Escobar
JF-Expert Member
- Sep 16, 2011
- 574
- 440
Mdogo wangu amekuwa akifuatilia madai yake tangu mwanzoni mwa mwezi wa pili pale NSSF Ilala. Alipojaza fomu aliambiwa arudi baada ya wiki mbili tu kila kitu kitakuwa tayari! Hivi ninavyoandika hapa ni mwezi wa pili kilasiku anapigwa kalenda na kinadada wa pale mapokezi, kila akifika pale ni ama bosi hayupo na hajasign cheque au mtandao uko chini. Naomba waandishi wa habari watembelee pale japo kwa mahojiano na wateja wowote mtakao wakuta ili mjue usumbufu na manyanyaso wayoyapata watanzania hawa wa hali ya chini baada ya kupoteza kazi kwa zaidi ya miezi sita na maisha yenyewe haya ya Dar es Salaam. Kutokana na usumbufu alioupata ndugu yangu mimi binafsi na workmate wenzangu tumeamua kuconvert to PPF japo siijui vizuri sana ila tu sitaki kusikia kitu kinaitwa NSSF tena maana mimi mwenyewe nimeshamsindikiza pale 3 times anaenda kuambulia story utadhani kaenda kuomba mkopo au msaada. Mbaya zaidi nasikia mkurugenzi wake yuko busy na harakati za kutaka ubunge huko kwao mafia huku shirika linadoda kwa utendaji mbovu!