Elections 2015 Ilani ya CCM 2015-2020 - Uchaguzi Mkuu 2015

Magu hana mbele wa nyuma....anajidai kujenga miundombinu inayogharimu mabilioni ya pesa ilimradi tu akumbukwe kama Nyerere..Fool prezida!!
 
Miaka 57 wameshindwa kufanya lolote la maana ije kuwa miaka hii mitano ,wanaweza ni ufisadi ,kuteka ,kuua ,kufunga kwenye viroba .
 
Kwa mujibu wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (2015-2020).

1. Ilani ya CCM: Serikali inaahidi itatenga kiasi cha shilingi milioni 50 kwa kila Kijiji, badala ya kupewa milioni 50 wamachinga ndio wanaichangia serikali elfu 20,000 kwa kila kitambulisho.

2. Ilani ya CCM: Serikali inaahidi itahakikisha wananchi wanaopakana na miundombinu ya gesi na ambako bomba la gesi linapita wananufaika na gesi. Walichoambulia wananchi ni kuona alama za njano bomba linakopita na virungu vya polisi.

3. Ilani ya CCM: Serikali inaahidi kuhamia Dodoma kabla ya 2020 tukaambiwa kufikia Desemba 2018 Rais atakuwa Dodoma, hadi leo namuona bado yupo Dar.

4. Ilani ya CCM: Serikali inaahidi kuongeza kwa kiwango kikubwa uzalishaji wa nishati kutoka 1,300MW hadi 5,000MW ifikapo 2020. Sina uhakika hata megawati 2,000 zimefika.

5. Ilani ya CCM: Serikali inaahidi kipaumbele kitakuwa katika kukuza na kuanzisha viwanda vidogo, vya kati na vikubwa. Leo hata aliyeanzisha wimbo wa Tanzania ya viwanda anaona aibu kutamka mbele za watu.

6. Ilani ya CCM: Katika kipindi cha miaka mitano ijayo, serikali ya CCM itaendeleza mapambano dhidi ya adui rushwa na ufisadi. Leo CCM imerudi kuwakaribisha Mafisadi papa waliowakataa 2015 akiwepo fisadi mkuu Lowassa.

7. Ilani ya CCM: Serikali ya CCM itahakikisha thamani ya Shilingi yetu inatengamaa. Leo 1USD = 2400TZS.

8. Ilani ya CCM: Serikali itahakikisha inaongeza mauzo ya bidhaa zetu nje ya nchi. Leo mazao ya Korosho na Mbaazi yamekosa soko.

9. Ilani ya CCM: Serikali itahakikisha inasimamia Deni la Taifa liendelee kuwa himilivu. Leo Deni limekua toka 35T walivyolikuta hadi 50T.

10: Ilani ya CCM: Serikali itasimamia kwa ufanisi matumizi ya fedha za umma kwa kuzingatia sheria na miongozo ya ununuzi wa umma, ukaguzi na kusimamia mali za Serikali. Tumeshuhudia Issue ya CAG na 1.5t, ndege zimenunuliwa bila kufuata kanuni ya manunuzi, uwanja wa ndege wa chato umejengwa bila bunge kuidhinisha bajeti yake.

11. Ilani ya CCM: Serikali itahakikisha inajenga zahanati kila kijiji, kila kata kuwa na Kituo cha Afya na kujenga hospitali kila Wilaya. Hili sina uhakika ngoja nimtag Waziri Ummy Mwalimu anaweza kuwa na takwimu.

Kama huu sio ulaghai kwa wananchi ni nini.

Ngoja niishie hapa, Mambo ni Mengi, muda Mchache.

Hizi ni facts anayepinga aje na data.
Sasa kampeni unafanyia kweye haka kajukwaa wasomaji hawazidi laki, na ni walewale wa kila siku ambao hiki ndio kijiwe chao,wakati watanzania wapo milioni 60 na wengi wao wapo vijijini na wanatumia simu za tochi na tbc television,unategemea kuingia ikulu kwa kuota ndoto za mchana


Leteni sera mbadala ,huu wimbo umechuja

Magu anachakuongea ,SGR,Ndege,elimu bure,wafanyakazi hewa,nidhamu ya watumishi,stigliers ,kapanua bandari karibu zote nchini,viwanja vya ndege ,vituo vya afya na dawa vimeongezeka,dawa za kulevya na ujambazi vimedhibitiwa kwa kiasi chake,ujangili wa wanyama pori umedhibitiwa,na mengineo mengi .

Cha kufanya lazima muwe unique,muwaambie watanzania mtawafanyia nini kikubwa zaidi,

Ikiwa mmeshindwa hata kujenga ofisi ya makao makuu ya chama ni kipi mtaweza ?,nafikiri ni porojo tu ndizo mnaziweza na kusubiria matukio

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom