Historia ya Mitaa mbali mbali ya Jiji la Dar Es Salaam

Mkuu usisahau Congo inaanzia Jangwani mpaka Gerezeni. Vile vile usisahau Aggrey inaanzia Kariakoo ya Muheza mpaka Samora.

Jamani mtaa mrefu zaidi ni Aggrey mtaa huu unaanzia pale TBL Ilala na unaishia Samora
Na mtaa mfupi zaidi kwa K'koo unafahamika kama MBUNI huko fire mtaa huu unaziusisha nyumba tatu tu
Tuendelee ................................
 
Mmetoka nje ya mada .mhuza mada kauliza asili ya mitaa ya dar .ni kwa nini inaitwa hiyo??kwa mfano kasema mtaa wa samora unaitwa hiyo kutokana na kiongozi wa msumbiji aliyeongoza mapambano zidi ya utawala wa makaburu.
 
Gang Chomba,
Ebu twende taratibu mtaa wa Lindi unaazia wapi na unaishia wapi? Halafu hunajua Aggrey unaanzia wapi na unaishia wapi?
Mtaa wa Lindi ni mrefu kuliko Aggrey, unaanzia Ilala Bungoni mpaka unakutana na Nkurumah (Hapo katikati kuna jengo la Ushirika na bustani ya Mnazi mmoja).
Mtaa wa Aggrey unaanzia Mtaa wa Muheza (Jirani na TBL) na unaishia Mtaa wa India.
 
Last edited by a moderator:
Asante Ritz kwa swali lako.
Awali ya yote napenda kukuelewesha kuwa sijasema mtaa wa Lindi ni mrefu kuliko yote Kariakoo.
Nimesema mtaa wa Lindi ni mrefu kuliko yote hapo Dar na unaanzia Mnazi mmoja mpaka Ilala...

mtaa wa lindi (SASA UNAITWA SOFIA KAWAWA) Unaanzia Nkrumah hadi Ilala
 
Mnabishania urefu badala ya asili yake kama mtoa mada alivyouliza, mngeanzisha uzi wenu kwingine.
 
watanzania kweli vilaza yaani hoja ya jmaa ni kutaka historia ya baadhi ya majina ya mitaa lkn woteee mnazungumzia urefu na ufupi wa mitaa. Jamani.WOTE MNAONGOZWA NA GIZA SIO NURU KWA HALI HII. DAAHH!!!
 
Mkuu hapo kwenye mtaa swahili umekosea kidogo, hauanzii kariakoo shimoni, umeanzia fire pale kwenye junction ya morogoro road na umoja wa mataifa
 
Nnamdi Azikiwe alikuwa ni kiongozi wa kwanza wa Nigeria mara baaya uhuru wa nchi hiyo. Barabara yetu ile maarufu imepewa jina hilo kama kumbukumbu yake. Alifariki mwaka 1996.

Samora Machel naye, kama Azikiwe, alikuwa ni kiongozi wa Msumbiji aliyepinga utawala wa amakaburu wa Afrika Kusini. Alifariki kwenye ajali ya ndege mwaka 1986. Mjane wake ndio mke wa Mandela wa sasa.

Hassan Omari Makunganya alikuwa kiongozi wa Wangindo (sina uhakika sana na kabila). Aliongoza watu wake kupigana na Wajerumani dhihi ya utawala wa Wajerumani. Alishirikiana na akina Kinjekitile Ngwale katika vita iliyojulikana kama Majimaji (1905 - 1907)

Asante mhe. sana Invisible kwa kuuhuisha uzi huu tena.
Naendelea...
Sam Nujoma...(Samuel Daniel Shafiishuna Nujoma) Barabara hii imepewa kumbukumbu ya rais wa kwanza wa Namibia huru (1990-2005). Mpigania uhuru huyu aliishi Tanzania miaka hiyo akipigania uhru wa nchi yake, katika mikoa ya Mbeya na Morogoro. Ili kuwakwepa makaburu waliokuwa wakimtafuta, alipewa jina la uongo (pseudonym) la Kinyakyusa Sam Mwakangale, akiwa mkoani Mbeya.

Luthuli....Barabara hii iliyopo eneo maarufu la Ikulu, imepewa jina kutokana na mwanasiasa maarufu wa Afrika kusini (alizaliwa Zimbabwe), Albert Luthuli (1898-1967).

Lumumba....Barabara hii ilinayoambaa na bustani ya Mnazi Mmoja hadi katika makutano na barabara ya Morogoro imepewa jina la kiongozi (rais) wa kwanza wa Congo huru (Congo DRC) ndugu Patrice Emery Lumumba (1925-1961). Mtaa huu ndiko iliko ofisi ndogo ya Chama cha Mapinduzi.

Mwingine atujuze majina haya ya mitaa ya Magila, Muhonda, Aggrey. Mkwepu n.k.

Sijajua ni nani alikuwa na maamuzi ya kuzipa majina barabara zetu hizi
 
Last edited by a moderator:
Asante mhe. sana Invisible kwa kuuhuisha uzi huu tena.
Naendelea...
Sam Nujoma...(Samuel Daniel Shafiishuna Nujoma) Barabara hii imepewa kumbukumbu ya rais wa kwanza wa Namibia huru (1990-2005). Mpigania uhuru huyu aliishi Tanzania miaka hiyo akipigania uhru wa nchi yake, katika mikoa ya Mbeya na Morogoro. Ili kuwakwepa makaburu waliokuwa wakimtafuta, alipewa jina la uongo (pseudonym) la Kinyakyusa Sam Mwakangale, akiwa mkoani Mbeya.

Luthuli....Barabara hii iliyopo eneo maarufu la Ikulu, imepewa jina kutokana na mwanasiasa maarufu wa Afrika kusini (alizaliwa Zimbabwe), Albert Luthuli (1898-1967).

Lumumba....Barabara hii ilinayoambaa na bustani ya Mnazi Mmoja hadi katika makutano na barabara ya Morogoro imepewa jina la kiongozi (rais) wa kwanza wa Congo huru (Congo DRC) ndugu Patrice Emery Lumumba (1925-1961). Mtaa huu ndiko iliko ofisi ndogo ya Chama cha Mapinduzi.

Mwingine atujuze majina haya ya mitaa ya Magila, Muhonda, Aggrey. Mkwepu n.k.

Sijajua ni nani alikuwa na maamuzi ya kuzipa majina barabara zetu hizi

Mkuu,hapo kwa Nujoma kupewa jina la kificho nimepapenda,ila na jina la Sam wangembadilisha wangemwita Tuntufye.
 
Last edited by a moderator:
Mtaa wa Lindi ni mrefu kuliko Aggrey, unaanzia Ilala Bungoni mpaka unakutana na Nkurumah (Hapo katikati kuna jengo la Ushirika na bustani ya Mnazi mmoja).
Mtaa wa Aggrey unaanzia Mtaa wa Muheza (Jirani na TBL) na unaishia Mtaa wa India.

Mtaa wa aggrey una asili ipi?hiyo aggrey ni jina la mtu kama aggrey mwanri?
 
mtaa wa ufipa ndio mtaa wa kwanza kinondoni kwa wauza BWIMBWI kama utaki sikulazimishi.
 
Back
Top Bottom