasisi fulani ya kidini au kiongozi fulani wa dini fulani wamechotwa na chama fulani au ni waserikali. Ni vyema kuachana na mijadala ya kitoto kwa kuruhusu na kuwa na misimamo thabiti ya wazi inayoeleweka.