ToR za directorate ziwe brainstormed openly na mapendekezo yawe open. By the way wanaweza fanya needs assessment ili kujua hiyo directorate ifanye nini kwa kanuni zipi. Na Director au wafanyakazi wa hiyo directorate wasiwe wachaga, wanyakyusa, wasukuma, wapare wala wahaya. Watoke kwenye minority and under-represented groups. Ila makabila yapewe fursa sawa katika kuomba kazi.
ToR za directorate ziwe brainstormed openly na mapendekezo yawe open. By the way wanaweza fanya needs assessment ili kujua hiyo directorate ifanye nini kwa kanuni zipi. Na Director au wafanyakazi wa hiyo directorate wasiwe wachaga, wanyakyusa, wasukuma, wapare wala wahaya. Watoke kwenye minority and under-represented groups. Ila makabila yapewe fursa sawa katika kuomba kazi.
..nategemea Mama Fatma Maghimbi wa CUF naye atashughulikiwa maana mumewe ametokea Kilimanjaro.
sasa wapewe nafasi miority groups japokuwa mtu mwenye uwezo kwa nafasi ile anatoka kwenye majority group?
si itakuwa kujinyima maendeleo huko?
Mzee Mwanakiji,
Naona sasa, Unaanza kujishushia heshima, Kila ukiamka Udini, Ukabila......Mambo unayoyandakika Humu yanasomwa na watanzania mamilioni.Na kama mengi ninavyoyaona unayaweka katika Hali ya Uchochezi.
Unapoona Vita vinaendelea nchi nyingine usidhani vilikuja tu, Kenya kwa ajili ya Mashada forums kuongelea Ukabila na kuweka probaganda za ugawanishi ndio zilichochea yale yaliyotokea last decembere.
Amani Tanzania hailindwi kwa uandishi unaoufanya sasa, Amani Tanzania Inakuja kwa kuchambua mambo yanayoweza kutijenga.
Swala unaliongelea kwasasa ni issue ya HR polices za makampuni ya Bongo kuwa refined and that is what is happenning. Ila ukileta Mambo ya UDINI,UKABILA NA MENGINEYO yanayofanana na hayo utakuwa Mchochezi.
Mimi sijawahi kufeel isolated Tanzania kwasababu sio Mchaga au Dini Fulani , Because I believe on Working Hard you can be wherever you want.
Leo wewe Uko Marekani si kwababu ni Fisadi au Mchaga, Balia ni kwa juhudi zako,We need to chang the perspective of the Dialogue and bring a bit of Construtive discussion.
Mwisho kama unataka Vita Tanzania, Ili Upate makaratasi Marekani, Acha Huo Mchezo , tutakushauri njia nyingine.
MUNGU IBARIKI TANZANIA DUMIHA AMANI, TUPE MOYO WA UVUMILIVU NA TUFUNGULIE NJIA YA KUSOLVE MATATIZO YETU BILA UZUSHI
Watoto wa MKAPA ni wachagga kwasababu mama ya ni Mchagga...Lakini Obama ni Mweusi kwasababu Mama yake ni mweupe!
Make sense?
Mzee Mwanakiji,
Naona sasa, Unaanza kujishushia heshima, Kila ukiamka Udini, Ukabila......Mambo unayoyandakika Humu yanasomwa na watanzania mamilioni.Na kama mengi ninavyoyaona unayaweka katika Hali ya Uchochezi.
Unapoona Vita vinaendelea nchi nyingine usidhani vilikuja tu, Kenya kwa ajili ya Mashada forums kuongelea Ukabila na kuweka probaganda za ugawanishi ndio zilichochea yale yaliyotokea last decembere.
Amani Tanzania hailindwi kwa uandishi unaoufanya sasa, Amani Tanzania Inakuja kwa kuchambua mambo yanayoweza kutijenga.
Swala unaliongelea kwasasa ni issue ya HR polices za makampuni ya Bongo kuwa refined and that is what is happenning. Ila ukileta Mambo ya UDINI,UKABILA NA MENGINEYO yanayofanana na hayo utakuwa Mchochezi.
Mimi sijawahi kufeel isolated Tanzania kwasababu sio Mchaga au Dini Fulani , Because I believe on Working Hard you can be wherever you want.
Leo wewe Uko Marekani si kwababu ni Fisadi au Mchaga, Balia ni kwa juhudi zako,We need to chang the perspective of the Dialogue and bring a bit of Construtive discussion.
Mwisho kama unataka Vita Tanzania, Ili Upate makaratasi Marekani, Acha Huo Mchezo , tutakushauri njia nyingine.
MUNGU IBARIKI TANZANIA DUMIHA AMANI, TUPE MOYO WA UVUMILIVU NA TUFUNGULIE NJIA YA KUSOLVE MATATIZO YETU BILA UZUSHI
kuna kujifunza kuwa wakweli na kuact honestly hata kama ni kwa uchungu. Kiongozi wa hicho kitengo cha ajira akitoka kwenye minority group hata kuwa na upendeleo wa kuangalia huyu anayeomba kazi ametoka kabila gani. Atakuwa na interest ya qualifications tu as kabila lake watakuwa ni kati ya waombaji wachache.
sasa nani ataamua kuwa "Na Director au wafanyakazi wa hiyo directorate wasiwe wachaga, wanyakyusa, wasukuma, wapare wala wahaya."? Kwa hiyo itabidi tuingize kwenye sheria kipengele kinachokataza hivi siyo? Na hao watakaotunga sheria hizo miongoni mwao wawemo wachagga, wanyakyusa, wasukuma, wapare na wahaya? Au itatungwa na Bunge la Minorities?
sasa mushi obama anaingia vipi hapa?
nitakupa definition kidogo kama huelewi:
mweusi anakuwa mweusi ikiwa bibi yake mmoja ni mweusi, haitegemei bibi upande gani even
mngazija,mchaga,mpemba wanakuwa makabila hayo ukioa, ukiolewa na mtoto pia anakuwa kabila hilo hata kama ukoo wa upande wa baba ni kabila jengine
gaijin said:mama maghimbi anasameheka manake damu ya mpemba kama ya mchaga.....ukioa au ukiolewa na mpemba na wewe unageuka mpemba.....na watoto wanageuka wapemba japo kama mama yao tu ni mpemba.lol
sasa huyo director kutoka minority group, akiona kuwa kuna minority katika waombaji tena kutoka kabila lake awape ka"upendeleo" ka aina fulani? Tutamzuiaje yeye kutowapendelea watu wa kabila lake au kula njama na minority mwingine ili wabadilishane wanaowapendelea ili wasioneshe ukabila "mkwere ampendelee msegeju, na msegeju ampendelee mkwere"?
A MODEST PROPOSAL
Na. M. M. Mwanakijiji
Kuna vumbi la chuki, fitina, wivu, kisasi, na hisia za kibaguzi dhidi ya jamii ya Wachagga nchini. Kuna kila dalili kuwa jamii ya Wachagga nchini siyo tu inaanza kutengwa lakini uwepo wake katika nafasi mbalimbali za uongozi inazua hoja ya ukabila kwa haraka zaidi yawezekana kuliko kabila jingine lolote nchini. Katika Tanzania yetu, wachagga wameanza kunyoshewa kidole siyo kwa siri tena bali kwa wazi kabisa tena na watu ambao wakati mwingine hawapati hata kigugumizi.
A MODEST PROPOSAL
Na. M. M. Mwanakijiji
Kuna vumbi la chuki, fitina, wivu, kisasi, na hisia za kibaguzi dhidi ya jamii ya Wachagga nchini. Kuna kila dalili kuwa jamii ya Wachagga nchini siyo tu inaanza kutengwa lakini uwepo wake katika nafasi mbalimbali za uongozi inazua hoja ya ukabila kwa haraka zaidi yawezekana kuliko kabila jingine lolote nchini. Katika Tanzania yetu, wachagga wameanza kunyoshewa kidole siyo kwa siri tena bali kwa wazi kabisa tena na watu ambao wakati mwingine hawapati hata kigugumizi.
Ubaguzi huo msingi wake mkubwa ni idadi ya wachagga katika nafasi mbalimbali za uongozi na hasa kuhusiana na elimu yao. Kuanzia mara tu baada ya uhuru jamii ya wachagga mojawapo ya jamii ambayo watu wake wengi wamesoma sana na kufanikiwa kielimu na kiuchumi imekuwa ikinyoshewa kidole cha kupendelewa.
