Hisabati/mathematics nightmare

Ile misingi inayotumika katika kujenga hoja wakati wa kuprove theorem ndiyo msingi inayotumika pia katika kujenga hoja ya kutatua matatizo mengine ya kijamii. Usichukulia reproduction ya material bali angalia application ya methods. Mathematician mzuri siyo mkurupukaji katika mambo yake; kila jambo analiangalia kwa makini na kina sana. Huo utamadunbi wa kuangalia mambo kwa kina ndio unawafanya wawe na mtazamo mpana sana wa kila jambo na hata katika mambo ya jamii. Utashangaa kuwa mathematician aliyeiva hawezi kukubali kuwa 3+1.0=4, ingawa watu wa kawaida wanaojua hesabu za kukokotoa tu watamshangaa.


Umesema vyema sana, "Mathematician Mzuri" kama haya mambo unayoyasema yanafanywa na mathematicians kwa nini kila mtu apitishwe kwenye tanuru la hesabu? wewe mwenyewe lini katika maisha yako uliishakutana na senerio iliyokufanya utumie logarithm.

Alafu umesema vyema zaidi "watu wa kawaida", kwa nini na watu wakawaida wanyimwe nafasi za kwenda chuo kikuu kwa sababu wamefail hesabu? why?
 
Umesema vyema sana, "Mathematician Mzuri" kama haya mambo unayoyasema yanafanywa na mathematicians kwa nini kila mtu apitishwe kwenye tanuru la hesabu? wewe mwenyewe lini katika maisha yako uliishakutana na senerio iliyokufanya utumie logarithm.

Alafu umesema vyema zaidi "watu wa kawaida", kwa nini na watu wakawaida wanyimwe nafasi za kwenda chuo kikuu kwa sababu wamefail hesabu? why?

Wewe unazungumzia hesabu za kukokotoa, wakati mimi nazungumzia hesabu za kufikiri. Ungesoma vizuri post yangu ya awali, huenda usingeuliza swali la matumzi ya logarithm. Hata hivyo, huwezi kujua hesabu za kufikiri iwapo hujui hesabu hizo ndogo za kukokotoa. Kuhusu kwenda chuo kikuu, siyo kweli kuwa ni lazima uwe umepasi hesabu, unaweza kwenda kusoma history ambayo hahitaji hesabu kabisa. Iila masomo ya sayansi yanahitaji hesabu.
 
Hisabati ni muhimu sana mkuu katika kuweza kuishi katika ulimwengu wetu. Ni lazima kuweza ulazima wa wanafunzi wote ingali wakiwa madarasa ya chini kusoma hisabati, hivyo kupata msingi mzuri wa hisabati. Kwa mfano huwezi kufanya hesabu za kugawanya kama hujui kujumlisha na kutoa, huwezi kutafuta mzingo wa mstatili kama hujui kujumlisha, huwezi kufanya calculus kama hujui kujui kujumlisha kutoa kuzidisha na kugawanya. Kwa hiyo mtu huwezi kufanya hisabati za juu (calculus and the likes) kama hujui simple arithmetics. Hizi hisabati za juu ndizo hutumika katika technology zote muhimu tuzitumiazo, unaweza kusema kuwa mkulima hahitaji kujua hisabati mbali ya bodmas lakini wataalamu wengine(wadau) wa kilimo wanatumia directly au indirectly hisabati za juu. Kwa mfano wanaotengeneza pembejeo za kilimo lazima watumie technology nzuri, kwenye kusafirisha mazao na pembejeo za kilimo ni dhahiri watatumia nishaji kama petrol ambayo upatikanaji wake unatumia technology ya hali ya juu katika utafiti wa petroleum, drilling, market research, financing, kuchambua hydrocarbons n.k.

Kwa mfano ukichukua watoto 1000 watakaoanza darasa la kwanza 2013 sio kwamba baada ya miaka 25 kupita wote watafikia hatua ya udaktari wa falsafa katika nyanja fulani, bali hatua za kielimu watakazofikia zitakuwa katika umbo la piramidi, watakaofikia phd(juu kabisa ya piramidi) watakuwa ni wachacha mno na watakaoishia elimu ya chini(form four) watakuwa ni wengi sana. Na hata hao walioishia form four kwa kiasi fulani kusoma hisabati kutakuwa kumewasaidia sana katika kutoa maamuzi, kufikiria, kupanua upeo na kuishi katika maisha ya kila siku.

Katika definition ya ulimwengu kwenye wikipedia wameandika hivi
More customarily, the universe is defined as everything that exists, (has existed, and will exist). According to our current understanding, the universe consists of three principles: spacetime, forms of energy, including momentum and matter, and the physical laws that relate them.

Kwa hiyo ili kuweza kujua hivi vitu hatuwezi kuepuka kutilia mkazo hisabati
 
hesabu ni muhimu lakini nafikiri tafakuri inayosisitizwa katika hesabu ndio kitu cha msingi zaidi, kwa hiyo kutafakari kwa kina na kupata suluhu ya matatizo ndio la msingi zaidi. hesabu huitaji ufikiri wa hali ya juu but hesabu yenyewe ni namba tu.

kitu cha kusisitiza hapa ni tafakuri katika matatizo yote.
 
ukisoma philosophy kuna topic ya logic, if.......... and .......... therefore.........
ili upate validity au invalidity ya argument au ili ujue kama ni sound au not sound argument.

hii ni topic ngumu inahitaji kufikiri kwa hali ya juu sana na hiyo ndio tafakuri inayotakiwa. hesabu sasa hutumika kama viashiria vya tafakuri katika hoja yani watu watatu walikuwa hapa hatuwajui 3x wengine 2x wakaondoka tunabaki na wangapi 3x-2x=?
 
yani tunavyokuwa tunatafakari tunavipa vitu namba zakutuwezesha kuvitofautisha na kuvikokotoa na kuturahisisha kuweka formular lakini cha msingi katika minamba si minamba yenyewe ila tafakuri. ambayo katika maisha ya kawaida bila kutafakari hata uvumbuzi na utoaji wa masuluhu ni ngumu kupata suluhu na kuencdelea kabisa.

na ndio maana sisi hatupati suluhu ya matatizo yetu kwa sababu hatujishughulishi kufikiri kwa kina tunachukulia vitu kama vilivyo kwa urahisirahisi tui. ningekuwa nashauri ni masomo gani ya lazima toka shule ya msingi falsafa ingekuwa namba moja.
 
yani tunavyokuwa tunatafakari tunavipa vitu namba zakutuwezesha kuvitofautisha na kuvikokotoa na kuturahisisha kuweka formular lakini cha msingi katika minamba si minamba yenyewe ila tafakuri. ambayo katika maisha ya kawaida bila kutafakari hata uvumbuzi na utoaji wa masuluhu ni ngumu kupata suluhu na kuencdelea kabisa.

na ndio maana sisi hatupati suluhu ya matatizo yetu kwa sababu hatujishughulishi kufikiri kwa kina tunachukulia vitu kama vilivyo kwa urahisirahisi tui. ningekuwa nashauri ni masomo gani ya lazima toka shule ya msingi falsafa ingekuwa namba moja.

Absolutely Iron Lady
 
hesabu ni muhimu lakini nafikiri tafakuri inayosisitizwa katika hesabu ndio kitu cha msingi zaidi, kwa hiyo kutafakari kwa kina na kupata suluhu ya matatizo ndio la msingi zaidi. hesabu huitaji ufikiri wa hali ya juu but hesabu yenyewe ni namba tu.

kitu cha kusisitiza hapa ni tafakuri katika matatizo yote.
Iron lady unaweza ukanikumbusha ni somo gani au topic ipi kwenye somo gani inafundisha namna ya kutafakuri, hasa kwenye ngazi ya shule ya msingi mpaka form six?
 
ukisoma philosophy kuna topic ya logic, if.......... and .......... therefore.........
ili upate validity au invalidity ya argument au ili ujue kama ni sound au not sound argument.

hii ni topic ngumu inahitaji kufikiri kwa hali ya juu sana na hiyo ndio tafakuri inayotakiwa. hesabu sasa hutumika kama viashiria vya tafakuri katika hoja yani watu watatu walikuwa hapa hatuwajui 3x wengine 2x wakaondoka tunabaki na wangapi 3x-2x=?

Iron Lady
tanzania kuna wana philosophy wangapi? ni sahihi philosophy kuchukuliwa kama issue ya kijamii, hasa tunapozungumzia maisha halisi ya mtanzania au mwanadamu?
 
yani tunavyokuwa tunatafakari tunavipa vitu namba zakutuwezesha kuvitofautisha na kuvikokotoa na kuturahisisha kuweka formular lakini cha msingi katika minamba si minamba yenyewe ila tafakuri. ambayo katika maisha ya kawaida bila kutafakari hata uvumbuzi na utoaji wa masuluhu ni ngumu kupata suluhu na kuencdelea kabisa.

na ndio maana sisi hatupati suluhu ya matatizo yetu kwa sababu hatujishughulishi kufikiri kwa kina tunachukulia vitu kama vilivyo kwa urahisirahisi tui. ningekuwa nashauri ni masomo gani ya lazima toka shule ya msingi falsafa ingekuwa namba moja.

falsafa ndio nini? kuna post nimeona unasema tafakuri inayosisitizwa kwenye hesabu ndio muhimu zaidi? ni tafakuri gani?
 
Iron lady unaweza ukanikumbusha ni somo gani au topic ipi kwenye somo gani inafundisha namna ya kutafakuri, hasa kwenye ngazi ya shule ya msingi mpaka form six?


mkuu hata hiyo hesabu yenyewe ni moja ya masomo yanayotusaidia kutafakari na namna ya kutafakari, form six form five na six kuna somo la general studies( GS ) kuna topic kabisa ya falsafa japo ni introduction to philosophy, haipo kiundani sana. ila kwa wanavyuo wengi kwa mfano UDSM mwaka wa kwanza kuna critical thinking and argumentation lazima kwa wale wa social science.
masomo haya yana msaada mkubwa sana kujenga uelewa na ufahamu juu ya mambo mbalimbali.
 
Iron Lady
tanzania kuna wana philosophy wangapi? ni sahihi philosophy kuchukuliwa kama issue ya kijamii, hasa tunapozungumzia maisha halisi ya mtanzania au mwanadamu?
ni sahihi kabisa kwa falsasa kuchukuliwa kama somo la kijamii kwani majibu mengi ya matatizo ya maisha yetu ya kila siku yapo katika falsafa. kwa sababu falsasa inatupa miongozo ya kutafakari na kuchanganua na kufananisha na kutofautisha na kutufanya tugundue ama tuunde suluhu mpya ya matatizo yanayotusibu.
falsasa juu ya uongozi na utawala,maadili,watu na namna ya kuishi kwao, imani zao, n.k yote haya yanahusu maisha yetu ya kila siku sisi kama binadamu.
kuhusu kuwako na wanafalsafa wangapi tanzania sina jibu kwa kweli,wachache sana niwajuao hata mwalimu alikuwa mwanafalsafa kwangu mimi.
 
falsafa ndio nini? kuna post nimeona unasema tafakuri inayosisitizwa kwenye hesabu ndio muhimu zaidi? ni tafakuri gani?
falsafa inahusu kutafakari kwa kina juu ya mambo yanayokuzunguka, ama matatizo na kuja na masuluhisho.
sasa kwenye hesabu kwanza ujue hesabu ni namba, sasa si anasema tafuta soln, ile process ya wewe kufikiri na kujiuliza nitoe ipi niweke ipi iwe vp ili upate suluhu ndio tafakuri ninayoizungumzia. kwa hiyo mimi naona hesabu humfanya mtu kutafakari kwa hali ya juu ili kupata hicho anachokiita soln. kule kutafakari kwangu ndio muhimu siyo namba.
na kama watu wakiibeba tafakari kwa namna ya pekee tukawa tunajiuliza mambo mengi yetu ya kila siku tutafika mbali.

sasa hivi mali za nchi zinaibwa ovyo wachache sana wanaojisumbua kujiuliza maswali kadha wa kadha, wengi wanaona kama sawa vile. lakini si sawa na bila kujiuliza basi hatuwezi kusogea hapa tulipo na kwenda kwingine.
 
falsafa inahusu kutafakari kwa kina juu ya mambo yanayokuzunguka, ama matatizo na kuja na masuluhisho.
sasa kwenye hesabu kwanza ujue hesabu ni namba, sasa si anasema tafuta soln, ile process ya wewe kufikiri na kujiuliza nitoe ipi niweke ipi iwe vp ili upate suluhu ndio tafakuri ninayoizungumzia. kwa hiyo mimi naona hesabu humfanya mtu kutafakari kwa hali ya juu ili kupata hicho anachokiita soln. kule kutafakari kwangu ndio muhimu siyo namba.
na kama watu wakiibeba tafakari kwa namna ya pekee tukawa tunajiuliza mambo mengi yetu ya kila siku tutafika mbali.

sasa hivi mali za nchi zinaibwa ovyo wachache sana wanaojisumbua kujiuliza maswali kadha wa kadha, wengi wanaona kama sawa vile. lakini si sawa na bila kujiuliza basi hatuwezi kusogea hapa tulipo na kwenda kwingine.

Pamoja sana dada yangu!
FALSAFA. Hapa ndipo tunapopasa kuanzia kwa katika kutafuta ufumbuzi wa matatizo yetu kama nchi! Tunapolalamika udini, ufisadi, ukabila, rushwa, n.k. Ni lazima tuumize kichwa tuzame katika TAFAKARI nzito juu ya Falsafa ituongozayo!
Critical Thinking anda Arguementation/Speculation ni msingi mkuu wa kupata, ku-excute and examine the philosophy ambayo nayo ni mama wa Logic, which is HUMANITY in Africa!
Watoto wetu wanatakiwa kujengewa mazingira ya Udadisi na Kujiuliza wakitafuta ufumbuzi wa hili na lile(hesabu ni msaada katika hili), wasimezeshwe tu mavitabu ya watu walioandika wakiongozwa na HULKA ZAO! Inasikitisha kumkuta msomi wa chuo kikuu akipimwa kwa uwezo wake wa kutafuta vitabu(references) na si uwezo wake wa ku-argue mambo na creativity zao! Ni upoyoyo!
Mungu wetu anaita sasa!
 
mkuu hata hiyo hesabu yenyewe ni moja ya masomo yanayotusaidia kutafakari na namna ya kutafakari, form six form five na six kuna somo la general studies( GS ) kuna topic kabisa ya falsafa japo ni introduction to philosophy, haipo kiundani sana. ila kwa wanavyuo wengi kwa mfano UDSM mwaka wa kwanza kuna critical thinking and argumentation lazima kwa wale wa social science.
masomo haya yana msaada mkubwa sana kujenga uelewa na ufahamu juu ya mambo mbalimbali.

sasa consider application ya hisabati na critical thinking kwenye maisha yetu ya kila, ni kipi kinapewa kipaumbele huwezi kukuta ni hesabu.
 
falsafa inahusu kutafakari kwa kina juu ya mambo yanayokuzunguka, ama matatizo na kuja na masuluhisho.
sasa kwenye hesabu kwanza ujue hesabu ni namba, sasa si anasema tafuta soln, ile process ya wewe kufikiri na kujiuliza nitoe ipi niweke ipi iwe vp ili upate suluhu ndio tafakuri ninayoizungumzia. kwa hiyo mimi naona hesabu humfanya mtu kutafakari kwa hali ya juu ili kupata hicho anachokiita soln. kule kutafakari kwangu ndio muhimu siyo namba.
na kama watu wakiibeba tafakari kwa namna ya pekee tukawa tunajiuliza mambo mengi yetu ya kila siku tutafika mbali.

sasa hivi mali za nchi zinaibwa ovyo wachache sana wanaojisumbua kujiuliza maswali kadha wa kadha, wengi wanaona kama sawa vile. lakini si sawa na bila kujiuliza basi hatuwezi kusogea hapa tulipo na kwenda kwingine.

