Inatosha - Lowassa Jiuzulu!

Hivi si Raisi ana mamlaka ya ya kumfuta kazi PM? Mjadala wote wa nini? Ingekuwa nchi zilizoendelea wahusika wangekuwa wameshajiengua mapema!!!!
 
mzee mwanakijiji
hii ni rasharasha,nilikuwa naongea na mmoja wa wajumbe wa kamati ya rais ya madini.kanimegea kiduchu kuhusu mkataba wa buzwagi,nimehuzunishwa sana na tena sana..kumbe EL na Karamagi wanahusika na deal la Buzwagi kwa asilimia 100%.kuhusu ripoti ya leo,inasemekana Rostam hauhusiki moja kwa moja na deal ili alijiingiza baadaye baada ya kuona kuna maslahi zaidi..Na ni mmoja ya watu ambao wameombwa na JK kujiuzuru,ila hawatatupwa!
 
...mgonja SASA WAKATI UMEFIKA WA KWENDA MAREKANI KWENYE JUMBA LAKE KUUNGANA NA MKE WAKE ANAYEJIRUSHA HAPO NA WATOTO WAWILI HAPO FLORIDA..KUENDELEA KUTUMBUA PESA ZA UFISADI ZINAZOTUNZWA SWISS...THE GUY MAY BE CLEAN BUT HIS WIFE NDIE ANA INFLUENCE UFISADI WOTE ...
 
Hivi kuna mtu anafikiri Lowassa atajiuzulu? Lowassa mpaka aambiwe na JK vinginevyo atang'ang'ania kama Kibaki aki hope yataisha baada ya siku tatu.

Karamangi na Msabaha watajiuzulu na kutolewa kafara. Bila kuondoka Lowassa
naona bado madudu yataendelea kufanyika.
 
Wakuu naomba kujua kama hii Bunge session huko bongo inaoneshwa live kwenye TV kama walivyoonesha sakata la Zitto
 
Madela nimekusikia!! Ila ujumbe unaopenyezwa toka kwenye mkutano (bado unaendelea) ni kuwa EL amewagomea kujiuzulu kwani "hana sababu ya kujiuzulu" na kama nilivyosema jana, jiandaeni kwa hotuba ya kuomba radhi na defiance!

Hata hivyo, tetesi ambazo zinaingia taratibu kama mnyoo ardhini zinaonesha kuwa Mawaziri wawili tayari wameandika barua za kujiuzulu... na mida yoyote kuanzia sasa tutajua who is out first..

siku za mwizi kutamba ni 39 tu ya 40 tunaye.
Huyu jamaa akibusu ardhi kwa kidevu, historia inajiandika, ndoto yake atashindwa kuota na wa TZ tutapata nguvu za kuwajibisha wengine.

Wezi wa mali ya umma hakuna hata haja ya kuwafunga jela, kwani Mijizi yote ya fedha za umma siku zote inatembea imebeba jela mgongoni mwao. Ukiwazibia matundu yote ya kukwapua fedha ya serikali, wanaanza kujitafuna mikia vidole na makalio mithili ya vibwengo mpaka wanajimaliza, wakishajimaliza wanajifungia jela wenyewe.
 
hivi nyie wabunge wetu huko dom mnajua kuwa Watz wamechoka? mnaosoma JF saa hizi mkiamuka asubuhi kesho mwambieni Kikwete wazi kuwa wabongo wamechoka kabisa.Kujiuzuru sio jadi ya wabongo,ila jueni kwamba saa inasema wakati umekwisha.Siku ya nne baada ya wizi wa kura Moi alijikuta ni abiria wa ndege kwenda Ujerumani na watoto wake. Washikaji juzi waligawana kwa muda shamba la Balali huko Bunju na Kerege bila kuwa na Raila !! Je angekuwepo Raila wetu hali ingekuwaje? Tafadhali Rais wangu KATA BILA HURUMA HUO MKONO WAKO WA KULIA tupa mbali.
 
Kujiuzulu kwa Karamagi na Msabaha (ndicho ninachotegemea kusikia) ni long overdue. Watu tumelalamika hapa siku kibao posts zimejaza mamia ya kurasa! Dr Msabaha kwa kweli namsikitikia, lakini najiuliza nini kilimkosesha uzalendo wa kutamka ule ukweli wa lile neno lake la kizaramo (nikumbusheni!) ili Lowassa ahojiwe na Kamati? Kweli ni mbuzi wa kafara, lakini kafara haramu! Yaani anaona bora atemeshwe mzigo kuliko kumtaja mwizi? Hii tabia wanayo vibaka wazoefu, ukiwaona vibaka watatu wanaiba ukafanikiwa kukamata wawili, kamwe hawamtaji mwenzao hata wakiambiwa wanachinjwa! Sasa huu si ushujaa, ni ukibaka tu! Nitamsifu Msabaha kama atamwaga ukweli wote kwenye hiyo barua yake ya kujiuzulu, better late than never!

Chief Kithuku,

Huyu mzee wa kizaramo (Msabaha) anajulikana kuwa na jazba za ajabu. Huyu ndio alikuwa katibu mkuu wa foreign wakati harakati za upinzani zilipoanza na akamfuatilia kwa makini Tanzania Rep UN wa wakati huo (Anthony Nyakyi) mpaka akatap phone conversation kuprove kuwa alikuwa (Nyakyi) na Mzee Edwin Mtei wa Chadema. Akashadadia mpaka Nyakyi akaondoka huko kwenye mission yetu UN.

Wakati huo alikuwa na kiburi cha ajabu nikashindwa kuelewa. Sasa anajidai kuwa yeye ndio atakuwa kondoo wa kafara? Bantu Please!!! Anataka nani amhurumie? Kwa kweli Kithuku umetoa challenge nzuri kwake...awataje waliomtuma ili asiende kujitafutia boyfriend kule Segerea akiwa peke yake. Yaani ngoma hii iko patamu kweli, ningependekeza utayarishe kinywaji upendacho, nyama choma na vinginevyo ili ujiburudishe wakati sakata hili linaendelea. Heheeeee, hoiiii!

Speaking of nyama choma, huyu Lowassa si iliripotiwa alikuwa ana choma nyama na mmoja wa mafisadi wa BoT? Kwanini hawa wasihamishie hizi session za kuchoma nyama kwenye gereza la Karanga pale Moshi?
 
Hajiuzulu wala hauzuliwi mtu hapa,CCM ni yetu wenyewe,tutaekana sawa na kuonyana mtu asirudie tena na iwe kosa lake la mwisho,ee mwenye kamaa ajinyonge ,ila sasa ndio wanaingia na kile kilichosemwa ari mpya ,wengine mkae chonjo maana Lowasa akitoka huko ni kama simba aliejeruhiwa wakati bado anautaka mnofu ,lakini kuna kitu kimoja watu wa Mkapa na yeye mwenyewe mbona bado wanapeta ,na yote haya yanayomfika Lowasa na Kikwete ni kumkumbatia Mkapa na kumhifadhi,naamini kabisa Mh.Kikwete ameyarisi haya madudu kutoka kwa Kaka Nkapa ambae ubabaishaji wake wa Ikulu upo wazi alikuwa mkali wa kukemea rushwa kumbe anasanya ,na saikolojia inatwambia mtu akiwa mkali sana basi ujue anaficha jambo !!! Na kweli Mh.Mkapa alikuwa anaficha mambo,baada ya kung'olewa pembe sasa mambo yote yanaonekana wazi kabisa ,kumbe ukali ule ulikuwa unamaana katika elimu ya saikolojia. !!!
 
Yaleyale ya mficha donda kuumbuliwa na uozo. Watu wamezungushia donda mitambara weeee, sasa linachuruzika miusaha chepechepe!
 
Kama lowasa hatajiuzulu, nchi hii inaelekea Kenya, atakuwa kama Kibaki. Hatakiwi lakini yumo tu!
 
Hajiuzulu wala hauzuliwi mtu hapa,CCM ni yetu wenyewe,tutaekana sawa na kuonyana mtu asirudie tena na iwe kosa lake la mwisho,ee mwenye kamaa ajinyonge ,ila sasa ndio wanaingia na kile kilichosemwa ari mpya ,wengine mkae chonjo maana Lowasa akitoka huko ni kama simba aliejeruhiwa wakati bado anautaka mnofu ,lakini kuna kitu kimoja watu wa Mkapa na yeye mwenyewe mbona bado wanapeta ,na yote haya yanayomfika Lowasa na Kikwete ni kumkumbatia Mkapa na kumhifadhi,naamini kabisa Mh.Kikwete ameyarisi haya madudu kutoka kwa Kaka Nkapa ambae ubabaishaji wake wa Ikulu upo wazi alikuwa mkali wa kukemea rushwa kumbe anasanya ,na saikolojia inatwambia mtu akiwa mkali sana basi ujue anaficha jambo !!! Na kweli Mh.Mkapa alikuwa anaficha mambo,baada ya kung'olewa pembe sasa mambo yote yanaonekana wazi kabisa ,kumbe ukali ule ulikuwa unamaana katika elimu ya saikolojia. !!!

.unajua sometimes huwa nafikiri ur just joking,lakini mjomba kwa hili nafikiri uondoe utani kama kweli ni utani, lakini kama unachosema uko serious...NO COMMENT,ila next time itabidi moderator asitufungie humu kwa kumalizia hasira zetu kwako kabla ya huyo Lowassa
 
We Mamvi na wenzako hizo pesa mlizokuwa mnaiba ili kuwanyima watanzania huduma muhimu mnataka mkazitumie Kuzimu.Maana mnaonekana nyinyi walafi saaana Mnakula mpaka mnaokoteza ma vinavyodondoka.Mimvi yote hiyo tulifikiri una busara kumbe ni kinyaa tupu. Wizi wenu hauna tofauti na wale wezi wa Ubungo.Majambazi wakubwa nyie
Gharama za umeme zinapanda kila kukicha na kusababisha wananchi kushindwa kununua huduma Nyingine muhimu.
 
Wasije wakaenda Ukraine kufanya shopping tu! Hawa jamaa wakamatwe kabla hawajaenda nje kwa matibabu.
 
UCHAMBUZI WA KISIASA

M. M.

RA ameingia Dodoma muda si mrefu uliopita... sijui anatokea wapi...

EL inadaiwa ametoa na machozi kutetea kitumbua chake na ya kuwa "anaonewa".

Watajwa wote na wenyewe wameweka ngumu ya kudai kuwa "hawakuhusika" na hivyo hawako tayari kujiuzulu (licha ya habari kuwa baadhi yao wanazo barua za kujiuzulu mikononi)

Dalili zinaonesha hata hivyo katika yote kuna angalau watu wawili ambao watatoswa mara moja. Mwanasheria Mkuu (nimepata nakala ya mtazamo wa kisheria wa Mikataba sita ya Tanesco na mapungufu yake ) na Msabaha.

Karamagi sababu kubwa ambayo inatajwa kuwa itachangia kuondolewa kwake ni hasa kutokana na kuigharimu CCM kuhusuiana na suala la Buzwagi. Lile liliwauma sana na wanataka alipe!

Hata hivyo, hadi hivi sasa Rais ndiye inaonekana ataamua uamuzi wa mwisho. Na jinsi inavyoonekana kuna mambo kadhaa.

- Kuvunja baraza siku chache zijazo kabla ya ujio wa Rais George Bush itampa JK ujiko au ni liability ya ujiko?

- Akivunja baraza atakomba waliokuwamo na wasiokuwamo na atakapounda upya wale walioachwa watakuwa wameondolewa kiungwana wakichanganywa na wengine wasiohusika (imagina kati ya mawaziri 30 anarusha 10 tu na Manaibu 30 anarusha 20 tu). Hapo itakuwa kifo cha wengi.

- Kama ilivyotokea kwenye sakata la Sukari (enzi za Idi Simba na Ngasongwa) mojawapo wa strategies zilizochukuliwa ni kuwakataza Mawaziri na Manaibu Waziri kushiriki mjadala ule kwa kile kilichoitwa "Collective responsibility".

Njia nyingine ambayo inaweza kutumika kumuondoa Waziri Mkuu ni ile ya kutumia utaratibu wa Kibunge (kura ya kutokuwa na imani).

Kwa kufuata kipengele cha Katiba cha 53A Kuna masharti kadhaa ya kufuata ili kuleta hoja hiyo Bungeni.

- Wabunge wapatao 64 (asilimia 20 ya wabunge wote) waandike taarifa ya azimio lao hilo siku 14 kabla ya kuleta hoja yenyewe.

- Spika aridhike kuwa masharti rahisi ya Kikatiba yametimizwa ambayo ni a. Lazima ihusiane na utendaji kazi wake au kukiuka sheria ya maadili ya uongozi; b. Iwe imepita miezi sita tangu ateuliwa na c. Iwe imepita miezi tisa baada ya hoja ya namna hiyo kuletwa Bungeni na kukataliwa.

Na endapo masharti hayo yatatimizwa na Spika ataridhika kuwa yametimizwa basi kura itapigwa na itakuwa imepitishwa kwa simple majority (yaani kwa wabunge wengi kuikubali).

Hata hivyo utaratibu huo kwa sasa siamini kama unawezekana kwani Bunge linamaliza kikao chake tarehe 18 na tukihesabu kuanzia kesho (Ijumaa) itakuwa ni siku 12 tu na hivyo sharti moja la Katiba halitatimizwa unless, Kikao cha Bunge kiongezewe siku mbili!

Sasa ukiondoa hilo la kura ya kutokuwa na imani. Lowassa anaweza kuondoka (ukiondoa tendo la Mungu) kwa njia kubwa tatu tu:

a. Ajiuzulu (kama hoja yangu hapa inavyosema)
b. Aondolewe na Rais kwani anatumika kwa ridhaa ya Rais.
c. Baraza kuvunjwa/kujiuzulu na yeye kutopendekezwa tena (itakuwa ni njia ya kiungwana zaidi ya kumuondoa).

Natumaini nimesaidia kidogo.
 
These are the moments I wish mchambuzi yuko hapa!!!


Siku kaka Mcha alo tuaga alisema kabisa. "Siku itakuja mtaomba ningekuwepo."

Lakini wapi bwana, asingefanya chochote cha maana zaidi ya kumtetea yule M Arusha mwizi asiye na huruma hata kwa wajukuu zake.

Wizi gani huo wa kujitafuna wenyewe?

Watu wamejaza ma GX barabara za kutembelea hakuna, umeme hakuna, maji hakuna.

Mamvi ni vema aadabishwe na wengine wote wafuatie.
 
Back
Top Bottom