Historia ya Mitaa mbali mbali ya Jiji la Dar Es Salaam

Dah mmenikumbusha mbali saaana..KWANZA NAOMBA WADAU WALIOWAHI KUISHI MITAA YA TANDAMTI, SUKUMA, NARUNG'OMBE NA LIVINGSTONE kati ya mwaka 1995 na 2005 tutambuane mana nimekulia huko jamani..KARIAKOO ni hatari sana
 
Kwa nini iliitwa majina hayo?

Azikiwe, Samora, Pamba, Garden, Mkwepu, Makunganya, Shauri Moyo, Jamhuri,
Uhuru, Kongo, Chole,............ongezea mingine,

Nitaeleza majina ya mitaa/barabara kabla na baada ya Uhuru:

1. New Street - Lumumba (hapa ndipo ilipokuwa ofisi ya chama cha Tanganyika Africa Association (TAA)
2. Ring Street - Jamhuri
3. Ronald Cameron - UN Road
4. Market street - Indira Ghandi (Hapa ndipo soko la kwa nza lilijengwa mnamo karne ya 19
5. Bagamoyo Street - Morogoro Road (Historia inasema hapa waliishi watu enye asili ya Kiarabu)

Wajerumani walipoona Dar es Salaam katika miaka ya 1900 ikiwa na idadi ya watu 22,500 waliamua kujenga soko kuu wakaliita New Market. Hapo wakoloni wa Kijerumani walijeenga kama ukumbi wenye fremu za chuma / nondo kwa matarajio ya kufanya maonesho ya kumbukumbu ya kutawazwa kwa Kaiser Wilhem wa Ujerumani. Matarajio yao hayakutumia kwani vita ya kwanza ya dunia ilianza. Watawala wa Kiingereza wakachukua utawala wa Tanganyika baada ya vita wakabadili matumizi ya ukumbi huo na kuufanya kambi kwa wapagazi wa kivita "carrier corps" kwa Kiswahili Kariakoo. Hiyo ndiyo historia ya Kariakoo.

Historia ya ukumbi wa Arnautoglu ni kwamba jina hilo limetokana na mwanzilishi wa kwanza wa mahali pa starehe maeneo ya Mnazi Mmoja. Huyu alikuwa na asili ya Kigiriki na Kituruki.

Nawasilisha
 
Mtaa wa lindi umeanzia ilala-unakutana na mtaa wa bungoni...una kwenda mpaka mnazi mmoja kukutana na barabara ya nkrumah..mbele kidogo na clock tower...
 
Asante Ritz kwa swali lako.
Awali ya yote napenda kukuelewesha kuwa sijasema mtaa wa Lindi ni mrefu kuliko yote Kariakoo.
Nimesema mtaa wa Lindi ni mrefu kuliko yote hapo Dar na unaanzia Mnazi mmoja mpaka Ilala...

Hii sio barabara ya uhuru?

Hivi mtaa na barabara unatofautishaje? Ufahamu wangu unaniambia barabara ni ndefu mfano ali hassan Mwinyi road au bibi titi road. Na mtaa ni mfupi mfano mtaa wa narung'ombe....... mtaa wa 7....
 
Nitakujibu mawili matatu
1 Ubungo Maziwa kuliwa na Kiwanda cha Maziwa, sijui bado kipo !sina uhakika.
2 Msasani inasemekana kulikuwa na Mzee mmoja maarufu aliyekua akiishi maeneo hayo aliyekuwa akiitwa Musa Hassan, sasa watu walikuwa wanasema tunakwenda kwa Musa Hassan,au kuna shughuli fulani kwa Musa Hassan. Baadaye ikaja kufupishwa Msasani.
3. Kariakoo inatokana na neno Carrier corps, yaani ushirika wa wapagazi(wabeba mizigo, makuli).

Kibirizi asili ni eneo/kitongoji/Kijiji (sina uhakika) huko Kigoma.
Sasa kama Dar kuna eneo au mahali panaitwa Kibirizi ,labda kuna jamaa mwenye asili ya Kibirizi Kigoma alikaa maeneohayo alikuwa na biashara mfano Duka,Karakana,Bar, Lodging(Guest House) au chochote akakiita jina Kibirizi.
je asili ya jina la Yombo au Buza limetokana na nini mkuu?
 
Samora Machel naye, kama Azikiwe, alikuwa ni kiongozi wa Msumbiji aliyepinga utawala wa amakaburu wa Afrika Kusini. Alifariki kwenye ajali ya ndege mwaka 1986. Mjane wake ndio mke wa Mandela wa sasa.
Sahihisho dogo tu: Samora alikuwa anapigana na utawala wa Wareno (siyo Afrika ya Kusini). Halafu maneno "Mjane wake (yaani mjane wa Samora) ndiyo mke wa Mandela sasa" yangewekwa kwenye past tense kwani tunafahamu kwamba Mandela amekwisha fariki.
 
Sahihisho dogo tu: Samora alikuwa anapigana na utawala wa Wareno (siyo Afrika ya Kusini). Halafu maneno "Mjane wake (yaani mjane wa Samora) ndiyo mke wa Mandela sasa" yangewekwa kwenye past tense kwani tunafahamu kwamba Mandela amekwisha fariki.
ILALA NI MUADHINI WA KIISLAM ALITEKUA AKIADHINI" LAILAA HAILALAA"
 
Sahihisho dogo tu: Samora alikuwa anapigana na utawala wa Wareno (siyo Afrika ya Kusini). Halafu maneno "Mjane wake (yaani mjane wa Samora) ndiyo mke wa Mandela sasa" yangewekwa kwenye past tense kwani tunafahamu kwamba Mandela amekwisha fariki.
Hii post ni ya mwaka 2012 enzi hizo Mandela akiwa hai. Wewe unaijibu leo?
 
Dar es Salaam ilikuwa ikiitwa
“Mzizima"

(Ikimaanisha mji wenye neema), ni mji wa zamani ulioanza mwanzoni mwa miaka ya 1857 .

Ingawa historia ya Mzizima ilianza tangu miaka 1000 iliyopita ambapo watu wa Bara (ambao walijichanganya na Wazaramo na kuwa kati yao)

ambao walitulia na kulima katika maeneo ya mbwa maji magogoni (kwa sasa kivukoni), Mjimwema na Gezaulole.

Jiji la Dar es Salaam
Mji ulianza kuonesha mabadiliko kutokana na ujio wa wa Masultani, Wajerumani na Waingereza.

Mwaka 1866 Sultan Seyyed Majid of Zanzibar aliupa jina la ambalo ndilo linalotumika sasa neno la kiarabu lililomaanisha “Mbingu ya Amani”.

Baaba ya kifo cha Sultan Majid mwaka 1870, Dar es Salaam ilianguka lakini iliinuka tena mara baada ya ulio wa kampuni ya Kijerumani ( German East Africa Company ) iliyoanzisha kituo cha biashara mwaka 1887 na kuuondoa utawala wa Kiarabu hata kutawala pwani ya Africa Mashariki.

Walijenga mamlaka kwa ajili ya kusimamia mambo malimbali ndani ya Africa Mashariki na kuanzisha biashara kwa ajili ya maendeleo ya njia ya reli ya kati.

Iliweza kukua kwa haraka kutokana na utawala pamoja na biashara ya Wajerumani Afrika ya Masahriki.

Mwaka 1891 ulikuwa mji mkuu wa “Gerrnan East Africa“.
Dar es Salaam zamani Mzizima, ni mji mkubwa katika Tanzania na unapatikana pembezoni mwa bahari ya Hindi.

Ni mji mashuhuri na ni muhimu kwani ni mji wa Kibiashara.

Jiji la Dar es Salaam
Wakati wa vita ya kwanza ya dunia Wajerumani Afrika Mashariki waliangushwa na Waingereza na tangu hapo ilijulikana kama Tanganyika.

Baada ya vita vya pili vya dunia, Dar es Salaam ilikuwa kwa haraka ikiwepo kuanzishawa kwa chama cha TANU(Tanganyika African National Union) ambacho kilisababisha Tanganyika kujipatia uhuru tarehe 9 Desemba 1961.

Dar es Salaam iliendelea kuwa mji mkuu mpaka ulipohamishiwa Dodoma mwaka 1973 , ambao ni mji ulio katikati ya nchi ya Tanzania.

Licha ya kutokuwa na tawala za mji mkuu lakini Dar es Salaam iliendelea kuwa makao makuu ya serikali.

Historia ya Ujerumani bado imekuwa ikionekana katika mji. Dar es Salaam ni mji muhimu kwa biashara na serikali.

Dar es salaam Ina Maeneo mengi Sana na Yana Asili yake

Ningependa kujua Maeneo Hayo Na Asili Ya hayo Majina Yanayopatikana Katika Mji wa Dar es salaam

Kwa Mfano

Kunduchi

Tegeta

Posta

Sinza

Manzese

Kariakoo

Kigambon

Ubungo

Mbagala

Kimara

Mbezi beach

Mbezi kimara

Gongo la mboto

Kawe

Morocco

Kinondon

Keko

Temeke

Ilala

Magomeni

Na maeneo mengine Kadha wa Kadha..........

Nawasilisha
 
Dar es Salaam ilikuwa ikiitwa
“Mzizima"

(Ikimaanisha mji wenye neema), ni mji wa zamani ulioanza mwanzoni mwa miaka ya 1857 .

Ingawa historia ya Mzizima ilianza tangu miaka 1000 iliyopita ambapo watu wa Bara (ambao walijichanganya na Wazaramo na kuwa kati yao)

ambao walitulia na kulima katika maeneo ya mbwa maji magogoni (kwa sasa kivukoni), Mjimwema na Gezaulole.

Jiji la Dar es Salaam
Mji ulianza kuonesha mabadiliko kutokana na ujio wa wa Masultani, Wajerumani na Waingereza.

Mwaka 1866 Sultan Seyyed Majid of Zanzibar aliupa jina la ambalo ndilo linalotumika sasa neno la kiarabu lililomaanisha “Mbingu ya Amani”.

Baaba ya kifo cha Sultan Majid mwaka 1870, Dar es Salaam ilianguka lakini iliinuka tena mara baada ya ulio wa kampuni ya Kijerumani ( German East Africa Company ) iliyoanzisha kituo cha biashara mwaka 1887 na kuuondoa utawala wa Kiarabu hata kutawala pwani ya Africa Mashariki.

Walijenga mamlaka kwa ajili ya kusimamia mambo malimbali ndani ya Africa Mashariki na kuanzisha biashara kwa ajili ya maendeleo ya njia ya reli ya kati.

Iliweza kukua kwa haraka kutokana na utawala pamoja na biashara ya Wajerumani Afrika ya Masahriki.

Mwaka 1891 ulikuwa mji mkuu wa “Gerrnan East Africa“.
Dar es Salaam zamani Mzizima, ni mji mkubwa katika Tanzania na unapatikana pembezoni mwa bahari ya Hindi.

Ni mji mashuhuri na ni muhimu kwani ni mji wa Kibiashara.

Jiji la Dar es Salaam
Wakati wa vita ya kwanza ya dunia Wajerumani Afrika Mashariki waliangushwa na Waingereza na tangu hapo ilijulikana kama Tanganyika.

Baada ya vita vya pili vya dunia, Dar es Salaam ilikuwa kwa haraka ikiwepo kuanzishawa kwa chama cha TANU(Tanganyika African National Union) ambacho kilisababisha Tanganyika kujipatia uhuru tarehe 9 Desemba 1961.

Dar es Salaam iliendelea kuwa mji mkuu mpaka ulipohamishiwa Dodoma mwaka 1973 , ambao ni mji ulio katikati ya nchi ya Tanzania.

Licha ya kutokuwa na tawala za mji mkuu lakini Dar es Salaam iliendelea kuwa makao makuu ya serikali.

Historia ya Ujerumani bado imekuwa ikionekana katika mji. Dar es Salaam ni mji muhimu kwa biashara na serikali.

Dar es salaam Ina Maeneo mengi Sana na Yana Asili yake

Ningependa kujua Maeneo Hayo Na Asili Ya hayo Majina Yanayopatikana Katika Mji wa Dar es salaam

Kwa Mfano

Kunduchi

Tegeta

Posta

Sinza

Manzese

Kariakoo

Kigambon

Ubungo

Mbagala

Kimara

Mbezi beach

Mbezi kimara

Gongo la mboto

Kawe

Morocco

Kinondon

Keko

Temeke

Ilala

Magomeni

Na maeneo mengine Kadha wa Kadha..........

Nawasilisha

Upo uzi unaozungumzia hayo majina.
 
Back
Top Bottom