Elections 2015 Ilani ya CCM 2015-2020 - Uchaguzi Mkuu 2015

Aug 8, 2013
10
33
ILANI YA CCM KWA AJILI YA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2015

91550FDD-E524-4DEA-8B5E-1EDF4C5406E1.jpeg

1. Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 wa kuwachagua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais wa Zanzibar, Wabunge, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Madiwani imeandaliwa ikiwa ni mkataba kati ya CCM na wananchi.
Ilani hii imeandikwa kwa kuzingatia Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2025 na Mwelekeo wa Sera za CCM zenye lengo na nia ya kuendelea kuwatumikia wananchi kwa kipindi cha miaka mitano ijayo (2015-2020).

2. Ilani hii ni tamko maalumukwa wapiga kura kuhusu nia ya CCM ya kuendelea kushika dola na kuwaongoza Watanzania kwa njia ya kidemokrasia, na hasa kuendelea kudumisha amani, umoja wa Kitaifa, usawa, ustawi wa wananchi, Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kwa kipindi kingine cha miaka mitano.

3. Nia na uwezo wa CCM wa kuendelea kuongoza Taifa hili unajidhihirisha katika uzoefu ambao tumeupata kwa miaka 38 tangu kuanzishwa kwake na kuwa madarakani, ambapo katika kipindi chote hiki kimeiwezesha nchi yetu kupata mafanikio makubwa katika nyanja za kiuchumi, kisiasa na kijamii.

4. Katika miaka mitano ijayo (2015-2020),CCM ikiwa madarakani, itazielekeza Serikali zake kutumia nguvu zake zote kuendelea kupambana na changamoto kubwa nne:-

Kwanza kuondoa umaskini; pili kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira hasa kwa vijana; tatu kuendeleza vita dhidi ya adui rushwa na ubadhirifu wa mali ya umma; na nne kuendelea kudumisha amani, ulinzi na usalama wa maisha ya wananchi na mali zao.

Vipaumbele:
1. Elimu
2. Afya
3. Kilimo
4. Miundombinu
5. Utawala bora
6. Mawasiliano

Angalia attachment...
 

Attachments

  • Ilani(Manifesto)-ya-CCM-2015-2020.pdf
    10 MB · Views: 268
Nionavyo:
Watanzania tumekwama hapa:
1. Elimu bora, na sio bora elimu kama ccm wanavyofanya. CCM wamechezea sana elimu hapa nchini. Kila kitu kimeparanganyika, kuanzia divisheni faifu. Elimu bora ni 'multiplier effect'
2. Uchumi.
Hapa ndio chimbuko la kuchukiwa CCM, bahati mbaya hawana habari. Uchumi umekufa!
 
Afya, utawala bora, miundombinu, kilimo ni matokeo ya elimu bora kwa watanzania na uchumi mzuri wa taifa!
 
Elimu bora! Uchumi mzuri huzalisha ajira! Ajira kama anavyosema Lowassa ni bomu la kulipuka muda wowote!
 
Nionavyo:
Watanzania tumekwama hapa:
1. Elimu bora, na sio bora elimu kama ccm wanavyofanya. CCM wamechezea sana elimu hapa nchini. Kila kitu kimeparanganyika, kuanzia divisheni faifu. Elimu bora ni 'multiplier effect'
2. Uchumi.
Hapa ndio chimbuko la kuchukiwa CCM, bahati mbaya hawana habari. Uchumi umekufa!

Nilishangaa kusikia kuna div 5, na nlisikitika kuona waziri wa elimu hajui kusoma wala haijui nchi yake!!! Nlihuzunika kuona twiga wanapandishwa ndege...bila kusahau uharamia wa pembe za ndovu!!! Wizi wa fedha za serikali...utumiaji wa mabavu na vyombo vya ulinzi!!

Kwa kuongezea tu, 1usd=2000+ tsh!!!
HII YOTE NI BAADA YA MIAKA ZAIDI YA 50 YA UHURU!!! WE NEED UKAWA NOTHING ELSE.
Cc baro The Tomorrow People na wooote ambao wanajidanganya ccm ndio jibu la shida za wa tz.
 
Last edited by a moderator:
Ccm wana kazi kubwa ya kuwambia watanzania ni nini wamesahau huko ikulu maana wamekuwa huko kwa miaka 54. Kama kwa miaka 54. Hawakufanya je watawezaje kufanya hayo kwa miaka 5? Elimu imekufa kabisa, afya ni ndio kabisa maana hakuna dawa kila hospitali ya serikali.kilimo nacho kinashida maana wakulima wamekopwa na hawana maslahi yeyote na kilimo chao.Miundombinu kama barabara zimejengwa lakini viwango Duni kabisa.Utawala bora ni hakuna maana rushwa imetamalaki kama ugonjwa wa kansa. CCM hawana jipya tena
 
Nilishangaa kusikia kuna div 5, na nlisikitika kuona waziri wa elimu hajui kusoma wala haijui nchi yake!!!
Kwa kuongezea tu, 1usd=2000+ tsh!!!
HII YOTE NI BAADA YA MIAKA ZAIDI YA 50 YA UHURU!!! WE NEED UKAWA NOTHING ELSE.

teh teh waziri wa elimu! ukawa dawa ya kuliponya taifa!
 
Ccm wana kazi kubwa ya kuwambia watanzania ni nini wamesahau huko ikulu maana wamekuwa huko kwa miaka 54. Kama kwa miaka 54. Hawakufanya je watawezaje kufanya hayo kwa miaka 5? Elimu imekufa kabisa, afya ni ndio kabisa maana hakuna dawa kila hospitali ya serikali.kilimo nacho kinashida maana wakulima wamekopwa na hawana maslahi yeyote na kilimo chao.Miundombinu kama barabara zimejengwa lakini viwango Duni kabisa.Utawala bora ni hakuna maana rushwa imetamalaki kama ugonjwa wa kansa. CCM hawana jipya tena

Duuu kazi wanayo! barabara chini ya kiwango, wamechakachua!
 
Nionavyo:
Watanzania tumekwama hapa:
1. Elimu bora, na sio bora elimu kama ccm wanavyofanya. CCM wamechezea sana elimu hapa nchini. Kila kitu kimeparanganyika, kuanzia divisheni faifu. Elimu bora ni 'multiplier effect'
2. Uchumi.
Hapa ndio chimbuko la kuchukiwa CCM, bahati mbaya hawana habari. Uchumi umekufa!

kweli kabisa mkuu vipaumbele vinapaswa kua hivyo,lakini Ni kituko wao natataka kuweka zaidi ya mambo 5.
inatosha akili zile zili ndo zimetufikisha hapa itakuwaje zitupeleke mbele?
 
Nionavyo:
Watanzania tumekwama hapa:
1. Elimu bora, na sio bora elimu kama ccm wanavyofanya. CCM wamechezea sana elimu hapa nchini. Kila kitu kimeparanganyika, kuanzia divisheni faifu. Elimu bora ni 'multiplier effect'
2. Uchumi.
Hapa ndio chimbuko la kuchukiwa CCM, bahati mbaya hawana habari. Uchumi umekufa!

kweli kabisa mkuu vipaumbele vinapaswa kua hivyo,lakini Ni kituko wao natataka kuweka zaidi ya mambo 5.
inatosha akili zile zili ndo zimetufikisha hapa itakuwaje zitupeleke mbele?
 
Sina hata muda wa kusoma. Najua ni wimbo mwingine unaokwenda kuimbwa majukwaani na wasanii walewale kisha utaishia hukohuko majukwaani.
 
Hapo kwenye elimu, wataboresha kwa kuleta laptop kwa walimu. Hayo nayo ni maendeleo ukilinganisha na miaka iliyo pita. "let's wait and see"
 
Elimu gani walioisimamia kwa miaka 54 ikaleta maendeleo?
Huduma za afya ambazo hakuna hata madawa hospitali?

Watanzania tuamke, tuwe critical thinkers.
 
Viwanda na mashirika hamna tena,sasa hili bomu la ajira mtalitatua vp?na huo uchumi wa kati tutafikaje?au mnataka vijana waendelee kuendesha bodaboda?
 
Back
Top Bottom