Hivi kweli mama zetu ndio wawe watunzaji wa mali zetu? Mnawajua mama zetu walivyo?

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Nov 28, 2013
10,309
35,731
Kisa cha mchezaji wa PSG Achraf Hakimi kuandikisha mali zake kwa jina la mama yake halafu mkewe kuambulia patupu mara baada ya kuachana kimewafanya wanaume wengi kupata muamko wa kutaka kuiga hiyo style. Lakini kuna mambo watu huenda wanasahau kuhusu hawa mama Zetu hususani huku Afrika. Kwa uchache sana nitaweka hapa.

Mama zetu wengi (huenda 90%) wako hivi;
1. Upeo duni wa kutunza na kuendeleza mali. (Kumuachia mali zako ni zaidi ya kucheza kamari)

2. Wako chini ya himaya ya waume zao (waume hao wanaweza kuwa ni baba zetu wa kutuzaa au baba wa kambo)

3. Wanategemewa na familia na koo zao. (Yaani kuna msururu wa ndugu wamekaa wanasubiri kuvuna kwa migongo ya mama zetu).

4. Waumini holela wa imani tofauti tofauti. (Leo unaweza kumkukuta kwa mganga wa kienyeji, kesho kwa Mwaposa, keshokutwa kwa Sharif Majini nk. Kote huko anamwaga pesa).

5. Hawajatulia kabisa (wengi ni single mothers walioshindikana, wadangaji, mijishangazi, walevi, washirikina, wafitini nk)

6. Maisha yao yamezungukwa na kuathiriwa na watu wa ovyo ovyo balaa (hapo kuna majirani, ndugu, jamaa, marafiki, mashosti nk na hao ndio wenye kuamua mtindo wa maisha ya mama zetu hususani mama zetu wakiwa na mali).

Hitimisho langu.
Mtu sahihi wa kumuandikisha umiliki wa mali zako:
-Wa kwanza ni wewe mwenyewe
-Wa pili ni mkeo
-Wa tatu ni mtoto wako wa kumzaa.
 
Ni akina mama wapi unaozungumzia ww?; Pwani ama bara?.
Wamama wa bara hawanaga hizo!
Wamama wa bara wana maadili achana na wale wanaowazaga kuiba pesa kwaajili ya;

√ Kucheza vikoba.

√ Viigodoro.

√ Kununua madera na vijora.

√ Nyama choma na chipsi kuku mataahira.

√ Kunufaisha michepuko kwa upumbavu wa "figa 1 haliwezi kuenjika sufuria jikoni".

√ Kujaza kabati kwa mawigi, makucha bandia, mikorogo n.k.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Mahali salama zaidi pa kutunza mali zako ni kwako mwenyewe, kama wewe mwenyewe huwezi kuzitunza, mama yako ndio akutunzie?
Mfano hakimi angezitunza mwenyewe kwa jina lake sasa hivi tungekuwa tunamcheka, sajili hata kikampuni cha mchongo na uandike nyumba magari na viwanja ni vya kampuni leo na kesho mwenzio akibadilika unamwambia mm sina kitu nyumba magari yote nimepewa na kampuni
 
Ni akina mama wapi unaozungumzia ww?; Pwani ama bara?.
Wamama wa bara hawanaga hizo!
Mama zetu ndio hawa hawa, na kiujumla tabia zao zinashahabiana, hakuna mama wengine zaidi ya hao.

Ukija Pwani na Kusini utakuta mama zetu kutwa kucheza vigodoro, kupaka rangi kucha na kusutana....

Ukienda kule Kaskazini utaambiwa mama zetu wanaua baba zetu ili kuvuna mali, kuvuka boda ili kwenda kupigwa miti.....

Ukienda kule Kanda ya ziwa, mama zetu wanafugwa kama ng'ombe, wanarithiwa kama mali zingine, wanapigwa kama ngoma, wanatumishwa kama punda.....

Sasa hao ndio mama zetu wakuandisha mali zetu wazimiliki?
 
Mfano hakimi angezitunza mwenyewe kwa jina lake sasa hivi tungekuwa tunamcheka, sajili hata kikampuni cha mchongo na uandike nyumba magari na viwanja ni vya kampuni leo na kesho mwenzio akibadilika unamwambia mm sina kitu nyumba magari yote nimepewa na kampuni
Vipi kuhusu Adebayor ambaye aliandikisha mali zake kwa jina la mama yake na mwisho wa siku mama yake akampiga tukio?
 
Unazungumzia wamama walozaliwa nyakati zipi ??

Tulishakubaliana, wakina Mama ni wale ambao angalau sahizi wanamiaka kuanzia 55 hivi nakuendelea.
Kule kanda ya ziwa wamama wa umri huo ndio wanauwawa kwa Imani za kishirikina au jamii kuwafirisi mali walizorithi kutoka kwa waume zao waliofariki.

Hapo kuna usalama wa kuwamilikisha mali zako?
 
Kisa cha mchezaji wa PSG Achraf Hakimi kuandikisha mali zake kwa jina la mama yake halafu mkewe kuambulia patupu mara baada ya kuachana kimewafanya wanaume wengi kupata muamko wa kutaka kuiga hiyo style. Lakini kuna mambo watu huenda wanasahau kuhusu hawa mama Zetu hususani huku Afrika. Kwa uchache sana nitaweka hapa.

-Wa tatu ni mtoto wako wa kumzaa.
Usisahau, mkeo naye ni mama kwa watoto wako..!! Kama wewe umemuamini ukamuandika kama mkeo, una hofu ipi mtu huyo huyo aliandikwa kama mama na watoto wako..!??
 
Mama zetu ndio hawa hawa, na kiujumla tabia zao zinashahabiana, hakuna mama wengine zaidi ya hao.

Ukija Pwani na Kusini utakuta mama zetu kutwa kucheza vigodoro, kupaka rangi kucha na kusutana....

Ukienda kule Kaskazini utaambiwa mama zetu wanaua baba zetu ili kuvuna mali, kuvuka boda ili kwenda kupigwa miti.....

Ukienda kule Kanda ya ziwa, mama zetu wanafugwa kama ng'ombe, wanarithiwa kama mali zingine, wanapigwa kama ngoma, wanatumishwa kama punda.....

Sasa hao ndio mama zetu wakuandisha mali zetu wazimiliki?


Wa mama wa pwani.

Wa mama wa kiislam

Wana tofauti kubwa na wamama wa bara na wamama wa kikristo.

Wamama wa pwani elimu dunia ama elimu ya kusimamia fedha na mali huwa hawafundishwi na jamii zao. ( dini ya kiislam na utamaduni wa pwani haumfundishi mwanamke mambo ya mali na pesa )

Wamama wa bara hata kama hawajaenda darasani..ila wanafundishwa elimu ya kusimamia fedha na mali kutoka kwa wakubwa zao.
 
Kisa cha mchezaji wa PSG Achraf Hakimi kuandikisha mali zake kwa jina la mama yake halafu mkewe kuambulia patupu mara baada ya kuachana kimewafanya wanaume wengi kupata muamko wa kutaka kuiga hiyo style. Lakini kuna mambo watu huenda wanasahau kuhusu hawa mama Zetu hususani huku Afrika. Kwa uchache sana nitaweka hapa.

-Wa pili ni mkeo
-Wa tatu ni mtoto wako wa kumzaa.
Watanzania wengi hii habari wanaisoma juu juu alichofanya hakimi kamuandika kila kitu bi mkubwa ila vitu vyote yeye ndio ana access navyo yaani mama yake hawezi fanya chochote bila hakimi maana document zote anazo hakimi ila mali kaandika majina ya mama na akajiandika yeye ndio next kin kwamba mama akitangulia basi vitu vyote vinakuwa chini yeye mama yeye ni kama bortion tu na hiyo ni kawaida kwa familia za waarabu kwao kufanya hvyo hii ni tofauti na Adebayor alipuandika kila kitu kwa mama yake halafu akamuachia mpaka document zikae kwake.
 
Usisahau, mkeo naye ni mama kwa watoto wako..!! Kama wewe umemuamini ukamuandika kama mkeo, una hofu ipi mtu huyo huyo aliandikwa kama mama na watoto wako..!??
Kuna tofauti kubwa sana kati ya mama yako na mkeo.
Kwa haraka sana, mama yako ni mtu aliyekuzaa na kukulea, hakuna kitu kingine alichonacho cha zaidi. Unapaswa kumpenda, kumtunza na kumheshimu. Lakini mtu huyo (mama yako) anaweza kuwa mjinga, kichaa, mwizi, malaya, mchawi nk na isiweze kufanya chochote kumkwepa kama mzazi wako. Kiujumla jumla hatoshei kuwa mmiliki wa mali zako.

Mkeo ni mwenzi wako kimaisha (Life Partner), mbia kamili wa maisha yako, mrithi kamili wa mali zako ikiwa leo haupo duniani. Unaamua kumchagua katikati ya wanawake wote waliopo duniani. Kiujumla jumla ni mtu sahihi kuwa mmiliki wa mali zako.
 
Mimi toka nimeanza ajira na share account na bimkubwa na yeye anaela nyingi kuliko mimi na tunaish vzr tu naweka ela kwake kwasabu anauwezo mkubwa wa kusave ela kuliko mimi
Tuwe wakweli hapa JF.
Ni lini wewe ulimtumia mama yako pesa ya vocha, sabuni au sukari?
 
Kuna tofauti kubwa sana kati ya mama yako na mkeo.
Kwa haraka sana, mama yako ni mtu aliyekuzaa na kukulea, hakuna kitu kingine alichonacho cha zaidi. Unapaswa kumpenda, kumtunza na kumheshimu. Lakini mtu huyo (mama yako) anaweza kuwa mjinga, kichaa, mwizi, malaya, mchawi nk na isiweze kufanya chochote kumkwepa kama mzazi wako. Kiujumla jumla hatoshei kuwa mmiliki wa mali zako.

Mkeo ni mwenzi wako kimaisha (Life Partner), mbia kamili wa maisha yako, mrithi kamili wa mali zako ikiwa leo haupo duniani. Unaamua kumchagua katikati ya wanawake wote waliopo duniani. Kiujumla jumla ni mtu sahihi kuwa mmiliki wa mali zako.
Hujanielewa...!! Nimesema hivi, mkeo naye ni mama kwa watoto wako. Anzia hapo
 
Back
Top Bottom