January Makamba kiongozi mwenye uzalendo licha ya kuwepo CCM

Tuacheni siasa za ushabiki mimi chadema mwenye msimamo mkali nasema january jembe lazima tukubali mwanzo mwisho yuko ccm lakini mpiganaji wa ukweli

Watu kama nyinyi mnapaswa muwaoneshe njia wale wasio weza kutenganisha masuala na matukio.
 
wabongo hatuna shkrani mtu akijithidi kwa nafasi aliyi nayo mnaponda,ye kafanya moja mwinginw afanye lingine kama zito katani,mnyika umeme,mdee ufisadi,kigwagwala afya ndo nchi itaenda.
 
Kuna watu wanataka tuamini kila jambo la kizalendo linafanywa na cdm. Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.
hizi semi za wahenga zina walakini!...ndo maana hawa wahenga ni wakufikirika tu,they never existed.

mkishamnyonga mnyonge si mnamzika?au ndo haki yake hiyo ya kuzikwa?...

nwayz Magamba siwezi kuwaamini hata kidogo...hii hoja ilishapelekwa bungeni na wabunge wa CDM na ccm wakaipinga eti itaongeza ukali wa maisha kwa hao hao wanyonge...na wakashadadia wenye nyumba wasilipe kodi. nyumba nyingi zinamilikiwa na haohao akina Chenge,Rostam,\magufuli especially maeneo kama masaki ambako kodi kwa mwezi zinafika USD10000 na hawalipi kwa kipato hicho....wabunge wa ccm wanaona ni sawa mfanyakazi wa mwenye gross ya 1M ni halali akilipa 300,000 kama kodi kwa mwezi ila aliyeingiza kama 15M kwa mwezi asilipe....halafu wanakuja kututaka tuwaonee huruma eti pesa hakuna serikalini!!

Huyu makamba niliona mail moja kuwa ana mkopo kule Barick na aliahidi kuwalipa resource zetu kupitia dada yake Mwamvita... chochote anachokifanya mi naona anafight for power tu hana lolote jipya.

yeyote anayedhani huyu ndiye hero wake ajiandae kuwa dissapointed big time.
 
kaka wewe subiri huu ufisadi una mwisho wake. ukiweka mada inayomsifia january hapo sawa. nasikia hata ip za watu zimeanza kutolewa siku hizi
Huko wanapopeleka hizo IP Address, sisi tutapeleka risiti za ada yake huko marekani ambako alisomeshwa na Azim Premji, mwenyekiti wa CCM Kigoma. Premji ndio aliekiua CCM na ndio maana kina Zitto, Kafulila, wanapeta hadi leo. Mzee huyu alichelewa sana kuvuliwa gamba.
 
Tuacheni siasa za ushabiki
Ndizo zipi hizo mpiganaji86. Kwa mbali naona kama wewe ni shabiki mkubwa wa Januari Makamba.
mimi chadema
Duh, kweli wewe ni kiboko mpiganaji86. Hata hivyo kama nimekuelewa ni kwamba unadai wewe ni mwanaChadema, sasa naomba nikuulize, huko Chadema umefuata nini?
mwenye msimamo mkali
Ndio msimamo upi huo mpiganaji86. Utakuwa mwenye msimamo mkali kweli kweli mpaka husiti kumsifia na kumtetea mpinzani wako.
nasema january jembe
Sawasawa, hiyo ni haki yako mpiganaji86 ila huo hasa ndio ushabiki unaoeleweka.
lazima tukubali mwanzo mwisho
Hapana, huna haki ya kulazimisha hilo mpiganaji86 na hii sasa ni zaidi ya ushabiki wa kawaida, ni mapenzi.
Ndio mpiganaji86, kama walivyo mafisadi wote wanaifilisi nchi hii, salama yao iko CCM. Nje ya CCM? Heri hata samaki anaweza akadumu kwa muda mfupi nje ya maji hata kama ni kwa kutapatapa.
lakini mpiganaji wa ukweli
mpiganaji86, bahati mbaya sana nashindwa kuelewa huko CCM anapigana na nani na anapigania nini. mpiganaji86, nakumbuka baba yake Januari akiwa katibu mkuu wa CCM aliwahi kuwakanya wabunge kuhakikisha wanatanguliza maslahi ya chama bungeni. Kumbe wakati huo alikuwa anamwandaa mwana na kumtayarishia makao huko bungeni kwa kuhakikisha njia inawekewa lami mrithi mteule aweze kupita kwa ulaini. Hata askari wa usalama barabarani nao walihakikisha hakuna gari lolote lingine linakuwa barabarani ajali isije ikatokea.
 
Huyu bwana doa lake ni kuwa ccm. Kama kweli ana akili na ni msafi ahame ccm...
 
Mh january makamba mbunge wa bumbuli(ccm) amepanga kuwasilisha hoja binafsi bungeni kuhusu upangaji wa nyumba,jinsi gani wapangaji wanavyopata wakati mgumu,kiasi gani madalali wamekuwa chanzo cha kupanda ovyo kwa bei za nyumba.ni kweli serikali inatakiwa iweke sheria za kumlinda mpangaju..big up january!

Load of crap !!!!!!!!. Wapangaji wanapata taabu kwa sababu ya supply and demand, simple and basic economic theory. Utamlinda vipi mpangaji wakati kuna nyumba mbili na wapangaji mia wanaotafuta nyumba?

Kwa wale waliokulia DSM miaka ya 70, 80 wanaelewa kuwa wenye nyumba ndio walikuwa wanatafuta wapangaji na kulikuwa hakuna sheria yoyote ya kulinda mpangaji.

Kama Makamba ni Mzalendo basi awe BOLD and GRANDIOSE. Awakilishe hoja ya kujenga nyumba. Tuone kama watakuwa na plan.
 
Hoja hii binafsi malengo yake ni mazuri kwa kweli, lakini tatizo ni kwamba, je January atafanikiwa?

Kipindi cha nyuma (kabla ya mwaka 2002), tulikuwa na Sheria inayoitwa “Rent Restriction ACT, ya mwaka 1984. Sheria hii ilipelekea uwepo wa ‘Housing Tribunal’, ambayo ilisimamia mambo mengi sana ya msingi, kuanzia mchakato wa wapangaji kupandisha kodi, mchakato wa kumwondoa mpangaji katika nyumba, n.k. Sheria hii ilisaidia sana kupunguza misuguano baina ya pande hizi mbili.

Mwaka 2002, Serikali ikaja na Sheria mpya - Land Disputes Settlement ACT 2002. Tofauti na sheria ya MWAKA 1984, ambayo ilitoa haki kwa pande zote mbili (wenye nyumba na wapangaji), sheria hii mpya ni kama vile ilitungwa ili kupendelea na kubeba wenye nyumba. Kwa mfano, tofauti na zamani, Sheria ya mwaka 2002 inawapa mwanya wenye nyumba kupandisha kodi watakavyo wao; Pia kodi haijalishi ubora na usalama wa makazi husika, ni kwamba tu unaambiwa kodi ni kiasi fulani, kama hutaki, nenda zako. Pia tofauti na sheria ya mwaka 1984 ambapo wapangaji walikuwa wanatozwa kodi kwa mwezi, chini ya sheria mpya ya mwaka 2002 wenye nyumba wanaamua mwenyewe kama anataka umlipe kodi ka mwezi, miezi sita au mwaka mzima. Sheria hii inawapa wakati mgumu sana wapangaji, kwani wenye nyumba pia wanapata mamlaka ya kutaifisha mali za wapangaji, iwapo wanashindwa kulipa kodi chini ya makubaliano.

Kwa vyovyote vile, Hoja Binafsi ya January imekujwa wakati muafaka sana, lakini Tatizo atakalokumbana nalo January na hoja yake hii, inatokana na ukweli kwamba wamiliki wengi wa nyumba katika maeneo mengi ya mijini ni Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa idara na taasisi mbalimbali za serikali, wabunge, maafisa wa taasisi za umma kama TRA n.k. Hawa wote wana nufaika na sheria mbovu iliyopo. Pia wizi na ufisadi wote katika serikali na taasisi zake unatokana na uchu wa watu husika kumiliki nyumba kwa mtindo wa kukusanya kodi kwa mkupuo n.k. Nyumba nyingi za kupanga, kuanzia Sinza, Kinondoni, Mwenge, Masaki, Upanga, Mikocheni, Mbezi nk., ni za watu hawa. Ni kutokana na sababu kama hizi, January kuungwa mkono katika hili itakuwa ni ngumu sana. Ili kufanikisha this noble cause, January anahitaji support kubwa ya umma, na sio kubezwa kama baadhi ya watu wanavyofanya hivi sasa.
 
january na SUGU wote ni wageni bungeni ... ukienda jimboni kwake january kafanya mambo makubwa sana... SUGU yeye anazunguka tanzania kuzindua album yake.... hongera sana january :poa wewe ni mbunge ninaye kukubali ikifuatiwa na zito na mnyika
mbona unamfatafata sana sugu alikuibia mke nini
 
Mh january makamba mbunge wa bumbuli(ccm) amepanga kuwasilisha hoja binafsi bungeni kuhusu upangaji wa nyumba,jinsi gani wapangaji wanavyopata wakati mgumu,kiasi gani madalali wamekuwa chanzo cha kupanda ovyo kwa bei za nyumba.ni kweli serikali inatakiwa iweke sheria za kumlinda mpangaju..big up january!

Kupeleka hoja kama hiyo ndo mnamwona kiwaango wakati bado wao wanajipandishia posho ovyo ovyo bila kuwajali waliowapigia kura wapo kwenye hali gani ndo anajifanya aje na hiyo hoja ya kinafiki itakayoishia kuongelewa bungeni pasipokuwa na utekelezaji
 
mnyonge mnyongeni lakin haki yake mpeni..!unapozungumzia "wabunge wa ccm pekee" na uwezo wao wa kufikiri na kuguswa na mambo yanayoiathiri jamii kwa kweli january anajitahidi sana..!

hongera sana jm..!
 
Mh january makamba mbunge wa bumbuli(ccm) amepanga kuwasilisha hoja binafsi bungeni kuhusu upangaji wa nyumba,jinsi gani wapangaji wanavyopata wakati mgumu,kiasi gani madalali wamekuwa chanzo cha kupanda ovyo kwa bei za nyumba.ni kweli serikali inatakiwa iweke sheria za kumlinda mpangaju..big up january!

jamaa yuko smart sana
 
Binafsi sio mungaji mkono wa magamba,lakini pia ni mpinzani mkubwa sana wa siasa za kishabiki!Napenda sana kwa moyo mweupe kabisa nimpongeze January Makamba mbunge wa bumbuli kwa hoja yakebinafsi ya kuitaka serikari itunge sheria ya kuwadhibiti wenye nyumba ili wasiwe wanapandisha bei za kupanga kiholela na pia kuwadhibiti wenye nyumba hao kuwalazimisha wapangaji kulipa kodi za muda mrefu.

Kiukweli hili ni eneo muhimu sana kwa sababu linahusisha watanzania wengi na linahusisha makazi kitu ambacho ni muhimu sana na cha msingi sana kwa Watanzania, nawapongeza pia kambi ya upinzani kwa kuunga mkono hoja hiyo kwani wamedhirisha kuwa hawapo kichama bali kimaslahi ya Watanzania walio wengi,hawakuangalia ni chama gani kimetoa hoja bali hoja yenyewe,Hongereni sana!

Jukumu ni la serikali kuharakisha kuandaa sera itakayo wezesha sheria kutungwa!BRAVO JANUARY!
 
Hakuna jipya, upuuzi tu. Hana lolote la maana katika hoja yake, kaikopi ile ya Texas...
 
Hakuna jipya, upuuzi tu. Hana lolote la maana katika hoja yake, kaikopi ile ya Texas...
Kwani wabunge wengine walikatazwa Kucopy? huu ndio ushabiki usiotakiwa, mimi sio mpangaji lakini nafahamu kero kubwa wanazopata wapangaji mfano mshahara wako ni laki 2 mwenye nyumba anataka kodi ya mwaka huoni kama hili ni eneo nyeti linalowagusa watu wengi?
 
Back
Top Bottom