IPSO FACTO: CHADEMA AND CUF MUST 'RESIGN'! So as you...if..! TUACHE UNAFIKI

Webs,

Salaam popote ulipo.

Naamini uwezo wa kufikiri na siwezi kuhoji elimu yako. Naijua.

Kwanza kabisa mimi ni MwanaCDM na nitachangia kama mmoja wa wale ambao umewashutumu kwamba hakuna wanachokifanya na hawana tofauti na CCM.

Naamini kwamba kuna mengi ninayoyafanya kwa nchi yangu na siko kama CCM hata kidogo.

Hii nchi imefika hapa ilipofika kwa sababu yako wewe. Wewe ndie wa kulaumiwa.

Kwa wepesi wa kutia moyo umeweza kutoa hasira zako. Sio kwa sababu huipendi nchi yako bali hujui jinsi ya kuisaidia. Kwa elimu yako na uzoefu wako ningetegemea ulione hilo.

Wewe na wengine wengi ambao mmekaa pembeni, hamshiriki katika uongozi wa vyama vya siasa wa serikali badala yake mnakuwa wepesi kulaumu 'vyama' ndio wakulaumiwa. kulaumiwa sana. CDM, CUF, CCM, NCCR etc ni vyama Waberoya. Ni vyama vinavyoundwa na watu. Viongozi wa taifa wa CHADEMA hawafiki mia moja (100)!! Viongozi wa Mikoa na Wilaya zote hawazidi mia tano (500). Wengine wote ni watanzania. Sasa unaposema watanzania hao hawafanyi lolote hivy 'tuwafute' halafu nani afanye sasa?? Is this not contradictory??

Ukweli unaoupinga kwenye nafsi yako ni kwamba CDM na vyama vingine havina wafuasi Milioni sita. Hakuna wanachama milioni 6 wa CDM wala CUF. Wananchi watu wazima wapo zaidi ya Milioni 20. Sasa hata ukivifuta CDM na CUF inakuwaje?

Nisaidie, nisaidie kufikiri, je ni wana CDM na wana CUF walichagua CCM? Unapotushambulia kosa letu ni nini? Kuichagua CCM au kutoichagua CCM.........hoja hii nitaianzishia thread yake ili ichangiwe vizuri. Ila tafadhali nijulishe.

Kwa muda wote utaoendelea kuwa 'mimi sina chama chochote vyama vyote ni kama CCM' basi nchi hii itaendelea kuwa kama ilivyo. Hasira unazopata wewe ukiwa pembezoni ni robo ya hasira ninazopata mimi niliyeko ndani ya uozo huo unaosikia harufu yake kwa mbali. Sogea karibu uusikie vizuri tufanye kazi ya kuondoa. Kupiga kelele huko pembezoni hauna tofauti na CDM au CUF waliokimya!!

Ukimya na kelele za pembeni ni kitu kilekile.

Otherwise, tutaendelea kujadili.
 
Mkuu umetao changamoto,Lakini swali ninani yuko tayari kumwanga unga,akale wapi,akafanye kazi gani,Je CCM wanafurahiya watu kufa ?.Jibu NDIO,nINI KIFANYIKE SASA,??????????????
 
I dropped history on my form two sababu hakukuwa na facts na nilikuwa napata D ama F!
How can CHADEMA or CUF resign! I might be missing something.

Resign is a verb, with a literal meaning of

  • Voluntarily leave a job or other position.
  • Give up (an office, power, privilege, etc)
Wataalamu wa lugha mtanisaidia, resign hutumika zaidi kwa watu (individuals) na si kwa organisation kama vyama vya kisiasa - CUF, CCM ama CHADEMA these are political parties. Political party is a political organization that typically seeks to influence government policy, usually by nominating their own candidates and trying to seat them in political office. Chama chochote cha siasa agenda yake ya kwanza ni kutwaa dola na kutawala kwa kuweka sera zake.

Kuwa mwanachama wa chama fulani ni kukubaliana na sera na ideology ya chama husika. Huwezi tamka CCM ijiuzulu badala yake utatamka Mwenyekiti, ama katibu wa CCM wajiuzulu sababu 1. 2, 3. ......Ukisema CHADEMA ama CUF wajiuzulu nadhani unakuwa unaweka unafiki kwa makusudi. Labda kama ujumbe wako ungekuwa viongozi wa CHADEMA na CUF wamemeshindwa kutekeleza sera zao na kutetea haki na maslahi ya wanachama wake kwa mbali ningekuelewa.

Mara nyingi nionapo article ndefu sana huwa naisoma na akili nyingine, huenda muandishi anajitahidi kulazimisha mawazo yake bila fact.....

Webs nitolee mfano popote duniani chama cha siasa (CUF, CHADEMA) kilichoamua kujiuzulu.

Hezbollah Party Resigns:
Lebanese Government Collapses As Political...12 Jan 2011
 
I dropped history on my form two sababu hakukuwa na facts na nilikuwa napata D ama F!
How can CHADEMA or CUF resign! I might be missing something.

Resign is a verb, with a literal meaning of

  • Voluntarily leave a job or other position.
  • Give up (an office, power, privilege, etc)
Wataalamu wa lugha mtanisaidia, resign hutumika zaidi kwa watu (individuals) na si kwa organisation kama vyama vya kisiasa - CUF, CCM ama CHADEMA these are political parties. Political party is a political organization that typically seeks to influence government policy, usually by nominating their own candidates and trying to seat them in political office. Chama chochote cha siasa agenda yake ya kwanza ni kutwaa dola na kutawala kwa kuweka sera zake.

Kuwa mwanachama wa chama fulani ni kukubaliana na sera na ideology ya chama husika. Huwezi tamka CCM ijiuzulu badala yake utatamka Mwenyekiti, ama katibu wa CCM wajiuzulu sababu 1. 2, 3. ......Ukisema CHADEMA ama CUF wajiuzulu nadhani unakuwa unaweka unafiki kwa makusudi. Labda kama ujumbe wako ungekuwa viongozi wa CHADEMA na CUF wamemeshindwa kutekeleza sera zao na kutetea haki na maslahi ya wanachama wake kwa mbali ningekuelewa.

Mara nyingi nionapo article ndefu sana huwa naisoma na akili nyingine, huenda muandishi anajitahidi kulazimisha mawazo yake bila fact.....

Webs nitolee mfano popote duniani chama cha siasa (CUF, CHADEMA) kilichoamua kujiuzulu.

Mkuu nadhani kuna tofauti kubwa ya resign na 'resign' kwa msomi kama wewe ulitakiwa kujua kuwa 'xxx' linaashiria maana isiyo rasmi! angalia title!
 
Sidhani kama CDM wako kama CCM, bali CDM wako somewhere in between half CCM and half water. CDM wamekalia kutoa matamko na kushindwa kuenergize base kubwa ambayo wanayo (Vijana).

Wapo wanaosema kwamba CDM walilipeleka swala la Gongo La Mboto Bungeni na Mh. Mbowe alimuomba spika kujadili jambo hilo bungeni lakini spika akamwambia kwamba swala lile sio Janga La Taifa. Swala muhimu linakuja jee Mbowe alipojibiwa hivyo alifanya nini? Jee alihoji kufahamu kutokana na muongozo wa Bunge Janga la Taifa linachambuliwa kama nini? What is the definition of National Tragedy? Jee hakuna njia mbadala ya kulipeleka swala hili kwenye Kamati za bunge na kuanzia kule?

CDM wanashindwa kukacapitalize haya mambo kuwapa political gain, ndio maana walikana uchaguzi kisha wakakubali. Then walimkana JK kisha wakamkubali..... In short CDM hawajui what position to stand.

CDM itaelendelea kutoa matamko kama UVCCM paka lini? Asilimia kubwa ya vijana wana support CDM, lakini poor leadership or poor political understanding ya viongozi wa CDM itakipeleka hiki chama pabaya.
 
Waberoya ana jazba na si mchambuzi makini.

1. CHADEMA NA CUF MUST RESIGN (WAJIUZULU)
Anaongea kana kwamba CHADEMA na CUF ni watu wawili. Mtu anayechagua maneno angesema "Kiongozi au viongozi fulani wa CHADEMA na CUF wajiuzulu. Sidhani kama Waberoya amewahi kusoma sheria ya vyama vya siasa na kuona kama kuna provision inayoelekeza chama kinaposhindwa kutenda au kutotenda kijiuzulu "chote".
2.WATU KWA NINI WALIENDA KAZINI SIKU ILIYOFUATA MABOMU?
Sasa hapa CHADEMA na CUF wangefanya nini? Rais ambaye ni wa CCM ndiye alipashwa kutangaza mapumziko na wala sio Dr Slaa au Prof Lipumba. Hata hivyo, kupumzika kungesaidia nini? Kwa hili wa "kujiuzulu" kama chama ni CCM na wala sio CUF au CHADEMA.
3. MBOWE NA MTEI KUWA MARAFIKI WA KIKWETE NA LOWASA
Hapa sioni tatizo. Upinzani sio uadui. Haikatazwi watu wa vyama tofauti kuwa marafiki. Mfano, wakati Lawrence Masha akiwa Mbunge na waziri wa CCM, baba yake alikuwa Mbunge wa Afrika Mashariki kupitia UDP. Vilevile, shangazi wa James Mbatia ameolewa katika familia ya kina Bomani, na James Mbatia aliwahi kuwa msemaji mkuu katika msiba wa kina Bomani. Huu ndio upinzani mzuri. Katika siasa hakuna uadui au urafiki wa kudumu.
4. MAGEUZI YA KWELI SI JUKUMU LA WANASIASA TU
Mageuzi na mabadiliko ya kweli hayaletwi na wanasiasa au vyama wanavyoviongoza. Mabadiliko yanaletwa na watu wenyewe. Inatubidi tujiulize kama watanzania tumefanya nini kutatua matatizo yetu badala ya kufikiri kuwa ni CHADEMA au CUF itakayotatua matatizo yetu. Binafsi nafiki, mtoa mada ameongozwa na jazba na hakuvitendea sawa vyama vya CHADEMA na CUF (hasa CHADEMA, maana naona CUF kaitaja kama boya tu).

Kwa yote uliyoyataja, wakulaumiwa ni CCM na wananchi kwa ujumla na wala sio CHADEMA au CUF kama vyama.
 
Tatizo la siasa ni kuwa unatakiwa uchange karata zako kwa akili na busara. Suala kama la mabomu Dr Slaa alisema ''hili ni janga la kitaifa na tunashikamana'' akimaanisha kuwa yupo pamoja na Waathirika bila kujali itikadi zao. Chadema walitaka suala lijadiliwe bungeni lakini zikatumika kanuni za makinda kuua hoja. Sijui kama ingekuwa busara Tundu Lissu au Chadema kuitisha maandamano huku watu wakiwa hospitalini na uwanja wa taifa!! hii ingekuwa political suicide.
Suala la mbagala lilitaka lijadiliwe bungeni, zikatumika kanuni za'' haya ni mambo ya uslama wa taifa, kanuni kama za Tangold, meremeta zilivyotumika dhidi ya Slaa.
Suala la Dowans nalo zikatumika kanuni za kamati ya nishati. Tukumbuke kuwa ni wapinzani (CUF et al)wanaoipiga vita Chadema sasa hata kutoa Mwanya wa Spika kuchagua kamati anavyojua yeye. Ninadhani tunapaswa kuwasaidia kimawazo na busara kuliko kuwatuhumu tu.

Kuna ukweli kuwa wapinzani wameshindwa kutumia fursa za kisiasa kwa baadhi ya mambo. Huu ni ukweli usiopingika. Upinzani umekuwa too slow ku-react katika issues. Ni lazima watambue kuwa udhaifu wa CCM ndiyo nguvu yao na wawe tayari wakati wote kuutumia udhaifu huo. Wapinzani wanajua kuwa Makinda amewekwa kuwadhibiti, sasa ni wajibu wao kutafuta njia mbadala kukabiliana naye, vinginevyo atawakwaza. Mfano Suala kama la Mh Lema halikufaa kufumbiwa macho liishe kinyemela, Suala la Dowans hadi anakuja jenerali wapinzani wapo kimya! Tumieni mikuatano kuwasiliana na wananchi, msitegemee bunge peke yake. Tumieni vyombo vya habari n.k.

Mwisho, na sisi wananchi ni sehemu ya tatizo, suala kama la katiba tumeliacha kwa wapinzani. Bila katiba mpya CCM na serikali yake itaendelea kutudangaya na kanuni za bunge, usalama wa taifa, tume n.k. Na hili ni moja ya mambo yanayoikwaza CDM na upinzani.
 
CDM ni chama safi kabisa, lakini mbinu zake tofauti na MATARAJIO ya Waberoya - ni kitu ambacho ni kawaida kabisa.

Mimi naona kama KATIBA itaandikwa upya karibuni, hilo ndio CDM na vyama vingine walishikie bango kuliko kingine chochote mpaka kieleweke. Tukiwa na katiba safi ina maana tutafaidika na chaguzi huru na pia serikali itasukumwa kuwajibika kwa watu kikatiba. TZ bado tuna nafasi na sanduku la kura kama KATIBA itarekebishwa.

Kuiondoa serikali ya CCM kwa maandamano kama walivyofanya Misri, nk kwa sasa mimi naona wala haina tija maana baada ya maandamano wakudandia watakua wengi tu, hata wakuja watajiingiza humo - HATA VYAMA VYA DINI VITATAKA UWAKILISHI KISIASA.
 
Vyama vinajengwa na kuimarishwa na watu mimi na wewe Waberoya, Mimi na wewe Mkuu hatuvisaidiii vyama kufanya yale tunayotaka.
kwa mfano Mwakembe mara kadhaa kamtuja Rostam Azizi kuwa ndiye mmiriki wa Dowans, mimi na wewe tumekaa kimya. Tunasubili Mwakyembe amkamate Azizi na kumhoji. Hakuna chombo cha habari wala waharakati waliibuka kunuunga mkono mwakyembe. Pili tumeshuudia mageuzi Tunisia, Misri, na sasa Libya niambie ni chama gani kimeongoza mageuzi kama sio wananchi wanye uchungu na nchi zao. Tuungane kuvisaidia vyama au watu makini ndani ya vyama, tupaze sauti tuikomboe nchi yetu.
 
Mfano atoe wapi wakati amekurupuka kwa kutaka sifa post ndefu ka gazeti la mzalendo sijawahi sikia chama kimejiuzulu.

Hawa ni UVCCM wa vyuo vikuu na nafikiri huyu yuko mwaka wa kwanza. Walitoa damu juzi, nafikiri bado ana kizunguzungu.
 
Mkuu umejitahidi, ila yaelekea lengo lako hasa ilikuwa ni kuishambulia CHADEMA. Watu wameshtukia hiyo...
 
Tatizo la siasa ni kuwa unatakiwa uchange karata zako kwa akili na busara. Suala kama la mabomu Dr Slaa alisema ''hili ni janga la kitaifa na tunashikamana'' akimaanisha kuwa yupo pamoja na Waathirika bila kujali itikadi zao. Chadema walitaka suala lijadiliwe bungeni lakini zikatumika kanuni za makinda kuua hoja. Sijui kama ingekuwa busara Tundu Lissu au Chadema kuitisha maandamano huku watu wakiwa hospitalini na uwanja wa taifa!! hii ingekuwa political suicide.
Suala la mbagala lilitaka lijadiliwe bungeni, zikatumika kanuni za'' haya ni mambo ya uslama wa taifa, kanuni kama za Tangold, meremeta zilivyotumika dhidi ya Slaa.
Suala la Dowans nalo zikatumika kanuni za kamati ya nishati. Tukumbuke kuwa ni wapinzani (CUF et al)wanaoipiga vita Chadema sasa hata kutoa Mwanya wa Spika kuchagua kamati anavyojua yeye. Ninadhani tunapaswa kuwasaidia kimawazo na busara kuliko kuwatuhumu tu.

Kuna ukweli kuwa wapinzani wameshindwa kutumia fursa za kisiasa kwa baadhi ya mambo. Huu ni ukweli usiopingika. Upinzani umekuwa too slow ku-react katika issues. Ni lazima watambue kuwa udhaifu wa CCM ndiyo nguvu yao na wawe tayari wakati wote kuutumia udhaifu huo. Wapinzani wanajua kuwa Makinda amewekwa kuwadhibiti, sasa ni wajibu wao kutafuta njia mbadala kukabiliana naye, vinginevyo atawakwaza. Mfano Suala kama la Mh Lema halikufaa kufumbiwa macho liishe kinyemela, Suala la Dowans hadi anakuja jenerali wapinzani wapo kimya! Tumieni mikuatano kuwasiliana na wananchi, msitegemee bunge peke yake. Tumieni vyombo vya habari n.k.

Mwisho, na sisi wananchi ni sehemu ya tatizo, suala kama la katiba tumeliacha kwa wapinzani. Bila katiba mpya CCM na serikali yake itaendelea kutudangaya na kanuni za bunge, usalama wa taifa, tume n.k. Na hili ni moja ya mambo yanayoikwaza CDM na upinzani.


Nakuunga mkono mkuu. Sasa kuna haja ya sisi wazalendo kuunda network kuwasiliana ili tulisongeshe kama Tunisia, Misri, Libya, Yemen, Bahrain, Jordan, Morocco na Algeria.
Maana vinginevyo tunabaki kuwa witnesses tu wa mabaya yanayotokea, bila kuchukua hatua zozote.
 
Waberoya ana jazba na si mchambuzi makini.

Kwa yote uliyoyataja, wakulaumiwa ni CCM na wananchi kwa ujumla na wala sio CHADEMA au CUF kama vyama.

Kaka maiti huwa hailaumiwi, ilipofikia sasani kuwa kuilaumu CCM ni makosa makubwa sana, maana utailaumu kwa kila kitu! wanaolaumiwa ni wazuri na wanalaumiwa kwa sababu kuna mengine mazuri wanayafanya! CCMhaina zuri ndugu, kuwalaumu ni wastage of time!

Mkuu umejitahidi, ila yaelekea lengo lako hasa ilikuwa ni kuishambulia CHADEMA. Watu wameshtukia hiyo...

Nashukuru kwa hilo kaka na nimeona sijaeleweka hapo, kuna watu wanaipenda CDM kuna watu tunaioenda na tuna matarajio makubwa na CDM! they have to do more than now! ama sivyo itafika 2060 CCM iko palepale bila kuwashtua hawa tunabaki na matumaini hewa!
 
Sidhani kama CDM wako kama CCM, bali CDM wako somewhere in between half CCM and half water. CDM wamekalia kutoa matamko na kushindwa kuenergize base kubwa ambayo wanayo (Vijana).

Wapo wanaosema kwamba CDM walilipeleka swala la Gongo La Mboto Bungeni na Mh. Mbowe alimuomba spika kujadili jambo hilo bungeni lakini spika akamwambia kwamba swala lile sio Janga La Taifa. Swala muhimu linakuja jee Mbowe alipojibiwa hivyo alifanya nini? Jee alihoji kufahamu kutokana na muongozo wa Bunge Janga la Taifa linachambuliwa kama nini? What is the definition of National Tragedy? Jee hakuna njia mbadala ya kulipeleka swala hili kwenye Kamati za bunge na kuanzia kule?

CDM wanashindwa kukacapitalize haya mambo kuwapa political gain, ndio maana walikana uchaguzi kisha wakakubali. Then walimkana JK kisha wakamkubali..... In short CDM hawajui what position to stand.

CDM itaelendelea kutoa matamko kama UVCCM paka lini? Asilimia kubwa ya vijana wana support CDM, lakini poor leadership or poor political understanding ya viongozi wa CDM itakipeleka hiki chama pabaya.

Tatizo la siasa ni kuwa unatakiwa uchange karata zako kwa akili na busara. Suala kama la mabomu Dr Slaa alisema ''hili ni janga la kitaifa na tunashikamana'' akimaanisha kuwa yupo pamoja na Waathirika bila kujali itikadi zao. Chadema walitaka suala lijadiliwe bungeni lakini zikatumika kanuni za makinda kuua hoja. Sijui kama ingekuwa busara Tundu Lissu au Chadema kuitisha maandamano huku watu wakiwa hospitalini na uwanja wa taifa!! hii ingekuwa political suicide.
Suala la mbagala lilitaka lijadiliwe bungeni, zikatumika kanuni za'' haya ni mambo ya uslama wa taifa, kanuni kama za Tangold, meremeta zilivyotumika dhidi ya Slaa.
Suala la Dowans nalo zikatumika kanuni za kamati ya nishati. Tukumbuke kuwa ni wapinzani (CUF et al)wanaoipiga vita Chadema sasa hata kutoa Mwanya wa Spika kuchagua kamati anavyojua yeye. Ninadhani tunapaswa kuwasaidia kimawazo na busara kuliko kuwatuhumu tu.

Kuna ukweli kuwa wapinzani wameshindwa kutumia fursa za kisiasa kwa baadhi ya mambo. Huu ni ukweli usiopingika. Upinzani umekuwa too slow ku-react katika issues. Ni lazima watambue kuwa udhaifu wa CCM ndiyo nguvu yao na wawe tayari wakati wote kuutumia udhaifu huo. Wapinzani wanajua kuwa Makinda amewekwa kuwadhibiti, sasa ni wajibu wao kutafuta njia mbadala kukabiliana naye, vinginevyo atawakwaza. Mfano Suala kama la Mh Lema halikufaa kufumbiwa macho liishe kinyemela, Suala la Dowans hadi anakuja jenerali wapinzani wapo kimya! Tumieni mikuatano kuwasiliana na wananchi, msitegemee bunge peke yake. Tumieni vyombo vya habari n.k.

Mwisho, na sisi wananchi ni sehemu ya tatizo, suala kama la katiba tumeliacha kwa wapinzani. Bila katiba mpya CCM na serikali yake itaendelea kutudangaya na kanuni za bunge, usalama wa taifa, tume n.k. Na hili ni moja ya mambo yanayoikwaza CDM na upinzani.

Asanteni sana wapendwa at least napata ahueni kuwa I have some people who think like I do.
 
Vyama vinajengwa na kuimarishwa na watu mimi na wewe Waberoya, Mimi na wewe Mkuu hatuvisaidiii vyama kufanya yale tunayotaka.
kwa mfano Mwakembe mara kadhaa kamtuja Rostam Azizi kuwa ndiye mmiriki wa Dowans, mimi na wewe tumekaa kimya. Tunasubili Mwakyembe amkamate Azizi na kumhoji. Hakuna chombo cha habari wala waharakati waliibuka kunuunga mkono mwakyembe. Pili tumeshuudia mageuzi Tunisia, Misri, na sasa Libya niambie ni chama gani kimeongoza mageuzi kama sio wananchi wanye uchungu na nchi zao. Tuungane kuvisaidia vyama au watu makini ndani ya vyama, tupaze sauti tuikomboe nchi yetu.


Kweli mkuu. Ni sisi wananchi wenyewe ndo wenye nguvu ya kuundoa utawala dhalimu wa CCM. Waberoya akisubiri mpaka CHADEMA au CUF walianzishe,nafikiri atasubiri mpaka kifo. Nguvu ya umma ni nguvu ya Mungu. Hivyo ni suala
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom