Je, kipaumbele cha CCM ni kuendelea kusalia madarakani au ni kuwaletea maendeleo Watanzania?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,162
Kutokana na mlolongo wa matukio yanayotokea nchini, nimekuwa nikijiuliza Sana, je kipaumbele Cha CCM, ni kuendelea kubaki madarakani au ni kuwaletea maendeleo watanzania?

Kipaumbele Cha utawala wowote wa serikali ni kuwaletea maendeleo wananchi wake na kama wasipofanya hivyo, watajikuta wanapigwa chini katika uchaguzi unaofuata.

Hali ni tofauti Sana nchini kwetu, Kwa kuwa ndani ya nchi hii, katika utawala wa CCM kipaumbele Chao kikubwa ni kuhakikisha kuwa chama Chao Cha CCM kinaendekea kubaki madarakani, Kwa njia zozote zile, ziwe za haramu au hallali, lakini kubaki madarakani, ndiyo priority no one kwao!

Ipo mifano mingi, mmojawapi wa mifano hiyo ni kuwa Kwa kutumia vyombo vya dola, kuhakikisha kuwa chama kilichopo madarakani, kinaendekea kusalia madarakani miaka yote.

Hiyo hali haihitaji ushahidi, Kwa kuwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, enzi za utawala wa Mwendazake, Hayati Magufuli, Dkt Bashiru Ally, aliwahi kulikiri waziwazi, mbele ya vyombo vya habari kuwa chama chale Cha CCM, kitaendelea kutumia vyombo vya dola wakati wote, kuendelea kusalia madarakani!

Hebu tujiulize ni kwanini serikali ya CCM inapata "kigugumizi" kikubwa Sana kutengeneza Katiba mpya itakayoendana na mfumo wa vyama vingi?

Jibu liko wazi, kuwa kutengeneza Katiba mpya, itakayokidhi mfumo wa vyama vingi, itakuwa sawasawa na kujitia kitanzi wenyewe CCM!

Siyo Siri tena kuwa Katiba yetu ya nchi ni ya mfumo wa chama kimoja.

ni kwanini CCM iendelee kupata "kigugumizi" kuibadilisha Katiba hiyo?

Jibu liko wazi, wao CCM wanajua kuwa wakiobadilisha Katiba hiyo na kuleta Katiba itakayokidhi mfumo wa vyama vingi, ndiyo itakuwa mwisho wa utawala wao wa kidikteta.

Hebu tujiulize, inakuwaje Rais aliyeko madarakani, ambaye pia ndiyo Mwenyekiti wa chama tawala Cha CCM, kupewa madaraka makubwa mno ya kiuteua viongozi mbalimbali wa vyombo vya dola, kama Mkuu wa Jeshi nchini, Mkuu wa Jeshi la Polisi, Jaji Mkuu, Wakuu wote wa Mikoa, wakuu wote wa wolaya, wakurugenzi wote wa wolaya (ambao ndiyo wasimamizi wakuu wa chaguzi mbalimbali kwenye maeneo yao)

Hivi Kwa kumpa madaraka makubwa kiasi hicho, ambayo ni sawasawa na kumfanya Mkuu huyo wa nchi awe dikteta, hivi nchi hii itawezaje kuifanya ipate maendeleo enddlevu?

Ndiyo maana siyo jambo la kishangaza hata kidogo Kwa nchi yetu, pamoja na kuwa tumepata huru wetu toka Kwa mkolloni zaidi ya miaka 60 hivi Sasa, nchi yetu Bado inakuwa na ukosefu wa mahitaji ya msingi wa Binadamu, ya Maji na Umeme!😎

Vyombo vya habari binafsi, ambavyo ndiyo tegemeo pekee lililokuwa limebaki Kwa watanzania, navyo vimetiwa "Kabali" na watawala na vinaelekezwa nini Cha kuripoti!

Kwa hali hiyo unategemea watawala wetu watulletee maendeleo sisi watanzania?

Jibu langu ni big NO.

Ni wazi kuwa watawala wetu, kipaumbele Chao Cha kwanza ni kuendelea kubaki madarakani FOR ANY MEANS
 
Kipaumbele Cha utawala wowote wa serikali ni kuwaletea maendeleo wananchi wake na kama wasipofanya hivyo...
 
Watanzania sio wapuuzi kama mnavyodhani, yaani ni watu wanaodhani katiba mpya ndio priority yao.

Watanzania sio wapuuzi wasio elewa stirling wa kuwachomoa anaongea lugha gani.

Asilimia kubwa ya hoja za CDM na wapinzani ni mahitaji yao (personal issues), lakini si hisia za watanzania.

Sikiliza jina la Magufuli linapotajwa mbele ya watanzania ndio utaelewa wanataka nini. Halafu jikumbushe huyo mtu alivyokuwa anaongoza nchi hiko ndio watanzania wanataka.
 
Watanzania sio wapuuzi kama mnavyodhani, yaani ni watu wanaodhani katiba mpya ndio priority yao.

Watanzania sio wapuuzi wasio elewa stirling wa kuwachomoa anaongea lugha gani...
Kama huyo unayemtaja angekuwa mpenda maendeleo ya wananchi, angeweza kuivunja Katiba ya nchi na kumwomdoa CAG kabla ya muda wake wa kustaafu?

Kumbuka kuwa CAG ndiyo "tochi" ya kuangalia matumizi yote ya serikali.

Najua kuwa "ugomvi" wa Mwendazake na CAG aliyepita, Profesa Assad ilikuwa ni kufichua wizi wa trillion 1.5 toka hazina😎
 
Kama huyo unayemtaja angekuwa mpenda maendeleo ya wananchi, angeweza kuivunja Katiba ya nchi na kumwomdoa CAG kabla ya muda wake wa kustaafu?

Kumbuka kuwa CAG ndiyo "tochi" ya kuangalia matumizi yote ya serikali.

Najua kuwa "ugomvi" wa Mwendazake na CAG aliyepita, Profesa Assad ilikuwa ni kufichua wizi wa trillion 1.5 toka hazina😎
Na sasa unadhani mambo murua au siyo.

Unacheza wewe.

Ignorance is a bliss

Muhimu ni kuelewa watanzania sio wapuuzi. Hayo mambo ya katiba mpya sio yao na hawana imani na viongozi wa upinzani.

Upinzani auwezi shinda uchsguzi ata wa haki, simply hawana majibu ya watanzania.
 
Kuweka kiingereza cha kijinga kwenye urari wa maisha ya vizazi vijavyo nao ni upuuzi.Tunajadili maisha endelevu yenye maono halafu weye unaleta hadithi za mzurulaji mbwia ugoro aliyeng'oka meno!
Ni hivi katiba mpya ni hadithi za wanaharakati uchwara na wapinzani; ila sio hoja za watanzania.

Lakini watanzania sio mafala wasiojua wanataka nini elewa hilo. Utaki endelea kuishi lala land.

Kumtukana Magufuli ni kielelezo cha ulimbukeni. You just don’t know na kucha zangu nazithamini.
 
Ni hivi katiba mpya ni hadithi za wanaharakati uchwara na wapinzani; ila sio hoja za watanzania....
Hata wakati wa kudai uhuru wa nchi hii kuna watu wenye akili mbovu kama weye waliwaaminisha wapumbavu wenzao kwamba hicho kitu kisingewezekana asilani mbele ya mkoloni.

Huwa hamuishi. Ni kama maua tu.Florida! Mnamea na kunyauka haraka!
 
Hata wakati wa kudai uhuru wa nchi hii kuna watu wenye akili mbovu kama weye waliwaaminisha wapumbavu wenzao kwamba hicho kitu kisingewezekana asilani mbele ya mkoloni.Huwa hamuishi.Ni kama maua tu.Florida!Mnamea na kunyauka haraka!
Katiba mpya sio shida ya watanzania

Na watanzania sio wapumbavu wanaona upinzani hakuna mwokozi.

Hayo mengine fantasy zako siwezi kukuzuia kuwaza.
 
Watanzania sio wapuuzi kama mnavyodhani, yaani ni watu wanaodhani katiba mpya ndio priority yao.

Watanzania sio wapuuzi wasio elewa stirling wa kuwachomoa anaongea lugha gani.

Asilimia kubwa ya hoja za CDM na wapinzani ni mahitaji yao (personal issues), lakini si hisia za watanzania.

Sikiliza jina la Magufuli linapotajwa mbele ya watanzania ndio utaelewa wanataka nini. Halafu jikumbushe huyo mtu alivyokuwa anaongoza nchi hiko ndio watanzania wanataka.
Uongo mtutu
 
Katiba mpya sio shida ya watanzania

Na watanzania sio wapumbavu wanaona upinzani hakuna mwokozi.

Hayo mengine fantasy zako siwezi kukuzuia kuwaza.
Ulikaa na kumuhoji Mtanzania mmojammoja akakueleza kwamba hitaji lake si katiba?

Mkishashiba ugali wenu na mkunungu mnawaza ujinga tu na kutumikishwa bila kujielewa.
 
Ulikaa na kumuhoji Mtanzania mmojammoja akakueleza kwamba hitaji lake si katiba?Mkishashiba ugali wenu na mkunungu mnawaza ujinga tu na kutumikishwa bila kujielewa.
Ujajifunza tu kwenye ufunguzi wa kuachia bwawa jinsi watanzania walivyomwelewa Magufuli.

Hizo hadithi za katiba mpya zipo vichwani mwenu tu, na wala hakuna kiongozi wa upinzani watanzania wanaomwamini. Ata kwa uchaguzi halali CCM inashinda asubuhi tu.
 
Back
Top Bottom