Mtu yeyote ambaye anaweza akafanya uchambuzi yakinifu hatoshangaa kukuta wataalamu wa kichagga katika nafasi mbalimbali za uongozi au taaluma nchini. Kwenye vyuo vikuu, kwenye idara za serikali na hata kwenye taasisi binafsi kumejaa watu wenye asili ya mkoa wa Kilimanjaro na hususan watu wa jamii ya Kichagga.
Endapo itatangazwa nafasi yoyote ya kitaalamu usishangazwe ukiona kuwa waombaji wengi wana majina ya "Kichagga".
Ni kwa sababu hiyo basi kuna kila dalili kuwa kutokana na wingi wao katika nafasi muhimu na vyeo mbalimbali (hata ndani ya Jeshi la Polisi) Wachagga siyo tu ni wengi lakini wanaonekana kufanikiwa zaidi. Hili ni tishio kwa baadhi ya watu. Ni tishio kwa watu ambao hawako tayari kuangalia jitihada za watu katika kufanikiwa kwao na matokeo yake kushutumu ukabila kila idadi ya Wachagga kwenye kitengo fulani inazidi mmoja.
Ushauri wangu ni kuwa, kwa vile Wachagga wameshasoma sana na kuendelea katika biashara karibu mikoa mingi nchini. Na kwa vile wanaendelea kufanikiwa pia katika nafasi mbalimbali za uongozi nchini, basi itakuwa vizuri kama watajitolea kuachilia nafasi hizo ili kuwapa nafasi watu wa makabila mengine.
Kwa vile ni wao wanaonekana kulalamikiwa kutokana na mambo ya kifisadi aidha kwa moja kwa moja au kwa kuashiria basi ni vizuri wawape watu wengine nafasi hizo hata kama watu hao hawajasoma sana. Hii yote itakuwa ni katika kudumisha mshikamano, umoja na udugu wa Taifa letu.
Endapo Wachagga wataachilia nafasi mbalimbali kama UCEO, Ukurugenzi, Ukuu wa Idara n.k watasababisha watu wawapende na kuwakubali kuwa ni wazalendo wa kweli. Sitoshangaa kuwa ndugu zetu wa Jamii ya Kichagga wakikaa pembeni, basi ufisadi utakoma serikalini, idara zitaongozwa na watu wazuri, na mara moja na daima Tanzania itaanza kukua katika uongozi.
Kwa kupendekeza nashauri wabunge wote ambao ni Wachagga au wana asili ya mkoa wa Kilimanjaro kuachia ngazi mara moja ili watu wa makabila mengine wapewe nafasi hizo. Siyo wao tu bali pia wabunge ambao wameoa au kuolewa uchagani vile vile wafuate nyazo hizo.
Wakishamaliza hao, wakuu wote wa idara za serikali ambao wana asili ya mkoa wa Kilimanjaro na hasa wa jamii ya kichagga (wamarangu, wamachame, wa Rombo, na wa Kibosho) na wao waamue kuachilia nafasi hizo kwa ndugu zao Wamakua, Wamwera, Wa Ndali, Wadigo n.k Katika hili Wapare hawahusishwi.
Tukishamaliza wakuu hao wa idara za serikali ningependekeza madaktari wote wenye kumiliki hospitali binafsi ambao ni wachagga au wameoa/kuolewa uchagani na wenyewe waamue kuingia ubia na watu wa makabila mengine kama wangengereko, wambuu, na wanjiro ili hayo makabila madogo na wenyewe wapate nafasi ya kujifunza fani hizi muhimu.
Zaidi ya yote, majaji na mahakimu wote ambao wana asili ya Uchaggani na wenyewe waamue kujitoa katika nafasi hizo kwani wingi wao pia unaonekana sana na hivyo kuwa kikwako kwa watu wa makabila mengine kufanikiwa zaidi katika nyanja ya sheria. Kwanza kabisa wale majaji wa Kichagga wa mahakama ya Rufaa na Mahakama Kuu wawe wa kwanza kuweka manyanga chini.
Katika kufanya hivyo jamii ya Watanzania ambao inaona ukabila wa wachagga katika sehemu nyingi itaridhika kwani kwa mara ya kwanza tutakuwa tumeshughulikia chanzo cha matatizo yetu mengi.