First lady ninawasiwasi kama unaelewa hesabu
hakuna tafakari yoyote inayohitajika wakati wa kunyambua milinganyo ya hisabati ni kukumbuka formula, procedure na kutililika tu
 
ni sahihi kabisa kwa falsasa kuchukuliwa kama somo la kijamii kwani majibu mengi ya matatizo ya maisha yetu ya kila siku yapo katika falsafa. kwa sababu falsasa inatupa miongozo ya kutafakari na kuchanganua na kufananisha na kutofautisha na kutufanya tugundue ama tuunde suluhu mpya ya matatizo yanayotusibu.
falsasa juu ya uongozi na utawala,maadili,watu na namna ya kuishi kwao, imani zao, n.k yote haya yanahusu maisha yetu ya kila siku sisi kama binadamu.
kuhusu kuwako na wanafalsafa wangapi tanzania sina jibu kwa kweli,wachache sana niwajuao hata mwalimu alikuwa mwanafalsafa kwangu mimi.

Unanitoa kwenye mada, lakini kama falsafa ni muhimu sana kwenye maisha yetu kwa nini hatufundishwi wote kama ilivyo hisabati,kwa nini falsafa haifundishwi form six kurudi chini? na huko vyuo vikuu kwa nini inafundishwa selectively? falsafa na hisabati ni nini cha muhimu zaidi katika maisha yetu? hisabati nimeishajua sio, inawezekana ikawa ni falsafa, kwa nini sijafundishwa? kwa nini nifundishwe vitu ambavyo sivihitaji kwenye maisha yangu.
 
First lady ninawasiwasi kama unaelewa hesabu
hakuna tafakari yoyote inayohitajika wakati wa kunyambua milinganyo ya hisabati ni kukumbuka formula, procedure na kutililika tu

nafikiri hilo si lengo la hesabu ila ni mazoea ya wafanya hesabu. kukariri na kutiririka.
lakini mimi nawachukulia wale wajuzi wazuri wa hesabu wana tafakari vizuri na kuwa na kumbukumbu nzuri.
ila kwa kufanya kila wakati kila wakati huwa kichwani kwa urahisi na kutohitaji kuitafakari sana ila kutoa majibu.
mfn wanaosoma hesabu inawapasa kuifanya kila siku wasisahau. lakini kwa mara ya kwanza huitaji kutafakari kwa kina ili kuelewa.
 
Unanitoa kwenye mada, lakini kama falsafa ni muhimu sana kwenye maisha yetu kwa nini hatufundishwi wote kama ilivyo hisabati,kwa nini falsafa haifundishwi form six kurudi chini? na huko vyuo vikuu kwa nini inafundishwa selectively? falsafa na hisabati ni nini cha muhimu zaidi katika maisha yetu? hisabati nimeishajua sio, inawezekana ikawa ni falsafa, kwa nini sijafundishwa? kwa nini nifundishwe vitu ambavyo sivihitaji kwenye maisha yangu.


mkuu
nimekutoaje kwenye mada wakati umeniuliza maswali na nimekujibu. na ninaendelea kukujibu, swala kwa nini hatufundishwi falsafa japo ni muhimu ni ubovu wa mitaala yetu ama tuseme vipaumbele vya watunga mitaala katika elimu zetu toka za awali hadi vyuo vikuu. unafikiri kwa nini hatuna somo la maadili katika mitaala yetu ina maana maadili si jambo jema kwetu na maisha yetu ya kila siku? na kama falsafa itafundishwa mashuleni kama somo la lazima tutaandaa kizazi kizuri sana chenye kuelewa na kutaka kuelewa udadisi na kuleta mabadiliko.
 
Back
Top Bottom