Kasheshe
JF-Expert Member
- Jun 29, 2007
- 4,694
- 787
Lakini hapa kuna mtego ambao Mkakati wa kina Lowassa utakwama. Kama mnakumbuka Mwakyembe alitoa wito kwa "mtu yeyote" mwenye maelezo kuhusu Richmond ajitokeze na kuonana na Kamati. Kwenye ripoti hiyo anasema hakuna mtu aliyejitokeza kwa hiari yake (hapa anawabana kina Karamagi, et al).
HIvyo wakija na "hatukupewa nafasi ya kusikilizwa" Mwakyemba atawaambia.. "tarehe... nilizungumza na vyombo vya habari na kutoa wito kwa "mtu yeyote"... hapo ndipo watakapojua kuwa mtego umetegwa aidha watautegua, ama watanaswa!
Nadhani ushauri huu uuende Dodoma mara moja!!!