Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,493
- 30,187
Kuna msemo wa wahenga usemao kuwa kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza......................
Kwa namna CCM ilivyosambaza mabango nchi nzima, wakati wapinzani wao wa kisiasa, vyama vya upinzani, wakiwa hoi bin taabani, naweza ulinganisha usemi huo na hali halisi ya hivi sasa.
Hivi unawezaje kulinganisha mapokezi makubwa mno anayoyapata Tundu Lissu, ukimlinganisha na John Magufuli, wakati akiwa hana bango hata moja nchi nzima?
Ni wazi kuwa watu wao wa "marketing" wanafanya kazi ya ziada katika kufanya hiyo "promo" kwa kumtangaza kwa nguvu zote huyo mgombea wao wa kiti cha Urais, John Pombe Magufuli na ya wagombea wengine wa CCM.
Nimekuwa pia nikijiuliza hivi nguvu yote wanayotumia CCM ni ya nini wakati walishautangazia ulimwengu, kuwa vyama vya upinzani vimeshajifia "natural death" kutokana na utendaji wa kutukuka wa Magufuli!
Nimejiuliza pia hivi ni serikali ya CCM hii hii ambayo imekuwa ikisema kwa miaka 5 mfululizo, ikiwagomea kabisa kabisa kuwaongezea mishahara ya wafanyakazi wa Umma kwa madai kuwa serikali haina fedha hizo za kuwaongezea mishahara watumishi hao, lakini wakati huo huo wananchi tukishuhudia chama tawala cha CCM kikitapanya mali ya Umma kwa kusambaza mabango kila mahali hadi kubandika mabango hayo kwenye miti na kwenye sehemu za "kujisaidia" watu uchochoroni?
Hivi wananchi wanajisikiaje kuhusu matumizi haya mabaya kabisa ya pesa, wakati hospitali zetu nyingi, wananchi wengi wanakufa, kwa kukosa dawa muhimu za panadol?
Hivi nyinyi maccm mnawezaje kufanya "promo" kwenye mikutano yenu ya CCM, kwa kuwalipa mamilioni ya pesa wasanii maarufu akina Diamond, wakati watoto wetu wanakalia matofali, kwa kukosa madawati mashuleni?
Imenenwa na wahenga kuwa kupanga ni kuchagua..............
Kwa hiyo kwa CCM kwao wamepanga, kipaumbele chao ni kufanya "promo ya kufa mtu" kwa mgombea wao Magufuli nchi nzima hadi yanakinaisha na kuleta kichefu chefu!
Kwa namna CCM ilivyosambaza mabango nchi nzima, wakati wapinzani wao wa kisiasa, vyama vya upinzani, wakiwa hoi bin taabani, naweza ulinganisha usemi huo na hali halisi ya hivi sasa.
Hivi unawezaje kulinganisha mapokezi makubwa mno anayoyapata Tundu Lissu, ukimlinganisha na John Magufuli, wakati akiwa hana bango hata moja nchi nzima?
Ni wazi kuwa watu wao wa "marketing" wanafanya kazi ya ziada katika kufanya hiyo "promo" kwa kumtangaza kwa nguvu zote huyo mgombea wao wa kiti cha Urais, John Pombe Magufuli na ya wagombea wengine wa CCM.
Nimekuwa pia nikijiuliza hivi nguvu yote wanayotumia CCM ni ya nini wakati walishautangazia ulimwengu, kuwa vyama vya upinzani vimeshajifia "natural death" kutokana na utendaji wa kutukuka wa Magufuli!
Nimejiuliza pia hivi ni serikali ya CCM hii hii ambayo imekuwa ikisema kwa miaka 5 mfululizo, ikiwagomea kabisa kabisa kuwaongezea mishahara ya wafanyakazi wa Umma kwa madai kuwa serikali haina fedha hizo za kuwaongezea mishahara watumishi hao, lakini wakati huo huo wananchi tukishuhudia chama tawala cha CCM kikitapanya mali ya Umma kwa kusambaza mabango kila mahali hadi kubandika mabango hayo kwenye miti na kwenye sehemu za "kujisaidia" watu uchochoroni?
Hivi wananchi wanajisikiaje kuhusu matumizi haya mabaya kabisa ya pesa, wakati hospitali zetu nyingi, wananchi wengi wanakufa, kwa kukosa dawa muhimu za panadol?
Hivi nyinyi maccm mnawezaje kufanya "promo" kwenye mikutano yenu ya CCM, kwa kuwalipa mamilioni ya pesa wasanii maarufu akina Diamond, wakati watoto wetu wanakalia matofali, kwa kukosa madawati mashuleni?
Imenenwa na wahenga kuwa kupanga ni kuchagua..............
Kwa hiyo kwa CCM kwao wamepanga, kipaumbele chao ni kufanya "promo ya kufa mtu" kwa mgombea wao Magufuli nchi nzima hadi yanakinaisha na kuleta kichefu chefu!