JK aenda Uingereza kikazi

IMG_1034.JPG



JK AELEKEA UINGEREZA LEO KWA ZIARA YA KIKAZI

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Bwana Said Meck Sadick muda mfupi kabla ya kuondoka nchini leo asubuhi kuelekea Uingereza kwa ziara ya kikazi.(picha na Freddy Maro).

Huyu tangu aingie madarakani anaitwa ni RAIS WA NCHI ZA NJE na si Rais wa Tanzania. Kwanini hizi safari asimwachie Bernad Membe ambaye ni Waziri wa Mambo ya nje??

Hakika JK anatia aibu maana kila siku yuko nje ya nchi na ndiyo maana kuna matukio yanayolikumba Taifa letu na yeye akiwa hana habari kabisa au kwa yale anayoyajua HUYAKIMBIA!!!!

Katika awamu zote za Urahisi,JK ndiyo ameonekana kuwa Rais dhaifu,mbambaishaji na asiyejiamini kwa jambo lolote!
 
Mara baada ya safari ya Davos and then Ethiopia, kuna uzi ulitoa record ya mweshimiwa kuwa alikuwa katimiza safari 322 (Sina hakika kama na ya Ethiopia ilikuwa Inclusive) anyway, hesabu za haraka haraka, kiongozi wa ngazi yake anapokuwa Abroad hupewa kama Us$ 450 kwa siku, tufanye huwa nje kwa siku 4 then chukua 322+1 ya leo utapata safari 323 siku 4 each safari ni kama siku 1292 hizo ndizo siku alizo kaa nje ya nchi yake so zidisha mara dola 450 jibu ni US$ 145350/= zidisha kwa Tsh (exchange rate 1550:1) jibu ni 225292500/ za kibongo, hiyo ni kwake pekee yake, ukichukulia msafara wake huwa na watu 20 mara hiyo pesa, jibu waweza pata mwenyewe, namtamani malaria Sugu na Faiza Fox hapa watusaidie.
 
Nimesikiliza taarifa ya habari ya saa 2 usiku TBC wanasema ilikuwa muhimu rais aende kwa sababu wanamtegemea sana atoe ushauri kwa mambo yanayoendelea Somalia.

Nimesoma comments za watu wengi wanasema badala ya kusema Rais anatakiwa afanye nini watu wanakosoa. Sisi kama wananchi tulitegemea anajua anatakiwa afanye nini ndio maana aliomba achaguliwe kuwa Rais wa nchi hii na baadhi ya watu ambao walikuwa wengi zaidi walimchagua wakijua kuwa ana maono ya kuwatoa watu katika dimbwi la umaskini. Nadhani hata yeye ameshajua hawezi kwahiyo ameona bora liende, na nchini ameshapaona pachungu hakukaliki. Haingii akilini eti unaonekena ni mshauri mzuri kwa nyumbani ya jirani lakini wanao wana matatizo hata kugusia hakuna unajifanya kama vile kila kitu kiko sawa.

Watu wanaotaka kuwa ma rais 2015 wafikiri mara 2 kama hawana maono yakutuvusha wakae pembeni kwasababu Rais anayekuja ana kazi kubwa sana. Tuhesabu miaka 10 (2005 - 2015) imepotea bure.
 
Huwa najiuliza rais Kikwete haguswi hata kidogo na masuala ya watanzania kama ufisadi na mauaji ya watu yanayofanywa na polisi kwa makusudi? Hivi hakuna kabisa hatua tunayoweza kuchukua?
 
Tanzania on sale

safari moja uanzisha nyingine, safari ni safari bora mguu uingie kwenye ndege. ongera baba chepe kwa kubandika kibandiko mlangoni cha malaria haikubaliki bali safari za nje zinakubalika,
 
Mara baada ya safari ya Davos and then Ethiopia, kuna uzi ulitoa record ya mweshimiwa kuwa alikuwa katimiza safari 322 (Sina hakika kama na ya Ethiopia ilikuwa Inclusive) anyway, hesabu za haraka haraka, kiongozi wa ngazi yake anapokuwa Abroad hupewa kama Us$ 450 kwa siku, tufanye huwa nje kwa siku 4 then chukua 322+1 ya leo utapata safari 323 siku 4 each safari ni kama siku 1292 hizo ndizo siku alizo kaa nje ya nchi yake so zidisha mara dola 450 jibu ni US$ 145350/= zidisha kwa Tsh (exchange rate 1550:1) jibu ni 225292500/ za kibongo, hiyo ni kwake pekee yake, ukichukulia msafara wake huwa na watu 20 mara hiyo pesa, jibu waweza pata mwenyewe, namtamani malaria Sugu na Faiza Fox hapa watusaidie.

Kwa mkuu huyu ni mara chache kukaa siku 4 huwa anakaa si chini ya siku 10. Naomba usifanye mahesabu utaumia zaidi
 
jamani mbona kiama tunacho lakini tulimchagua wenyewe mbona masalma hasikiki siku hizi kuna nini?????????????????????
 
Nimesikiliza taarifa ya habari ya saa 2 usiku TBC wanasema ilikuwa muhimu rais aende kwa sababu wanamtegemea sana atoe ushauri kwa mambo yanayoendelea Somalia.

Nimesoma comments za watu wengi wanasema badala ya kusema Rais anatakiwa afanye nini watu wanakosoa. Sisi kama wananchi tulitegemea anajua anatakiwa afanye nini ndio maana aliomba achaguliwe kuwa Rais wa nchi hii na baadhi ya watu ambao walikuwa wengi zaidi walimchagua wakijua kuwa ana maono ya kuwatoa watu katika dimbwi la umaskini. Nadhani hata yeye ameshajua hawezi kwahiyo ameona bora liende, na nchini ameshapaona pachungu hakukaliki. Haingii akilini eti unaonekena ni mshauri mzuri kwa nyumbani ya jirani lakini wanao wana matatizo hata kugusia hakuna unajifanya kama vile kila kitu kiko sawa.

Watu wanaotaka kuwa ma rais 2015 wafikiri mara 2 kama hawana maono yakutuvusha wakae pembeni kwasababu Rais anayekuja ana kazi kubwa sana. Tuhesabu miaka 10 (2005 - 2015) imepotea bure.
Kama ni Somalia afadhali hata Mwai Kikaki maoni yake yatakuwa muhimu kuliko Kikwete. Kibaki ana majeshi yake kule yanapambana na Al Shabab. Sasa ni ushauri gani huo ambao lazima aufungie safari hadi London. Anadhani wote ni mazuzu.
 
Hata kama akipata safari ya lazima tayari watanzania hawana tena imani naye kutokana na safari nyingi anazofanya zisizo na tija kwa taifa
 
Fofofo unataka hoja gani zaidi zijengwe dhidi ya safari anazofanya mkweree zaidi ya kuwa safari hizo anzofanya ni ghali sana na sisi walipa kodi zinatuumiza hasa ikikumbiukwa kuwa zahanati zetu hazina dawa na serikali haina pesa mpaka inawakopa wastaafu mishahara yao!! Unasema humtetei mkweree lakini ukweli ni kwamba unamtetea yeye pamoja na maslahi yako wewe mwenyewe unayopata pale mnaposafiri nae!!
 
nimeona raisi mmoja wa west africa atakaa mkutano ukiisha Thursday ataonana na wananchi wake then kugeuza, na wakati wa mkutano ataonana na Price of wales na ameingia leo Wed. sijui JK aliwahi nini

na anarudi lini TZ? hivi tunapewaga timetable ya safari zake au?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom