Je, Viongozi wa Idara ambao ni Wachagga waachie ngazi!??

Status
Not open for further replies.
Haya mambo ya wingi wa wachagga katika nafasi mbalimbali yana chanzo chake. Ikitokea kazi yoyote sasa hivi wengi watakaoomba na sifa kuwanazo bila shaka ni wachagga. La kujiuliza ni kwamba hali hii imetokeaje?
Kiini kipo kwenye elimu. Wakati moto wa shule za kata ndio kwanza unashika kasi baadhi ya maeneo Tanzania, watu wa Kilimanjaro waliliona hilo miaka mingi iliyopita na kuhakikisha wanakuwa na shule za kata. Hawakuishia hapo. Walikwenda pia katika mikoa mingine ambako wenyeji bado walikuwa usingizini kielimu nako wakasoma tena kwa bidii na malengo. Sasa kama hali ndiyo hii, nani na kulaumiwa?
hata leo kuna maeneo ambayo hata ukijenga shule bure bado zinakosa wanafunzi wa kusoma kwa kuwa wazazi hawataki watoto wao wasome. Nani alaumiwe kwa haya yote?
Ufumbuzi si kuwazuia wachagga. Ufumbuzi ni kuhakikisha watu wa maeneo mengine wanasoma pia na hii itakuja kama watapata mwamko wa elimu. Haya yakifanyika, matunda yaweza kuonekana baada ya kipindi cha miaka ishirini hivi na hakuna njia ya mkato.
Kwa wakati huu, wengine wataendelea kuwa machinga na vibarua kwa wale waliokwenda shule. Au tuseme wote tukiwa mameneja, nani atakuwa tarashi? Njia ya kukwepa utarishi ni moja tu: shule!!!
 
Sisi wachagga tunaapa: Tutaendelea kukamata nafasi nyeti serikalini, kwenye siasa, kwenye mashirika ya uma na ya watu binafsi, Tutaendelea kukamata Elimu nzuri, Tutaendelea kuongoza kwenye biashara, Tutaendelea kuoa/kuolewa na watu wenye madaraka makubwa serikalini na kwenye taasisi nyeti, Tutaendelea kujipendelea kila inapowezekana.

Hakuna mtu wa kutuzuia kwa kuwa tumedhamiria na hatutarudi nyuma.

Ahsante Mungu kwa kutupendelea na kuendelea kutubariki.

Wenye wivu na Wajinyonge, lakini Mungu awasamehe kwa kuwa hawajui walitendalo.

Amina.
 
MwanaKijiji hii ina ukweli ndani yake.
Angalia TRA wamejaa wachagga kweli na wanapendeleana kweli ukienda mzaramu au msukuma na aende mchagga utaona wewe utakavyo kadiriwa kodi ni tofauti na mchagga.
Hata ukikuta mwalimu mchagga atapendelea mchagga naona ndio mafunzo ya kichagga kupendeleana.
Hii ina ukweli chunguzeni.
 
MwanaKijiji hii ina ukweli ndani yake.
Angalia TRA wamejaa wachagga kweli na wanapendeleana kweli ukienda mzaramu au msukuma na aende mchagga utaona wewe utakavyo kadiriwa kodi ni tofauti na mchagga.
Hata ukikuta mwalimu mchagga atapendelea mchagga naona ndio mafunzo ya kichagga kupendeleana.
Hii ina ukweli chunguzeni.

Mkishamaliza mawivu yenu, mtupigie makofi.

Nyie endeleeni kulalama, sisi tunasonga mbele.
 
Sisi wachagga tunaapa: Tutaendelea kukamata nafasi nyeti serikalini, kwenye siasa, kwenye mashirika ya uma na ya watu binafsi, Tutaendelea kukamata Elimu nzuri, Tutaendelea kuongoza kwenye biashara, Tutaendelea kuoa/kuolewa na watu wenye madaraka makubwa serikalini na kwenye taasisi nyeti, Tutaendelea kujipendelea kila inapowezekana.

Hakuna mtu wa kutuzuia kwa kuwa tumedhamiria na hatutarudi nyuma.

Ahsante Mungu kwa kutupendelea na kuendelea kutubariki.

Wenye wivu na Wajinyonge, lakini Mungu awasamehe kwa kuwa hawajui walitendalo.

Amina.
Mungu hana upendeleo hata kidogo
 
A MODEST PROPOSAL

Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna vumbi la chuki, fitina, wivu, kisasi, na hisia za kibaguzi dhidi ya jamii ya Wachagga nchini. Kuna kila dalili kuwa jamii ya Wachagga nchini siyo tu inaanza kutengwa lakini uwepo wake katika nafasi mbalimbali za uongozi inazua hoja ya ukabila kwa haraka zaidi yawezekana kuliko kabila jingine lolote nchini. Katika Tanzania yetu, wachagga wameanza kunyoshewa kidole siyo kwa siri tena bali kwa wazi kabisa tena na watu ambao wakati mwingine hawapati hata kigugumizi.

Ubaguzi huo msingi wake mkubwa ni idadi ya wachagga katika nafasi mbalimbali za uongozi na hasa kuhusiana na elimu yao. Kuanzia mara tu baada ya uhuru jamii ya wachagga mojawapo ya jamii ambayo watu wake wengi wamesoma sana na kufanikiwa kielimu na kiuchumi imekuwa ikinyoshewa kidole cha kupendelewa.

Mtu yeyote ambaye anaweza akafanya uchambuzi yakinifu hatoshangaa kukuta wataalamu wa kichagga katika nafasi mbalimbali za uongozi au taaluma nchini. Kwenye vyuo vikuu, kwenye idara za serikali na hata kwenye taasisi binafsi kumejaa watu wenye asili ya mkoa wa Kilimanjaro na hususan watu wa jamii ya Kichagga.

Endapo itatangazwa nafasi yoyote ya kitaalamu usishangazwe ukiona kuwa waombaji wengi wana majina ya "Kichagga".

Ni kwa sababu hiyo basi kuna kila dalili kuwa kutokana na wingi wao katika nafasi muhimu na vyeo mbalimbali (hata ndani ya Jeshi la Polisi) Wachagga siyo tu ni wengi lakini wanaonekana kufanikiwa zaidi. Hili ni tishio kwa baadhi ya watu. Ni tishio kwa watu ambao hawako tayari kuangalia jitihada za watu katika kufanikiwa kwao na matokeo yake kushutumu ukabila kila idadi ya Wachagga kwenye kitengo fulani inazidi mmoja.

Ushauri wangu ni kuwa, kwa vile Wachagga wameshasoma sana na kuendelea katika biashara karibu mikoa mingi nchini. Na kwa vile wanaendelea kufanikiwa pia katika nafasi mbalimbali za uongozi nchini, basi itakuwa vizuri kama watajitolea kuachilia nafasi hizo ili kuwapa nafasi watu wa makabila mengine.

Kwa vile ni wao wanaonekana kulalamikiwa kutokana na mambo ya kifisadi aidha kwa moja kwa moja au kwa kuashiria basi ni vizuri wawape watu wengine nafasi hizo hata kama watu hao hawajasoma sana. Hii yote itakuwa ni katika kudumisha mshikamano, umoja na udugu wa Taifa letu.

Endapo Wachagga wataachilia nafasi mbalimbali kama UCEO, Ukurugenzi, Ukuu wa Idara n.k watasababisha watu wawapende na kuwakubali kuwa ni wazalendo wa kweli. Sitoshangaa kuwa ndugu zetu wa Jamii ya Kichagga wakikaa pembeni, basi ufisadi utakoma serikalini, idara zitaongozwa na watu wazuri, na mara moja na daima Tanzania itaanza kukua katika uongozi.

Kwa kupendekeza nashauri wabunge wote ambao ni Wachagga au wana asili ya mkoa wa Kilimanjaro kuachia ngazi mara moja ili watu wa makabila mengine wapewe nafasi hizo. Siyo wao tu bali pia wabunge ambao wameoa au kuolewa uchagani vile vile wafuate nyazo hizo.

Wakishamaliza hao, wakuu wote wa idara za serikali ambao wana asili ya mkoa wa Kilimanjaro na hasa wa jamii ya kichagga (wamarangu, wamachame, wa Rombo, na wa Kibosho) na wao waamue kuachilia nafasi hizo kwa ndugu zao Wamakua, Wamwera, Wa Ndali, Wadigo n.k Katika hili Wapare hawahusishwi.

Tukishamaliza wakuu hao wa idara za serikali ningependekeza madaktari wote wenye kumiliki hospitali binafsi ambao ni wachagga au wameoa/kuolewa uchagani na wenyewe waamue kuingia ubia na watu wa makabila mengine kama wangengereko, wambuu, na wanjiro ili hayo makabila madogo na wenyewe wapate nafasi ya kujifunza fani hizi muhimu.

Zaidi ya yote, majaji na mahakimu wote ambao wana asili ya Uchaggani na wenyewe waamue kujitoa katika nafasi hizo kwani wingi wao pia unaonekana sana na hivyo kuwa kikwako kwa watu wa makabila mengine kufanikiwa zaidi katika nyanja ya sheria. Kwanza kabisa wale majaji wa Kichagga wa mahakama ya Rufaa na Mahakama Kuu wawe wa kwanza kuweka manyanga chini.

Katika kufanya hivyo jamii ya Watanzania ambao inaona ukabila wa wachagga katika sehemu nyingi itaridhika kwani kwa mara ya kwanza tutakuwa tumeshughulikia chanzo cha matatizo yetu mengi.

Mwanakijiji; yawezekana wewe ukawa tatizo namba moja. Umewezaje kulitolea jibu swali ambalo halipo au umelianzisha mwenyewe, ukalijadili na kulitolea ushauri mwenyewe! Huo ni upembuzi wa level gani?

By the way huwezi ukamwachia mzembe kiutendaji au ukaachia nafasi ya kazi kwa goigoi ambaye hata sababu za msingi hakuna -eti kujenga mshikamano! Mshikamano upi hasa? Wanaoogopa kujiendeleza waje wasubirie kuachiwa nafasi na wachagga wanaotaka kuendeleza mshikamano?

Wanaoanzisha watoto madrassa na kuwachelewesha kusoma lugha zisizolenga kumpa upanuzi wa akili ndio unashauri wachagga wawaachie nafasi kuimarisha mshikamano na ndio hao hao wanaotangaza kuwa serikali imekuwa ikiwapa nafasi wakristu, hoja ambazo hazina tija?...na pia unataka wachagga waache kusoma au kujiendeleza kwa kuogopa kuja kuambiwa 'wengi wamesoma na hivyo inabidi wawaachie wengine nafasi'?

Na wachaga watakapoacha kujiendeleza au waache kusoma ili ku-balance na waliofanya uzembe kujiendeleza au pale ambapo serikali imezembea kuwaendelea, kwa maana yako - unataka nchi nzima watu wake wote warudi hatua nyuma, wenye elimu warudi nyuma, wasitende kazi ili ku-neutralize perception ya wachache kuwa wataonekana wapo wengi maeneo ya kazi! Huo ni upofu, na dalili za kuelekea kupungukiwa ktk judgement na arguments.


Katika nchi yoyote duniani, hata Marekani, Ufaransa, UK, Canada, Israel na penginepo; kuna makundi ya jamii fulani ambazo ni lazima ziwepo na ndio msingi wa mafanikio na challenge kwa mataifa husika ikianzia na uongozi, biashara, siasa, elimu, technologia na hata maeneo ya majeshi...! Hii haikwepeki au haizuiliki.

Na kama Mwanakijiji umeshindwa kutafakari haya na kupata majibu sahihi, basi dira na mwelekeo wa ujenzi wa Taifa ni finyu au umeshindwa kuupatia mwongozo sahihi kwa nia ya kuwaelimisha wengine. Hapa unawapotosha na kuwaaminisha kuwa Wachagga na 'Uchagga' vinaelekea kuwa hoja ya kitaifa badala la mambo mengine ya msingi. Unawakengeua watanzania ambao wengi wamekombolea kutokana na mafanikio ya Kabila hili, aidha kea ajira, kibiashara, kisiasa, au aina nyingiezo za kijamii.


Kwa taarifa yako, Kisiasa, Mkoa wa Kilimanjaro na Wachagga wenyewe wameanza kujitambua hata kabla ya miaka ya 1870 hadi 1900, wachagga hawakukubali Ukoloni ukanyage ktk ardhi yao kirahisi. Hata Wakoloni walipojiimarisha maeneo mengine ya Tanganyika, ilibidi wafanye mbinu kubwa sana kuwapata watu wachache kuwaelimisha ili hatimaye waje wawtumie kama chambo ili kuingia kuwatawala, au hata kukusanya kodi, mambo ambayo pia walikwama, hadi ilipofika miaka ya 1945 hadi 1960, ndio wakifikia hatua angalau za kusema wachagga wamejigawa kuukubali uhuru wa kuongozwa toka makao makuu ya Tanganyika - enzi hizo, chini ya Governor aliyekabidhi jukumu kwa waziri mkuu Nyerere na hatimaye kuwa Rais.


Kwa dokezo hilo fupi unaweza kutambua kuwa wachagga hawajaanzia 'kuona mbele' ktk tawala hizi za awamu ya pili, ya tatu na ya nne kama unavyoliwasilisha, bali mizizi yao ipo mbali kuliko unavyodhamiria kuliweka watanzania walipokee. Kuna mamia ya Watanzania wameweka makazi Mitaa kibao ya Uingereza, Marekani, Botswana, Kenya nk, hasa utadhani ni kama wenyeji. Na wenginea wanafundisha vyuo vikuu kibao ktk nchi hizo na nyinginezo kibao. Je na hao wakirudi Tanzania utawaambiaje? Waachane na elimu na utajiri wao li wafanane na wengine ili tu kujenga mshikamano?
Hapo umepotoka. Hivyo nchi haifiki popote!

Tuijadili hali hii na niliyoyadokeza, hakika tuwe na 'Critical Thinking' na sio 'superficially' -ya kijuujuu tu ili kuwapendeza tu baadhi ya watu. Tanzania inahitaji wasomi, watu wanaoweza kuzalisha, wenye skills na resources mbalimbali ktk kulikomboa taifa na sio mkusanyiko wa watu wanaopenda kuonekana maskini, wanaojirudisha nyuma au waoga, na wanaoona wengine kuwa wamefika mbali ambapo wao kamwe hawatofika - eti wamekata tamaa! Wanabaki kushikilia dhana potofu kama ukabila, udini nk..! La hasha Mwanakijiji!


Naomba kuwasilisha!
 
Ninafikiri huyu ni Mwanakijiji akijifunza kuwa "satirist" kwa kufuata nyayo za Satirist John Swift, the original author of "A Modest Proposal".
 
Mwanakijiji; yawezekana wewe ukawa tatizo namba moja. Umewezaje kulitolea jibu swali ambalo halipo au umelianzisha mwenyewe, ukalijadili na kulitolea ushauri mwenyewe! Huo ni upembuzi wa level gani?

By the way huwezi ukamwachia mzembe kiutendaji au ukaachia nafasi ya kazi kwa goigoi ambaye hata sababu za msingi hakuna -eti kujenga mshikamano! Mshikamano upi hasa? Wanaoogopa kujiendeleza waje wasubirie kuachiwa nafasi na wachagga wanaotaka kuendeleza mshikamano?

Wanaoanzisha watoto madrassa na kuwachelewesha kusoma lugha zisizolenga kumpa upanuzi wa akili ndio unashauri wachagga wawaachie nafasi kuimarisha mshikamano na ndio hao hao wanaotangaza kuwa serikali imekuwa ikiwapa nafasi wakristu, hoja ambazo hazina tija?...na pia unataka wachagga waache kusoma au kujiendeleza kwa kuogopa kuja kuambiwa 'wengi wamesoma na hivyo inabidi wawaachie wengine nafasi'?

Na wachaga watakapoacha kujiendeleza au waache kusoma ili ku-balance na waliofanya uzembe kujiendeleza au pale ambapo serikali imezembea kuwaendelea, kwa maana yako - unataka nchi nzima watu wake wote warudi hatua nyuma, wenye elimu warudi nyuma, wasitende kazi ili ku-neutralize perception ya wachache kuwa wataonekana wapo wengi maeneo ya kazi! Huo ni upofu, na dalili za kuelekea kupungukiwa ktk judgement na arguments.


Katika nchi yoyote duniani, hata Marekani, Ufaransa, UK, Canada, Israel na penginepo; kuna makundi ya jamii fulani ambazo ni lazima ziwepo na ndio msingi wa mafanikio na challenge kwa mataifa husika ikianzia na uongozi, biashara, siasa, elimu, technologia na hata maeneo ya majeshi...! Hii haikwepeki au haizuiliki.

Na kama Mwanakijiji umeshindwa kutafakari haya na kupata majibu sahihi, basi dira na mwelekeo wa ujenzi wa Taifa ni finyu au umeshindwa kuupatia mwongozo sahihi kwa nia ya kuwaelimisha wengine. Hapa unawapotosha na kuwaaminisha kuwa Wachagga na 'Uchagga' vinaelekea kuwa hoja ya kitaifa badala la mambo mengine ya msingi. Unawakengeua watanzania ambao wengi wamekombolea kutokana na mafanikio ya Kabila hili, aidha kea ajira, kibiashara, kisiasa, au aina nyingiezo za kijamii.


Kwa taarifa yako, Kisiasa, Mkoa wa Kilimanjaro na Wachagga wenyewe wameanza kujitambua hata kabla ya miaka ya 1870 hadi 1900, wachagga hawakukubali Ukoloni ukanyage ktk ardhi yao kirahisi. Hata Wakoloni walipojiimarisha maeneo mengine ya Tanganyika, ilibidi wafanye mbinu kubwa sana kuwapata watu wachache kuwaelimisha ili hatimaye waje wawtumie kama chambo ili kuingia kuwatawala, au hata kukusanya kodi, mambo ambayo pia walikwama, hadi ilipofika miaka ya 1945 hadi 1960, ndio wakifikia hatua angalau za kusema wachagga wamejigawa kuukubali uhuru wa kuongozwa toka makao makuu ya Tanganyika - enzi hizo, chini ya Governor aliyekabidhi jukumu kwa waziri mkuu Nyerere na hatimaye kuwa Rais.


Kwa dokezo hilo fupi unaweza kutambua kuwa wachagga hawajaanzia 'kuona mbele' ktk tawala hizi za awamu ya pili, ya tatu na ya nne kama unavyoliwasilisha, bali mizizi yao ipo mbali kuliko unavyodhamiria kuliweka watanzania walipokee. Kuna mamia ya Watanzania wameweka makazi Mitaa kibao ya Uingereza, Marekani, Botswana, Kenya nk, hasa utadhani ni kama wenyeji. Na wenginea wanafundisha vyuo vikuu kibao ktk nchi hizo na nyinginezo kibao. Je na hao wakirudi Tanzania utawaambiaje? Waachane na elimu na utajiri wao li wafanane na wengine ili tu kujenga mshikamano?
Hapo umepotoka. Hivyo nchi haifiki popote!

Tuijadili hali hii na niliyoyadokeza, hakika tuwe na 'Critical Thinking' na sio 'superficially' -ya kijuujuu tu ili kuwapendeza tu baadhi ya watu. Tanzania inahitaji wasomi, watu wanaoweza kuzalisha, wenye skills na resources mbalimbali ktk kulikomboa taifa na sio mkusanyiko wa watu wanaopenda kuonekana maskini, wanaojirudisha nyuma au waoga, na wanaoona wengine kuwa wamefika mbali ambapo wao kamwe hawatofika - eti wamekata tamaa! Wanabaki kushikilia dhana potofu kama ukabila, udini nk..! La hasha Mwanakijiji!


Naomba kuwasilisha!
Well said kiongozi. Waambie watu waache kulialia hovyo. Waamke wachape kazi.


The Following User Says Thank You to Msaki001 For This Useful Post:

Asprin (Today)​
 
Kama post hii angeiweka mgeni hapa Jf kamwe tungehoji uwezo wake wa kufikiri,lakini ikija kwa ID kama hii basi inazua maswali mengi zaidi ya majibu. Nakumbuka mwalimu wangu nikiwa fom3 alileta maswali page moja nzima ila akasema maswali yajibiwe nyuma ya karatasi ya maswali yan kwa ufipi majibu pia si zaid ya page. Sa mwanakijiji umeleta maswali zaidi ya hoja yako. Lakini bila kujiuliza maswali zaidi mi nadhani tatizo si uchaga. Mwl.JKN alikemea ukabila na udini ila hakuutokomeza. Umekaa mioyon mwa watu sasa ndo unarudi. Hilo jambo liliwakumba ata wahaya. Mpaka mwl akasema hafikirii kama mchaga au mhaya atawahi kuwa Rais. Huo ndo ukabila wenyewe. Mwanakijiji mi si mchagga ila tangu nzaliwe sijawahi kusoma popote job qualification ikawa ni uchaga,aya ni maneno ya watu. Kwa mawazo yako,kweli uwezekano mkubwa upo mchaga anatuingiza mkenge lakini kwa nini sie tumelala?tumesubiri elimu ianze kutolewa kama viti maalum? Haiwezekani tuamke tushindane tuwang'oe wachaga kihalali ila si kuwaachisha ngazi. Sehemu muhimu ni ngumu na wazaramo,watindiga,nk ni wavivu pia mi nawahusisha na watu wa imani moja au utamaduni mmoja. Mfano,watu wanalalama eti benki wamejaa wachaga sasa nenda vyuoni kama IFM, UDSMbcom TIA ,IAA,SAUT b/admin. fanya risechi utakuta kila chuo kozi tajwa apo juu 50%+ ni wachaga wakati wazaramo pale magomen wanafunga barabara kucheza ngoma. Hapa mabinti wako bize kutafuta hina na udi mzuri wakati Manka,Mushi wanatoka madarasan kukimbia kuwapokea zamu wazee wao pale madukani au bar counter! Unategemea baadae uyu mchenza ngoma awe benki baada ya miaka3, haiwezekani! Kukemewa kwa ukabila waliukubali wahaya kimyakimya ila hata nipingwe apa nenda sehemu yoyote duniani utakuta kama kuna mhaya yuko brilliant! Hata watu wanaulizana,ukimwona mhaya mbumbumbu ujue kachangia damu na wageni wa uhaya! Ila tukija hadharani tunawapinga kujiridhisha. Mi sio mdini ila angalia hata mabalozi wa Roma/papa duniani watokao Tanzania wengi ni wahaya na wachaga mapadre! Prove me wrong if u can! Haya makabila hayabebwi na pale yanapobebwa yanabebeka kirahisi! Jaman naomba tuwe na torelance kwa wanaotaka kujikwamua! Ila kama kuna mafisadi basi hawajatuma na kabila labda utueleza kama wakishapora rasilimali zetu wanapeleka hesabu kwa viongoz wa makabila. Tusifike huko! Mwl nyerere alisema kila mtu akiulizwa alifikaje Tanzania,hamna atakaesalia wote ni wa kuja. Mwanakijiji nadhani hapa unaielewa historia ya Tz kuanzia wangoni, wairak,wahaya,wachaga ,wapemba nk. Tukianza kutafuta Wazanzibar wenye asili ya Z'bar kamwe akina Karume na Seif watarudi kwao. Ielewe historia ya zbar si ngumu ata ukibase kuanzia 1840 utapata ukweli. Hata wale wanaojiita wazaramo pia hawajazaliwa Dsm labda kama hauitaki historia. Kwa kudokeza wazaramo wengi ni Wahaya na Wasukuma ambao walitoka Mwanza na kanda ya ziwa wakileta biashara zao dar na kushindwa kurudi wakaitwa Wazamiaji,yani 'kibantu ni wazaramo'hawa walianzia sehemu za watumwa kama mwembetogwa leo hii paitwa fire kuelekea mtongani na katikati pale walikuwa wanauza watumwa waliofungwa minyororo kooni/shingoni pakaitwa kariakoo! Hii ni historia na tukiielewa makabila hawatachukiana. Kabaka wa Buganda aliambiwa na British missionary kwamba Those who shall destroy your kingdom shall come from the west,basi kila mfanyabiashara alipoingia Buganda kupitia magharibi Kabaka alimnyonga. Tusifike huko,tusinyongane,mwache kila mwenye akili halali aitumie Kihalali,cha muhimu tulinde maadili. ChristMass njema mwanakijiji wa Ughaibuni.
 
Jamani wachagga sio wafanyabiashara ni wachuuzi "petty traders" hawana mchango wowote kwenye uchumi wa nchi. Hakuna mchagga hata mmoja aliyesajiri biashara yake DSE. Hata huko serikalini wamepungua sana na wachache ndo hao akina Mgonja Kweka Mramba Masawe, wameshakuwa wateja wa akina Mkono Magafu Makani!

Haters wa wachagga ni wengi hakuna mfano....

lakini mkubali mkatae mkoa wa kilimanjaro umeendelea kwa juhudi za wakazi wake......

mfano mdogo...wakati miji na vijiji vingi nchini vimejaa nyumba za nyasi full suit...kwa wachagga siku hizi HAKUNA MTU MWENYE NYUMBA YA NYASI,.....HATA LOFA WA MWISHO ANA NYUMBA YA BATI......LAKINI ASILIMIA 90 % YA NYUMBA NI ZA MATOFALI ....NA NYINGI NI ZA KISASA.....KAMA ZA MBEZI BEACH .....hili sitanii ...ambaye haamini ...aombe kumtembelea rafiki yake yeyote hususan msimu huu wa sikukuu kijijini ili aweze kuona mwenyewe tofauti kubwa ya kimakazi kati ya vijiji vya uchagani na ...mikoa mingine.....sasa hivi familia zinashindana kujenga angalau gorofa kwa kila kaya....

.......wachagga wengi tu wameajiriwa kwenye international organisations ..ambao waanaangalia sifa na si kabila la mtu..wapo lesotho,botswana,ulaya na amerika.....wanajuwa kuwa wanaonewa wivu kwa hiyo wanajitahidi zaidi ....

......aliyeanza kuwachukia wachaga sio kikwete ni nyerere....pamoja na mazuri yake ..ukweli nyerere hakuwapenda wachagga..ambao utawala wa mangi hata kabla ya uhuru ulikuwa pekee tanganyika uliokamilika kidola ukiwa na mfumo wake wa utawala...,bunge na ikulu ya kisasa[ilitaifishwa],BENDERA,siku ya wachagga[chagga day],mfumo wa elimu,kilimo,vyou [chuo cha ushirika,uwalimu etc]..kituo cha utafiti wa kahawa,hoteli ya kitaliii ..na akiba ya fedha za kigeni ...[paundi milioni 2]...KNCU ndio ilikuwa ikitumika kama chombo cha uwekezaji cha CHAGGA COUNCIL....hiii tofauti ilianza zamani na hata kabla kabisa ya uhuru ilipelekea chifu wa wachaga kutaka kujitenga na Tanganyika na kuunda jamhuri ya kilimanjaro...[arusha,tanga na kilimanjaro]...hofu hii ilifanya mwalimu toka awali awa black list wachaga kwenye uongozi wa juuu nchini.....na hata kuharibu historia yao kwa kutaifisha mali za chagga concil ikiwemo akiba yao ya fedha....katika kufanikisha kuvunja umoja wa chagga council...mwalimu alitumia mbinu ya mkoloni ya devide and rule.....akitumia mwanya uliotokea wakati wa uchaguzi mkuu wa chagga council....miaka ya nyuma na kumteua solomoni eliufoo toka kwenye kundi la chama kilichoshindwa uchaguzi..kwenye serikali yake ya awali[1960]....chagga walikuwa na vyama vya kisiasa

Lakini napenda tujue kuwa hii nchi haiataendelea kama baadhi ya watu ...wataendelea kutumiwa kama punda tu ......na kutengwa kwenye fursa za kuwa na madaraka ya juu nchini hasa urais na waziri mkuu......sasa kibaya ni kuwa hata huku chini ambako kunataka utaalamu mnataka kuwatenga nako....lakini ukweli ni kuwa historia ya kujivunia ya mafanikio inakuwa kama kiyoo kwa watoto wa jamii ya chagga hata wale ambao hawajawahi kufika vijijini!
 
watu wengi hawajui kuwa hoteli ya mwanzo ya kitalii ikimilikiwa Taasisi ya kiuchumi ya CHAGGA COUNCIL -kncu....ndio lilikuwa jengo la kwanza kwa ukanda huu kuwa na LIFT ya umeme......ile hoteli inakaribia miaka 80 na ile lift bado ipo ...nadhani watunzani wa historia inabidi wakaihifadhi ile lift kama lift ya kwanza kabisa Tanganyika....na ya pili ukiondoa jengo la mwanzo kuwa na lift pale nairobi kwa afrika mashariki na kati............pia ni vema ile hoteli ikakaraabatiwa katika hali yake halisi ili kuhifadhi historia ya mwanzo ya utalii nchini....
 
Hivi kweli hizo nafasi hao wachagga walipewa kwa kujuana au kwa elimu yao??

tuache hizi hila za kichagaa zitatupeleka pabaya sana...

mbona hamuongelei wahaya au wanyakyusa...


Tupige vita ukabila..
 
Mama kwenye hiyo directorate Wachagga wataruhusiwa kuomba nafasi? Je Mchagga ataruhusiwa kuwemo katika nafasi za uongozi wa hiyo directorate? Binafsi nisingependa wachagga wawemo...

Kama nimekuelewa vizuri, umeandika kwa fasihi kubwa sana ukijitahidi kuonyesha jiitihada za jamii fulani, mafanikio na wivu kutoka jamii nyingine. Mwalimu alijaribu kupunguza kasi ya [wakilimanjaro] hasa upande wa sekondari alipoondoa mtihani wa kitaifa ambao nusu ya waliofaulu walitoka mkoa huo. Nafasi zikagawiwa kimikoa, hata ile watu wasiojali elimu walipewa nafasi kujaza idadi. Wakilimanjaro wakaazisha private schools, wakiuza kahawa na ndizi wanasomesha watoto. Wale waliopata upendeleo wa bure watoto wao wakawa hawajishughulishi shuleni, matokeo yake idadi ya wanaoingia chuo kikuu ikawa inatoka kule kule katika private schools.
Ni makosa kuivuta jamii moja nyuma isubiri nyingine isiyo na hamasa. Kulalamika kuwa mchaga ni daktari haina mantiki kwasababu daktari hachaguliwii, engineer hachaguliwii wala mwanasheria au mhasibu. Hadi hapo jamii zingine zitakapoona umuhimu wa elimu na si ngoma au unyago, tuwaache waliiona mbele na watazame.
Hii ni sawa na kumwambia Mwanakijiji asisome vitabu ili asiwe na hoja kwa kumsubiri Nguruvi3 siku atakapoamua kusoma vitabu wawe sawa !!!!!
 
sawa wachaga wakishaachia ngaza kabila gani lifuatie? wanyakusa, wazaramo, wahehe wasukuma au?
 
Kama nimekuelewa vizuri, umeandika kwa fasihi kubwa sana ukijitahidi kuonyesha jiitihada za jamii fulani, mafanikio na wivu kutoka jamii nyingine. Mwalimu alijaribu kupunguza kasi ya [wakilimanjaro] hasa upande wa sekondari alipoondoa mtihani wa kitaifa ambao nusu ya waliofaulu walitoka mkoa huo. Nafasi zikagawiwa kimikoa, hata ile watu wasiojali elimu walipewa nafasi kujaza idadi. Wakilimanjaro wakaazisha private schools, wakiuza kahawa na ndizi wanasomesha watoto. Wale waliopata upendeleo wa bure watoto wao wakawa hawajishughulishi shuleni, matokeo yake idadi ya wanaoingia chuo kikuu ikawa inatoka kule kule katika private schools.
Ni makosa kuivuta jamii moja nyuma isubiri nyingine isiyo na hamasa. Kulalamika kuwa mchaga ni daktari haina mantiki kwasababu daktari hachaguliwii, engineer hachaguliwii wala mwanasheria au mhasibu. Hadi hapo jamii zingine zitakapoona umuhimu wa elimu na si ngoma au unyago, tuwaache waliiona mbele na watazame.
Hii ni sawa na kumwambia Mwanakijiji asisome vitabu ili asiwe na hoja kwa kumsubiri Nguruvi3 siku atakapoamua kusoma vitabu wawe sawa !!!!!

Umenena, Mimi nilielewa kama ulivyoelewa wewe.
 
a modest proposal

na. M. M. Mwanakijiji

kuna vumbi la chuki, fitina, wivu, kisasi, na hisia za kibaguzi dhidi ya jamii ya wachagga nchini. Kuna kila dalili kuwa jamii ya wachagga nchini siyo tu inaanza kutengwa lakini uwepo wake katika nafasi mbalimbali za uongozi inazua hoja ya ukabila kwa haraka zaidi yawezekana kuliko kabila jingine lolote nchini. Katika tanzania yetu, wachagga wameanza kunyoshewa kidole siyo kwa siri tena bali kwa wazi kabisa tena na watu ambao wakati mwingine hawapati hata kigugumizi.

Ubaguzi huo msingi wake mkubwa ni idadi ya wachagga katika nafasi mbalimbali za uongozi na hasa kuhusiana na elimu yao. Kuanzia mara tu baada ya uhuru jamii ya wachagga mojawapo ya jamii ambayo watu wake wengi wamesoma sana na kufanikiwa kielimu na kiuchumi imekuwa ikinyoshewa kidole cha kupendelewa.

Mtu yeyote ambaye anaweza akafanya uchambuzi yakinifu hatoshangaa kukuta wataalamu wa kichagga katika nafasi mbalimbali za uongozi au taaluma nchini. Kwenye vyuo vikuu, kwenye idara za serikali na hata kwenye taasisi binafsi kumejaa watu wenye asili ya mkoa wa kilimanjaro na hususan watu wa jamii ya kichagga.

Endapo itatangazwa nafasi yoyote ya kitaalamu usishangazwe ukiona kuwa waombaji wengi wana majina ya "kichagga".

Ni kwa sababu hiyo basi kuna kila dalili kuwa kutokana na wingi wao katika nafasi muhimu na vyeo mbalimbali (hata ndani ya jeshi la polisi) wachagga siyo tu ni wengi lakini wanaonekana kufanikiwa zaidi. Hili ni tishio kwa baadhi ya watu. Ni tishio kwa watu ambao hawako tayari kuangalia jitihada za watu katika kufanikiwa kwao na matokeo yake kushutumu ukabila kila idadi ya wachagga kwenye kitengo fulani inazidi mmoja.

Ushauri wangu ni kuwa, kwa vile wachagga wameshasoma sana na kuendelea katika biashara karibu mikoa mingi nchini. Na kwa vile wanaendelea kufanikiwa pia katika nafasi mbalimbali za uongozi nchini, basi itakuwa vizuri kama watajitolea kuachilia nafasi hizo ili kuwapa nafasi watu wa makabila mengine.

Kwa vile ni wao wanaonekana kulalamikiwa kutokana na mambo ya kifisadi aidha kwa moja kwa moja au kwa kuashiria basi ni vizuri wawape watu wengine nafasi hizo hata kama watu hao hawajasoma sana. Hii yote itakuwa ni katika kudumisha mshikamano, umoja na udugu wa taifa letu.

Endapo wachagga wataachilia nafasi mbalimbali kama uceo, ukurugenzi, ukuu wa idara n.k watasababisha watu wawapende na kuwakubali kuwa ni wazalendo wa kweli. Sitoshangaa kuwa ndugu zetu wa jamii ya kichagga wakikaa pembeni, basi ufisadi utakoma serikalini, idara zitaongozwa na watu wazuri, na mara moja na daima tanzania itaanza kukua katika uongozi.

Kwa kupendekeza nashauri wabunge wote ambao ni wachagga au wana asili ya mkoa wa kilimanjaro kuachia ngazi mara moja ili watu wa makabila mengine wapewe nafasi hizo. Siyo wao tu bali pia wabunge ambao wameoa au kuolewa uchagani vile vile wafuate nyazo hizo.

Wakishamaliza hao, wakuu wote wa idara za serikali ambao wana asili ya mkoa wa kilimanjaro na hasa wa jamii ya kichagga (wamarangu, wamachame, wa rombo, na wa kibosho) na wao waamue kuachilia nafasi hizo kwa ndugu zao wamakua, wamwera, wa ndali, wadigo n.k katika hili wapare hawahusishwi.

Tukishamaliza wakuu hao wa idara za serikali ningependekeza madaktari wote wenye kumiliki hospitali binafsi ambao ni wachagga au wameoa/kuolewa uchagani na wenyewe waamue kuingia ubia na watu wa makabila mengine kama wangengereko, wambuu, na wanjiro ili hayo makabila madogo na wenyewe wapate nafasi ya kujifunza fani hizi muhimu.

Zaidi ya yote, majaji na mahakimu wote ambao wana asili ya uchaggani na wenyewe waamue kujitoa katika nafasi hizo kwani wingi wao pia unaonekana sana na hivyo kuwa kikwako kwa watu wa makabila mengine kufanikiwa zaidi katika nyanja ya sheria. Kwanza kabisa wale majaji wa kichagga wa mahakama ya rufaa na mahakama kuu wawe wa kwanza kuweka manyanga chini.

Katika kufanya hivyo jamii ya watanzania ambao inaona ukabila wa wachagga katika sehemu nyingi itaridhika kwani kwa mara ya kwanza tutakuwa tumeshughulikia chanzo cha matatizo yetu mengi.
wachaga waacheni wawe juu na wazidi kuendelea-jamii zote hazwez kuwa sawa-ndio maana ujamaa ulishindikana-ukianza na wachaga leo kesho utakuja na kabila wengine-waacheni wawe juu na wazidi kuwa juu-hata mungu alisema mwenye nacho huongezewa-thus naomba wazid kuongezewa zaid na zaid
 
Haya Maswala ya Kabila Fulani Kuwepo Sehemu Mbalimbali Nchini ni Tatizo Lakini Tuangaliea Kwenda Mbele Kwamba Haya Matatizo Yanaletwa na Uongozi Mbaya. Kama Kweli Wachaga Wanashikilia Hizi Nafasi na Ni Nafasi za Serikali. Hii Sio Picha Nzuri kwa Nchi, Lazima Tudiversify Nchi Kwani Nchi Sio ya Kabila Moja. Kitu Kingine cha Kuangalia ni Swala la Ajira Tanzania, Hili Swala la Ajira ni Tatizo Kubwa na Kama Nchi Tunategemea Kazi Zijengwe na Serikali Badala ya Policy Makers Kuimarisha Private Sectors, Tupo Njiani Kupata Matatizo Makubwa. Tukianngalia Nchi Imekuwa Ikiongozeka na Population Ipo 43million Mark na Namba ya Vijana Nchini Inazidi Kukua. Sisi Wananchi Tuhakikishe Tunajenga Katiba ili Kuimarisha Sehemu Zote za Serikali na Policies.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom