Elections 2015 Ilani ya CCM 2015-2020 - Uchaguzi Mkuu 2015

...miiiayoo...
Toa porojo na upuuzi wenu wa kila siku
Maneno ya mzee wa megawati Ngeleja
 
Pamoja na yote hayo bado hatuwakubali hivyo tutawaweka pembeni. Nadhani unaona hata wanaccm wenzako huwaoni kwenye hii post wakikuunga mkono.
 
Hakuna kitu hapo madini wanafaidi wakina Bush na Queen Elizabeth sisi tunasubiri misaada toka KUWAIT Kwa Sadam Hussein haaaaaaaaaaaaa haaaaaaa! shame on us!
 
Hakuna kitu hapo madini wanafaidi wakina Bush na Queen Elizabeth sisi tunasubiri misaada toka KUWAIT Kwa Sadam Hussein haaaaaaaaaaaaa haaaaaaa! shame on us!
Timu yenu ya mafisadi ndio unataka iyafaidi madini?
 









Gazeti la NIPASHE Oktoba 15, 2015 limebeba kichwa cha habari gharama za kutimiza ahadi 10 kwa MAGUFULI na LOWASSA ni Trilioni 92. MAGUFULI ahadi zake zinahitaji trilioni 63.64 na LOWASSA trilioni 28.29 katika awamu yao ya kwanza ya miaka mitano. MAGUFULI anaonekana kuwa na dhamira ya dhati katika kuleta mabadiliko yenye tija kwani ahadi zake zinahitaji uwekezaji mkubwa zaidi ya mpinzani wake.Trilioni 63.64 kwa miaka mitano ni wastani wa trilioni 12.73 kwa mwaka huku Lowassa akihitaji trilion 5.66 kwa mwaka. MAGUFULI ameweka malengo makubwa yanayotekelezeka lakini pia ambayo yatamlazimu kupiga vita rushwa na ufisadi kwa nguvu zote kama alivyokwishaahidi mara kadhaa pamoja na kusimamia nidhamu ya ukusanyaji mapato na matumizi serikalini ili fedha zipatikane kuwahudumia watanzania. Huyu anayehitaji trilioni 5.66 kwa mwaka ataruhusu ufujaji mkubwa wa fedha za serikali. Hivyo MAGUFULI ndiyo kura ya mabadiliko ya kweli Oktoba 25.



AHADI 10 ZA MAGUFULI HIZI HAPA



1. MAJI-Kuboresha huduma za maji safi na salama kwa wananchi waishio vijijini na mijini,kukamilisha miradi mikubwa ya maji,kupanua miradi ya kitaifa katika meneo mbalimbali nchini kwa kuchimba visima virefu,kujenga mabwawa katika mikoa yenye ukame. Kuanzisha mfuko wa maji wa taifa (Nationa water Investment Fund) kwa ajili ya kuharakisha ujenzi wa miradi ya maji nchini. Pia ameahidi serikali yake kushirikiana na sekta binafsi katika kujenga miundombinu ya uondoshaji wa maji taka kwa mfumo wa ubia ili uendane na kasi ya ukuaji wa miji yetu.



2. ELIMU-Yeye na Chama Chake wanaamini elimu bora ina nafasi ya kipekee katika kufanikisha ujenzi wa misingi ya uchumi wa kisasa wa taifa linalojitegemea. Kwa kutambua ukweli huu,serikali ijayo ya CCM chini yake itaipa elimu umuhimu wa kipekee ili kuhakikisha inakidhi mahitaji ya sasa ya nchi kwa kumuandaa kila mtanzania kukabiliana na changamoto zinazomzunguka. Kulipa madeni yote ya walimu na kuboresha maslahi na makazi yao pamoja na kuanzisha tume ya walimu itakayosimamia maendeleo ya walimu kote nchini ikiwemo kupandishwa madaraja kwa wakati.Kumaliza tatizo la madawati na upungufu wa vitabu vya kujifunza na kufundishia pamoja na kutoa elimu bila ada kuanzia ngazi ya msingi hadi sekondari. Kujenga vyuo vya ufundi stadi VETA kila wilaya.



Kurekebisha utaratibu wa utoaji mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu ili kila mwanafunzi anayestahili apate bila usumbufu na kwa wakati.Kuhakikisha ujenzi wa vyuo vikuu vikubwa 2; Chuo Kikuu Cha Kilimo na Sayansi Shirikishi Cha Mwl.J.K. Nyerere (Butiama-Mara) na Chuo Kikuu Cha Sayansi Za Madini Shinyanga.



3. AFYA-Kuongeza idadi ya waganga na wauuguzi pamoja na kuimarisha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba katika vituo vyote vya tiba nchini.Kuboresha maslahi ya watumisha wa sekta ya afya kwa kuwalipa mishahara bora,kuwajengea nyumba ili kuwapa motisha ya kufanya kazi.

Serikali ya CCM chini ya MAGUFULI itwaweka utaratibu utakaowawezesha wananchi wote kuwa na bima za afya ili wamudu gharama za matibabu. Kukamilisha ujenzi wa zahanati kwa kila kijiji,kituo cha afya kila kata,hospitali kila wilaya na hospitali ya rufaa kwa kila mkoa. Tutaendelea kupunguza kwa kasi zaidi vifo vya mama na mtoto ili ikiwezekana kuvimaliza kabisa.Tutaanzisha pia mamlaka ya kudhibiti na kuzuia dawa za kulevya.



4. KUKUZA VIWANDA-Kujenga viwanda mama na kuimarisha vilivyopo. Kuhamasisha sekta binafsi kuanzisha viwanda vikubwa na vya kati na kuweka utaratibu wa kuvilinda dhidi ya bidhaa zisizo na ubora zinazoingia nchini kinyume na utaratibu. Kujenga mazingira rafiki yatakayowezesha kupunguza gharama za uwekezaji na uendeshaji wa viwanda.Kuanzisha viwanda vya msingi vinavyotumia malighafi ya chuma na makaa katika maeneo ya Liganga na Mchuchuma.



5. USAFIRISHAJI NA UCHUKUZI
Barabara-Tutaimarisha mfuko wa barabara,kuboresha mfumo wa ufuatiliaji na kuanzisha wakala utakaosimamia kazi za ujenzi na matengenezo ya barabara za miji,majiji na halmashauri ambazo ziko chini ya TAMISEMI. Tutamalizia ujenzi wa barabara kuu za lami zenye urefu wa kilometa 2,358 na kujenga barabara mpya za lami zenye urefu wa kilometa 3,419 zitakazounganisha mikoa na wilaya zote nchini. Kukamilisha ujenzi wa flyovers katika jiji la Dar. Tutawashirikisha wakandarasi wadogo wadogo wa kitanzania wanaoonesha nia ya kushiriki kazi kubwa za ujenzi wa barabara ili kuwajengea uwezo na kuwapatia fursa za kushiriki katika sekta ya ujenzi.



Reli-Tutashirikiana na sekta binafsi kuanza na kukamilisha ujenzi wa reli zifuatazo kwa kiwango cha kimataifa (standard gauge); Dar-Tabora-Mwanza/Kigoma; Uvinza-Msongati(Burundi); Isaka-Kigali(Rwanda); Mtwara-Songea-Mbambabay(na matawi ya kwenda Mchuchuma na Liganga);Tanga-Arusha-Musoma na Kaliua-Mpanda-Karema. Kuyajengea uwezo mashirika yetu ya reli ya TRL na TAZARA ili yatoe huduma bora na kwa ufanisi.



Usafiri wa majini- Kuimarisha miundombinu ya usafiri wa majini kwa kuimarisha miundombinu katika bandari za Zanzibar, Dar, Mtwara,Tanga,Mafia,Mwanza,Kigoma,Bukoba,Kyela na Musoma. Kununua meli mpya za abiria na mizigo katika ziwa Victoria, Tanganyika na Nyasa.



Usafiri wa anga-Kukamilisha ujenzi wa viwanja vya Dar,Zanzibar,Kigoma,Shinyanga,Dodoma,Mwanza,Lindi,Tanga,Geita pamoja na ukarabati wa viwanja vya Iringa,Njombe,Simiyu,Musoma,Moshi na Arusha. Kushirikiana na sekta binafsi kuliimarisha shirika letu la ndege la Taifa.



6. NISHATI-Kuongeza uzalishaji na upatikanaji wa umeme wa uhakika na gharama nafuu nchini pamoja na usambazaji wa umeme vijijini ili 60% ya watanzania wawe na umeme wa uhakika ifikapo 2020. Tutahimiza matumizi ya gesi asilia katika matumizi ya nyumbani na viwandani ili kupunguza matumizi ya kuni na mkaa hivyo kuhifadhi mazingira.



7.UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI:Serikali ya CCM awamu ya 5 chini ya MAGUFULI itwawawezesha wananchi kiuchumi kwa kuhakikisha kuwa: Inatenga milioni 50 kwa kila kijiji na kila mtaa kama mfuko wa mzunguzko kwa ajili ya kuwakopesha vijana na wanawake wajasiriamali kupitia vikundi; kutenga maeneo maalumu katika kila halmashauri kwa ajili ya wafanyabiashara ndogondogo kwa kuyajengea miundombinu yote muhimu;Kuondoa kero za ushuru na kodi zinazotozwa kwao.Kuhakikisha 30% ya zabuni za manunuzi ya halmashauri kwa ajili ya kampuni ndogo zinazomilikiwa na vijana na wanawake katika halmashauri husika.



8. MAHAKAMA MAALUM YA MAKOSA YA RUSHWA NA UHUJUMU UCHUMI
-Mahakama hii itaharakisha uchunguzi na utoaji hukumu kwa makosa ya Rushwa,Ufisadi,Ukwepaji kodi na yote yanayotambulika kama uhujumu uchumi.



Itaendelea kesho.....
 
Elimu gani walioisimamia kwa miaka 54 ikaleta maendeleo?
Huduma za afya ambazo hakuna hata madawa hospitali?

Watanzania tuamke, tuwe critical thinkers.

Kwanza kama hukusoma mlaumu Mzazi wako kwasababu sisi sote tumesomeshwa na wazazi wetu na si serikali. Yawezekana hata kujenga kwako kukakushinda kwasababu tu serikali haijakuwezesha lakini usisahau wengine wanajenga, kuna wengine wameshindwa hata kuoa na kila wakiulizwa wanasema bado masha magumu Mara hawajajipanga lakini mtaani haimaanishi wengine hawaoi ..maanake nini? siyo kila kitu kitaweza kufanywa na kila mtu kama huyo mtu ataacha mambo yajibadirishe, mafanikio yako ni matunda ya juhudi zako mwenyewe
 
Ilani hii ya CCM ni tamko maalumu kwa wapiga kura kuhusu nia ya CCM ya kuendelea kushika dola na kuwaongoza Watanzania kwa njia ya kidemokrasia, na hasa kuendelea kudumisha amani, umoja wa Kitaifa, usawa, ustawi wa wananchi, Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kwa kipindi kingine cha miaka mitano.Nia na uwezo wa CCM wa kuendelea kuongoza Taifa hili unajidhihirisha katika uzoefu ambao tumeupata kwa miaka 38 tangu kuanzishwa kwake na kuwa madarakani, ambapo katika kipindi chote hiki kimeiwezesha nchi yetu kupata mafanikio makubwa katika nyanja za kiuchumi, kisiasa na kijamii
 
Wakuu ...

Nataka ccm waje wanijibu maswali yafuatayo?

Ilani ya ccm iko wapi?
Je magufuli ndiyo anayotekeleza?
Kama haitekelezi anatekeleza ipi ?
Hivi kujenga uwanja wa ndege chato ilikuwa kwenye ilani ya ccm?
Kama inatekelezwa ni kwa asilimia ngapi?
Kununua ndege mbili ilikuwa ndani ya ilani ya Ccm?

Vipaumbele vya ilani ni nini?
.bado sijaelewa mpaka sasa ilani IPI inatekelezwa!!
 
Kwa mujibu wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (2015-2020).

1. Ilani ya CCM: Serikali iliahidi itatenga kiasi cha shilingi milioni 50 kwa kila Kijiji, badala ya kupewa milioni 50 wamachinga ndio wanaichangia serikali elfu 20,000 kwa kila kitambulisho.

2. Ilani ya CCM: Serikali iliahidi itahakikisha wananchi wanaopakana na miundombinu ya gesi na ambako bomba la gesi linapita wananufaika na gesi. Walichoambulia wananchi ni kuona alama za njano bomba linakopita na virungu vya polisi.

3. Ilani ya CCM: Serikali iliahidi kuhamia Dodoma kabla ya 2020 tukaambiwa kufikia Desemba 2018 Rais atakuwa Dodoma, hadi leo namuona bado yupo Dar.

4. Ilani ya CCM: Serikali iliahidi kuongeza kwa kiwango kikubwa uzalishaji wa nishati kutoka 1,300MW hadi 5,000MW ifikapo 2020. Sina uhakika hata megawati 2,000 zimefika.

5. Ilani ya CCM: Serikali iliahidi kipaumbele kitakuwa katika kukuza na kuanzisha viwanda vidogo, vya kati na vikubwa. Leo hata aliyeanzisha wimbo wa Tanzania ya viwanda anaona aibu kutamka mbele za watu.

6. Ilani ya CCM: Katika kipindi cha miaka mitano ijayo, serikali ya CCM itaendeleza mapambano dhidi ya adui rushwa na ufisadi. Leo CCM imerudi kuwakaribisha Mafisadi papa waliowakataa 2015 akiwepo fisadi mkuu Lowassa.

7. Ilani ya CCM: Serikali ya CCM itahakikisha thamani ya Shilingi yetu inatengamaa. Leo 1USD = 2400TZS.

8. Ilani ya CCM: Serikali iliahidi itahakikisha inaongeza mauzo ya bidhaa zetu nje ya nchi. Leo mazao ya Korosho na Mbaazi yamekosa soko.

9. Ilani ya CCM: Serikali iliahidi itahakikisha inasimamia Deni la Taifa liendelee kuwa himilivu. Leo Deni limekua toka 35T walivyolikuta hadi 50T.

10: Ilani ya CCM: Serikali iliahidi itasimamia kwa ufanisi matumizi ya fedha za umma kwa kuzingatia sheria na miongozo ya ununuzi wa umma, ukaguzi na kusimamia mali za Serikali. Tumeshuhudia Issue ya CAG na 1.5t, ndege zimenunuliwa bila kufuata kanuni ya manunuzi, uwanja wa ndege wa chato umejengwa bila bunge kuidhinisha bajeti yake.

11. Ilani ya CCM: Serikali iliahidi itahakikisha inajenga zahanati kila kijiji, kila kata kuwa na Kituo cha Afya na kujenga hospitali kila Wilaya. Hili sina uhakika ngoja nimtag Waziri Ummy Mwalimu anaweza kuwa na takwimu.

Kama huu sio ulaghai kwa wananchi ni nini.

Ngoja niishie hapa, Mambo ni Mengi, muda Mchache.

Hizi ni facts anayepinga aje na data.
 
Kwa mujibu wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (2015-2020).

1. Ilani ya CCM: Serikali inaahidi itatenga kiasi cha shilingi milioni 50 kwa kila Kijiji, badala ya kupewa milioni 50 wamachinga ndio wanaichangia serikali elfu 2,000 kwa kila kitambulisho.

2. Ilani ya CCM: Serikali inaahidi itahakikisha wananchi wanaopakana na miundombinu ya gesi na ambako bomba la gesi linapita wananufaika na gesi. Wananchi walichoambulia ni kuona alama za njano bomba linapopitia na virungu.

3. Ilani ya CCM: Serikali inaahidi kuhamia Dodoma kabla ya 2020 tukaambiwa kufikia Desemba2018 Rais atakuwa Dodoma, hadi leo namuona bado yupo Dar.

4. Ilani ya CCM: Serikali inaahidi kuongeza kwa kiwango kikubwa uzalishaji wa nishati kutoka 1,300MW hadi 5,000MW ifikapo 2020. Sina uhakika hata megawati 2,000 zimefika.

5. Ilani ya CCM: Serikali inaahidi kipaumbele kitakuwa katika kukuza na kuanzisha viwanda vidogo, vya kati na vikubwa. Leo hata aliyeanzisha wimbo wa Tanzania ya viwanda anaona aibu kutamka mbele za watu.

6. Ilani ya CCM: Katika kipindi cha miaka mitano ijayo, serikali ya CCM itaendeleza mapambano dhidi ya adui rushwa na ufisadi. Leo CCM imerudia kuwakaribisha Mafisadi papa waliowakataa 2015 akiwepo fisadi mkuu Lowassa.

7. Ilani ya CCM: Serikali ya CCM itahakikisha thamani ya Shilingi yetu inatengamaa. Leo 1USD = 2400TZS.

8. Ilani ya CCM: Serikali itahakikisha inaongeza mauzo ya bidhaa zetu nje ya nchi. Leo mazao ya Korosho na Mbaazi yamekosa soko.

9. Ilani ya CCM: Serikali itahakikisha inasimamia Deni la Taifa liendelee kuwa himilivu. Leo Deni limekua toka 35T walivyolikuta hadi 50T.

10: Ilani ya CCM: Serikali itasimamia kwa ufanisi matumizi ya fedha za umma kwa kuzingatia sheria na miongozo ya ununuzi wa umma, ukaguzi na kusimamia mali za Serikali. Tumeshuhudia Issue ya CAG na 1.5t, ndege zimenunuliwa bila kufuata kanuni ya manunuzi, uwanja wa ndege wa chato umejengwa bila bunge kuidhinisha bajeti yake.

11. Ilani ya CCM: Serikali itahakikisha inajenga zahanati kila kijiji, Kata kuwa na Kituo cha Afya na kujenga hospitali Lila Wilaya. Hili sina uhakika ngoja nimtag Waziri Ummy Mwalimu.

Kama huu sio ulaghai kwa wananchi ni nini.

Ngoja niishie hapa, Mambo ni Mengi, muda Mchache.

Hizi ni facts anayepinga aje na data.

mkuu kipengele cha kwanza ni elf 20 sio elf 2 za wamachinga na wataokutwwa hawana kitambulisho mpaka wauza uji stand za mabasi faini ni elf 50 kwa mtu, ni lazima uwe nacho
 
Back
Top Bottom