Mbeya: Ashikiliwa kwa tuhuma za kupatikana na nyara za Meno ya Tembo yenye uzito wa kilogramu 7.5

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989
Meno.JPG
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kipindi cha kuanzia Septemba mosi hadi 12, limefanya oparesheni na Misako yenye tija katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Mbeya na kupata mafanikio ikiwa ni pamoja na kukamata watuhumiwa 29 wakiwemo wa kupatikana na nyara za serikali (Meno ya Tembo), kufanya uharibifu wa miundombinu ya shirika la umeme (TANESCO) Mbeya na watuhumiwa wanaojihusisha na matukio ya utapeli.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia JOSEPH WILLIAM [30] Mkazi wa Majengo Jijini Mbeya kwa tuhuma za kufanya uharibifu wa miundombinu ya umeme (TANESCO) Mkoa wa Mbeya.

Septemba 05, 2023 huko Mtaa wa Mafiati, Jijini Mbeya, mtuhumiwa alikamatwa akiwa na vifaa mbalimbali vya umeme ambavyo ni Earth Wire, PVC 2.5 meter 7.5, Earth Wire – Bare 3.5 meter 30, Praise moja, Msumemo mmoja ambavyo alikiri kuiba kwenye Transforma ya Umeme Mali ya Shirika la Umeme Tanzania lililopo maeneo ya Hospitali ya K’S.

Aidha, katika upekuzi uliofanywa nyumbani kwake Mtaa wa Nonde Jijini Mbeya alikutwa na vifaa vingine ambavyo ni Solar Street Light Panel yenye 35 watts na Light IP 65 – 200 ambavyo ni mali ya Halmashauri ya Jiji la Mbeya.

Sambamba na hilo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watuhumiwa wawili SYLVESTER RAFAEL @ HAULE [32] Mkazi wa Ipogoro mkoani Iringa na SHUKURU MLOWE [35] Mkazi wa Njombe kwa tuhuma za kujihusisha na matukio ya utapeli kwa njia ya mtandao [simu ya mkononi].

Watuhumiwa walikamatwa Septemba 06, 2023 huko Igawa, Wilaya ya Mbarali na walikuwa wakitafutwa kutokana na kujihusisha na matukio ya utapeli kwa njia ya mtandao was imu katika maeneo ya Jiji la Mbeya, Dodoma, Iringa na Njombe ambapo pia waliruka dhamana ya Polisi.

Watuhumiwa wamekutwa na Gari yenye namba za usajili T.511 DER aina ya Toyota Passo, simu za mkononi 5 ndogo (Analogue) za aina mbalimbali na laini za mitandao mbalimbali.

Aidha, katika muendelezo wa Misako, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Askari wa TANAPA linamshikilia SELEMAN EZEKIA [34] Mkazi wa Kijiji cha Imalilo Songwe kwa tuhuma za kupatikana na nyara za serikali [Meno ya Tembo] mawili yenye uzito wa kilogramu 7.5

Mtuhumiwa alikamatwa Septemba 02, 2023 huko katika Kijiji cha Madundasi Wilaya ya Mbarali katika msako wa Pamoja wa Jeshi la Polisi na Askari wa TANAPA. Mtuhumiwa alikutwa akiwa ameficha nyara hizo kwenye mfuko wa sandarusi ili asafirishe kuupeleka Mbeya Mjini. Taratibu za kumfikisha mahakamani zinaendelea.
 
Back
Top Bottom