Victoire
JF-Expert Member
- Jul 4, 2008
- 24,141
- 56,601
Ndo maana kuna majukwaa:SIASA,mahusiano,michezo na mengineyoNimefuatilia kwa karibu posting zinazofanyika kwa siku za hivi karibuni nyingi na kugundua kwamba nyingi zinahusu mahusiano na mambo ya mapenzi ukilinganisha zile zinazohusu mijadala juu ya mustakabali wa nchi kuhusu rushwa, matumizi mabaya ya madaraka, uhujumu uchumi, EPA na mafisadi wake na siasa za nchi yetu kwa ujumla.
Nikiangalia kwa karibu kulikuwa na wimbi la watu kujiunga na JF some 6 months ago ambapo mijadala juu ya ufisadi ilikuwa imepamba moto na ninajikuta nalazimika kufikiria kwamba kulikuwa na msukumo fulani kutoka kwa mafisadi kuingiza "watu wao" kwa wingi hapa JF na kupost issues za mahusiano ili kupindisha attention ya watu kutoka kwenye kupigia kelele ufisadi na badala yake tuzame kwenye kujadili mambo yanayohusu mahusiano na mapenzi.
Ikibidi Mods watupe data za aina za posting kwa siku za karibuni (at least for the past 6 months) ili tupime ukweli wa fikira zangu.
Mnalionaje wazo hili, je lina ukweli wowote?