Hoja ya Mkonge kuimaliza CCM Tanga - Zitto na Mnyika watikisa Korogwe

Zitto alivamia ajenda ya Wabunge wa Majimbo ya Korogwe, kwa vyovyote vile alitegemea wangempinga. Angetaka afanikishe ajenda yake, ambayo kimsingi ni nzuri, angewahusisha wenzake wenye dhamana na majimbo hayo. Tatizo lilikuwa ni njia na wala siyo malengo (kama kweli alikuwa nayo, na kama alikuwa na nia ya kizalendo ya kutaka mafanikio kwenye hili). Kama alikuwa anafanya siasa, kama inavyojidhihirisha sasa, matokeo ndiyo hayo - kukumbana na upinzani na ushindani mkali!

Mimi binafsi nimejifunza: Hoja yangu binafsi ya uchimbaji dhahabu Nzega nliyoiwasilisha kwenye zaidi ya mikutano 5 ya Bunge haijawahi kupatiwa nafasi kwa visingizio visivyo na maana kwa vile tu ni ya kipambanaji na mimi niliifanya ni yangu binafsi, sasa nimeamua kuunganisha wadau wengi zaidi ili tushirikiane kuiweka sawa na kuiwasilisha tena. Na sasa nimeamua kuwasilisha hoja binafsi bungeni kuhusiana na ajenda ya 'ajira kwa vijana' lakini nitawashirikisha wabunge wenzangu vijana kabla ya kufanya hivyo ili tufanikishe upatikanaji wa ufumbuzi wa pamoja wa tatizo hili...

Mh. Kigwangalla,

Katika matamshi uliyowahi kunishangaza ni hili la leo. Kumbe tatizo kwako si ukweli wa hoja bali ni njia aliyotuia Zitto.

Kwa namna moja umewatukana Wabunge wa Korogowe na wana CCM wote kwamba wanachojali ni njia wanayoitaka wao hata kama jambo lenyewe ni la ukweli na manufaa.

Principle ya ukweli ni kwamba ukweli hauhitaji njia ya kuufikisha. Ukweli hauna wakati muafaka. Wakati wote ni wakati wa kuutoa ukweli.

Mwenye tatizo ni anayeambiwa ukweli na si ukweli wenyewe. Hivyo, hapa mwenye tatizo ni wewe na wote mlioukataa ukweli wa Zitto.

Kama Zitto akisema DSalaam itakumbwa na Tsunami basi Kigwangala unatuambia kuwa Zitto achague njia ya kutuambia ili wabunge wa CCM Dar wasimpinge.

Kingwangwala ninaamini wewe ni Doctor.

Kama Zitto akisema jimboni kwako kipindupindu kinawashambulia wapiga kura wako basi unatuambia kuwa afanye caucas na wewe na wana-Tabora ili mkubaliane na ukweli huo na ndipo muuunge mkono.

Ndugu yangu,

Hakuna siku uliyojiaibisha kama leo, ningekuwa wewe ningefuta kauli hii kwa njia yoyote.
 
Ni bahati mbaya kuwa hoja ya mwanasiasa wa chama tawala imejadiliwa na wasomi tena wengi ni vijana wapenda mageuzi! Ukumbukeni upinzani alioupata Obama dhidi ya sera yake ya afya kwa wote(masikini watibiwe bure),hiki ndicho kilichomkuta Zitto.Ni jambo jema watoto wangu kuvaa vizuri lkn kama utatengeneza mazingira ya watoto wangu na mama yao wote kujua kuwa wewe umeguswa na uchakavu wa nguo zao kuliko mimi,it's obvious that I won't accept it.Kama kweli umewahurumia na probably kutokana na ujinga wangu nilikuwa sijalifikiria hilo,na nia yako siyo kujijenga wewe wala chama chako jimboni kwangu bali ni kuliendeleza taifa,why can't you let me be part of it kabla ya kujitambulisha kitaifa kuwa ni hoja yako?Na kama lengo ni kujijenga na chama chako,wewe ungeshabikia mpango wa kukuangusha mwenyewe?Haipendezi wasomi kujadili vitu kinafiki,let's be realistic all the time.
 
quote_icon.png
By HKigwangalla

Zitto alivamia ajenda ya Wabunge wa Majimbo ya Korogwe, kwa vyovyote vile alitegemea wangempinga. Angetaka afanikishe ajenda yake, ambayo kimsingi ni nzuri, angewahusisha wenzake wenye dhamana na majimbo hayo. Tatizo lilikuwa ni njia na wala siyo malengo (kama kweli alikuwa nayo, na kama alikuwa na nia ya kizalendo ya kutaka mafanikio kwenye hili). Kama alikuwa anafanya siasa, kama inavyojidhihirisha sasa, matokeo ndiyo hayo - kukumbana na upinzani na ushindani mkali!

Mimi binafsi nimejifunza: Hoja yangu binafsi ya uchimbaji dhahabu Nzega nliyoiwasilisha kwenye zaidi ya mikutano 5 ya Bunge haijawahi kupatiwa nafasi kwa visingizio visivyo na maana kwa vile tu ni ya kipambanaji na mimi niliifanya ni yangu binafsi, sasa nimeamua kuunganisha wadau wengi zaidi ili tushirikiane kuiweka sawa na kuiwasilisha tena. Na sasa nimeamua kuwasilisha hoja binafsi bungeni kuhusiana na ajenda ya 'ajira kwa vijana' lakini nitawashirikisha wabunge wenzangu vijana kabla ya kufanya hivyo ili tufanikishe upatikanaji wa ufumbuzi wa pamoja wa tatizo hili...

Na wewe kumbe punguani.
 
Naona kuna kitu hakieleweki vizuri hapa, kwamba mimi sina tatizo na Zitto na njia aliyotumia ila nimeongea hapa kwa kutoa uzoefu wangu mdogo nilioupata Bungeni kama mtu akitaka kufanikisha jambo lake mle ndani. Nikaenda mbele nikaeleza jinsi nilivyokwama kwa sababu tu sikujipanga vizuri. Zitto mwenyewe anajua vizuri kuliko hata mimi hiki ninachokiongelea> Kwa ukweli kuna siasa mle ndani na kuna wakati mtu unataka kufanikisha jambo lako. Ni yeye aliyeibuka na muswada binafsi wa PBO (parliamentary budget office) na kwa kuwa aliona ni muswada muhimu sana, alilazimika kutushirikisha wabunge wengi zaidi bila kujali vyama vyetu. Na mimi nakiri nilijifunza kitu pale. Bungeni kuna lobbying na kuna kukurupuka, na hata kama una uchungu na una hoja nzuri namna gani, kama zisipofanikiwa zitajulikana vipi, na zitasaidia vipi watanzania? In fact mimi sina tatizo na hoja ya Zitto, mimi naiunga mkono kabisa, nikiwa kama mdau mkubwa sana wa kilimo na maisha ya watanzania wakulima.

Wale wabunge Korogwe kila siku wanaongelea ajenda yao hiyo ya Mkonge (ndiyo mtoto pekee wa kisiasa waliye naye), na kila siku wanapambana na kampuni ya Katani Ltd na serikali na jinsi zao hilo lisivyoleta faida kwa wanakorogwe wa kawaida na jinsi wale vibarua na wafanyakazi wa mle kwenye mashamba ya mkonge walivyodhulumiwa pesa zao, walishawasilisha hoja zao zinazohusu zao hilo zikakataliwa, walishauliza maswali yao yakajibiwa kwa kuundwa kwa tume itakayochunguza mkonge na tuhuma zote zinazotolewa, leo ghafla wasikie hoja ya Zitto, hivi kibinadam wale wanasiasa wanaotaka kuonekana nao wanatetea wananchi wao wangekubali? Na hata hivyo majibu ya serikali yalikuwa wazi tu, kwa ufupi, yalitegemewa! Kwa sababu siku mbili kabla ya hapo Mhe. Stephen Hillary Ngonyani(MB, Korogwe Rural) aliuliza swali na akaahidiwa tume itaundwa ili kuchunguza suala la mkonge na makando kando yake, sasa jibu la serikali lilikuja limeisha-printiwa kabisa likimwambia Zitto kuhusu hatua hizo zilizochukuliwa na serikali. Kwa vyovyote vile hata kama Mhe. Yusuph Nassir (MB, Korogwe Urban) angekwama kuwasilisha ile hoja yake ya pingamizi bado tu Mhe. Zitto Zuberi Kabwe (MB, Kigoma North) angepewa jibu lile lile la Waziri Maghembe, lisingekuwa tofauti! Si kitu kigeni, ni utaratibu ambao Zitto mwenyewe anaujua vizuri.

Mimi nilitoa tathmini yangu na msimamo wangu hautabadilika. Kama kuna mtu alidhani nahitaji heshima kutoka kwake kwa kufumba mdomo wangu, basi na asiniheshimu, anitukane na wala haininyimi usingizi! Sifanyi mambo kwa kumuogopa mtu ama kwa kumuonesha mtu kuwa mimi ni shujaa, nafanya ninachoona sahihi tu na hiyo ndiyo dira yangu, period!
 
Kilimo cha Mkonge ni wakulima wangapi wa Korogwe wanaweza kukilima kama kilimo chao? na ni wangapi watabaki kama manamba wa mashamba ya Mkonge ya wakulima wenye uwezo?

Hoja dhaifu, na wewe Kigwangallah unaejidai kuunga mkono, huwaambii ukweli wenzako, unawatia kwenye mkenge.

Theoretically, mwana siasa yeyote anaweza akaipamba au akaiponda hoja atakavyo, kuzungusha maneno ndio fani yao.

Practically, hoja ya mkonge ni dhaifu sana kwa mkulima (manamba) wa Korogwe, ukiondooa wale wenye misingi mikubwa. Wengine watabaki kuwa manamba, vibarua na wasaidizi wa wenye mashamba ya Mkonge. Ukweli ubaki kuwa Ukweli.

Mohamed Enterprise kisha komba mashamba mengi sana (yaliokuwa ya wazungu enzi hizo kabla hayaja-taifishwa) kuanzia Korogwe mpaka Same. Na huku kwingine kuanzia Mdaula mpaka Morogoro. Nani asiojuwa hilo?

Simlaumu METL kwa hilo, haya mashamba yanataka misingi mikubwa na yeye ana uwezo wa kuikopa hiyo mitaji. Kamkulima kakungoja ruzuku kanayameza hayo? Maaweee!
 
Naona kuna kitu hakieleweki vizuri hapa, kwamba mimi sina tatizo na Zitto na njia aliyotumia ila nimeongea hapa kwa kutoa uzoefu wangu mdogo nilioupata Bungeni kama mtu akitaka kufanikisha jambo lake mle ndani. Nikaenda mbele nikaeleza jinsi nilivyokwama kwa sababu tu sikujipanga vizuri. Zitto mwenyewe anajua vizuri kuliko hata mimi hiki ninachokiongelea> Kwa ukweli kuna siasa mle ndani na kuna wakati mtu unataka kufanikisha jambo lako. Ni yeye aliyeibuka na muswada binafsi wa PBO (parliamentary budget office) na kwa kuwa aliona ni muswada muhimu sana, alilazimika kutushirikisha wabunge wengi zaidi bila kujali vyama vyetu. Na mimi nakiri nilijifunza kitu pale. Bungeni kuna lobbying na kuna kukurupuka, na hata kama una uchungu na una hoja nzuri namna gani, kama zisipofanikiwa zitajulikana vipi, na zitasaidia vipi watanzania? In fact mimi sina tatizo na hoja ya Zitto, mimi naiunga mkono kabisa, nikiwa kama mdau mkubwa sana wa kilimo na maisha ya watanzania wakulima.

Wale wabunge Korogwe kila siku wanaongelea ajenda yao hiyo ya Mkonge (ndiyo mtoto pekee wa kisiasa waliye naye), na kila siku wanapambana na kampuni ya Katani Ltd na serikali na jinsi zao hilo lisivyoleta faida kwa wanakorogwe wa kawaida na jinsi wale vibarua na wafanyakazi wa mle kwenye mashamba ya mkonge walivyodhulumiwa pesa zao, walishawasilisha hoja zao zinazohusu zao hilo zikakataliwa, walishauliza maswali yao yakajibiwa kwa kuundwa kwa tume itakayochunguza mkonge na tuhuma zote zinazotolewa, leo ghafla wasikie hoja ya Zitto, hivi kibinadam wale wanasiasa wanaotaka kuonekana nao wanatetea wananchi wao wangekubali? Na hata hivyo majibu ya serikali yalikuwa wazi tu, kwa ufupi, yalitegemewa! Kwa sababu siku mbili kabla ya hapo Mhe. Stephen Hillary Ngonyani(MB, Korogwe Rural) aliuliza swali na akaahidiwa tume itaundwa ili kuchunguza suala la mkonge na makando kando yake, sasa jibu la serikali lilikuja limeisha-printiwa kabisa likimwambia Zitto kuhusu hatua hizo zilizochukuliwa na serikali. Kwa vyovyote vile hata kama Mhe. Yusuph Nassir (MB, Korogwe Urban) angekwama kuwasilisha ile hoja yake ya pingamizi bado tu Mhe. Zitto Zuberi Kabwe (MB, Kigoma North) angepewa jibu lile lile la Waziri Maghembe, lisingekuwa tofauti! Si kitu kigeni, ni utaratibu ambao Zitto mwenyewe anaujua vizuri.

Mimi nilitoa tathmini yangu na msimamo wangu hautabadilika. Kama kuna mtu alidhani nahitaji heshima kutoka kwake kwa kufumba mdomo wangu, basi na asiniheshimu, anitukane na wala haininyimi usingizi! Sifanyi mambo kwa kumuogopa mtu ama kwa kumuonesha mtu kuwa mimi ni shujaa, nafanya ninachoona sahihi tu na hiyo ndiyo dira yangu, period!
Umeelezea vizuri.....
Actually Zitto naye ana hoja nzuri, ila kuna research na publications nyingi ambazo zinagongana kuhusu Trend ya synthetic fibres na katani vs Oil prices...
Kuhusu environmental savy societies, hilo bado ni questionable kwa sababu trend inaonyesha kuwa China ndiyo imeongeza import bill yake up to 30% ( a bit more). Na siyo kwa sababu ya mazingira.
Kwa nchi kama Tanzania, Kenya na Madagascar ni lazima waangalie elasticity kabla ya kufanya big moves.
Na ni ukweli kama Zomba anavyosema..... katani is labor intensive na wage bill yake huleta mfarakano kati ya wamiliki na wafanyakazi.
Katani (based on manambas) played a big role kwenye uhuru especially from trade unions, but it was like a curse when government owned the farms ... profitability yake, apart from the introduction of synthetic fibres inaliwa sana na laborers.
 
Zitto alivamia ajenda ya Wabunge wa Majimbo ya Korogwe, kwa vyovyote vile alitegemea wangempinga. Angetaka afanikishe ajenda yake, ambayo kimsingi ni nzuri, angewahusisha wenzake wenye dhamana na majimbo hayo. Tatizo lilikuwa ni njia na wala siyo malengo (kama kweli alikuwa nayo, na kama alikuwa na nia ya kizalendo ya kutaka mafanikio kwenye hili). Kama alikuwa anafanya siasa, kama inavyojidhihirisha sasa, matokeo ndiyo hayo - kukumbana na upinzani na ushindani mkali!
Nimeisomaaa..., nimeisoma tenaaa... nikarudia tenaaaa...! Lakini lazima nikiri kuwa nimeshindwa kuielewa point ya Dr. Hamisi Kigwangalla, MD, MPH, MBA! Mara Zitto kavamia ajenda ya watu, ajenda yenyewe iliyovamiwa ni ya watu hao hao ila kwa kuwa Zitto kavamia, watu hao hao kikawaida, kama anavyodai Dr. Hamisi Kigwangalla, MD, MPH, MBA, lazima wapinge ajenda yao hiyo, kwa sababu? imevamiwa na mpinzani!

Imekuwa kawaida kwa Wapinzani na hasa wale wa Chadema kulaumiwa kwa kupinga kila kitu, sasa hapa Zitto anakumbana na upinzani na ushindani mkali kwa kuivamia ajenda, hivi kumbe kuvamia ni sawa na kupinga! Je kama Zitto angetoa ajenda ya kupinga hoja ya wabunge hao wa Tanga, Dr. Hamisi Kigwangalla, MD, MPH, MBA, bila shaka angemaka aha, mnaona, kazi ya hawa jamaa ni kupinga tuu hata kile chenye manufaa kwa taifa!

Kaazi kweli kweli...
 
Nimeisomaaa..., nimeisoma tenaaa... nikarudia tenaaaa...! Lakini lazima nikiri kuwa nimeshindwa kuielewa point ya Dr. Hamisi Kigwangalla, MD, MPH, MBA! Mara Zitto kavamia ajenda ya watu, ajenda yenyewe iliyovamiwa ni ya watu hao hao ila kwa kuwa Zitto kavamia, watu hao hao kikawaida, kama anavyodai Dr. Hamisi Kigwangalla, MD, MPH, MBA, lazima wapinge ajenda yao hiyo, kwa sababu? imevamiwa na mpinzani!

Imekuwa kawaida kwa Wapinzani na hasa wale wa Chadema kulaumiwa kwa kupinga kila kitu, sasa hapa Zitto anakumbana na upinzani na ushindani mkali kwa kuivamia ajenda, hivi kumbe kuvamia ni sawa na kupinga! Je kama Zitto angetoa ajenda ya kupinga hoja ya wabunge hao wa Tanga, Dr. Hamisi Kigwangalla, MD, MPH, MBA, bila shaka angemaka aha, mnaona, kazi ya hawa jamaa ni kupinga tuu hata kile chenye manufaa kwa taifa!

Kaazi kweli kweli...
Unachoshindwa kukielewa ni kuwa hii hoja ilishazungumziwa bungeni.
Na serikali inafanya uchunguzi. Sasa kuipitisha kinguvu na ku-override kamati ni kama aina fulani ya uanasiasa kuingilia utaalam.
Kama tatizo ni ukiritimba wa kamati, labda unaweza kuwa na hoja.
Ndio maana umeambiwa walikuwa wanapigania PBO. Au kwa huku umangani huwa inaitwa CBO (Congressional Budget Office).... ambayo kazi yake ni kuangalia feasibility ya miswaada mbalimbali inayoletwa na wawakilishi/wabunge.
Kuliko kutoa Data google, ni vizuri ku-establish mwanamahesabu ambaye bunge lita rely on, ambaye atapitisha au atapingana na data ambazo mbunge atazileta!!
Not merely an economist, but an Actualist(Non-partisan) is needed for that, ili hivi vikamati visiwe vinaundwa kupeana ulaji.
Nimemuelewa, ila kama hujamuelewa jaribu kujifunza how legislations come into effect from the time they are introduced to the signing.
 
In fact mimi sina tatizo na hoja ya Zitto, mimi naiunga mkono kabisa, nikiwa kama mdau mkubwa sana wa kilimo na maisha ya watanzania wakulima.

Mheshimiwa, mbona taarifa zinaonesha wewe ulikuwa wa kwanza kuipinga hiyo hoja bungeni?
 
Hongereni makamanda wa CDM kwa kuivuruga ccm Korogwe
Suala la kilimo cha mkonge lingechukuliwa kama la kiuchumi badala ya la kisiasa lina mantiki sana hasa katika kukuza ajira ya vijana na watu wetu wengine. Sekta ya kilimo cha mkonge kama ilivyo kwa sekta ya viwanda vya nguo, ni sekta yenye potential kubwa sana ya kukuza ajira nyingi nchini. Lakini kwa bahati mbaya hata mchumi kama Zitto anataka kuli-politisize badala ya kulifanya la kiuchumi! Too bad! Tunaangalia maslahi ya vyama vyetu na "kuchukua" nchi 2012, badala ya maslahi ya watu wetu, hasa vijana wasiokuwa na ajira! Nia yetu isingekuwa kuivuruga CCM Korogwe, bali kusaidia kuinua kilimo cha mkonge ili kuinua uchumi wa nchi na kuzalisha ajira zaidi kwa watanzania.
 
Tanzania inakera Kila kitu siasa!!!!!!!!! Ona sasa kilimo siasa migomo ya waalimu, madaktari siasa! Nchi inakera hii Ajira kwa vijana, siasa! tena mtu anasema nitafute waungaji mkono ili tujadili then mkishajadili iweje sasa hilo Bunge limeshajadili mambo mengi na hata yasipotekelezwa halina meno, yako wapi maazimio ya Richmond je ile tume ya million kadhaa za kupitishia bajeti katoka Ruhanjo kwa kustaafu na yule mwingine aliyekuwa na cheo kama mama Brandinda ambaye waziri mkuu hakuwa na mammla ya kumng'oa!
 
Dr. Hamisi Kigwangalla, MD, MPH, MBA
Mabadiliko ya kweli yataletwa na sisi...!

Hebu tupe ufafanuzi kwenye red sisi CCM, VIJANA AU WAPINZANI?
Usilete lugha za kisanii hapa tunaongelea maendeleo ya wana Korogwe na Tanzania kwa ujumla, huu ni mfano dhahiri wa mnachofanya mkiwa Bungeni dhihaka na uwongo na hicho ndicho kinachorudisha maendeleo ya Taifa letu, nchi zote Afrika ya mashariki ukiachia Tanzania angalau zina mwelekeo wa kupiga maendeleo nyie mnachojua kupigania ni posho tu.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Naona kuna kitu hakieleweki vizuri hapa, kwamba mimi sina tatizo na Zitto na njia aliyotumia ila nimeongea hapa kwa kutoa uzoefu wangu mdogo nilioupata Bungeni kama mtu akitaka kufanikisha jambo lake mle ndani. Nikaenda mbele nikaeleza jinsi nilivyokwama kwa sababu tu sikujipanga vizuri. Zitto mwenyewe anajua vizuri kuliko hata mimi hiki ninachokiongelea> Kwa ukweli kuna siasa mle ndani na kuna wakati mtu unataka kufanikisha jambo lako. Ni yeye aliyeibuka na muswada binafsi wa PBO (parliamentary budget office) na kwa kuwa aliona ni muswada muhimu sana, alilazimika kutushirikisha wabunge wengi zaidi bila kujali vyama vyetu. Na mimi nakiri nilijifunza kitu pale. Bungeni kuna lobbying na kuna kukurupuka, na hata kama una uchungu na una hoja nzuri namna gani, kama zisipofanikiwa zitajulikana vipi, na zitasaidia vipi watanzania? In fact mimi sina tatizo na hoja ya Zitto, mimi naiunga mkono kabisa, nikiwa kama mdau mkubwa sana wa kilimo na maisha ya watanzania wakulima.

Wale wabunge Korogwe kila siku wanaongelea ajenda yao hiyo ya Mkonge (ndiyo mtoto pekee wa kisiasa waliye naye), na kila siku wanapambana na kampuni ya Katani Ltd na serikali na jinsi zao hilo lisivyoleta faida kwa wanakorogwe wa kawaida na jinsi wale vibarua na wafanyakazi wa mle kwenye mashamba ya mkonge walivyodhulumiwa pesa zao, walishawasilisha hoja zao zinazohusu zao hilo zikakataliwa, walishauliza maswali yao yakajibiwa kwa kuundwa kwa tume itakayochunguza mkonge na tuhuma zote zinazotolewa, leo ghafla wasikie hoja ya Zitto, hivi kibinadam wale wanasiasa wanaotaka kuonekana nao wanatetea wananchi wao wangekubali? Na hata hivyo majibu ya serikali yalikuwa wazi tu, kwa ufupi, yalitegemewa! Kwa sababu siku mbili kabla ya hapo Mhe. Stephen Hillary Ngonyani(MB, Korogwe Rural) aliuliza swali na akaahidiwa tume itaundwa ili kuchunguza suala la mkonge na makando kando yake, sasa jibu la serikali lilikuja limeisha-printiwa kabisa likimwambia Zitto kuhusu hatua hizo zilizochukuliwa na serikali. Kwa vyovyote vile hata kama Mhe. Yusuph Nassir (MB, Korogwe Urban) angekwama kuwasilisha ile hoja yake ya pingamizi bado tu Mhe. Zitto Zuberi Kabwe (MB, Kigoma North) angepewa jibu lile lile la Waziri Maghembe, lisingekuwa tofauti! Si kitu kigeni, ni utaratibu ambao Zitto mwenyewe anaujua vizuri.

Mimi nilitoa tathmini yangu na msimamo wangu hautabadilika. Kama kuna mtu alidhani nahitaji heshima kutoka kwake kwa kufumba mdomo wangu, basi na asiniheshimu, anitukane na wala haininyimi usingizi! Sifanyi mambo kwa kumuogopa mtu ama kwa kumuonesha mtu kuwa mimi ni shujaa, nafanya ninachoona sahihi tu na hiyo ndiyo dira yangu, period!


Mh. Hamisi
Hizi unazoleta hapa JF ni porojo za kisiasa, kama kweli una uchungu na nchi yako basi ulichopaswa kufanya ni kuwaunga akina Zitto bila kujali tofauti za kichama, hata hao wabunge wa Korogwe wangeweza kuungana na kina Zitto kwani lengo si kupata umaarufu wa kisiasa Zitto tayari ni maarufu, kinachopiganiwa ni maslahi ya Taifa; tatizo la wabunge wetu hasa CCM hawaangalii maslahi ya Taifa letu ndio sababu nchi imeingizwa kwenye mikataba mibovu; unapodai ndani ya Bunge kuna Lobbying je lobbying zinafanywa kwa maslahi ya Taifa au maslahi yenu binafsi wabunge? Inasikitisha sana kuona mbunge kijana na mwenye elimu kama wewe kuja kuandika PUMBA kama hizi laiti kama angeandika mbunge mwenye elimu ya darasa la saba kama Ngonyani tungeelewa; mpo ndani ya bunge kama rubber stamp tu hamna jipya sasa waachieni hao wapinzani angalau wana nia ya kuyaweka hadharani. Dira huna mnatekeleza maazimio ya NEC na si watanzania waliowachagua SHAME ON YOU!!!!

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Sioni namna BEE policy ya Africa Kusini inavyoweza ku-fit kwenye mazingira yetu, BEE inafaa Afrika Kusini kwa sababu za kihistoria! Tanzania hatuna siasa za Whites and Blacks! Kwa hiyo hatuhitaji "Black Economic Empowerment, BEE"

mkuu na wewe tumia akili kidogo hatuendi ku copy na ku paste BEE hapa kwetu ila BEE inaweze kuwa modified na ikafiti mazingira yetu, cha maana ni kujifunza inavo work SA na ilivopokelewa na changamoto zake then policy makers na wataalam wanaweza kuitengeneza upya ifae hapa kwetu
 
ASANTENI WAH ZITTO NA MNYIKA:
SASA TUNAHITAJI KAMPENI YA 'OPERESHENI FUFUA MKONGE' UTIKISE KILA KIJIJI KATIKA MIKOA HUSIKA ILI TUKAWASAIDIE WANANCHI HAWA


Vichaa wetu Mnyika na Kabwe, mpka hapo ni zaidi ya BAO LA KISIGINO golini mwake CCM kwa mikoa ya mkonge kote nchini.

Hadi hivi sasa ni dhahiri kwamba ulaghai wa CCM kwa wananchi kwa upande mmoja na kwingineko kuwakomoa wasipate maendeleo yote ni mambo ambayo sasa yamebainika kwa wananchi hadi vijiji vya ndani ndani huko Korogwe.

Hadi hapa CHADEMA tushikane bega kwa bega na wananchi wa mikoa hii ya Morogoro, Pwani na Kilimanjaro kwa kuwatembelea huko huko mashambani kupitia kampeni mpya tutakayoiita
'Oparesheni Fufua Mkonge' ili tunaporudi bungeni iwe ni kweli tunawashilisha sauti zao zilizosalitiwa na wabunge wa CCM akiwamo 'Prof' Majimafupi.

CDM makao makuu pamoja na BAVICHA, ova; turudishe matumaini kwa vijana waliokosa ajira na wakulima waliodumaa kimapato kupitia kampeni hii kote vijijini!!!!!!!
Tumia lugha ya heshima hasa unapowa adress waheshimiwa wabunge utwaitaje wabunge hawa vijana wapambanaji vichaa?? hapa hakuna nafasi ya maneno ya kihuni, please be decent!!
 
Zitto alivamia ajenda ya Wabunge wa Majimbo ya Korogwe, kwa vyovyote vile alitegemea wangempinga. Angetaka afanikishe ajenda yake, ambayo kimsingi ni nzuri, angewahusisha wenzake wenye dhamana na majimbo hayo. Tatizo lilikuwa ni njia na wala siyo malengo (kama kweli alikuwa nayo, na kama alikuwa na nia ya kizalendo ya kutaka mafanikio kwenye hili). Kama alikuwa anafanya siasa, kama inavyojidhihirisha sasa, matokeo ndiyo hayo - kukumbana na upinzani na ushindani mkali!

Mimi binafsi nimejifunza: Hoja yangu binafsi ya uchimbaji dhahabu Nzega nliyoiwasilisha kwenye zaidi ya mikutano 5 ya Bunge haijawahi kupatiwa nafasi kwa visingizio visivyo na maana kwa vile tu ni ya kipambanaji na mimi niliifanya ni yangu binafsi, sasa nimeamua kuunganisha wadau wengi zaidi ili tushirikiane kuiweka sawa na kuiwasilisha tena. Na sasa nimeamua kuwasilisha hoja binafsi bungeni kuhusiana na ajenda ya 'ajira kwa vijana' lakini nitawashirikisha wabunge wenzangu vijana kabla ya kufanya hivyo ili tufanikishe upatikanaji wa ufumbuzi wa pamoja wa tatizo hili...

Si wametishia kukunyamazisha lakini? uliahidi kusema kitu, mpaka sasa hujasema sasa naona umeamua kuwa kada mwaminifu. SIASA KWELIKWELI
 
Naona kuna kitu hakieleweki vizuri hapa, kwamba mimi sina tatizo na Zitto na njia aliyotumia ila nimeongea hapa kwa kutoa uzoefu wangu mdogo nilioupata Bungeni kama mtu akitaka kufanikisha jambo lake mle ndani. Nikaenda mbele nikaeleza jinsi nilivyokwama kwa sababu tu sikujipanga vizuri. Zitto mwenyewe anajua vizuri kuliko hata mimi hiki ninachokiongelea> Kwa ukweli kuna siasa mle ndani na kuna wakati mtu unataka kufanikisha jambo lako. Ni yeye aliyeibuka na muswada binafsi wa PBO (parliamentary budget office) na kwa kuwa aliona ni muswada muhimu sana, alilazimika kutushirikisha wabunge wengi zaidi bila kujali vyama vyetu. Na mimi nakiri nilijifunza kitu pale. Bungeni kuna lobbying na kuna kukurupuka, na hata kama una uchungu na una hoja nzuri namna gani, kama zisipofanikiwa zitajulikana vipi, na zitasaidia vipi watanzania? In fact mimi sina tatizo na hoja ya Zitto, mimi naiunga mkono kabisa, nikiwa kama mdau mkubwa sana wa kilimo na maisha ya watanzania wakulima.

Wale wabunge Korogwe kila siku wanaongelea ajenda yao hiyo ya Mkonge (ndiyo mtoto pekee wa kisiasa waliye naye), na kila siku wanapambana na kampuni ya Katani Ltd na serikali na jinsi zao hilo lisivyoleta faida kwa wanakorogwe wa kawaida na jinsi wale vibarua na wafanyakazi wa mle kwenye mashamba ya mkonge walivyodhulumiwa pesa zao, walishawasilisha hoja zao zinazohusu zao hilo zikakataliwa, walishauliza maswali yao yakajibiwa kwa kuundwa kwa tume itakayochunguza mkonge na tuhuma zote zinazotolewa, leo ghafla wasikie hoja ya Zitto, hivi kibinadam wale wanasiasa wanaotaka kuonekana nao wanatetea wananchi wao wangekubali? Na hata hivyo majibu ya serikali yalikuwa wazi tu, kwa ufupi, yalitegemewa! Kwa sababu siku mbili kabla ya hapo Mhe. Stephen Hillary Ngonyani(MB, Korogwe Rural) aliuliza swali na akaahidiwa tume itaundwa ili kuchunguza suala la mkonge na makando kando yake, sasa jibu la serikali lilikuja limeisha-printiwa kabisa likimwambia Zitto kuhusu hatua hizo zilizochukuliwa na serikali. Kwa vyovyote vile hata kama Mhe. Yusuph Nassir (MB, Korogwe Urban) angekwama kuwasilisha ile hoja yake ya pingamizi bado tu Mhe. Zitto Zuberi Kabwe (MB, Kigoma North) angepewa jibu lile lile la Waziri Maghembe, lisingekuwa tofauti! Si kitu kigeni, ni utaratibu ambao Zitto mwenyewe anaujua vizuri.

Mimi nilitoa tathmini yangu na msimamo wangu hautabadilika. Kama kuna mtu alidhani nahitaji heshima kutoka kwake kwa kufumba mdomo wangu, basi na asiniheshimu, anitukane na wala haininyimi usingizi! Sifanyi mambo kwa kumuogopa mtu ama kwa kumuonesha mtu kuwa mimi ni shujaa, nafanya ninachoona sahihi tu na hiyo ndiyo dira yangu, period!

NADHANI MTU WA KUKUJIBU VIZURI NI zITTO MWENYEWE. MNA MAMBO MNAYOYAJUA SISI HATUYAJUI
 
Updates juu ya ziara ya CHADEMA mkoani Tanga nimepost hapo juu.
Kumbe makamanda hawalengi suala la mkonge tu, bali maendeleo kwa ujumla.
Nimefurahi sana walivyogusia elimu maana Tanga kwakweli inashika mkia, nafikiri hata Singida na Shinyanga hivi sasa zina nafuu.
Naamini wana Tanga mtafunguka macho na kuona njia.
Ufisadi sasa basi, imetosha!
 
Zitto alivamia ajenda ya Wabunge wa Majimbo ya Korogwe, kwa vyovyote vile alitegemea wangempinga. Angetaka afanikishe ajenda yake, ambayo kimsingi ni nzuri, angewahusisha wenzake wenye dhamana na majimbo hayo. Tatizo lilikuwa ni njia na wala siyo malengo (kama kweli alikuwa nayo, na kama alikuwa na nia ya kizalendo ya kutaka mafanikio kwenye hili). Kama alikuwa anafanya siasa, kama inavyojidhihirisha sasa, matokeo ndiyo hayo - kukumbana na upinzani na ushindani mkali!

Mimi binafsi nimejifunza: Hoja yangu binafsi ya uchimbaji dhahabu Nzega nliyoiwasilisha kwenye zaidi ya mikutano 5 ya Bunge haijawahi kupatiwa nafasi kwa visingizio visivyo na maana kwa vile tu ni ya kipambanaji na mimi niliifanya ni yangu binafsi, sasa nimeamua kuunganisha wadau wengi zaidi ili tushirikiane kuiweka sawa na kuiwasilisha tena. Na sasa nimeamua kuwasilisha hoja binafsi bungeni kuhusiana na ajenda ya 'ajira kwa vijana' lakini nitawashirikisha wabunge wenzangu vijana kabla ya kufanya hivyo ili tufanikishe upatikanaji wa ufumbuzi wa pamoja wa tatizo hili...
Hoja hapa ni ishu ya mkonge..unatuletea mambo ya uchimbaji wa madini. Ungestik kwenye mambo ya mkonge mkuu iyo hoja yako ungeianzisha wadau wachangie!! Magamba bwana..utawajua kwa kurupuka yao.
 
Mie sioni kam watu wa Tanga wanajijali kwani hawangeichagua CCm wakati wanajua ndiyo iliyowafikisha hapo na bila kuwahurumia. Kila kitu Tanga ni hovyo hovyo yuUvuvi zii, Mkonge ZII, Reli Ziii, Bandari ziii etc etct ziiiiiiiii lakini bado wako na majambazi wao tu leave them!!!!

Nungana na wewe. Tanga tumelala sijui tumelishwa nini. Tanga ya miaka 20 iliyopita siyo kabisa leo ni uozo lakini bado ndugu zangu wameng`ang`ana na majambazi ya ccm.Kila kitu Tanga kimekufa, kimebaki kimebaki kiwanda cha saruji.Leo hii wanaume Zitto na Mnyika wanakuja kuwafumbua wasambaa na wazigua macho, msomi kama Kigwangala anaibuka na hoja mbovu.Wabunge wote wa Tanga ni utumbo mtupu hakuna la maana wanasimamia.

Ndugu zangu Wasambaa,Wabondei,Wazigua na Wadigo na wale wote muishio huko amkeni, acheni kuota mchana,ccm haitawasidia kabisa mtabaki kulia kila siku. Kosa lenu ni kuwachagua wabunge wa chama cha majambazi ya rasilimali zetu
 
Back
Top Bottom