Jihadhari na Mfuko wa Plastic (Rambo) Barabarani

Karibu sana, Ila tu mimi si Kaka ni Dada, nimekusamehe bila malipo

Nashukuru kwa taarifa mkuu lakini kwenye post yako umesema kati ya waliopatwa na hili tatizo ni mke wako na hapa unasema wewe nidada umenichanganya
 
Nyie madreva wa bongofleva, mnaponzwa na magari ya automatic kiasi kwamba hata kwenda veta mkapate shule ya nidhamu ya barabarani hakuna.
Hapo juu nilikoweka rangi ndo 'nidhamu ya dereva' akiwa barabarani si mchana au usiku.
Kabla ya kupata leseni za vishoka, pitieni driving school utafundishwa hayo.

asante mkuu,sasa ni vizuri na wewe ungetoa msaada jinsi ya kujilinda.
 
Tunashukuru kwa taarifa mkuu lakini hii mifuko ya Rambo inakazi nyingi mno! kuna maeneo fulani ya uswazi (Uswahilini) huwa wao wanaiita ni selfconteiner yaani wanaitumia kwaajili yakuendea haja, alfajiri na mapema we damka uone watu wanavyopishana na mifuko ya Malboro kwenda kutupa vinyesi.
 
Asante kwa taarifa muhimu. Kwa njia hii pia tunaweza kuimarisha ulinzi shirikishi kwa kupeana taarifa za kuzuia halifu.
 
Intelijensia iko wapi? Waambieni wapande plaiveti ka na vyuma vya moto, wapitie mitaa ya hizo rambo zenu wapate pancha zenu hizo. Kibaka na bange zake akijipendekeza atenguliwe nyonga, kiuno au hata ugoko. Maumivu yakizidi apelekwe kwa daktari. Tuna mambo ya kuhangaika nayo ebo! Asante anyway kwa info mkuu.
 
Amavubi
Asante sana kwa taarifa zako ambazo ni nzuri na muhimu sana
Ila mbona unajichanganya
Angalia ulivyoanza thread umesema walioumizwa sana ni pamoja na Mke wangu
Then hapo chini comment iliyofuata unasema sio kaka ni dada
Inakuwaje hapo
Inaonyesha kuwa ni habari muhimu ya ki_umbea umbea asante kwa tahadhari hii ya muhimu dume jike
 
Amavubi
Asante sana kwa taarifa zako ambazo ni nzuri na muhimu sana
Ila mbona unajichanganya
Angalia ulivyoanza thread umesema walioumizwa sana ni pamoja na Mke wangu
Then hapo chini comment iliyofuata unasema sio kaka ni dada
Inakuwaje hapo

Usimwamini muongo hata kama anasema ukweli
 
Nyie madreva wa bongofleva, mnaponzwa na magari ya automatic kiasi kwamba hata kwenda veta mkapate shule ya nidhamu ya barabarani hakuna.
Hapo juu nilikoweka rangi ndo 'nidhamu ya dereva' akiwa barabarani si mchana au usiku.
Kabla ya kupata leseni za vishoka, pitieni driving school utafundishwa hayo.
Kweli mkuu, unajua niliposoma huu uzi nimeshangaa kuwa kuna 'dereva' anayetahadharishwa asikanyage hivyo vitu kama vile ni kawaida wa madereva kuvikanyaga! Lakini umenikumbusha kuwa kuna wale wa vyuo vya kata!!!
 
Intelijensia iko wapi? Waambieni wapande plaiveti ka na vyuma vya moto, wapitie mitaa ya hizo rambo zenu wapate pancha zenu hizo. Kibaka na bange zake akijipendekeza atenguliwe nyonga, kiuno au hata ugoko. Maumivu yakizidi apelekwe kwa daktari. Tuna mambo ya kuhangaika nayo ebo! Asante anyway kwa info mkuu.
Haahaaahaaaa! Asante mkuu kwa kunivunja mbavu.. Tatizo ni kuwa ili hiyo operation iwepo lazima wakubwa wao wakae kama kwa siku mbili 'kupanga' hiyo 'mikakati', walipane posho ya kukaa, ndo waidhinishe hiyo kitu...
 
Asante kwa taarifa muhimu sana@ Amavubi... Ila watu wameconcentrate kwenye jambo ambalo,uhalisia wake unaujua wewe mwenyewe... Kama Amavubi ni F au ni M...na ama Mrembo ni F au M...na ama hao wawili ni mtu mmoja mwenye ID mbili tofauti,na tena jinsia ni siri yake..
 
Asante kwa taarifa muhimu sana@ Amavubi... Ila watu wameconcentrate kwenye jambo ambalo,uhalisia wake unaujua wewe mwenyewe... Kama Amavubi ni F au ni M...na ama Mrembo ni F au M...na ama hao wawili ni mtu mmoja mwenye ID mbili tofauti,na tena jinsia ni siri yake..
Pamoja mkuu....imeandikwa.....waacheni watoto wadogo waje kwangu.......................
 
Intelijensia iko wapi? Waambieni wapande plaiveti ka na vyuma vya moto, wapitie mitaa ya hizo rambo zenu wapate pancha zenu hizo. Kibaka na bange zake akijipendekeza atenguliwe nyonga, kiuno au hata ugoko. Maumivu yakizidi apelekwe kwa daktari. Tuna mambo ya kuhangaika nayo ebo! Asante anyway kwa info mkuu.

He he daktari kagoma mkuu,maumivu yakizidi aende kwa mganga wa kienyeji
 
KUMEZUKA WIMBI JIPYA LA UHALIFU, HII IKO NAMNA HII:-

UNAKUTA MFUKO WA NYLON( MAARUFU KAMA MIFUKO YA CONDOM,RAMBO,PLASTIC) BARABARANI. UKIUKANYAGA TU LAZIMA UTAPATA PUNCHER MAANA NDANI YAKE KUNA KIBAO KILICHOPIGILIWA MISUMARI ZAIDI YA UNAVYOFIKIRIA WEWE.

UKISHUKA GARINI KUANGALIA KULIKONI WIMBI LA VIBAKA LINAKUVAMIA NA HAKUNA UTAKACHOBAKIA NACHO ZAIDI YA GARI MAANA LITAKUWA HALINA UPEPO BAADHI YA MAGURUDUMU.VIBAO NI VINGI KWA UMBALI MFUPI MFUPI.

HII IMETOKEA JANA TABATA KISUKURU MAENEO YA MAKOKA MIDA YA SAA TATU USIKU. WALIOPATA PUNCHER NI PAMOJA NA MKE WANGU NA MAGARI MENGINE KIBAO, WALIOLIFANIKIWA KUIBIWA SIJAPATA TAARIFA BADO ILA TULIJI-ORGANISE NA KUPITA NJIA ZOTE NA KUVUKUSANYA.

WATAKUPIGA KIASI GANI HIYO INATEGEMEA KIWANGO CHA BANGI WALICHOVUTA NA UNAJEURI KIASI GANI.

TAHADHARI.

USIKANYAGE MFUKO WA NYLON ( KWEPA). UKIKANYAGA BAHATI MBAYA JIANDAE VYEMA KABLA YA KUSHUKA GARINI AU TEMBEA NA PUNCHER UMBALI KIDOGO.

MTAARIFU NA MWENZAKO.

__._,_.___


To photos, videos, and web pages.

Karibu sana, Ila tu mimi si Kaka ni Dada, nimekusamehe bila malipo


Mkuu umesema waliopata pancha ni pamoja na mke wako, halafu unasema wewe si kaka ni dada, pamekaaje hapo?
 
Back
Top Bottom