Je haiwapasi Bernard Membe na Hussein Mwinyi kujiuzulu nyadhifa zao?

jogoolashamba

JF-Expert Member
Nov 18, 2012
348
71
Yawapasa Mwinyi na Membe kuwa wangekuwa wameachia ngazi kwa matukio waliyohusika nayo. Membe kupeleka jeshi Malawi kutangaza vita, na Mwinyi kuharibu silaha za kijeshi.

Membe ana tabia ya kukurupuka ovyo mara nyingi sana na maswala ya kimataifa! Nimemsikia akikataa kwa nguvu sana kuwapa haki mashoga wakati sijaona maandamano ya hao mashoga anaopingana nao. Tanzania ushoga ni kosa la jinai kwa mujibu wa kanuni ya Adhabu, hao mashoga ambao waliopindukia sheria hiyo na kuanza kupambana naMembe ofisini kwake kweli inawezekana. hajaenda polisi kuripoti kuwa anabughudhiwa na mashoga lakini anapanda jukwaani kumlalamikia Cameroon kuwa Tanzania mashoga hawatapewa haki zao. Si kukurupuka huko na kuaibisha Taifa?

Swala la kupeleka majeshi kuzuia ndege za Malawi kuruka juu ya anga ya Malawi lilikuwa la kijinga na la kututia aibu Watanzania. Katika Mataifa ya wastaarabu kama Ulaya Membe angekuwa amekwisha kujiuzulu yeye mwenyewe kwa hiari yake, lakini kwetu Africa ukiwa rafiki wa Bosi hata ukiangamiza kaTaifa kenyewe bado uko huru kuishi na ofisi yako.

Ona Mwinyi alivyolibomoa jeshi,kwanza mabomu yote Mbagala yakalipuliwa, akaanza kwenda kutembelea wahanga sawa na mwizi aliyebomoa usiku asubuhi akaenda kuwapa pole wahanga. Kama aibu hiyo haikutosha kumlazimisha ajiuzulu akaunguza kambi yote ya Gongolamboto. Hakuna askari hata mmoja aliyejeruhiwa, nimeambiwa askari wote waliondolewa kambini kuanzia saa nane mchana. Hata ndege ya SwissAir ilitaarifiwa isishuke mchana saa nane hiyo hiyo. Nasikia SwisAir walishindwa kutekeleza onyo kwa sababu ya dege kubwa lililokuwa limejaza mafuta tele KIA na limeelekeza pua yake chini tayari kushuka, lingejaribu kugeuza pua kuielekeza juu uzito wake ungesababisha likakalia ******. Hivyo dege likalazimika kutua na Mungu Bariki likaruka tena na kuondoka kabla mabomu hayajaanza kulipuka.

Wakazi wa Gongo la Mboto hawakujulishwa wala hakukuwa na maandalizi ya ambulance wala zima moto. Atakayeniambia kuwa mabomu yaliyoanza kulipuka saa mbili usiku yalikuwa ni Accident nitataharuki. Dawa ni mihela ya walipa kodi ipo tele na wahanga wamejengewa mijumba mipya, hakuna hasara. Hata ingekuwa ajali ingemlazimu Mwinyi ajiuzulu, lakini wapi huyooo afya na huko akaenda kumteka nyara Ulimboka, na mpaka leo nchi inajulikana ina wateka nyara lakini hawajulikani, hata watuhumiwa kuhojiwa hakuna lazima. Rafiki wa JK huyo.
 
Yawapasa Mwinyi na Membe kuwa wangekuwa wameachia ngazi kwa matukio waliyohusika nayo. Membe kupeleka jeshi Malawi kutangaza vita, na Mwinyi kuharibu silaha za kijeshi.

Membe ana tabia ya kukurupuka ovyo mara nyingi sana na maswala ya kimataifa! Nimemsikia akikataa kwa nguvu sana kuwapa haki mashoga wakati sijaona maandamano ya hao mashoga anaopingana nao. Tanzania ushoga ni kosa la jinai kwa mujibu wa kanuni ya Adhabu, hao mashoga ambao waliopindukia sheria hiyo na kuanza kupambana naMembe ofisini kwake kweli inawezekana. hajaenda polisi kuripoti kuwa anabughudhiwa na mashoga lakini anapanda jukwaani kumlalamikia Cameroon kuwa Tanzania mashoga hawatapewa haki zao. Si kukurupuka huko na kuaibisha Taifa?

Swala la kupeleka majeshi kuzuia ndege za Malawi kuruka juu ya anga ya Malawi lilikuwa la kijinga na la kututia aibu Watanzania. Katika Mataifa ya wastaarabu kama Ulaya Membe angekuwa amekwisha kujiuzulu yeye mwenyewe kwa hiari yake, lakini kwetu Africa ukiwa rafiki wa Bosi hata ukiangamiza kaTaifa kenyewe bado uko huru kuishi na ofisi yako.

Ona Mwinyi alivyolibomoa jeshi,kwanza mabomu yote Mbagala yakalipuliwa, akaanza kwenda kutembelea wahanga sawa na mwizi aliyebomoa usiku asubuhi akaenda kuwapa pole wahanga. Kama aibu hiyo haikutosha kumlazimisha ajiuzulu akaunguza kambi yote ya Gongolamboto. Hakuna askari hata mmoja aliyejeruhiwa, nimeambiwa askari wote waliondolewa kambini kuanzia saa nane mchana. Hata ndege ya SwissAir ilitaarifiwa isishuke mchana saa nane hiyo hiyo. Nasikia SwisAir walishindwa kutekeleza onyo kwa sababu ya dege kubwa lililokuwa limejaza mafuta tele KIA na limeelekeza pua yake chini tayari kushuka, lingejaribu kugeuza pua kuielekeza juu uzito wake ungesababisha likakalia ******. Hivyo dege likalazimika kutua na Mungu Bariki likaruka tena na kuondoka kabla mabomu hayajaanza kulipuka.

Wakazi wa Gongo la Mboto hawakujulishwa wala hakukuwa na maandalizi ya ambulance wala zima moto. Atakayeniambia kuwa mabomu yaliyoanza kulipuka saa mbili usiku yalikuwa ni Accident nitataharuki. Dawa ni mihela ya walipa kodi ipo tele na wahanga wamejengewa mijumba mipya, hakuna hasara. Hata ingekuwa ajali ingemlazimu Mwinyi ajiuzulu, lakini wapi huyooo afya na huko akaenda kumteka nyara Ulimboka, na mpaka leo nchi inajulikana ina wateka nyara lakini hawajulikani, hata watuhumiwa kuhojiwa hakuna lazima. Rafiki wa JK huyo.


Wakali wa jukwaa la siasa vipi? Nimeuliza swali halali kabisa mbona hamjibu? Au kuna maswali magumu yasiyojibika kwenu? Nilikuwa namsikia Kibanda mpaka kapata kesi ya uhaini kwa kuhimiza jeshi lipindue nchi. Sijui kama ni kweli lakini huko huko jeshini ndiko waliko waharibifu, Mwinyi hakulipua hayo mabomu yeye kama ambavyo Lowassa hakufunga mitambo ya Richmond. Wataalamu waliofunga mitambo ya Richmond hata mmoja wao hatuwajui maskini Lowassa ndiyo akajiuzulu. Vipi Mwinyi asamehewe katika kosa ambalo ni baya zaidi?
 
Pumbavu we! Tena usirudie kuandika uharo wako hapa! Mi kuna komredi wangu amefariki pale Gongo la Mboto halafu unasema hamna wanajeshi waliokufa? Huyu nimesoma nae OD&H na namfahamu kabisa personally...Embu acha ujinga Heshimu marehemu bwana.
 
yan wewe pumbavu nataman nikuone ana kwa ana.usikebei wasio stairi.kuna shujaa na mzalendo kama membe?usipende kutumiwa
 
Pumbavu we! Tena usirudie kuandika uharo wako hapa! Mi kuna komredi wangu amefariki pale Gongo la Mboto halafu unasema hamna wanajeshi waliokufa? Huyu nimesoma nae OD&H na namfahamu kabisa personally...Embu acha ujinga Heshimu marehemu bwana.

Matusi kibao, naona wameguswa wakubwa. Nasikia walishatuma hata chinjachinja kumsaka mmliki wa JF na hayawani wake aliyeanzisha hoja hii. Lakini sikuwahi kusikia mazishi ya wanajeshi waliokufa Gongolamboto. Kambi kubwa ile, ingelipuka ghafla askari wako kambini tungeonana?

Sikutaka kujibu haraka haraka, nimetumia google kutafuta taarifa ya Askari waliokufa katika maafa ya Gongolamboto sikuapata hata moja. Nimepata blogspot moja inaitwa maishani.blogspot.com ambayo ina taarifa ya "JK awatoa hofu wakazi Gongolamboto. Imeandika hivi "Watu watano waliokufa katika tukio hilo ni wale wa familia moja" siyo askari.

Pai nitakuwekea sehemu ya hotuba ya JK:

"TAARIFA MAALUM KUHUSU MAAFA YA GONGOLAMBOTO ILIYOTOLEWA KWA VYOMBO VYA HABARI NA MHE. RAIS JAKAYA KIKWETE TAREHE 17 FEBRUARI, 2011, IKULU JIJINI DAR ES SALAAM.

images
Ndugu Wananchi, Kama mjuavyo, jana usiku jiji la Dar es Salaam lilipata mtikisiko mkubwa kutokana na milipuko ya mabomu iliyokuwa inatokea katika ghala kuu la Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania lililoko Gongolamboto katika viunga vya Dar es Salaam.

Milipuko hiyo imesababisha maghala 23 kuteketea kabisa na majengo kadhaa ya shughuli mbalimbali hapo kikosini kuharibika kwa viwango mbalimbali. Mabweni mawili ya kuishi wanajeshi nayo yaliteketea. Aidha, risasi nyingi, mabomu mengi, silaha na magari kadhaa nayo yameharibiwa na mengine kuteketea. Jeshi letu na nchi yetu imepata hasara kubwa sana.

Katika maafa haya makubwa kwa taifa letu, raia nao wameathirika kwa namna mbalimbali. Nyumba kadhaa za kuishi na majengo ya huduma za jamii nayo yameharibiwa na mabomu yaliyoangukia humo. Zipo ambazo zimeungua kabisa na zipo zilizopata uharibifu mkubwa na zipo zilizopata uharibifu wa viwango vya chini.

Lakini baya zaidi, katika mlipuko huo, ndugu zetu 20 wamepoteza maisha na wengine zaidi wamejeruhiwa kwa aina na viwango mbalimbali. Baadhi yao walifika katika hospitali za Amana, Temeke na Muhimbili na kupatiwa matibabu. Wengine wameruhusiwa na wengine wapatao 135 bado wamelazwa. Idadi kamili hupanda na kushuka kutegemea na kupokelewa na kuruhusiwa kwa majeruhi.

Ndugu Wananchi,


Hakika taifa limepata hasara kubwa kwa ndugu zetu kufariki na kujeruhiwa. Napenda kutumia nafasi hii kwa uchungu mkubwa kuelezea masikitiko yangu na taifa kwa ndugu zetu waliopoteza maisha wakati ambapo taifa lilikuwa bado linauhitaji sana mchango wao.

Naomba ndugu wa marehemu wapokee mkono wa rambirambi kutoka kwangu na kupitia kwangu kutoka kwa Watanzania wenzetu wote. Tuwaombee kwa Mwenyezi Mungu marehemu wetu wapate mapumziko mema. Amin.

Aidha, kwa niaba yangu na ya Watanzania wenzangu wote, nawapa pole nyingi ndugu zetu wote waliojeruhiwa na kupata mshituko kutokana na milipuko ya mabomu iliyotokea jana usiku. Tunazidi kuwaombea wapone upesi ili waendelee na kazi zao za kujenga taifa pamoja na kujiletea maendeleo yao binafsi.

Leo asubuhi na baadae mchana nilitembelea eneo la tukio kule Gongolamboto na kuwatembelea wagonjwa katika hospitali za Amana, Temeke na Muhimbili. Nimeona madhara na hasara tuliyoipata pale Gongolamboto. Nimewaona na kuwafariji wagonjwa wetu. Nimezungumza na madaktari na wauguzi katika hospitali hizo. Nimewashukuru na kuwapongeza kwa kazi kubwa na nzuri waliyoifanya usiku kucha ya kuwahudumia na kuokoa maisha ya ndugu zetu hao. Nimewatia moyo na kuwataka waendelee kuwahudumia vyema.

Ndugu Wananchi, Napenda pia kutumia nafasi hii kuwapongeza viongozi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na wa Bohari Kuu ya Madawa kwa kuhakikisha kuwa dawa na vifaa vya tiba vinapatikana kwa urahisi na kwa wakati, Hali hiyo ndiyo iliyosaidia kuokoa maisha na kuwapunguzia machugu ndugu zetu waliojeruhiwa.

Baraza la Usalama


Ndugu Wananchi, Leo alasiri mpaka usiku huu, tulikuwa na mkutano wa dharura wa Baraza la Usalama la Taifa. Hiki ndicho chombo cha juu cha kumshauri Rais kuhusu masuala yahusuyo usalama wa taifa letu. Kwa uzito na unyeti wa tukio, niliamua kuitisha mkutano wa Baraza hilo mara baada ya maafa hayo kutokea. Katika mkutano wetu, tumelitafakari kwa kina tukio hili na mambo mbalimbali yanayotokana na kuhusiana nalo. Baraza limeazimia kama ifuatavyo:"

Sioni mahali ambapo Rais amejulisha wanajeshi wangapi wameathirika. Au mlizika kisrisiri bila kufuata taratibu za kijeshi? Tabia ya kutoa matusi ovyo ni tabia ya wanyonge wasiokuwa na hekima ya kujua hekima ya kutoa hadharani.
 
yan wewe pumbavu nataman nikuone ana kwa ana.usikebei wasio stairi.kuna shujaa na mzalendo kama membe?usipende kutumiwa

Matusi kibao! Wewe kama unakula kwa Membe na unajua roho yake ya uzalendo heri kwako. Wewe ndiyo Mpumbavu ambaye unao ushahidi wa uzalendo wa Membe lakini huna hata la kuonyesha (mimi sisemi kuonesha- siyo muumini wa lugha za kuokoteza) kutangaza uzalendo huo.

Mimi nimekupa mifano hai, Membe anao Mashoga ambao badala ya kuwapeleka polisi anabishana na nchi za Magharibi kuhusu yeye kukubali kuwafuga au kuwakataa. Katika kujaribu kuficha aibu yake ya kuwa na mashoga hao anamwambia Cameroon kuwa yeye Membe hawataki hao mashoga.

Pia Membe amekurupuka kumlazimisha Joyce Banda ammegee kipande cha Malawi kwa kutumia majeshi yetu. Uvamizi namna hiyo ni kutangaza vita na taifa jirani. Pia "huo unaoita uzalendo" wa Membe ndiyo umefanya tatizo la mpaka kati ya Tanzania na Malawi kutopata ufumbuzi. Ni aibu ya kwenda tunasumbua watu eti tunatafuta suluhu wakati Mama Joy kishaghairi. Juzi Membe huyo huyo alisema mgogoro utapelekwa SADC, SADC wamekutana Dar es salaam hapahapa juzi Membe hakujua hata namna ya kupeleka hoja yake. Sasa anadai atapeleka kwa BARAZA LA USULUHISHI la maRais Wastaafu.

Kama huoni kuwa haya ni aibu kwa taifa na yanatosha yeye kujiuzulu basi wewe ndiye mjinga. Kutangaza uzalendo wa mtu usiokuwa na vigezo wakati vigezo vya upumbavu wake vinaonekana wazi ni dalili tosha kuwa wewe ndiyo unatumiwa.
 
Membe mimi sijawahi kumfuatilia sana lakini Mwinyi ni kilaza jamani hakuna mahali anafit ni kubebwa kwa mbeleko tu aibu kubwa kuwa na waziri kama huyu
 
Xmas njema.


Duh! Kumbe nchi imejaa wajanja wanaongoja na kupigania zamu zao za kuchukua chao?! Sijaona nani aliyekasirishwa na njama zilizokuwepo za kulipua zana za kijeshi ili kutoa mwanya kwa wakubwa kwenda kununua zingine.

Huu ndiyo ujinga wa Mtanzania, Zitto Kabwe anapiga kelele kuna wakubwa wana mihela katika mabenki Uswiss. Wakati wanayaweka na namna wanavyoyapeleka huko hajali hata kuwaumbua wakubwa hawa. Nasikia tu Zitto Kabwe anataka uRais 2015. Najua hoja yake ya msingi ni kuwa apewe uRais ili afuatilie mihela iliyoko uSwiss.

Samahani nimesema"ujinga wa waTz", waTz ukiwaita wajinga huwa wanakasirika sana na ole wako ndiyo uwe unataka wakupigie kura, hutapata! Basi waTz nyie ni wajanja sana msininunie, mpumbavu ni mimi, hata Gobore na Mark_Anthony wamekwisha kunisema hivyo hapo juu.

Songeni mbele, waTz barabara nyie, mna uhuru wa kupanga na kuchagua. Chagueni Membe na Mwinyi ndiyo wazalendo hao.
 
Membe Fisadi mkubwa juzi kati aliingizwa mkenge Mwanza .Akakodi ndege kwenda na kurudi kule katoa pesa mostkly wahuni waliitwa last minutes kuojoa jahazi hakuna watu na wakala wakatimua .Sasa kabakia kumtumia Malecela kuwarubuni akina Pengo wamuunge mkono kwenye urais .
 
Membe Fisadi mkubwa juzi kati aliingizwa mkenge Mwanza .Akakodi ndege kwenda na kurudi kule katoa pesa mostkly wahuni waliitwa last minutes kuojoa jahazi hakuna watu na wakala wakatimua .Sasa kabakia kumtumia Malecela kuwarubuni akina Pengo wamuunge mkono kwenye urais .

Weweeee! Andika vizuri basi na kwa ufasaha stori yenyewe ili na JK aione labda iatamtia "nguvu" za kumhoji huyo Membe! Unaandika kama dharura isyokuwa na substance bwana! Ona zangu zilivyojaa substance. Nashangaa JK hataki ku"react", au huwa hasomi JF?

Mimi nadhani kama anataka kuwa kama JK (Nyerere) anapaswa kujua yanayosemwa juu yake na Mawaziri wake. Najua Nyerere angekuwa kishawaita Ikulu Membe kutoa maelezo ilikuwaje Membe anaona Mashoga ndani ya TZ wakati Polisi hawawaoni, na Mwinyi kwa nini hakuwaondoa raia katika eneo la hatari ya milipuko ya silaha za kijeshi akaondoa wanajeshi tu.Kama JK hakujua nina hakika sasa anajua na ingekuwa Nyerere angewafukuza kazi.
 
Weweeee! Andika vizuri basi na kwa ufasaha stori yenyewe ili na JK aione labda iatamtia "nguvu" za kumhoji huyo Membe! Unaandika kama dharura isyokuwa na substance bwana! Ona zangu zilivyojaa substance. Nashangaa JK hataki ku"react", au huwa hasomi JF?

JK knows maana Membe he is always na Riz
Siku chache kabla ya sikuu ya Uhuru kulikuwa na ugeni mnene wa Kitaifa Dar wote mwajua baadaye waluhudhuria sherehe za Uhuru .Membe left kwenda Mwanza kwa ndege ya kukodi eti kwenda kutoa msaada .He gave 40mn TZS yeye pekee na wengine wakaongeza .Maandalizi ya kuhuni kisa anataka kukamata Mwanza .Mtoto wa Mangula ni mmoja wa waliokuwa kwenye msafara wa Membe kama watu wa usalama nk .Wakiona aibu baada ya Membe kuwekwa pembeni kungojea watu waongezwe kwa kuitwa jamani kuna pilau wakajaa pale hotelini .Kama Membe anabisha au watu wa Membe waseme .

Akarudi Dar haraka kwa ndege ile ile ya kukodi .Ukitaka kujua habari za Membe fika kwa Mzee Kingunge ambaye amesha mpiga marufuku kufika kwake .Anamtaka Membe arudishe pesa za waarabu ambazo anachezea kutafuta Urais.Kingunge anamtuhumu kumtumia Malecela anaye tumiwa kwenda kwa Pengo ili apate kuungwa mkono .
Nina mengi nangojea time .
 
JK knows maana Membe he is always na Riz
Siku chache kabla ya sikuu ya Uhuru kulikuwa na ugeni mnene wa Kitaifa Dar wote mwajua baadaye waluhudhuria sherehe za Uhuru .Membe left kwenda Mwanza kwa ndege ya kukodi eti kwenda kutoa msaada .He gave 40mn TZS yeye pekee na wengine wakaongeza .Maandalizi ya kuhuni kisa anataka kukamata Mwanza .Mtoto wa Mangula ni mmoja wa waliokuwa kwenye msafara wa Membe kama watu wa usalama nk .Wakiona aibu baada ya Membe kuwekwa pembeni kungojea watu waongezwe kwa kuitwa jamani kuna pilau wakajaa pale hotelini .Kama Membe anabisha au watu wa Membe waseme .

Akarudi Dar haraka kwa ndege ile ile ya kukodi .Ukitaka kujua habari za Membe fika kwa Mzee Kingunge ambaye amesha mpiga marufuku kufika kwake .Anamtaka Membe arudishe pesa za waarabu ambazo anachezea kutafuta Urais.Kingunge anamtuhumu kumtumia Malecela anaye tumiwa kwenda kwa Pengo ili apate kuungwa mkono .
Nina mengi nangojea time .

Unajua Lunyungu mimi nakerwa sana na mambo haya. Inakuwa kana kwamba hakuna sheria ndani ya nchi au kwmba wakubwa hawa wako juu ya sheria. Kwa nini habari hizi hazionekani katika magazeti ya mitaani ili wananchi wa kawaida nao wazijue? Au na wandishi wetu wa habari za magarazeti wana tuhela wamefichiwa huko uSwiss wasiandike vitu vya namna hii. Fikiria Membe kukodi dege zima wakati kuna ticha hata ile siti moja hawezi kuinunua!

Mbaya zaidi ni Mahakama na vyombo vyote vya sheria kuwa na siri nzito za kufunika. Kwa mfano sakata la Mwinyi kulipua Magala ya silaha lilishafikishwa kwa DPP Feleshi na mshambenga mmoja kwa baraua ya tarehe 24 Februari 2011 na ushahidi huu huu ninaousoma JF. Barua hii ilimtaka DPP achunguze uhujumu uchumi kwa kichwa "Notice of commission of economic crimes- Section 25 of CAP 200 (RE2002)". Unajua DPP alijibu nini? Naye kwa kichwa hiko hiko cha "Notice of commission of economic crimes- Section 25 of CAP 200 (RE2002)" cha barua Kumb na J/C.190/3/116 DPP ilijibu hivi "However we would like to inform you that under Section 25 of the Economic and Organized Crime Control Act, Cap 200, RE 2002, the duty to notify the DPP of occurance of Economic and Organized Crimes is vested either to the Police Officers In charge of the conduct of criminal invstigation or to any person in charge of a department of Government or other Public authority empowered by written Law to conduct investigation of an offence triable by the same Act."

Nadhani kuna kila sababu ya kumlazimisha JK aseme wazi kama anasoma au hasomi JF. Na kama anasoma lakini haelewi kwa nini achukue hatua, basi JF iwakaribishe akina Zitto Kabwe, Mbowe na akina Lipumba wasome halafu kama JK atakuwa bado haoni madaraka yake yanatakiwa kufanya kitu basi tujihesabu hatua Rais ndani ya nchi, Bunge limpigie kura ya kutokuwa na imani naye.

Najua njia ni ndefu mno lakini ndiyo njia ninayoiona mimi. Fikiria DPP anajua kuwa kuna uhujumu uchumi, lakini anataka aambiwe na police na siyo Shambenga aliyeshuhudia tukio live, si uhuni huo wa kutaka kuharibu nchi kwa amkusudi? Au anaogopa kuwaparamia akina Mwinyi na akina Membe kuwa wangeweza kumtumia watekaji nyara kutoka serikalini huko huko akapotelea msitu wa Mabwepande. Unajua Ulimboka alikuwa na mafuta mengi sana wakadhani wamemmaliza kumbe bado akajikokota mpaka akapata msaada wa wapita njia! Sidhani kama Feleshi angepona hivyo.
 
Matusi kibao! Wewe kama unakula kwa Membe na unajua roho yake ya uzalendo heri kwako. Wewe ndiyo Mpumbavu ambaye unao ushahidi wa uzalendo wa Membe lakini huna hata la kuonyesha (mimi sisemi kuonesha- siyo muumini wa lugha za kuokoteza) kutangaza uzalendo huo.

Mimi nimekupa mifano hai, Membe anao Mashoga ambao badala ya kuwapeleka polisi anabishana na nchi za Magharibi kuhusu yeye kukubali kuwafuga au kuwakataa. Katika kujaribu kuficha aibu yake ya kuwa na mashoga hao anamwambia Cameroon kuwa yeye Membe hawataki hao mashoga.

Pia Membe amekurupuka kumlazimisha Joyce Banda ammegee kipande cha Malawi kwa kutumia majeshi yetu. Uvamizi namna hiyo ni kutangaza vita na taifa jirani. Pia "huo unaoita uzalendo" wa Membe ndiyo umefanya tatizo la mpaka kati ya Tanzania na Malawi kutopata ufumbuzi. Ni aibu ya kwenda tunasumbua watu eti tunatafuta suluhu wakati Mama Joy kishaghairi. Juzi Membe huyo huyo alisema mgogoro utapelekwa SADC, SADC wamekutana Dar es salaam hapahapa juzi Membe hakujua hata namna ya kupeleka hoja yake. Sasa anadai atapeleka kwa BARAZA LA USULUHISHI la maRais Wastaafu.

Kama huoni kuwa haya ni aibu kwa taifa na yanatosha yeye kujiuzulu basi wewe ndiye mjinga. Kutangaza uzalendo wa mtu usiokuwa na vigezo wakati vigezo vya upumbavu wake vinaonekana wazi ni dalili tosha kuwa wewe ndiyo unatumiwa.

Brother inaelekea wewe ni mfuasi wa ushoga. Maana hasira ulizonazo kwa tamko la Membe kuhusu ushoga ni dhahiri kwamba hili linakuhusu kwa karibu na inawezekana ukawa ni mnufaika wa ule mpango kamambe wa Cameron. Ni aibu kwa mwanaume wa kiafrika kama wewe kujidhihirisha na kushabikia ushoga! Nenda basi huko wanakofunga ndoa za jinsia moja!
 
JK knows maana Membe he is always na Riz
Siku chache kabla ya sikuu ya Uhuru kulikuwa na ugeni mnene wa Kitaifa Dar wote mwajua baadaye waluhudhuria sherehe za Uhuru .Membe left kwenda Mwanza kwa ndege ya kukodi eti kwenda kutoa msaada .He gave 40mn TZS yeye pekee na wengine wakaongeza .Maandalizi ya kuhuni kisa anataka kukamata Mwanza .Mtoto wa Mangula ni mmoja wa waliokuwa kwenye msafara wa Membe kama watu wa usalama nk .Wakiona aibu baada ya Membe kuwekwa pembeni kungojea watu waongezwe kwa kuitwa jamani kuna pilau wakajaa pale hotelini .Kama Membe anabisha au watu wa Membe waseme .

Akarudi Dar haraka kwa ndege ile ile ya kukodi .Ukitaka kujua habari za Membe fika kwa Mzee Kingunge ambaye amesha mpiga marufuku kufika kwake .Anamtaka Membe arudishe pesa za waarabu ambazo anachezea kutafuta Urais.Kingunge anamtuhumu kumtumia Malecela anaye tumiwa kwenda kwa Pengo ili apate kuungwa mkono .
Nina mengi nangojea time .

Hivi kweli ndugu yangu umewahi kuona mlango wa darasa? Unavyoandika humu unaakisi ubovu wa elimu yako, kama unayo. Umemtaja Kingunge ambaye ni wakala wa mafisadi na mtu aliyepoteza heshima mbele ya jamii na hakuna kiongozi mwenye akili timamu anayeweza kwenda kwake kwa mashauri ya hekima. Kingunge amepoteza uhalali wa kuwa veteran wa siasa pale alipokubali kuwa mdomo na wakala wa mafisadi. Kingunge anajua nini kuhusu fedha za waarabu? Si ni huyu huyu Kingunge mnyonyaji aliyekuwa ananyonya wananchi wenzie waliomlisha na kumsomeshea watoto na wajukuu zake kwa kodi ? Bora unukuu mtu mwingine, siyo huyu ajuza ambaye hata kule kwao Kipatimu hana heshima.
 
Brother inaelekea wewe ni mfuasi wa ushoga. Maana hasira ulizonazo kwa tamko la Membe kuhusu ushoga ni dhahiri kwamba hili linakuhusu kwa karibu na inawezekana ukawa ni mnufaika wa ule mpango kamambe wa Cameron. Ni aibu kwa mwanaume wa kiafrika kama wewe kujidhihirisha na kushabikia ushoga! Nenda basi huko wanakofunga ndoa za jinsia moja!

Kiswigo wewe ndiyo una heshima yenyewe ya kuwa mfuasi wa mashoga na kuwashabikia. Unatafisiri hasira zangu kufuata msimamo wako na hila zako za kujaribu kuchafua watu kwa kuwaita mashoga ili kuficha tabia yako hiyo.

Inaelekea hujasoma habari nilizoandika kuhusu Jenerali Defao. Mlimwandama na ushoga wenu mpaka wanamuziki wenzie wakamkimbia mpaka akalazwa hospitali. Mpaka leo Jenerali Defao hajatokea tena jukwaa la muziki kwa sababu ya tabia mbaya ya WaTz kuvamia watu kwa matusi. Hii ndiyo tabia yenu mashoga wa Tz, ukimkuta shoga anajiuza atajihami kwa kumimina matusi ili wastaarabu wote waone aibu wamwache, na tusi wanalotumia ni- ******-.

Membe wako huyo alipokuwa anaongea na Cameroon kuhusu msimamo wa Tz juu ya mashoga alitakiwa awe amekwisha kuwatia jela. Ningekusomea hata vifungu vya sheria vinavyopiga marufuku ushoga katika nchi hii lakini sina muda na wewe kwa sababu naona unataka kuficha hisia na tabia zako za ushoga kwa kuita wengine mashoga. .

Mwambie huyo ******* wako aliyekutuma kuniita shoga atuonyeshe ndani ya Tz hao mashoga aliokwisha kuwakuta na matendo ya ushoga wako wapi? Asiende anaropoka nchi za nje kusema Tz ina mashoga wakati sisi hatuwaoni walipo, siyo swala la kufichwa na kuanza kutuhumiana kwa kutafsiri hisia za watu mtandaoni kama unavyodhani wewe. Cameroon anao na wamekwisha kujitangaza hadharani mpaka kwa maandamano.

Tuambie wewe kama nishoga tujue ili Membe atakapokuwa anajieleza ulaya tujue anamzungumzia Kiswigo, na hata hivyo nitashangaa kwa sababu utakuwa umetakiwa kuwa umehukumiwa kwa kosa la ushoga.
 
Vipi waungwana? Jadala ndiyo limekwisha na wenzetu wanaendelea na kibarua chao? Mimi nilidhani baada ya waTz kujua midhambi mikubwamikubwa watapiga makelele kuwa "Wamechoka kupiga honi". Duh! Ndiyo sababu Kikwete wetu alikimbia mpaka kuzimia ili afike paleeeee! Ukishafika hapo basi hukamatiki tena. Waungwana Jogoolashamba naomba kula zenu 2015, urahis au Ubunge wa Mkuranga, hata Mwinyi alitoka Zanzibar akaanzia Mkuranga. Nipeni na mimi Mkuranga jamani nikaonje kidogo, kuna ulaji huko waliko wenzetu.
 
Matusi kibao, naona wameguswa wakubwa. Nasikia walishatuma hata chinjachinja kumsaka mmliki wa JF na hayawani wake aliyeanzisha hoja hii. Lakini sikuwahi kusikia mazishi ya wanajeshi waliokufa Gongolamboto. Kambi kubwa ile, ingelipuka ghafla askari wako kambini tungeonana?

Sikutaka kujibu haraka haraka, nimetumia google kutafuta taarifa ya Askari waliokufa katika maafa ya Gongolamboto sikuapata hata moja. Nimepata blogspot moja inaitwa maishani.blogspot.com ambayo ina taarifa ya "JK awatoa hofu wakazi Gongolamboto. Imeandika hivi "Watu watano waliokufa katika tukio hilo ni wale wa familia moja" siyo askari.

Pai nitakuwekea sehemu ya hotuba ya JK:

"TAARIFA MAALUM KUHUSU MAAFA YA GONGOLAMBOTO ILIYOTOLEWA KWA VYOMBO VYA HABARI NA MHE. RAIS JAKAYA KIKWETE TAREHE 17 FEBRUARI, 2011, IKULU JIJINI DAR ES SALAAM.

images
Ndugu Wananchi, Kama mjuavyo, jana usiku jiji la Dar es Salaam lilipata mtikisiko mkubwa kutokana na milipuko ya mabomu iliyokuwa inatokea katika ghala kuu la Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania lililoko Gongolamboto katika viunga vya Dar es Salaam.

Milipuko hiyo imesababisha maghala 23 kuteketea kabisa na majengo kadhaa ya shughuli mbalimbali hapo kikosini kuharibika kwa viwango mbalimbali. Mabweni mawili ya kuishi wanajeshi nayo yaliteketea. Aidha, risasi nyingi, mabomu mengi, silaha na magari kadhaa nayo yameharibiwa na mengine kuteketea. Jeshi letu na nchi yetu imepata hasara kubwa sana.

Katika maafa haya makubwa kwa taifa letu, raia nao wameathirika kwa namna mbalimbali. Nyumba kadhaa za kuishi na majengo ya huduma za jamii nayo yameharibiwa na mabomu yaliyoangukia humo. Zipo ambazo zimeungua kabisa na zipo zilizopata uharibifu mkubwa na zipo zilizopata uharibifu wa viwango vya chini.

Lakini baya zaidi, katika mlipuko huo, ndugu zetu 20 wamepoteza maisha na wengine zaidi wamejeruhiwa kwa aina na viwango mbalimbali. Baadhi yao walifika katika hospitali za Amana, Temeke na Muhimbili na kupatiwa matibabu. Wengine wameruhusiwa na wengine wapatao 135 bado wamelazwa. Idadi kamili hupanda na kushuka kutegemea na kupokelewa na kuruhusiwa kwa majeruhi.

Ndugu Wananchi,


Hakika taifa limepata hasara kubwa kwa ndugu zetu kufariki na kujeruhiwa. Napenda kutumia nafasi hii kwa uchungu mkubwa kuelezea masikitiko yangu na taifa kwa ndugu zetu waliopoteza maisha wakati ambapo taifa lilikuwa bado linauhitaji sana mchango wao.

Naomba ndugu wa marehemu wapokee mkono wa rambirambi kutoka kwangu na kupitia kwangu kutoka kwa Watanzania wenzetu wote. Tuwaombee kwa Mwenyezi Mungu marehemu wetu wapate mapumziko mema. Amin.

Aidha, kwa niaba yangu na ya Watanzania wenzangu wote, nawapa pole nyingi ndugu zetu wote waliojeruhiwa na kupata mshituko kutokana na milipuko ya mabomu iliyotokea jana usiku. Tunazidi kuwaombea wapone upesi ili waendelee na kazi zao za kujenga taifa pamoja na kujiletea maendeleo yao binafsi.

Leo asubuhi na baadae mchana nilitembelea eneo la tukio kule Gongolamboto na kuwatembelea wagonjwa katika hospitali za Amana, Temeke na Muhimbili. Nimeona madhara na hasara tuliyoipata pale Gongolamboto. Nimewaona na kuwafariji wagonjwa wetu. Nimezungumza na madaktari na wauguzi katika hospitali hizo. Nimewashukuru na kuwapongeza kwa kazi kubwa na nzuri waliyoifanya usiku kucha ya kuwahudumia na kuokoa maisha ya ndugu zetu hao. Nimewatia moyo na kuwataka waendelee kuwahudumia vyema.

Ndugu Wananchi, Napenda pia kutumia nafasi hii kuwapongeza viongozi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na wa Bohari Kuu ya Madawa kwa kuhakikisha kuwa dawa na vifaa vya tiba vinapatikana kwa urahisi na kwa wakati, Hali hiyo ndiyo iliyosaidia kuokoa maisha na kuwapunguzia machugu ndugu zetu waliojeruhiwa.

Baraza la Usalama


Ndugu Wananchi, Leo alasiri mpaka usiku huu, tulikuwa na mkutano wa dharura wa Baraza la Usalama la Taifa. Hiki ndicho chombo cha juu cha kumshauri Rais kuhusu masuala yahusuyo usalama wa taifa letu. Kwa uzito na unyeti wa tukio, niliamua kuitisha mkutano wa Baraza hilo mara baada ya maafa hayo kutokea. Katika mkutano wetu, tumelitafakari kwa kina tukio hili na mambo mbalimbali yanayotokana na kuhusiana nalo. Baraza limeazimia kama ifuatavyo:"

Sioni mahali ambapo Rais amejulisha wanajeshi wangapi wameathirika. Au mlizika kisrisiri bila kufuata taratibu za kijeshi? Tabia ya kutoa matusi ovyo ni tabia ya wanyonge wasiokuwa na hekima ya kujua hekima ya kutoa hadharani.
Mpe ndoo huyo gobore atemee mapovu!! hana jipya!!
 
Jipya halipo? Huoni WaZenj sasa hivi wanataka uhuru wao na nchi yao? Lakini Hussein alikuta Zenj hana jimbo la Ubunge akaja Mkuranga akapata. Gobor......Gobore?! Roho mbaya tu hutaki wengine tupate ulaji? Au Mangikule una mapesa (siku hizi siyo vijisenti) Uswiss? Najua mtaendelea kuiba tu, waTz huchachamaa wakati wa uchaguzi tu, utadhani wanajua hata maana ya uchaguzi kumbe wanapeleka mafisadi katika ulaji!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom